Hadhi na haki za mwanamke katika jamii za Kigiriki hapo zamani

(a) UgirikiTunajifunza katika historia ya Ulimwengu kuwa jamii ya Wagiriki ilikuwa miongoni mwa jamii zilizoanza kustarabika.

Hadhi na haki za mwanamke katika jamii za Kigiriki hapo zamani

(a) Ugiriki
Tunajifunza katika historia ya Ulimwengu kuwa jamii ya Wagiriki ilikuwa miongoni mwa jamii zilizoanza kustarabika. Lakini utakuta kuwa hadhi ya mwanamke katika jamii hiyo ilikuwa chini sana. Bwana E.A. Allen katika kitabu chake "History of Civilization Vol. 3" anasema mwanamke wa Kigiriki alilazimishwa kuolewa pasina idhini yake. Mumewe huyo alihesabiwa kuwa Bwana (Lord) wake. Mwanamke alihesabiwa kuwa ni kama mtoto na kwahiyo alitakiwa kumtii mumewe bila kuhoji. Wanawake huko Ugiriki waligawanyika katika makundi matatu:



(i)Makahaba (Malaya) ambao kazi yao ilikuwa ni kuwastarehesha wanaume tu.
(ii)Watumishi ambao kazi yao ilikuwa kuangalia na kutunza siha za mabwana zao.
(iii)Wake amabo kazi yao ni kuzaa na kulea watoto.



Mke alitakiwa awe mwadilifu na achunge murua wake lakini haikuwa vibaya kwa mwanamume kujamii nje ya ndoa. Matokeo ya utaratibu huu ni kuwa wanawake makahaba wakawavutia watu wa ngazi zote - wanafalsafa, washairi, wanahistoria, wanafasihi na wasanii. Picha na sanamu za wanawake walio uchi zikazidi kuchochea zinaa na ufasiki. Ndoa ikaja kuonekana kuwa kero na zinaa ikawa jambo takatifu. Kuzama katika uzinifu kuliwapeleka Wagiriki kuchonga na kuabudu Aphrodite - mungu wa kike wa urembo na mahaba.


Kwa mujibu wa mafundisho ya Wagiriki ni kuwa huyo "Aphrodite" anasemekana kuwa alikuwa ni mungu wa kike aliyeolewa na mungu mwingine. Lakini hakutosheka na mume huyo mmoja. Akaanza kuzini na miungu wengine watatu na akawa pia anazini na binaadamu mmoja. Mungu huyo alipofanya jimai na binaadamu, wakazaa mungu wa kiume aliyeitwa Cupid yaani mungu wa mapenzi. Uzinifu wa "Aphrodite" na kuabudiwa kwake na Wagiriki ni kielelezo cha namna jamii hii iliwatukuza makahaba na kuupa uzinzi hadhi kubwa.


Kutokana na haya tunajifunza kuwa mwanzoni mwanamke katika jamii ya Ugiriki alidunishwa sana. Baadaye jamii ilipopiga hatua mbele katika maendeleo ya kiuchumi, hadhi duni ya mwanamke ilibadilishwa sura. Mwanamke aligeuzwa kuwa chombo cha kuwastarehesha wanaume jambo ambalo lililzidi kumdunisha na kumdhalilisha.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1046

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Namna ya kuosha maiti hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
NI LIPI HASA LENGO LA KUFARADHISHWA SWALA ZA FARADHI NA KUWEPO KWA SWALA ZA SUNNAH (SUNA)

Lengo la Kusimamisha SwalaBila shaka swala imepewa umuhimu mkubwa kiasi cha kufanywa nguzo kubwa ya Uislamu kutokana na lengo lake.

Soma Zaidi...
Njia za kudhibiti riba

Ufumbuzi wa tatizo la ribaRiba imeenea na kuzoeleka duniani kwa kiasi ambacho watu wengi wanadhani kuwa bila riba hakuna shughuli yoyote ya uchumi inayowezekana.

Soma Zaidi...
Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga

Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.

Soma Zaidi...
Adhabu ya mzinifu katika jamii ya kiislamu

(iii) Adhabu ya UzinifuKatika Sheria ya Kiislamu mtu haadhibiwi mpaka atende kwa uwazi matendo yenye kuvuruga utaratibu na amani ya jamii.

Soma Zaidi...
Taratibi za malezi ya watoto wadogo baada ya talaka katika uislamu

Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi?

Soma Zaidi...