Hadhi na haki za mwanamke katika jamii za Kigiriki hapo zamani

(a) UgirikiTunajifunza katika historia ya Ulimwengu kuwa jamii ya Wagiriki ilikuwa miongoni mwa jamii zilizoanza kustarabika.

Hadhi na haki za mwanamke katika jamii za Kigiriki hapo zamani

(a) Ugiriki
Tunajifunza katika historia ya Ulimwengu kuwa jamii ya Wagiriki ilikuwa miongoni mwa jamii zilizoanza kustarabika. Lakini utakuta kuwa hadhi ya mwanamke katika jamii hiyo ilikuwa chini sana. Bwana E.A. Allen katika kitabu chake "History of Civilization Vol. 3" anasema mwanamke wa Kigiriki alilazimishwa kuolewa pasina idhini yake. Mumewe huyo alihesabiwa kuwa Bwana (Lord) wake. Mwanamke alihesabiwa kuwa ni kama mtoto na kwahiyo alitakiwa kumtii mumewe bila kuhoji. Wanawake huko Ugiriki waligawanyika katika makundi matatu:



(i)Makahaba (Malaya) ambao kazi yao ilikuwa ni kuwastarehesha wanaume tu.
(ii)Watumishi ambao kazi yao ilikuwa kuangalia na kutunza siha za mabwana zao.
(iii)Wake amabo kazi yao ni kuzaa na kulea watoto.



Mke alitakiwa awe mwadilifu na achunge murua wake lakini haikuwa vibaya kwa mwanamume kujamii nje ya ndoa. Matokeo ya utaratibu huu ni kuwa wanawake makahaba wakawavutia watu wa ngazi zote - wanafalsafa, washairi, wanahistoria, wanafasihi na wasanii. Picha na sanamu za wanawake walio uchi zikazidi kuchochea zinaa na ufasiki. Ndoa ikaja kuonekana kuwa kero na zinaa ikawa jambo takatifu. Kuzama katika uzinifu kuliwapeleka Wagiriki kuchonga na kuabudu Aphrodite - mungu wa kike wa urembo na mahaba.


Kwa mujibu wa mafundisho ya Wagiriki ni kuwa huyo "Aphrodite" anasemekana kuwa alikuwa ni mungu wa kike aliyeolewa na mungu mwingine. Lakini hakutosheka na mume huyo mmoja. Akaanza kuzini na miungu wengine watatu na akawa pia anazini na binaadamu mmoja. Mungu huyo alipofanya jimai na binaadamu, wakazaa mungu wa kiume aliyeitwa Cupid yaani mungu wa mapenzi. Uzinifu wa "Aphrodite" na kuabudiwa kwake na Wagiriki ni kielelezo cha namna jamii hii iliwatukuza makahaba na kuupa uzinzi hadhi kubwa.


Kutokana na haya tunajifunza kuwa mwanzoni mwanamke katika jamii ya Ugiriki alidunishwa sana. Baadaye jamii ilipopiga hatua mbele katika maendeleo ya kiuchumi, hadhi duni ya mwanamke ilibadilishwa sura. Mwanamke aligeuzwa kuwa chombo cha kuwastarehesha wanaume jambo ambalo lililzidi kumdunisha na kumdhalilisha.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1103

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Aina ya biashara zilizo haramu kwenye uislamu

Hapa utajifunza aina za biashara ambazo ni haramu.

Soma Zaidi...
NI ZIPI SWALA ZA SUNNAH: (qabliya (kabliya) na baadiya, tahajudi, tarawehe, qiyamu layl, shukr, istikhara)

Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi.

Soma Zaidi...
Hukumu ya Talaka kabla ya kufanya jimai

Talaka Kabla ya Jimai:Mwanamume au mwanamke anaweza kughairi na kuamua kuvunja ndoa mapema kabla ya kufanya tendo Ia ndoa.

Soma Zaidi...
Hawa ndio wanaoruhusiwa kurithi

Hii ni orodha ya watu ambao wanaweza kurithi malibya marehrmu.

Soma Zaidi...
Hadathi ya kati na kati

Posti hiibinakwenda kukufundisha kuhusu hadathi ya kati na kati.

Soma Zaidi...
Taratibu za kumuona mchumba katika uislamu

Hspa utajifunza taratibu za kuonana na mchumba katika uislamu.

Soma Zaidi...