Kujiepusha na Vishawishi vya Zinaa

Kujiepusha na Vishawishi vya ZinaaKatika macho ya sheria kitendo cha zinaa kinahesabiwa pale wanapokutana kimwili mwanamume na mwanamke nje ya ndoa.

Kujiepusha na Vishawishi vya Zinaa

Kujiepusha na Vishawishi vya Zinaa
Katika macho ya sheria kitendo cha zinaa kinahesabiwa pale wanapokutana kimwili mwanamume na mwanamke nje ya ndoa. Lakini katika maadili ya Kiislamu kitendo chochote kitakacho fanywa na mwanamume au mwanamke ambacho kitapelekea kuleta matamanio ya jimai nje ya ndoa, kinahesabiwa kuwa ni kitendo cha uzinifu wa ama yake. Kwa mfano mtu kumwangalia kwa matamanio mwanamke asiye kuwa mkewe, kufurahia tusi, uzuri wa sauti ya mwanamke asiyekuwa mkewe,kufurahia maongezi na mwanamke asiyekuwa mkewe au maharimu wake na kumtembelea mara kwa mara mwanamke asiyekuwa mkewe au maharimu wake atakuwa amefanya uzinifu kwa macho, masikio, ulimi na miguu yake.


Hapana sheria yoyote itakayomkamata kwa uzinifu, lakini muumini wa kweli atajihukumu mwenyewe na kujihesabu kuwa ni mkosaji mbele ya Allah (s.w). Hivyo atatubia kwa Mola wake na kujiepusha mbali na vishawishi hivi vya zinaa. Kuhusu zinaa ya viungo mbali mbali vya mwili Mtume (s.a.w) amesema:



"Macho yanazini na uziniji wa macho ni mtazamo mbaya (kutizama kwa matamanio (evil look), mikono inazini na zinaa ya mikono ni kuvuruga amani (kufanya mabaya); miguu inazini na zinaa ya miguu ni kuendea maovu; uziniji wa ulimi ni maongezi mabaya au yasiyo maana; na uzinifu wa moyo (nafsi) ni matamanio mabaya. Hatimaye viungo vya sin vinathibitisha (kwa kuviunga mkono) au kuvikatalia.



Mtazamo muovu ni hatari zaidi katika kuwapelekea watu katika kitendo cha zinaa. Katika Qur'an tunaamrishwa tujiepushe na mtazamo muovu katika aya zifuatazo: Waambie Waislam wanaume wainamishe macho yao (was it izame yaliyokatazwa), na wazilinde tupu zao, hili nitakaso kwao, bila shaka Mwenyezi Mungu anazo habari za yote wanayofanya Na waambie Waislam wanawake wainamishe macho yao, na walinde tupu zao (24:30-31).



Utekelezaji wa amri hii umefafanuliwa katika Hadith mbali mbali za Mtume (s.a.w). Mtume (s.a.w) amesema: Mwana wa Adam! Mtazamo wako wa kwanza unasamehewa, lakini kuwa mwangalfu kuwa hutazami mara ya pili. (Al-Jassaas). Mtume (s.a.w) alimuusia Au (r.a):



Ewe Au, usirudie mtazamo wa pili baada ya ule wa kwanza. Mtazamo wa kwanza unasamehewa lakini sio ule wa pili. (AbuDaud).
Jabir (r. a) alimuuliza Mtume kuwa atafanya nini endapo macho yake yatamwangukia mwanamke bila kudhamiria? Mtume (s.a. w) alimuelekeza kuwa ageuze macho yake pale pale. (Abu- Daud).



Mwanamke kuonesha urembo wake na mapambo yake ni kitendo kiovu kinachoambatanishwa na mtazamo muovu. Hiki ni kishawishi kingine cha zinaa na wanawake wamekatazwa kufanya hivyo katika Qur'an: Wala wasidhihirishe viungo vyao isipokuwa vinavyodhihirika "(24:31). "Wala msionyeshe mapambo yenu kama walivyokua wakionyesha mapambo yao wanawake wa zama za ujahili (33:33).



Sauti ya mwanamke ni kishawishi kingine cha zinaa endpao ataongea kwa kuilegeza. Hivyo wanawake Wakiislamu wanaonywa wasifanye hivyo: "... Kama mnamuogopa Mwenyezi Mungu, basi msilegeze sauti (zenu) mnaposema na wanaume) iii asitamani mtu mwenye ugonjwa moyoni mwake (kufanya mabaya na nyinyi) na semeni maneno mazuri' (33:32).



Si sauti yake tu iliyokishawishi cha zinaa bali hata sauti ya mapambo ya mwanamke huwavutia wanaume na kuwapelekea kwenye fikra mbaya ya zinaa. Katika Qur'an wanawake wa Kiislamu wanakatazwa kudhihirisha sauti za mapambo yao:


Wala wasipige miguu yao (wasitingishe) iii yajulikane wanayoyaflcha katika mapambo yao (24:3 1). Manukato yenye harufu kali kwa wanawake pia ni kichocheo kingine cha zinaa. Mtume (s.a.w) kasema: Mwanamke anayetumia manukato na kupita mbele ya watu ni muovu. (At- Tirmidh). Uislamu umeweka tahadhari hizi na nyinginezo ambazo mtu binafsi, akizingatia inakuwa ni ngao madhubuti ya kuikinga jamii na uovu wa Zinaa.




                   


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 147

Post zifazofanana:-

DARASA LA VYAKULA, MBOGA, MATUNDA NA VIRUTUBISHO
Soma Zaidi...

Kitabu cha Afya 03
Yajuwe mambo yanayoathiri afya ya miili yetu, jifunze mambo mengi kuhusu afya. Soma Zaidi...

game
Karibu kwenye uwanja wa Game. Soma Zaidi...

ZIJUWE NYANJA KUU 6 ZA AFYA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

Hija ya kuaga kwa mtume, na hutuba ya mwisho aliyotowa mtume katika hija
Mwaka mmoja baada ya msafara wa Tabuuk Bara Arab zima ilikuwa chini ya Dola ya Kiislamu. Soma Zaidi...

Bongoclass ni nini, ipo wapi bongoclass na ni zipi kazi zake?
Bonoclass ni muunganiko wa maneno mawili, kutoka katika lugha mbili yaani lugha ya kiingereza na lugha ya kiswahili. Soma Zaidi...

Kiapo ya Mtume Ayub na utekelezwaji wake
Mkewe Ayyuub(a. Soma Zaidi...

FAIDA ZA VITAMINI C NA UMUHIMU WA VITAMINI C MWILINI
Utafahamu faida za vitamini C mwilini pamoja na kujuwa umuhimu wa vitamini C Soma Zaidi...

kuna uhusiano gani kati ya masundosundo naukimwi na je mtu anaweza asiwe nadalili zote hizo hulizo ziainisha akatokewa na masundosundo
Soma Zaidi...

HUKUMU ZA KUSOMA QURAN, HUKUMU ZA TAJWID, HUKUMU ZA NUN SAKINA, MIM SAKINA, QLQALA NA IQLAB, TANWIN NA MADA
Soma Zaidi...

Dawa ya kutibu mapunye
DAWA YA MAPUNYEMatibabu ya mapunye inategemea ni wapi mapunjye yapo. Soma Zaidi...

VYANZO VYA VYAKULA VYA VITAMINI NA FAIDA ZAKE
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...