Kujiepusha na Vishawishi vya Zinaa

Kujiepusha na Vishawishi vya Zinaa

Kujiepusha na Vishawishi vya ZinaaKatika macho ya sheria kitendo cha zinaa kinahesabiwa pale wanapokutana kimwili mwanamume na mwanamke nje ya ndoa.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Kujiepusha na Vishawishi vya Zinaa

Kujiepusha na Vishawishi vya Zinaa
Katika macho ya sheria kitendo cha zinaa kinahesabiwa pale wanapokutana kimwili mwanamume na mwanamke nje ya ndoa. Lakini katika maadili ya Kiislamu kitendo chochote kitakacho fanywa na mwanamume au mwanamke ambacho kitapelekea kuleta matamanio ya jimai nje ya ndoa, kinahesabiwa kuwa ni kitendo cha uzinifu wa ama yake. Kwa mfano mtu kumwangalia kwa matamanio mwanamke asiye kuwa mkewe, kufurahia tusi, uzuri wa sauti ya mwanamke asiyekuwa mkewe,kufurahia maongezi na mwanamke asiyekuwa mkewe au maharimu wake na kumtembelea mara kwa mara mwanamke asiyekuwa mkewe au maharimu wake atakuwa amefanya uzinifu kwa macho, masikio, ulimi na miguu yake.


Hapana sheria yoyote itakayomkamata kwa uzinifu, lakini muumini wa kweli atajihukumu mwenyewe na kujihesabu kuwa ni mkosaji mbele ya Allah (s.w). Hivyo atatubia kwa Mola wake na kujiepusha mbali na vishawishi hivi vya zinaa. Kuhusu zinaa ya viungo mbali mbali vya mwili Mtume (s.a.w) amesema:



"Macho yanazini na uziniji wa macho ni mtazamo mbaya (kutizama kwa matamanio (evil look), mikono inazini na zinaa ya mikono ni kuvuruga amani (kufanya mabaya); miguu inazini na zinaa ya miguu ni kuendea maovu; uziniji wa ulimi ni maongezi mabaya au yasiyo maana; na uzinifu wa moyo (nafsi) ni matamanio mabaya. Hatimaye viungo vya sin vinathibitisha (kwa kuviunga mkono) au kuvikatalia.



Mtazamo muovu ni hatari zaidi katika kuwapelekea watu katika kitendo cha zinaa. Katika Qur'an tunaamrishwa tujiepushe na mtazamo muovu katika aya zifuatazo: Waambie Waislam wanaume wainamishe macho yao (was it izame yaliyokatazwa), na wazilinde tupu zao, hili nitakaso kwao, bila shaka Mwenyezi Mungu anazo habari za yote wanayofanya Na waambie Waislam wanawake wainamishe macho yao, na walinde tupu zao (24:30-31).



Utekelezaji wa amri hii umefafanuliwa katika Hadith mbali mbali za Mtume (s.a.w). Mtume (s.a.w) amesema: Mwana wa Adam! Mtazamo wako wa kwanza unasamehewa, lakini kuwa mwangalfu kuwa hutazami mara ya pili. (Al-Jassaas). Mtume (s.a.w) alimuusia Au (r.a):



Ewe Au, usirudie mtazamo wa pili baada ya ule wa kwanza. Mtazamo wa kwanza unasamehewa lakini sio ule wa pili. (AbuDaud).
Jabir (r. a) alimuuliza Mtume kuwa atafanya nini endapo macho yake yatamwangukia mwanamke bila kudhamiria? Mtume (s.a. w) alimuelekeza kuwa ageuze macho yake pale pale. (Abu- Daud).



Mwanamke kuonesha urembo wake na mapambo yake ni kitendo kiovu kinachoambatanishwa na mtazamo muovu. Hiki ni kishawishi kingine cha zinaa na wanawake wamekatazwa kufanya hivyo katika Qur'an: Wala wasidhihirishe viungo vyao isipokuwa vinavyodhihirika "(24:31). "Wala msionyeshe mapambo yenu kama walivyokua wakionyesha mapambo yao wanawake wa zama za ujahili (33:33).



Sauti ya mwanamke ni kishawishi kingine cha zinaa endpao ataongea kwa kuilegeza. Hivyo wanawake Wakiislamu wanaonywa wasifanye hivyo: "... Kama mnamuogopa Mwenyezi Mungu, basi msilegeze sauti (zenu) mnaposema na wanaume) iii asitamani mtu mwenye ugonjwa moyoni mwake (kufanya mabaya na nyinyi) na semeni maneno mazuri' (33:32).



Si sauti yake tu iliyokishawishi cha zinaa bali hata sauti ya mapambo ya mwanamke huwavutia wanaume na kuwapelekea kwenye fikra mbaya ya zinaa. Katika Qur'an wanawake wa Kiislamu wanakatazwa kudhihirisha sauti za mapambo yao:


Wala wasipige miguu yao (wasitingishe) iii yajulikane wanayoyaflcha katika mapambo yao (24:3 1). Manukato yenye harufu kali kwa wanawake pia ni kichocheo kingine cha zinaa. Mtume (s.a.w) kasema: Mwanamke anayetumia manukato na kupita mbele ya watu ni muovu. (At- Tirmidh). Uislamu umeweka tahadhari hizi na nyinginezo ambazo mtu binafsi, akizingatia inakuwa ni ngao madhubuti ya kuikinga jamii na uovu wa Zinaa.




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Afya File: Download PDF Views 1120

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

dondoo 100 za Afya
dondoo 100 za Afya

Basi tambua haya;- 61.

Soma Zaidi...
Namna ya kufanya ngozi kuwa laini
Namna ya kufanya ngozi kuwa laini

Posti hii inahusu zaidi njia au namna ya kufanya ili ngozi iweze kuwa laini bila kuwa na make up yoyote.

Soma Zaidi...
AFYA NA MAGONJWA
AFYA NA MAGONJWA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
VIJUE VIDONDA VYA TUMBO, SABABU ZAKE NA DALILI ZAKE
VIJUE VIDONDA VYA TUMBO, SABABU ZAKE NA DALILI ZAKE

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Kitabu Cha  Afya na Lishe
Kitabu Cha Afya na Lishe

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
DONDOO 100 ZA AFYA
DONDOO 100 ZA AFYA

Pata dondoo 100 za Afya

Soma Zaidi...
UGONJWA WA MALARIA NA TAKWIMU ZA ATHARI YAKE KIDUNIA
UGONJWA WA MALARIA NA TAKWIMU ZA ATHARI YAKE KIDUNIA

Malaria ni katika maradhi ambayo husambazwa na na mbu jike aina ya anopheles.

Soma Zaidi...
darasa la lishe
darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
MAZINGIRA
MAZINGIRA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...