Haki za kielimu za mwanamke katika uislamu

Haki ya ElimuKatika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?

Haki za kielimu za mwanamke katika uislamu

Haki ya Elimu
Katika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?a Mola wako aliyeumba" (96: 1). Aya hii na nyingi nyinginezo zinazosisitiza elimu katika Uislamu hazikumbagua mwanamke. Pia Mtume (s.a.w) katika kusisitiza elimu amesema: "Kutafuta elimu ni faradhi kwa kila Muislam mwanamume na kila Muilsm mwanamke ".


Bali kutokana na tabia ya jamii nyingine ulimwenguni ya kuwanyanyasa wan awake na kuwaona kuwa ni nuksi, wasiostahiki kulelewa vizuri na kuelimishwa, Uislamu umetoa motisha mkubwa wa ahadi ya kupata malipo makubwa kutoka kwa Allah (s.w) kwa kuwalelea watoto wa kike vizuri na kuwaelimisha ipasavyo. Katika Hadith iliyosimuliwa na Imam Ahmed, Mtume (s.a.w) amesema:



Yeyote atakayewalea mabinti wawili hadi wakakua, yeye na mimi Siku ya Kiyama tutakuwa kama hivi. (Akaonesha vidole vyake viwili iii kupigia mfano watakavyokuwa karibu sana huko Peponi). (Ahmad)



Lengo Ia mafundisho haya ya Mtume (s.a.w) ni kuwaondosha watu katika zile fikra dhaifu za kuwaona watoto wa kike kama kwamba si watu. Na katika Hadith nyingine iliyosimuliwa pia na Ahmed, Mtume (s.a.w) amesema: Yeyote ambaye amemzaa binti, na hakumzika yungali hai, na hakumtukana au kumkashfu, na hakumpendelea mtoto wake wa kiume zaidi kuliko huyo wa kike, Allah atamuingiza Peponi. (Ahmad)



Zaidi ya mafundisho haya Mtume (s.a.w) alionesha mfano katika maisha yake mwenyewe, kwa kuwaheshimu na kuwatendea vizuri binti zake, kiasi ambacho aliwahi kusema juu ya binti yake, Fatma; "Fatma ni sehemu yangu mimi, furaha yake ni yangu, na ghadhabu zake ni uchungu wangu ".



Umuhimu wa kuwaelimisha watoto wa kike uko wazi. Tumeona kuwa katika jamii ya Kiislamu hapana budi kuwepo wanawake madaktari, wauguzi, walimu n.k. Ni dhahiri kuwa itabidi waelimishwe kwanza ndio waweze kupata ujuzi wa kufanya kazi hizo.



Wanawake wajifunze fani zipi za Elimu? Qur'an haijaweka mipaka yoyote inayowakataza wanawake fani fulani fulani za elimu. Kama kuna fani ya elimu ambayo ni haramu kwa wanawake basi fani hiyo itakuwa pia haramu kwa wanaume. Kwa mfano kujifundisha uchawi ni haramu kwa Waislamu wote (wanaume na wanawake),Qur'an (2: 102).
Ingawa kila mtu anayohaki ya kujipatia elimu, katika fani na kiwango chochote anachoweza, kipo kiwango fulani cha elimu ambacho ni lazima kila mtu awe nacho. Elimu ya lazima ni pamoja na kujua misingi ya Uislamu - Imani na Nguzo za Uislamu, namna ya kutekeleza Kwa ukamilifu Ibada maalum kama vile, kusimamisha swala, zakati, funga, hija, n.k., kujua wajibu katika familia na katika jamii, kujua katika maisha yetu ya kila siku lipi ni halali kulitenda na lipi ni haramu kwa mujibu wa Qur'an na Sunnah. Kwa ujumla elimu juu ya mambo haya ya msingi, tunaiita elimu ya mwongozo". Elimu hii ni faradh am kwa kila muislamu mwanamume na mwanamke.



Ingawa wanawake hawajazuiliwa kusomea fani yoyote ya elimu, bado tunaweza kusema kuwa zipo baadhi ya fani za elimu ambazo .ni vizuri sana wanawake wakizisomea kwani zitawafaa sana katika kutimiza jukumu Ia uzazi na malezi ya jamii, kama vile elimu ya tiba (medicine) uuguzi (nursing), ualimu, uendeshaji wa nyumba (home management), saikolojia, n.k. Fani nyingine za elimu zinabakia kuwa ni halali kwao kama zilivyo halali kwa wanaume.



Kutokana na mifano hii michache katika maeneo haya ya haki tuliyojaribu kuyabainsiha humu, Uislam kama ulivyo Dini ya haki, humpa kila mtu haki yake bila ya ubaguzi wa ama yoyote.




                   


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 152

Post zifazofanana:-

Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu
- Ni taasisi za kifedha zinazohusika na kuhifadhi akiba na mali za watu zenye thamani kubwa kama dhahabu, n. Soma Zaidi...

Wajbu wa wazazi kwa watoto wao
Wajibu wa Wazazi kwa Watoto Wazazi wanawajibu kwa watoto wao. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka sura kwenye quran na fadhila za sura mbalimbali kwenye quran
Soma Zaidi...

SABABU ZA KUTOKA KWA MIMBA (sababu za kuharibika kwa ujauzito)
Tafiti zinaonesha kuwa karibia asilimia 10% mpaka 25% ya wanawake wanaopata ujauzito, mimba zao hutoka. Soma Zaidi...

HUKUMU ZA MADD
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

TABIA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

JIFUNZE FIQH
Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka. Soma Zaidi...

Maumivu ya tumbo kitomvuni, sababu zake na dalili zake
Hapa utajifunza sababu za kuwepo na maumovu ya tumbe kitomvuni. Soma Zaidi...

Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?
Assalamu Alaykum Warahmatu-llah Wabarakaatuh Naomba kuuliza: Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini? Soma Zaidi...

HUDUMA YA KWANZA KWA MTU ANAYETOKWA NA DAMU YA PUA
Kama mtu anatokwa na damu za pua, basi juwa kuwa anahitaji huduma ya kwanza. Soma Zaidi...

Faida za kula Tangawizi
tangawizi ni katika viungio vya mboga vyenye faida, pia ni kinywaji, zijuwe leo faida za tangawizi Soma Zaidi...

DUA 94 - 114
DUA ZA KUONDOA WASIWASI, SIHIRI NA UCHAWI 94. Soma Zaidi...