picha

FAIDA ZA VITAMINI C NA UMUHIMU WA VITAMINI C MWILINI

Utafahamu faida za vitamini C mwilini pamoja na kujuwa umuhimu wa vitamini C

FAIDA ZA VITAMINI C NA UMUHIMU WA VITAMINI C MWILINI


FAIDA ZA VITAMINI C MWILINI


Kama tulivyokwisha kuona vyakula vya vitamini C kama vile papai, machungwa, mananasi, maembe, malimao na ndimu. Pia tuliona baadhi ya kazi za vitamini C ambazo ni kusaidia katika kuuwa kemikali mbaya mwilini, kuipa nguvu miili yetu ya kupambana na maradhi. Katika makala hii nitakwenda kukujuza umuhimu wa vitamin C katuka mwili wa kila kiumbe akiwemo binadamu.


Faida na umuhimu wa vitamini C
1.Hulinda mwili dhidi ya maradhi ya kiseyeye (scurvy): Haya ni maradhi ambayo hufanya mwili uweze kutoa damu kwenye mafinzi, mwili kuchubuka kwa urahisi, kuchelewa kupona kwa majeraha. Kusoma zaidi kuhusu ugonjwa huu pitia zaidi makala zetu.


2.Kulinda mwili zidi ya maambukizi na mashambulizi:
Tafiti mbalimbali zilizofanya zinaonesha kuwa vitamini C inaweza kusaidia kupunguza nguvu za virusi waletao mafua na homa ya mafua. Baadhi ya tafiti zinadiriki kusema kuwa vitamini hivi kuponyesha mafua yaa kwa haraka, lakini ambalo halina shaka ni kuwa vitamini c vinaweza kupunguza kupata mafua ya mara kwa mara au kufanya mafua yaondoke kwa haraka.


3.Vitamini C ni muhimu sana katika mfumo wa kinga mwilini. Kwani vitamini C husaidia katika Antimicrobial yaani katika kuzuia vijidudu shambulizi mwilini kama bakteria na virusi, pia vitamini C husaidia katika Natural killer cell yaani katika kuuwa vijidudu shambulizi ama kuvizuia visiendelee kukua mwilini, pia vitamini C husaidia katika kuimarisha mfumo wa kinga kwa kuimarisha seli hai nyeupe ziitwazo lymphocyte hizi ndizo seli ambazo askari mkuu wa mwili dhidi ya vimelea vya maradhi kama virisi, fangasi, protozoa na bakteria.


4.Kulinda miili yetu dhidi ya saratani (cancer):
Tafiti mbalimbali zimefanywa kuhusu aina ya saratani na zinavyohusiana na vitamini C kama saratani ya matiti na mapafu. Ijapokuwa tafiti hizi hazikuweza kuthibitisha moja kwa moja kuwa vitamini C vinasaidia kuondoa saratani hizi kalaki kuna mambo ambayo tafiti hizi yametufungua mawazo:
A. Vitamini C husaidia kuborsha afya na kuishi vyema kwa wagonjwa wa saratani
B. Vitamini C inaweza kuuwa seli zinazotengeneza uvimbe wa saratani


5.Husaidia kulind miili yetu dhidi ya maradhi yanayohusu mishipa ya damu na moyo (cardiovascular)


6.Husaidia kulinda miili yetu dhidi ya maradhi ya ubongo na kusahasahau




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 1476

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 web hosting    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mara moja

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mapema, kwa sababu ya kuwepo kwa saratani ya matiti, kuna dalili ambazo zikijitokeza zinapaswa kutolewa taarifa mara moja bila kuchelewa kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Madhara ya vyakula vya kisasa

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kuwepo kwa vyakula vya kisasa, vyakula vya kisasa ni vyakula vya madukani ambavyo vimetengenezwa na kuwekwa kwenye maduka

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo baada ya kula

Zijuwe sababu kuu za kuwepo kwa maumivu ya tumbo baada ya kula chakula

Soma Zaidi...
Vyakula vya kuoambana na mafua

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula vya kuoambana na mafua

Soma Zaidi...
Hasara za kitunguu swaumu wakati wa ujauzito

Posti hii inahusu zaidi hasara za kitunguu swaumu wakati wa ujauzito.

Soma Zaidi...
Zaituni (Olive)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula zaituni/ Olive

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za parachichi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula parachichi

Soma Zaidi...
Chakula cha minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula vya minyoo

Soma Zaidi...