Ugonjwa wa mfumo wa kinga ya mwili inavyoshambulia ini.
Ugonjwa huu hupelekea kuvimba kwenye ini yako ambayo hutokea wakati mfumo wa kinga ya mwili wako unaposhambulia ini lako.
DALILI
1. Uchovu
2. Usumbufu wa tumbo
3. Maumivu ya viungo
4. Ngozi ya manjano na weupe wa macho (jaundice)
5. Ini Kuongezeka
6. Mishipa ya damu isiyo ya kawaida kwenye ngozi.
7. Kichefuchefu na kutapika
8. Kupoteza hamu ya kula
9. Vipele vya ngozi
10. Mkojo wa rangi nyeusi
11. Kwa wanawake huweza, kupoteza hedhi
Matatizo ya uharibifu wa ini
1. Kuongezeka kwa shinikizo la damu . Damu kutoka kwa utumbo, wengu na kongosho huingia kwenye ini kupitia mshipa mkubwa wa damu unaoitwa portal vein. Ikiwa tishu zenye kovu huzuia mzunguko wa kawaida kwenye ini lako, damu hii hurudi nyuma, na hivyo kusababisha shinikizo la damu kuongezeka ndani ya mshipa wa mlango.
2. Majimaji kwenye tumbo lako (Ascites). Ugonjwa wa ini unaweza kusababisha kiasi kikubwa cha Majimaji kurundikana kwenye fumbatio lako.
3. Kushindwa kwa ini. Hii hutokea wakati uharibifu mkubwa wa seli za ini hufanya iwe vigumu kwa ini yako kufanya kazi ipasavyo. Katika hatua hii, kupandikiza ini ni chaguo pekee.
4. Saratani ya ini. Watu walio na Kinga ndogo kwenye ini wana hatari zaidi ya kansa ya Ini.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Sababu za mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu.
Post hii inahusu zaidi mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu na kwa kitaalamu huitwa retention of urine.
Soma Zaidi...Naomb niulize ukiingiliana na mwanmke mweny ukimwi unaweza kuambikizwa na kusaambaaa kwa mda gan ndan ya mwil
Muda gani ukimwi huweza kuonekana mwilini ama kugundulika kama umeathirika, ni dalili zipo hujitokeza punde tu utakapoathirika
Soma Zaidi...Maambukizi kwenye mrija wa mkojo(urethritis )
Posti hii inahusu zaidi maambukizi kwenye mrija wa mkojo, maambukizi haya usababishwa na virusi na bakteria.
Soma Zaidi...NINI SABABU YA VIDONDA VYA TUMBO
NENO LA AWALI Hapa utaweza kujifunza mambo mengi kuhusu vidonda vyatumbo.
Soma Zaidi...Nini chanzo cha malaria
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu chanzo cha ugonjwa wa malaria
Soma Zaidi...