Post hii inahusu zaidi dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa, ni dawa ambayo matumizi yake yanaweza kuingilia pote kwenye kutuliza kifafa na pia kwa wagonjwa wa akili.
1. Dawa hii ya diazepam kazi yake ni kutuliza mtu mwenye kifafa aweze kusinzia ila akili yake iweze kutulia na kufanya kazi vizuri, pia dawa hii ufanya Kazi Ile Ile kwa wagonjwa wa akili ambapo kama mtu amecharuka na kwa kukosa kutulia tunaweza kumpatia dawa hii Ili akaweza kulala na kutulia na baadae akiamka akili inakuwa sawa kabisa.
2. Dawa hii inaweza kutumiwa pia na watu wenye akili sawa ila kwa sababu ya matatizo ya maisha wanaweza kuwa na wasiwasi na kutotulia kwa hiyo watu was hivi tunawapatia dawa hii , na pia hali ya kutotulia utofautiana Kuna wale wenye wasiwasi mkubwa Wana dozi yao na wale wenye wasiwasi ila sio mkubwa na wenyewe wanapewa dozi yao lengo na kazi ya diazepam ni kumfanya mgonjwa atulie na baadae akiamka anaamka akiwa sawa na akili inakuwa imeshajitengeneza sawa.
3. Kwa wale wenye wasiwasi wa kawaida usio mkubwa wanapewa kuanzia dozi kuanzia milligrams mbili na pia dozi inawezekana kuongezewa kulingana na hali ya mgonjwa, dozi hii inaweza kuendelea mpaka milligrams kumi na tano mpaka ishilini na pia mgonjwa upata dawa ndani ya masaa manane na pamoja na dawa hii kuleta usingizi Ili kufanya ubongo kuwa sawa na Kuna dozi ya wale watu wenye usingizi unaopita kiasi wenyewe wanapewa dozi tofauti kuanzia milligrams tano na mwisho ni kumi na tano.
4. Dozi ya wasiwasi wa usio mkubwa utofautiana na dozi ya wasiwasi mkubwa.
Mgonjwa akiwa na wasiwasi mkubwa na kutotulia kwa kawaida huwa na maumivu kwa namna Moja au nyingine, kwa hiyo anaweza akapewa dawa hii kwa njia ya matako na pajani na pia dawa inawezekana kupitia kwenye mishipa ya damu na milligrams ubadilika kulingana na hali ya mgonjwa na badala ya masaa manane dozi yake huwa ndani ya masaa manane, kadri ya umri na uzito wa mgonjwa.
5. Pia na wale wenye kifafa dozi yao utofautiana na wale wenye wasiwasi pamoja na magonjwa ya akili kwa wenye kifafa dawa yao kwa mara nyingi upitia kwenye mishipa ya damu na kwa kawaida mgonjwa uanza kupewa dawa kuanzia milligrams kumi mpaka ishilini baada ya dakika telathini mpaka dakika sitini kwa kupitia kwenye mishipa ya damu, milligrams kwa kawaida zinaweza kuanzia mia mbili mpaka mia tatu kwa kulingana na uzito na umri wa mgonjwa.
6. Pia dawa hii kwa wagonjwa wa kifafa na degedege kwa watoto inawezekana kutolewa kwa njia ya mishipa ya damu ila inawezekana kupitia kwenye paja na kweye matako pia ila njia inayopendekezwa ni kwa njia ya mishipa ya damu kwa hiyo kama mgonjwa anapata shida kwenye mishipa ya damu njia ya matako au kwenye paja inawezekana kutumika kwa kadri ya maelekezo maalumu.
7. Dawa hii inawezekana kutumiwa na watu mbalimbali ila Kuna watu wanaopaswa kuitumia kwa taahadhari watu Hawa ni wale wenye matatizo katika upumuaji,walevi wa pombe, na pia epuka kutumia dawa hii mara kwa mara, pia wale wenye matatizo ya Figo na magonjwa ya ini wanapaswa kuitumia kwa taahadhari pia au kama Kuna dawa nyingine wasitumie kabisa.
8. Pia dawa hii Kuna wale ambao hawapaswi kuitumia kabisa,wale wenye aleji na dawa hii,wanaopumua vibaya au wenye athma kwa mda huo , wale walio na magonjwa sugu ya Figo,au ugonjwa wa ini umwkuwa kwenye hali ya usugu hawapaswi kuitumia kabisa.
9. Dawa hii pia Ina maudhi madogo madogo kama vile uchovu na kukosa nguvu,kusikia kama vile umevurugwa kwenye akili,hasa kwa wenye umri mkubwa, maumivu kwenye misuli, maumivu ya kichwa, maumivu kwenye tumbo, mkojo kushindwa kutoka kwa wakati hasa kupata mkojo kwa mda mrefu ukomu akunywa na kula Kawaida, magonjwa ya damu kama vile upungufu wa damu, kuwepo kwa njano,pia na matatizo kwenye ngozi kama vile upele na ngozi kuwasha,
10. Baada ya kuona Dalili kama hizi na mgonjwa anatumia dawa ya diazepam ni vizuri kufahamh kwamba hii ni kazi ya dawa,ila maudhi haya yakizidi ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya kwa sababu Maudhi mengine ni hatari kwa afya hasa kupungukiwa damu na mengine,kwa hiyo dawa hii ni vizuri kabisa kutolewa hospital sio nyumbani.
11. Kwa hiyo dawa hii inapaswa kutolewa kulingana na wataalamu wa afya na pia ni vizuri kabisa kutolewa hospital kwa sababu ya maudhi madogo madogo na kwa sababu ya matokeo yake sio Vizuri kabisa dawa hii kutolewa kienyeji kienyeji na wagonjwa wa akili pamoja na degedege,kwa sababu Kuna watu ambao hawapaswi kutumia dawa hii unaweza kuwapatia kumbe hawapaswi kuitumia kabisa dawa hii na ukakuta unaleta madhara badala ya kutibu.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 1573
Sponsored links
👉1
Kitau cha Fiqh
👉2
Kitabu cha Afya
👉3
kitabu cha Simulizi
👉4
Simulizi za Hadithi Audio
👉5
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉6
Madrasa kiganjani
Dawa ya UTI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya UTI Soma Zaidi...
Dawa ya fangasi uumeni
kama unasumbuliwa na fangasi uumeni, nitakujuza dawa yake, sababu za fangasi uumeni, matibabu yake na njia za kuwaepuka Soma Zaidi...
Dawa ya penicillin ambayo uzuia asidi ya bakteria.
Post hii inahusu zaidi dawa ya phenoxy-methyl penicillin ambayo upambana na aina ya bakteria ambao utoa sumu Ili kuzuia dawa isifanye kazi. Soma Zaidi...
Fahamu dawa zinazotumika kwenye matibabu ya kansa
Post hii inahusu zaidi dawa ambazo zinatumika kwenye matibabu ya kansa, dawa hizi usaidia kuharibu seli ambazo ambazo hazistahili kwa kitaalamu huitwa malignant seli. Soma Zaidi...
Fahamu zaidi kuhusiana na Dawa inayotibu shinikizo la damu. iitwayo LASIX
Lasix (Furosemide) iko katika kundi la dawa zinazoitwa vidonge vya maji (loop diuretics) vidonge vya maji. Lasix hutumiwa kupunguza uvimbe mwilini unaosababishwa na kushindwa kwa moyo, ugonjwa wa ini, au ugonjwa wa figo. Kwa matibabu ya dalili nyingi.La Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya kutibu kikohozi inayoitwa expectorant
Post hii inahusu zaidi dawa aina ya expectorant katika matibabu ya kikohozi,ni dawa ambayo usaidia au uzuia kikohozi kuendelea kutokea. Soma Zaidi...
Dawa ya chango na maumivu ya hedhi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya chango na dawa ya maumivu ya hedhi Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa za kutibu minyoo
Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto. Soma Zaidi...
Fahamu dawa zinazopunguza maumivu
Post hii inahusu zaidi dawa zinazofanya kazi ya kupunguza maumivu kwa kawaida dawa hizi ufanya kazi kwa kupitia kwenye mfumo wa fahamu. Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya fluconazole.
Post hii inahusu zaidi dawa ya fluconazole ni dawa ya kutibu fangasi za aina au za sehemu mbalimbali, Soma Zaidi...