Fahamu dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa


image


Post hii inahusu zaidi dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa, ni dawa ambayo matumizi yake yanaweza kuingilia pote kwenye kutuliza kifafa na pia kwa wagonjwa wa akili.


Fahamu dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa.

1. Dawa hii ya diazepam kazi yake ni kutuliza mtu mwenye kifafa aweze kusinzia ila akili yake iweze kutulia na kufanya kazi vizuri, pia dawa hii ufanya Kazi Ile Ile kwa wagonjwa wa akili ambapo kama mtu amecharuka na kwa kukosa kutulia tunaweza kumpatia dawa hii Ili akaweza kulala na kutulia na baadae akiamka akili inakuwa sawa kabisa.

 

2. Dawa hii inaweza kutumiwa pia na watu wenye akili sawa ila kwa sababu ya matatizo ya maisha wanaweza kuwa na wasiwasi na kutotulia kwa hiyo watu was hivi tunawapatia dawa hii , na pia hali ya kutotulia utofautiana Kuna wale wenye wasiwasi mkubwa Wana dozi yao na wale wenye wasiwasi ila sio mkubwa na wenyewe wanapewa dozi yao lengo na kazi ya diazepam ni kumfanya mgonjwa atulie na baadae akiamka anaamka akiwa sawa na akili inakuwa imeshajitengeneza sawa.

 

3. Kwa wale wenye wasiwasi wa kawaida usio mkubwa wanapewa kuanzia dozi kuanzia milligrams mbili na pia dozi inawezekana kuongezewa kulingana na hali ya mgonjwa, dozi hii inaweza kuendelea mpaka milligrams kumi na tano mpaka ishilini na pia mgonjwa upata dawa ndani ya masaa manane na pamoja na dawa hii kuleta usingizi Ili kufanya ubongo kuwa sawa na Kuna dozi ya wale watu wenye usingizi unaopita kiasi wenyewe wanapewa dozi tofauti kuanzia milligrams tano na mwisho ni kumi na tano.

 

4. Dozi ya wasiwasi wa usio mkubwa utofautiana na dozi ya wasiwasi mkubwa.

 Mgonjwa akiwa na wasiwasi mkubwa na kutotulia kwa kawaida huwa na maumivu kwa namna Moja au nyingine, kwa hiyo anaweza akapewa dawa hii kwa njia ya matako na pajani na pia dawa inawezekana kupitia kwenye mishipa ya damu na milligrams ubadilika kulingana na hali ya mgonjwa na badala ya masaa manane dozi yake huwa ndani ya masaa manane, kadri ya umri na uzito wa mgonjwa.

 

5. Pia na wale wenye kifafa dozi yao utofautiana na wale wenye wasiwasi pamoja na magonjwa ya akili kwa wenye kifafa dawa yao kwa mara nyingi upitia kwenye mishipa ya damu na kwa kawaida mgonjwa uanza kupewa dawa kuanzia milligrams kumi mpaka ishilini baada ya dakika telathini mpaka dakika sitini kwa kupitia kwenye mishipa ya damu, milligrams kwa kawaida zinaweza kuanzia mia mbili mpaka mia tatu kwa kulingana na uzito na umri wa mgonjwa.

 

6. Pia dawa hii kwa wagonjwa wa kifafa na degedege kwa watoto inawezekana kutolewa kwa njia ya mishipa ya damu ila inawezekana kupitia kwenye paja na kweye matako pia ila njia inayopendekezwa ni kwa njia ya mishipa ya damu kwa hiyo kama mgonjwa anapata shida kwenye mishipa ya damu njia ya matako au kwenye paja inawezekana kutumika kwa kadri ya maelekezo maalumu.

 

7. Dawa hii inawezekana kutumiwa na watu mbalimbali ila Kuna watu wanaopaswa kuitumia kwa taahadhari watu Hawa ni wale wenye matatizo katika upumuaji,walevi wa pombe, na pia epuka kutumia dawa hii mara kwa mara, pia wale wenye matatizo ya Figo na magonjwa ya ini wanapaswa kuitumia kwa taahadhari pia au kama Kuna dawa nyingine wasitumie kabisa.

 

8. Pia dawa hii Kuna wale ambao hawapaswi kuitumia kabisa,wale wenye aleji na dawa hii,wanaopumua vibaya au wenye athma kwa mda huo , wale walio na magonjwa sugu ya Figo,au ugonjwa wa ini umwkuwa kwenye hali ya usugu hawapaswi kuitumia kabisa.

 

9. Dawa hii pia Ina maudhi madogo madogo kama vile uchovu na kukosa nguvu,kusikia kama vile umevurugwa kwenye akili,hasa kwa wenye umri mkubwa, maumivu kwenye misuli, maumivu ya kichwa, maumivu kwenye tumbo, mkojo kushindwa kutoka kwa wakati hasa kupata mkojo kwa mda mrefu ukomu akunywa na kula Kawaida, magonjwa ya damu kama vile upungufu wa damu, kuwepo kwa njano,pia na matatizo kwenye ngozi kama vile upele na ngozi kuwasha,

 

10. Baada ya kuona Dalili kama hizi na mgonjwa anatumia dawa ya diazepam ni vizuri kufahamh kwamba hii ni kazi ya dawa,ila maudhi haya yakizidi ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya kwa sababu Maudhi mengine ni hatari kwa afya hasa kupungukiwa damu na mengine,kwa hiyo dawa hii ni vizuri kabisa kutolewa hospital sio nyumbani.

 

11. Kwa hiyo dawa hii inapaswa kutolewa kulingana na wataalamu wa afya na pia ni vizuri kabisa kutolewa hospital kwa sababu ya maudhi madogo madogo na kwa sababu ya matokeo yake sio Vizuri kabisa dawa hii kutolewa kienyeji kienyeji na wagonjwa wa akili pamoja na degedege,kwa sababu Kuna watu ambao hawapaswi kutumia dawa hii unaweza kuwapatia kumbe hawapaswi kuitumia kabisa dawa hii na ukakuta unaleta madhara badala ya kutibu.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Fahamu dawa ya haloperidol katika matibabu ya akili
Post hii inahusu dawa ya haloperidol katika matibabu ya magonjwa ya akili, ni mojawapo ya dawa ambayo utumiwa na wagonjwa ambao wamechananyikiwa. Soma Zaidi...

image Dawa ya kutibu ugonjwa wa PID
PID ni mashambulizi ya bakteria kwenye mfumo wa uzazi kwa wanawake. Hapa nitakujulisha dawa Soma Zaidi...

image Zijue kazi za chanjo ya DTP au DPT (Donda Koo,Pepopunda, na kifaduro))
Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya DTP au DPT ambayo Inazuia magonjwa ya Donda Koo, Pepopunda na kifaduro. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu dawa ya Nystatin
Post hii inahusu zaidi dawa ya Nystatin ni mojawapo ya dawa ambayo utumika kwenye ngozi. Soma Zaidi...

image Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo Aspirin.
Aspirini Ni dawa ya kutuliza maumivu.Majina yanayoaminika zaidi katika kutuliza maumivu sasa yanapatikana kwa njia mbadala inayookoa gharama kwa kutumia Aspirini. Aspirini inayopendwa na familia kwa miongo kadhaa, mara nyingi hutumiwa kupunguza maumivu ya kichwa, maumivu ya homa, na uvimbe wa mwili. Maumivu yanapotokea, fikia uaminifu wa familia ya madawa ya kulevya zaidi na Aspirin. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu dawa ya kaoline
Post hii inahusu dawa ya kaoline katika kutibu au kuzuia kuharisha ni dawa ambayo imependekezwa kutumiwa hasa kwa wale walioshindwa kutumia dawa ya loperamide. Soma Zaidi...

image Faida za dawa za NMN
Posti hii inahusu zaidi faida za dawa za NMN maana yake ni Nicotinamide mononucleotide ni dawa ambazo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali kama vile. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu dawa za kifua kikuu
Post hii inahusu dawa za kifua kikuu ni dawa ambazo utumika kutibu kifua kikuu, kwanza kabisa kabla ya kuanza kufahamu dawa hizo ni vizuri kabisa kufahamu kifua kikuu nini hili kuweza pia kufahamu dawa zake. Soma Zaidi...

image Fahamu dawa za kutuliza aleji au mzio
Post hii inahusu zaidi dawa hydrocortisone kwa kutuliza aleji au mzio, kwa kawaida Kuna mda mtu anapotumia dawa Fulani anakuwa na mabadiliko mbalimbali kama vile kifua kubana , viupele na mambo kama hayo. Soma Zaidi...

image Dawa ya quinenes katika kutibu Malaria
Post hii inahusu zaidi dawa e quinine katika kutibu Malaria ni dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria ikiwa dawa nyingine zimeshindwa kufanya kazi. Soma Zaidi...