Fahamu dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa

Fahamu dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa

Post hii inahusu zaidi dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa, ni dawa ambayo matumizi yake yanaweza kuingilia pote kwenye kutuliza kifafa na pia kwa wagonjwa wa akili.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Fahamu dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa.

1. Dawa hii ya diazepam kazi yake ni kutuliza mtu mwenye kifafa aweze kusinzia ila akili yake iweze kutulia na kufanya kazi vizuri, pia dawa hii ufanya Kazi Ile Ile kwa wagonjwa wa akili ambapo kama mtu amecharuka na kwa kukosa kutulia tunaweza kumpatia dawa hii Ili akaweza kulala na kutulia na baadae akiamka akili inakuwa sawa kabisa.

 

2. Dawa hii inaweza kutumiwa pia na watu wenye akili sawa ila kwa sababu ya matatizo ya maisha wanaweza kuwa na wasiwasi na kutotulia kwa hiyo watu was hivi tunawapatia dawa hii , na pia hali ya kutotulia utofautiana Kuna wale wenye wasiwasi mkubwa Wana dozi yao na wale wenye wasiwasi ila sio mkubwa na wenyewe wanapewa dozi yao lengo na kazi ya diazepam ni kumfanya mgonjwa atulie na baadae akiamka anaamka akiwa sawa na akili inakuwa imeshajitengeneza sawa.

 

3. Kwa wale wenye wasiwasi wa kawaida usio mkubwa wanapewa kuanzia dozi kuanzia milligrams mbili na pia dozi inawezekana kuongezewa kulingana na hali ya mgonjwa, dozi hii inaweza kuendelea mpaka milligrams kumi na tano mpaka ishilini na pia mgonjwa upata dawa ndani ya masaa manane na pamoja na dawa hii kuleta usingizi Ili kufanya ubongo kuwa sawa na Kuna dozi ya wale watu wenye usingizi unaopita kiasi wenyewe wanapewa dozi tofauti kuanzia milligrams tano na mwisho ni kumi na tano.

 

4. Dozi ya wasiwasi wa usio mkubwa utofautiana na dozi ya wasiwasi mkubwa.

 Mgonjwa akiwa na wasiwasi mkubwa na kutotulia kwa kawaida huwa na maumivu kwa namna Moja au nyingine, kwa hiyo anaweza akapewa dawa hii kwa njia ya matako na pajani na pia dawa inawezekana kupitia kwenye mishipa ya damu na milligrams ubadilika kulingana na hali ya mgonjwa na badala ya masaa manane dozi yake huwa ndani ya masaa manane, kadri ya umri na uzito wa mgonjwa.

 

5. Pia na wale wenye kifafa dozi yao utofautiana na wale wenye wasiwasi pamoja na magonjwa ya akili kwa wenye kifafa dawa yao kwa mara nyingi upitia kwenye mishipa ya damu na kwa kawaida mgonjwa uanza kupewa dawa kuanzia milligrams kumi mpaka ishilini baada ya dakika telathini mpaka dakika sitini kwa kupitia kwenye mishipa ya damu, milligrams kwa kawaida zinaweza kuanzia mia mbili mpaka mia tatu kwa kulingana na uzito na umri wa mgonjwa.

 

6. Pia dawa hii kwa wagonjwa wa kifafa na degedege kwa watoto inawezekana kutolewa kwa njia ya mishipa ya damu ila inawezekana kupitia kwenye paja na kweye matako pia ila njia inayopendekezwa ni kwa njia ya mishipa ya damu kwa hiyo kama mgonjwa anapata shida kwenye mishipa ya damu njia ya matako au kwenye paja inawezekana kutumika kwa kadri ya maelekezo maalumu.

 

7. Dawa hii inawezekana kutumiwa na watu mbalimbali ila Kuna watu wanaopaswa kuitumia kwa taahadhari watu Hawa ni wale wenye matatizo katika upumuaji,walevi wa pombe, na pia epuka kutumia dawa hii mara kwa mara, pia wale wenye matatizo ya Figo na magonjwa ya ini wanapaswa kuitumia kwa taahadhari pia au kama Kuna dawa nyingine wasitumie kabisa.

 

8. Pia dawa hii Kuna wale ambao hawapaswi kuitumia kabisa,wale wenye aleji na dawa hii,wanaopumua vibaya au wenye athma kwa mda huo , wale walio na magonjwa sugu ya Figo,au ugonjwa wa ini umwkuwa kwenye hali ya usugu hawapaswi kuitumia kabisa.

 

9. Dawa hii pia Ina maudhi madogo madogo kama vile uchovu na kukosa nguvu,kusikia kama vile umevurugwa kwenye akili,hasa kwa wenye umri mkubwa, maumivu kwenye misuli, maumivu ya kichwa, maumivu kwenye tumbo, mkojo kushindwa kutoka kwa wakati hasa kupata mkojo kwa mda mrefu ukomu akunywa na kula Kawaida, magonjwa ya damu kama vile upungufu wa damu, kuwepo kwa njano,pia na matatizo kwenye ngozi kama vile upele na ngozi kuwasha,

 

10. Baada ya kuona Dalili kama hizi na mgonjwa anatumia dawa ya diazepam ni vizuri kufahamh kwamba hii ni kazi ya dawa,ila maudhi haya yakizidi ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya kwa sababu Maudhi mengine ni hatari kwa afya hasa kupungukiwa damu na mengine,kwa hiyo dawa hii ni vizuri kabisa kutolewa hospital sio nyumbani.

 

11. Kwa hiyo dawa hii inapaswa kutolewa kulingana na wataalamu wa afya na pia ni vizuri kabisa kutolewa hospital kwa sababu ya maudhi madogo madogo na kwa sababu ya matokeo yake sio Vizuri kabisa dawa hii kutolewa kienyeji kienyeji na wagonjwa wa akili pamoja na degedege,kwa sababu Kuna watu ambao hawapaswi kutumia dawa hii unaweza kuwapatia kumbe hawapaswi kuitumia kabisa dawa hii na ukakuta unaleta madhara badala ya kutibu.

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 1788

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Neno la awali
Neno la awali

Asalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh Sifanjema zinamstahikia Allah Mola wa viumbe, muumba wa mbingu na ardhi na vilivyomo.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya fluconazole.
Fahamu kuhusu dawa ya fluconazole.

Post hii inahusu zaidi dawa ya fluconazole ni dawa ya kutibu fangasi za aina au za sehemu mbalimbali,

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kutuliza magonjwa ya akili inayoitwa Chlorpromazine
Fahamu dawa za kutuliza magonjwa ya akili inayoitwa Chlorpromazine

Post hii inahusu zaidi dawa zinazosaidis katika kutuliza magonjwa ya akili, dawa hii kwa kitaamu huiitwa chlorpromazine ni dawa ambayo utumiwa na watu wenye tatizo la magonjwa ya akili na kwa kiasi kikubwa huwa sawa.

Soma Zaidi...
Dawa na matibabu ya presha ya kushuka
Dawa na matibabu ya presha ya kushuka

Hapa utajifuanza dalili za presha ya kushuka, na dawa ya presha ya kushuka na nJia za kuzuiaama kudhibiti presha ya kushuka

Soma Zaidi...
IJUE DAWA YA AMOXLINE (antibiotic) NA MATUMIZI YAKE
IJUE DAWA YA AMOXLINE (antibiotic) NA MATUMIZI YAKE

Posti hii inahusu zaidi dawa ya amoxline .jinsi inavyofanya kazi mwilini.pamoja na matumizi yake.

Soma Zaidi...
Dawa ipi ya manjano kwa mtoto mwenye umri miaka miwili?
Dawa ipi ya manjano kwa mtoto mwenye umri miaka miwili?

Ugonjwa wa manjano ni moja kati ya maradhibyanayosumbuwa ini. Ugonjwa huu unahitaji uangalizi wa haraka hospitali. Posti hii itakwenda kukujuza ninivufanyebendapobmtoto wako ana ugonjwa wa manjano.

Soma Zaidi...
Njia ya kupitisha dawa kwenye mdomo na vipengele vyake
Njia ya kupitisha dawa kwenye mdomo na vipengele vyake

Posti hii inahusu zaidi njia ya kupitisha dawa kwenye mdomo na vipengele vyake, hii njia dawa umengenywa kwenye tumbo na kupitia kwenye utumbo mdogo na baadae kwenye damu,

Soma Zaidi...
Dawa ya fluconazole kama dawa ya fangasi
Dawa ya fluconazole kama dawa ya fangasi

Post hii inahusu zaidi dawa za fangasi na matumizi yake kwa kutumia dawa ya fluconazole kama dawa mojawapo ya fangasi.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya Acetohexamide
Fahamu kuhusu dawa ya Acetohexamide

Post hii inahusu zaidi dawa ya Acetohexamide kwa matibabu ya sukari, kama tulivyoona katika post iliyopita kwamba kuna kipindi ambacho kongosho linatoa insulini lakini seli haziko tayari kupokea hiyo insulini.

Soma Zaidi...
 Fahamu dawa ya maumivu aina ya indomethacin
Fahamu dawa ya maumivu aina ya indomethacin

Post hii inahusu zaidi dawa ya kutibu au kutuliza maumivu, kwa majina huiitwa indomethacin ni dawa inayotumika kutuliza maumivu ya Kawaida.

Soma Zaidi...