Dua Sehemu ya 01

Zijue fadhila za kuomba dua, tambua umuhimu na mahimizo juu ya kuomba dua?

Dua Sehemu ya 01

KITABU CHA DUA
Hiki ni kitabu cha dua na ni waqfu kwa ajili ya Allah. Hakiuzwi na na sio ruhusa kukiuza. Kwa anayetaka kukiprint ni bure awasiliane nasi pindi akitaka kufanya hivyo.

Tumeandika kitabu hiki kwa kutarajia radhi za Allah na kutoa mafundisho kwa waislamu na si vinginevyo.

DUA
Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani. Na dua ni ibada kama ibada nyingine.

Dua ni jambo lenye kupendeza kama walivyosema maulamaa na masalafi wema walotangulia. Umuhimu wa dua na msisitizo wake unapatikana katika quran na sunnah.

Dua zimesisitizwa sana katika quran na sunnah hata mtume akasema ' ' ' ' ' ' ' 'na aombe mmoja wenu haya yake (dua) kwa Allah mpaka chumvi.'. Hivyo si kuomba mambo kakubwa tu na matatizo tulonayo ila mpaka chumvi.

FADHILA ZA DUA

1.Dua ni ibada. Basi utambue ewe ndugu muislamu kuwa dua ni ibada. Imepokewa hadithi kutoka kwa Nuuman Ibn Bashir ' ' kuw Mtume wa Allah ' ' ' amesema "' ' ' ''hakika dua ni ibada' (imepokewa na Tirmidh na ameisahihisha).

2.Dua ndio jambo tukufu zaidi kwa Allah kama Mtume ' ' ' aliposema katika hadithi iliyosimuliwa na Abu Huraurah ' ' kuwa Mtume amesema 'hakuna kitu kitukufu mbele ya Allah kuliko dua' (imapokewa na tirmidh, imam Ahmad na Alhaakim kwa isnad sahihi) ' ' ' ' ' ' ' ' '

3.Allah anamchukia mtu ambaye hamuombi. Abuu Hurairah ' ' amesema kuwa Mtume ' ' ' amesema "' ' ' ' ' ' ' '" 'mtu yeyote ambaye hamuombi Allah, Allah humchukia mtu huyo' (amepokea hadithi tirmidh)

4.Allah anapenda kuombwa. Katika masimulizi ya Ibn Mas'ud ' ' Mtume ' ' ' ' amesema 'muombeni Allah katika fadhila zake, hakika Mwenyezimungu Mtukufu (' ') anapenda kuombwa' (amepokea Tirmidh).

5.Dua ni malango wa rehema. Katika masimulizi ya ibn 'Umar ' ' kuwa Mtume ' ' ' ' amesema "' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' '"' 'mwenye kufunguliwa mlango wa dua, hufunguliwa mlango wa rehema.' (amepokea Tirmidh).

6.Dua huondosha mabalaa na majanga. Katika masimulizi ya Ibn 'Umar, ' ' Mtume ' ' ' ' amesema 'hakika dua hunufaisha kwa (hukinga) yale yanayoshuka (yanayotokea), na yale ambayo hayajashuaka ( hayajatokea). Basi jilazimisheni na (kuomba) dua enyi waja wa Allah.

ADABU ZA KUOMBA DUA.

1.kuelekea qibla. Amesimulia Abdallah Ibn Zayd ' ' kuwa 'alitoka Mtume ' ' ' ' kwenda kuomba dua ya mvua akaelekea kibla'. (amepokea Bukhari).

2.Kunyanyua mikono miwili juu. Amesimulia Abuu Musa ' ' kuwa 'aliomba Mtume ' ' ' ' dua akanyanyua mikono yake mpaka nikaona weupe wa kwapa lake' (amepokea Bukhari). Na amesimulia Ibn 'Abas kuwa Mtume ' ' ' ' amesema ' "' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' 'muombeni Allah kwa matumbo ya viganya vyenu, wala msimuombe kwa migongo ya viganja vyenu.'. (amepokea Abuu Daud na Bayhaqiy).

3.Kuanza dua kwa kwa kumsifu Allah na kumshukuru (kama kusema alhamdu lillah '.) na kumswalia Mtume ' ' ' '. Amesimulia 'Abdullah Ibn Mas'ud ' ' kuwa nilikuwa nikiswali, wakati Mtume yupo na Abuubakar na 'Umar, basi nilipokaa nikaanza kumshukuru Allah na kumsifu na nikamswalia Mtume ' ' ' ' kisha nikajiombea dua, akasema mtume ' ' ' ' 'omba utapewa, omba utapewa'. (amepokea tirmidh kwa isnad sahih). Na katika masimulizi ya Fudailah Ibn 'Ubayd ' ' amesema 'hakika amefundisha mtume ' ' ' ' uma wake jinsi ya kuomba dua akasema 'pindi anapoomba dua mmoja wenu basi aanze na tahmid (kumshukuru Allah) na thanaai (kumsifu Allah) kisha amswalie Mtume ' ' ' ' kisha aombe chochote anachotaka' '"' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' '"' (amepokea Abuu Daud, tirmidh, Ibn Hiban na baihaqy).

4.Kuanza kuomba dua kwa kujiombea mwenyewe. Kwa anayetaka kumuombea mtu mwingine dua anatakiwa aanze na kujiombea mwenyewe. Amesimulia Ubaiya Ibn K'ab ' ' kuwa ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' 'alikuwa mtume ' ' ' ' anapomkumbuka mtu na akataka kumuombea dua huanza kwa kujiombea mwenyewe kwanza.' (amepokea tirmidh kwa isnad sahih).

5.Kurudia rudia katika kuomba na kusisitiza maombi yako. Ila usiharakishe majibu kutaka kujibiwa haraka hata ukawa unamlaumu Allah. Amesimulia Abdallah ibn Ms'ud ' ' kuwa alikuwa Mtume ' ' ' ' anapenda kuomba mara tatutatu na (akawa) anaomba istighfar (msamaha) mara tatutatu. (amepokea Abu Daud kwa isnad salih).

6.Kuwa na yaqini juu ya kujibiwa na kujiepusha na yaliyo haramu. Mtu anatakiwa asiwe na shaka juu ya kujibiwa dua yake. Amesimulia Abuu Hurairah ' ' kuwa Mtume ' ' ' ' amesema "' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' '"' 'muombeni Allah mkiwa na yakini juu ya kujibiwa na jueni kuwa Allah hakubali dua ya mtu ambaye moyo wake umeghafilika naye. (amepokea Tirmidh na Alhaakim).

7.Usiharakishe kujibiwa. Isitokee mtu akawa na haraka ya kutaka maombi yake yajibiwe kama anavyotaka yeye kwa haraka hata akawa analaumu. Amesemulia Abuuhurairah ' ' kuwa Mtume ' ' ' ' amesema "' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' '" 'atajibiwa (dua yake ) mmoja wenu maadam hajaharakisha (kujibiwa) akawa anasema nimeomba na wala sijajibiwa'. (amepokea Bukhari na Muslim). Na katika masimulizi mengine ya Abuuhrairah kuwa mtume amesema 'hataacha mja kujibiwa dua yake maadam hajaomba madhamdhi au kukata udugu'. (amepokea Muslim na Abuu Daud). Hii ina maana dua itajibiwa tu ila isiwe ya kuomba madhambi au kukata udugu.

8.Kuitikia 'aamiin'. Mwenye kuomba dua basi aitikie 'aamiin' eidha awe mwenyewe pekee au yupo na kundi la watu. Amesimulia Abuuhurairah ' ' kuwa Mtume ' ' ' ' 'atakapoomba dua mmoja wenu basi na aitikie 'aamiin' mwenyewe'. (amepokea Ibn 'Adiy).

MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA.
1.kuchunga adabu za dua kama zilivyotajwa hapo juu.

2.Kuwa twahara nje na ndani. Yaani kujiepusha na mambo maovu na machafu ya siri na yasiyo ya siri. Amesema Mtume ' ' ' ' 'hakika Allah ni mzuri na anapenda (vitu) vizuri.'. (amepekea Bukhari na Muslim) Hivyo mtu anatakiwa ahakikishe ni mzuri ndani na nje.

3.kujiweka mbali na yaliyo haramu yote, na kujiepusha kula na kunywa bya haramu au kuvaa vilivyo haramu. Amesema Mtume ' ' ' ' 'ukitaka dua maombi yako basi kifanye kizuri chakula chako (kisiwe cha haramu) ' (amepekea Bukhari na Muslim). Na pia katika hadithi ndefu iliyo sahihi katika kuwa mtume anashangaa mtu ambaye chakula chake haramu, kinywaji chake haramu, a mavazi yake haramu. Isitoshe mtu huyu amechafuka na manywele yapo timtim. Vipi atajibiwa dua yake mtu huyu. (amepekea Bukhari na Muslim).

4.Kuzingatia nyakati ambazo dua hujibiwa. Tutaziona hapo mbele.

5.Sifa ya dua yenyewe. Tutaona dua zenye sifa ya kujibiwa.

6.Hali inayozunguruka dua. Tutaona hali ambazo dua hujibiwa.


         › WhatsApp ‹ Whatsapp



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 210


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

haya ndiyo mambo yanayaribu swala na yanayobatilisha swala
Soma Zaidi...

Maudhui ya Qur-an na Mvuto wa Ujumbe Wake
Soma Zaidi...

Zingatio:
Swala husimama kwa kuhifadhiwa na kuswaliwa kwa khushui na kudumu na swala katika maisha yote. Soma Zaidi...

Ni kwa nini lengo la Funga na swaumu halifikiwi na wafungaji?
Kwa nini Lengo la Funga halifikiwi na Wafungaji Wengi? Soma Zaidi...

Nini maana ya Kushahadia nguzo ya kwanza ya uislamu
Soma Zaidi...

Hija ya Kuaga na Kutawafu kwa Mtume (s.a.w)
Hija ya Kuaga na Kutawafu kwa Mtume (s. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Bani Israil
Soma Zaidi...

Madai ya Makafiri dhidi ya kuwepo kwa Allah (s.w) na Udhaifu wa Madai hayo.
2. Soma Zaidi...

hizi ndio nguzo za swala, swala za faradhi na suna
Soma Zaidi...

Imam Ibn Majah na Sunan Ibn Majah
Soma Zaidi...

NAMNA ZA ZAKA (AINA NA MGAWANYIKO WA ZAKA) ZAKA IPO MAKUNDI MANGAPI?
Soma Zaidi...

Mafunzo ya swala
Jifunze namna ya kuswali, zijuwe aina za swala na ujifunze masharti ya swala, kwa nini swala hazijibiwi? nini kifanyike? Soma Zaidi...