Zijue fadhila za kuomba dua, tambua umuhimu na mahimizo juu ya kuomba dua?
KITABU CHA DUA
Hiki ni kitabu cha dua na ni waqfu kwa ajili ya Allah. Hakiuzwi na na sio ruhusa kukiuza. Kwa anayetaka kukiprint ni bure awasiliane nasi pindi akitaka kufanya hivyo.
Tumeandika kitabu hiki kwa kutarajia radhi za Allah na kutoa mafundisho kwa waislamu na si vinginevyo.
DUA
Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani. Na dua ni ibada kama ibada nyingine.
Dua ni jambo lenye kupendeza kama walivyosema maulamaa na masalafi wema walotangulia. Umuhimu wa dua na msisitizo wake unapatikana katika quran na sunnah.
Dua zimesisitizwa sana katika quran na sunnah hata mtume akasema ููููุณูุฃููู ุฃูุญูุฏูููู
ู ุฑูุจูููู ุญูุงุฌูุชููู ุญูุชููู ููุณูุฃููููู ุงููู
ูููุญู โna aombe mmoja wenu haya yake (dua) kwa Allah mpaka chumvi.โฆโ. Hivyo si kuomba mambo kakubwa tu na matatizo tulonayo ila mpaka chumvi.
FADHILA ZA DUA
1.Dua ni ibada. Basi utambue ewe ndugu muislamu kuwa dua ni ibada. Imepokewa hadithi kutoka kwa Nuuman Ibn Bashir ุฑุถูุงููู ุนูู kuw Mtume wa Allah ุตููุงููู ุนููู ูุณูู
amesema "โ ุงูุฏููุนูุงุกู ูููู ุงููุนูุจูุงุฏูุฉูโhakika dua ni ibadaโ (imepokewa na Tirmidh na ameisahihisha).
2.Dua ndio jambo tukufu zaidi kwa Allah kama Mtume ุตููุงููู ุนููู ูุณูู
aliposema katika hadithi iliyosimuliwa na Abu Huraurah ุฑุถูุงููู ุนูู kuwa Mtume amesema โhakuna kitu kitukufu mbele ya Allah kuliko duaโ (imapokewa na tirmidh, imam Ahmad na Alhaakim kwa isnad sahihi)
ููููุณู ุดูููุกู ุฃูููุฑูู
ู ุนูููู ุงูููููู ุชูุนูุงููู ู
ููู ุงูุฏููุนูุงุกู โ
3.Allah anamchukia mtu ambaye hamuombi. Abuu Hurairah ุฑุถูุงููู ุนูู amesema kuwa Mtume ุตููุงููู ุนููู ูุณูู
amesema "โ ู
ููู ููู
ู ููุณูุฃููู ุงูููููู ููุบูุถูุจู ุนููููููู โ"
โmtu yeyote ambaye hamuombi Allah, Allah humchukia mtu huyoโ (amepokea hadithi tirmidh)
4.Allah anapenda kuombwa. Katika masimulizi ya Ibn Masโud ุฑุถูุงููู ุนูู Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
amesema โmuombeni Allah katika fadhila zake, hakika Mwenyezimungu Mtukufu (ุบุฒู ูุฌูู) anapenda kuombwaโ (amepokea Tirmidh).
5.Dua ni malango wa rehema. Katika masimulizi ya ibn โUmar ุฑุถูุงููู ุนูู kuwa Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
amesema "โ ู
ููู ููุชูุญู ูููู ู
ูููููู
ู ุจูุงุจู ุงูุฏููุนูุงุกู ููุชูุญูุชู ูููู ุฃูุจูููุงุจู ุงูุฑููุญูู
ูุฉู ููู
ูุง ุณูุฆููู ุงูููููู ุดูููุฆูุง ููุนูููู ุฃูุญูุจูู ุฅููููููู ู
ููู ุฃููู ููุณูุฃููู ุงููุนูุงููููุฉู โ"โ โmwenye kufunguliwa mlango wa dua, hufunguliwa mlango wa rehema.โฆโ (amepokea Tirmidh).
6.Dua huondosha mabalaa na majanga. Katika masimulizi ya Ibn โUmar, ุฑุถูุงููู ุนูู Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
amesema โhakika dua hunufaisha kwa (hukinga) yale yanayoshuka (yanayotokea), na yale ambayo hayajashuaka ( hayajatokea). Basi jilazimisheni na (kuomba) dua enyi waja wa Allah.
ADABU ZA KUOMBA DUA.
1.kuelekea qibla. Amesimulia Abdallah Ibn Zayd ุฑุถูุงููู ุนูู kuwa โalitoka Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
kwenda kuomba dua ya mvua akaelekea kiblaโ. (amepokea Bukhari).
2.Kunyanyua mikono miwili juu. Amesimulia Abuu Musa ุฑุถูุงููู ุนูู kuwa โaliomba Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
dua akanyanyua mikono yake mpaka nikaona weupe wa kwapa lakeโ (amepokea Bukhari). Na amesimulia Ibn โAbas kuwa Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
amesema โ "โ ุฅูุฐูุง ุฏูุนูููุชู ุงูููููู ููุงุฏูุนู ุจูุจูุทูููู ููููููููู ูููุงู ุชูุฏูุนู ุจูุธููููุฑูููู
ูุง ููุฅูุฐูุง ููุฑูุบูุชู ููุงู
ูุณูุญู ุจูููู
ูุง ููุฌููููู โmuombeni Allah kwa matumbo ya viganya vyenu, wala msimuombe kwa migongo ya viganja vyenu.โฆโ. (amepokea Abuu Daud na Bayhaqiy).
3.Kuanza dua kwa kwa kumsifu Allah na kumshukuru (kama kusema alhamdu lillah โฆ.) na kumswalia Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
. Amesimulia โAbdullah Ibn Masโud ุฑุถูุงููู ุนูู kuwa nilikuwa nikiswali, wakati Mtume yupo na Abuubakar na โUmar, basi nilipokaa nikaanza kumshukuru Allah na kumsifu na nikamswalia Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
kisha nikajiombea dua, akasema mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
โomba utapewa, omba utapewaโโ. (amepokea tirmidh kwa isnad sahih). Na katika masimulizi ya Fudailah Ibn โUbayd ุฑุถูุงููู ุนูู amesema โhakika amefundisha mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
uma wake jinsi ya kuomba dua akasema โpindi anapoomba dua mmoja wenu basi aanze na tahmid (kumshukuru Allah) na thanaai (kumsifu Allah) kisha amswalie Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
kisha aombe chochote anachotakaโโ โ"โ ุฅูุฐูุง ุตููููู ุฃูุญูุฏูููู
ู ููููููุจูุฏูุฃู ุจูุชูุญูู
ููุฏู ุงูููููู ููุงูุซููููุงุกู ุนููููููู ุซูู
ูู ููููุตูููู ุนูููู ุงููููุจูููู ุตูู ุงููู ุนููู ูุณูู
ุซูู
ูู ููููุฏูุนู ุจูุนูุฏู ุจูู
ูุง ุดูุงุกู โ"โ (amepokea Abuu Daud, tirmidh, Ibn Hiban na baihaqy).
4.Kuanza kuomba dua kwa kujiombea mwenyewe. Kwa anayetaka kumuombea mtu mwingine dua anatakiwa aanze na kujiombea mwenyewe. Amesimulia Ubaiya Ibn Kโab ุฑุถูุงููู ุนูู kuwa ุนููู ุฃูุจูููู ุจููู ููุนูุจูุ ุฃูููู ุฑูุณูููู ุงูููููู ุตูู ุงููู ุนููู ูุณูู
ููุงูู ุฅูุฐูุง ุฐูููุฑู ุฃูุญูุฏูุง ููุฏูุนูุง ูููู ุจูุฏูุฃู ุจูููููุณููู โalikuwa mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
anapomkumbuka mtu na akataka kumuombea dua huanza kwa kujiombea mwenyewe kwanza.โ (amepokea tirmidh kwa isnad sahih).
5.Kurudia rudia katika kuomba na kusisitiza maombi yako. Ila usiharakishe majibu kutaka kujibiwa haraka hata ukawa unamlaumu Allah. Amesimulia Abdallah ibn Msโud ุฑุถูุงููู ุนูู kuwa alikuwa Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
anapenda kuomba mara tatutatu na (akawa) anaomba istighfar (msamaha) mara tatutatu. (amepokea Abu Daud kwa isnad salih).
6.Kuwa na yaqini juu ya kujibiwa na kujiepusha na yaliyo haramu. Mtu anatakiwa asiwe na shaka juu ya kujibiwa dua yake. Amesimulia Abuu Hurairah ุฑุถูุงููู ุนูู kuwa Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
amesema "โ ุงุฏูุนููุง ุงูููููู ููุฃูููุชูู
ู ู
ููููููููู ุจูุงูุฅูุฌูุงุจูุฉู ููุงุนูููู
ููุง ุฃูููู ุงูููููู ูุงู ููุณูุชูุฌููุจู ุฏูุนูุงุกู ู
ููู ููููุจู ุบูุงูููู ูุงููู โ"โ
โmuombeni Allah mkiwa na yakini juu ya kujibiwa na jueni kuwa Allah hakubali dua ya mtu ambaye moyo wake umeghafilika naye. (amepokea Tirmidh na Alhaakim).
7.Usiharakishe kujibiwa. Isitokee mtu akawa na haraka ya kutaka maombi yake yajibiwe kama anavyotaka yeye kwa haraka hata akawa analaumu. Amesemulia Abuuhurairah ุฑุถูุงููู ุนูู kuwa Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
amesema
"โ ููุณูุชูุฌูุงุจู ูุฃูุญูุฏูููู
ู ู
ูุง ููู
ู ููุนูุฌููู ููููููู ุฏูุนูููุชู ููููู
ู ููุณูุชูุฌูุจู ููู โ" โatajibiwa (dua yake ) mmoja wenu maadam hajaharakisha (kujibiwa) akawa anasema nimeomba na wala sijajibiwaโ. (amepokea Bukhari na Muslim). Na katika masimulizi mengine ya Abuuhrairah kuwa mtume amesema โhataacha mja kujibiwa dua yake maadam hajaomba madhamdhi au kukata uduguโ. (amepokea Muslim na Abuu Daud). Hii ina maana dua itajibiwa tu ila isiwe ya kuomba madhambi au kukata udugu.
8.Kuitikia โaamiinโ. Mwenye kuomba dua basi aitikie โaamiinโ eidha awe mwenyewe pekee au yupo na kundi la watu. Amesimulia Abuuhurairah ุฑุถูุงููู ุนูู kuwa Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
โatakapoomba dua mmoja wenu basi na aitikie โaamiinโ mwenyeweโโ. (amepokea Ibn โAdiy).
MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA.
1.kuchunga adabu za dua kama zilivyotajwa hapo juu.
2.Kuwa twahara nje na ndani. Yaani kujiepusha na mambo maovu na machafu ya siri na yasiyo ya siri. Amesema Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
โhakika Allah ni mzuri na anapenda (vitu) vizuri.โฆโ. (amepekea Bukhari na Muslim)
Hivyo mtu anatakiwa ahakikishe ni mzuri ndani na nje.
3.kujiweka mbali na yaliyo haramu yote, na kujiepusha kula na kunywa bya haramu au kuvaa vilivyo haramu. Amesema Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
โukitaka dua maombi yako basi kifanye kizuri chakula chako (kisiwe cha haramu) โ (amepekea Bukhari na Muslim). Na pia katika hadithi ndefu iliyo sahihi katika kuwa mtume anashangaa mtu ambaye chakula chake haramu, kinywaji chake haramu, a mavazi yake haramu. Isitoshe mtu huyu amechafuka na manywele yapo timtim. Vipi atajibiwa dua yake mtu huyu. (amepekea Bukhari na Muslim).
4.Kuzingatia nyakati ambazo dua hujibiwa. Tutaziona hapo mbele.
5.Sifa ya dua yenyewe. Tutaona dua zenye sifa ya kujibiwa.
6.Hali inayozunguruka dua. Tutaona hali ambazo dua hujibiwa.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!
Umeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inakwenda kukupa orodha ya dua 10 ambazo unaweza kuziomba kila siku.
Soma Zaidi...Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Posti hii inakwenda kukufundisha dua za kuomba wakati wa kuwa na maumivu kwenye mwili wako.
Soma Zaidi...Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...