picha

Namna ya kuswali swala ya maiti: nguzo zake, sunnah zake na maandalizi juu ya maiti

3.

Namna ya kuswali swala ya maiti: nguzo zake, sunnah zake na maandalizi juu ya maiti

Namna ya kuiswali sala ya maiti

3. Kumswalia Maiti.

Masharti ya Swala ya Maiti.
- Kwa wenye kumswalia maiti, watekeleze masharti ya kawaida ya swala.
- Masharti ya maiti anayeswaliwa:
1. Maiti awe muislamu
2. Maiti iwe imeoshwa na kukafiniwa
3. Maiti iwekwe mbele ya wanaoisalia.


- Inajuzu kusalia maiti iliyo masafa ya mbali (swala ya ghaibu).
- Maiti zikiwa nyingi zipangwe mbele, za kiume zikiwa karibu na imamu kisha kusaliwa zote kwa pamoja.
oMaiti isiwe ya shihidi.
- Kwa mujibu ya Hadith ya Mtume (s.a.w), mashahidi hawaoshwi wala kusaliwa.



Nguzo za Swala ya maiti.
- Swala ya maiti inaswaliwa wima; haina rukuu, sijda wala kikao.
- Nguzo za swala ya maiti ni;
i.Nia
ii.Takbira ya kuhirimia
iii.Kusoma Suratul-Faatiha.
iv.Takbira ya Pili.
v.Kumswalia Mtume (s.a.w) kama tufanyavyo kwenye Tahiyyatu.
vi.Takbira ya Tatu.
vii.Kumuombea dua maiti.
viii.Takbira ya Nne.
ix.Kuombea dua waislamu wote, kisha kutoa Salaam.



Namna ya kutekeleza swala ya Maiti hatua kwa hatua.
Utaratibu wa kusimamisha swala ya maiti ni kama ifuatavyo;
a)Maiti iwekwe mbele.
b)Imamu asimame katikati ya mwili wa maiti ikiwa maiti ni ya kike, na usawa wa mabega kama maiti ni ya kiume.
c)Maamuma watasimama kwenye mistari (safu) kwa idadi ya witiri; 1, 3, 5, n.k.
d)Baada ya hapo swala itaanza na kuendelea kama ifuatavyo:
i.Nia - ambayo ni kukusudia moyoni.
ii.Kuleta takbira ya kwanza; kwa kusema, “Allaah Akbar”
iii.Imamu na maamuma watasoma suratul-Faatiha – kimya kimya.
iv.Imamu ataleta Takbira ya Pili kisha maamuma – kimya kimya kwa maamuma na si lazima kuinua mikono wao.
v.Kumswalia Mtume (s.a.w) kama ilivyo katika Tahiyyatu, wote – kimya kimya.
vi.Imamu ataleta takbira ya Tatu kisha maamuma- kama walivyofanya awali.
vii.Wote kumuombea maiti dua kimya kimya, ikiwemo:


“Allaahumma ghfir lihayyinaa wamaayyitinaa washaahidinaa waghaaibinaa waswaaghirinaa wakaabirinaa wadhakirnaa waunthaanaa. Allaahumma man ahyaytahuu minnaa faahyi ‘alal Islaam. Waman tawaffaytahuu minnaa tawaffahuu ‘alal Imaani. Allaahumma laa tahirimnaa ajirahuu walaa taftinaa ba’adahuu”


Tafsiri:
“Ewe Allah tusamehe sisi, na maiti wetu, na mashahidi, na wasiokuwepo miongoni wetu, vijana wadogo miongoni mwetu na wakubwa miongoni mwetu, wanamume wetu, na wanawake wetu. Ewe Allah, yeyote yule miongoni mwetu utakayemewezesha kuishi, mjaalie aishi katika Kiislamu na yeyote miongoni mwetu utakayemfisha, mfishe katika Imani (ya Kiislamu). Ewe Allah, usitukatishe ujira kutoka kwake na wala usitufitinishe baada yake.”



- Au kwa kifupi tuweza kumuombea maiti kama ifuatavyo;
“Allaahumma ghfir lahuu warhamhuu wa-afihii wa-afu-anhu”
Tafsiri:
“Ewe Allah, Mghufirilie na Umrehemu”.



viii.Imamu ataleta Takbira ya nne na maamuma kufuatihia kama awali.
ix.Wote watawaombea waislamu dua – (pia si lazima kuleta dua hii).
Rejea Qur’an (59:10).



x.Imamu kutoa salaam na maamuma kufuatishia bila kutoa sauti kama ilivyo kwenye swala ya kawaida kwa kusema;
“Assalaamu ‘alaykum Warahmatullaah (Wabarakaatuh)”
Tafsiri:
“Amani iwe juu yenu na Rehema za Allah na Baraka zake”.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 5989

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 ai web app    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Namna ya kuswali hatuwa kwa hatuwq

Post hii itakufundisha jinsi ya kuswali hatuwa kwa hatuwa.

Soma Zaidi...
Msimamo wa Uislamu juu ya Utumwa

- Watumwa walikuwa wakikamatwa na kutezwa nguvu bila kujali utu na ubinaadamu wao.

Soma Zaidi...
Wenye ruhusa za kutofunga ramadhan

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake.

Soma Zaidi...
Maana ya Twahara na umuhimu wake katika uislamu

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya Twahara Kwa mujibu wa mafundisho ya Uislamu

Soma Zaidi...
Sunnah za swaumu, sunnah ambazo zinaambatans ns kufungabmwezi wa Ramadhani

Yajuwe mambo ambayo yanapendeza kuyafanya wakati ukiwa umefunga Ramadhani.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa

Post hii itakufundisha taratibu za kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa.

Soma Zaidi...