Dalili zake mtoto mwenye Ugonjwa wa Maambukizi kwenye koo

Pisti hii inahusu zaidi dalili za mtoto mwenye Maambukizi ya ugonjwa wa Dondakoo, tunajua wazi kuwa ugonjwa huu uwashambulia hasa watoto wadogo ambao wako chini ya miaka mitano, kwa hiyo zifuatazo ni baadhi ya Dalili zinazoweza kujitokeza kwa watoto hawa.

Dalili za ugonjwa wa Dondakoo.

1. Kukoroma wakati wa kuingiza hewa.

Hii ni mojawapo ya Dalili ya kuwepo kwa ugonjwa wa Dondakoo kwa mtoto ambapo mtoto anapokuwa anaingiza hewa ndan huwa anakoroma  hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye koo, kwa hiyo walezi wa watoto wadogo wanapaswa kutambua Dalili hii mapema na kuchukua hatua, ingawa kukoroma kunaweza kufanana na mafua ya kawa ila kukoroma kwa maambukizi ya Dondakoo utokea pale hewa inapokuwa inaingia ndani .

 

2. Kiwango cha mapigo ya moyo kuongezeka.

Hii nayo ni mojawapo ya Dalili ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye koo yanayosababishwa na bakteria kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi hasa ya mda mrefu na sehemu mbalimbali za moyo ushambuliwa ambazo ufanya mapigo ya moyo kwenda mbio na wakati mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa homa pia usababisha mapigo ya moyo kuongezeka, kwa hiyo tunapaswa kutibu ugonjwa huu mapema ili kuepuka kuwepo kwa matatizo mengine.

 

3. Kuvimba kwa sehemu ya juu ya tezi.

Dalili hii ujitokeza kwa mtoto hasa hasa kama Ugonjwa umesbaa sana, matezi yanaanza kuvimba kwa sehemu ya juu, hali hii tunapaswa kuitafautisha na tonslis ambapo matezi ya chini ndo uvimba kwa hiyo tukiona tu matezi ya juu yamevimba na mtoto anashindwa kimeza vizuri moja kwa moja tunapaswa kutambua kuwa ni ugonjwa wa Dondakoo na kutafuta matibabu mara moja.

 

4. Vidonda kwenye koo na sauti kubwa nzito.

Kwa sababu ya Maambukizi kwenye koo, hali ya kooni ushambuliwa na kusababisha madonda ambayo uleta maumivu kwa mtoto kwa hiyo mtoto kushindwa kumeza na wakati mwingine kama ananyonya ushindwa kabisa kwa hiyo hali hii upelekea kuwepo kwa madonda ambayo usababisha sauti kubwa nzito, kama mtoto haongei utagundua pale anapolia ambapo sauti yake ibadilika kabisa, kwa hiyo walezi wanapaswa kugundua dalili hii mara moja na kupata matibabu.

 

5. Kupumua kwa shida na wakati mwingine kupumua haraka haraka.

Hii ni mojawapo ya Dalili ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye koo ambapo koo linakuwa limearibiwa na bakteria na Maambukizi yanakuwa yameenea kwenye kifua ambapo kusababisha matatizo kwenye upumuaji na pengine mtoto upumua kwa haraka haraka.kwa hiyo tunapaswa kutofautisha kupumua kwa mafua ya kawaida na kupumua kwa sababu ya Maambukizi ya Dondakoo.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Author Tarehe 2022/01/06/Thursday - 01:49:25 pm     Share On Facebook or WhatsApp Imesomwa mara 2565

Post zifazofanana:-

Ugonjwa wa macho
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa macho, ni ugonjwa ambao ushambulia zaidi sehemu za nje za macho ambazo kwa kawaida uitwa conjunctiva na cornea hizi sehemu zikipata maambukizi zisipotibiwa mapema uweza kusababisha upofu kwa mgonjwa. Soma Zaidi...

Dalili za saratani ya kibofu Cha nyongo
Saratani ya kibofu cha nyongo ni Saratani inayoanzia kwenye kibofu cha nyongo. Nyongo yako ni kiungo kidogo, chenye umbo la peari upande wa kulia wa tumbo lako, chini ya ini lako. Kibofu cha nyongo huhifadhi nyongo, Kioevu cha usagaji chakula kinachozalishwa na ini lako. Saratani ya kibofu cha nyongo si kawaida. Saratani ya nyongo inapogunduliwa katika hatua zake za awali, uwezekano wa kupona ni mzuri sana. Lakini saratani nyingi za kibofu cha nyongo hugunduliwa katika hatua ya mwisho, wakati ubashiri mara nyingi huwa mbaya sana. Soma Zaidi...

Utaratibu wa lishe kwa vijana
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa vijana Soma Zaidi...

Miungurumo haiishi tumboni nikishika upande wa kushoto wa tumbo kuna maumivu kwa mbali je mm nitumie dawa gan kuondoa tatizo hilo
Kukawa na gesi tumboni kunaweza kuwa ni dalili ya shida kwenye afya, hasa katika mfumo wa chakula. Hali itakuwa sio nzuri endapo utakosea hamu ya kula na kuhisivkushiba muda wowote. Soma Zaidi...

Fahamu Magonjwa yanayowapata watoto chini ya miaka mitano
Posti hii inaelezea kuhusiana na Magonjwa mbalimbali ambayo watoto chini ya miaka wanaweza kuyapata kiurahi. Soma Zaidi...

Zijue sehemu za mwili zinazochomwa chanjo.
Posti hii inahusu zaidi sehemu ambazo zinapaswa kudungwa chanjo, hizi ni sehemu zile zilizopendekezwa kwa ajili ya kuchoma chanjo kwa kadiri ya kazi ya chanjo. Soma Zaidi...

Njia za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha.
Posti inahusu zaidi njia maalum za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha,Ni njia za uzazi ambazo wanaonyesha wanatumia kwa sababu kuna njia nyingine zikitumiwa na wanaonyonyesha zinaweza kuleta matatizo kwa watoto au kusababisha maziwa kutokuwa na vitamini vinavyohitajika kwa sababu dawa hizo uingiliana na uzalishaji wa maziwa. Soma Zaidi...

Njia za kujikinga na kisukari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujikinga na kisukari Soma Zaidi...

Aina za mishipa inayosafilisha damu mwilni
Post hii inahusu zaidi mishipa inayosafilisha damu mwilni, ni Aina tatu za mishipa ambazo usafilisha damu kutoka sehemu Moja kwenda nyingine Soma Zaidi...

Mambo ya kuzingatia unapokuwa unatoa huduma ya kwanza
Huduma ya kwanza ni huduma inayotolewa kwa mtu yeyote aliyepata ajali au mgonjwa yeyote kabla hajapelekwa hospitalini Soma Zaidi...

Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepaliwa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepaliwa Soma Zaidi...

Magonjwa yanayowashambulia watoto wachanga
Watoto wachanga ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano, watoto hawa hushambulia na maginjwa mara kwa mara na kusababisha ukuaji wao kuwa dunk, Soma Zaidi...