picha

Dalili zake mtoto mwenye Ugonjwa wa Maambukizi kwenye koo

Pisti hii inahusu zaidi dalili za mtoto mwenye Maambukizi ya ugonjwa wa Dondakoo, tunajua wazi kuwa ugonjwa huu uwashambulia hasa watoto wadogo ambao wako chini ya miaka mitano, kwa hiyo zifuatazo ni baadhi ya Dalili zinazoweza kujitokeza kwa watoto hawa.

Dalili za ugonjwa wa Dondakoo.

1. Kukoroma wakati wa kuingiza hewa.

Hii ni mojawapo ya Dalili ya kuwepo kwa ugonjwa wa Dondakoo kwa mtoto ambapo mtoto anapokuwa anaingiza hewa ndan huwa anakoroma  hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye koo, kwa hiyo walezi wa watoto wadogo wanapaswa kutambua Dalili hii mapema na kuchukua hatua, ingawa kukoroma kunaweza kufanana na mafua ya kawa ila kukoroma kwa maambukizi ya Dondakoo utokea pale hewa inapokuwa inaingia ndani .

 

2. Kiwango cha mapigo ya moyo kuongezeka.

Hii nayo ni mojawapo ya Dalili ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye koo yanayosababishwa na bakteria kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi hasa ya mda mrefu na sehemu mbalimbali za moyo ushambuliwa ambazo ufanya mapigo ya moyo kwenda mbio na wakati mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa homa pia usababisha mapigo ya moyo kuongezeka, kwa hiyo tunapaswa kutibu ugonjwa huu mapema ili kuepuka kuwepo kwa matatizo mengine.

 

3. Kuvimba kwa sehemu ya juu ya tezi.

Dalili hii ujitokeza kwa mtoto hasa hasa kama Ugonjwa umesbaa sana, matezi yanaanza kuvimba kwa sehemu ya juu, hali hii tunapaswa kuitafautisha na tonslis ambapo matezi ya chini ndo uvimba kwa hiyo tukiona tu matezi ya juu yamevimba na mtoto anashindwa kimeza vizuri moja kwa moja tunapaswa kutambua kuwa ni ugonjwa wa Dondakoo na kutafuta matibabu mara moja.

 

4. Vidonda kwenye koo na sauti kubwa nzito.

Kwa sababu ya Maambukizi kwenye koo, hali ya kooni ushambuliwa na kusababisha madonda ambayo uleta maumivu kwa mtoto kwa hiyo mtoto kushindwa kumeza na wakati mwingine kama ananyonya ushindwa kabisa kwa hiyo hali hii upelekea kuwepo kwa madonda ambayo usababisha sauti kubwa nzito, kama mtoto haongei utagundua pale anapolia ambapo sauti yake ibadilika kabisa, kwa hiyo walezi wanapaswa kugundua dalili hii mara moja na kupata matibabu.

 

5. Kupumua kwa shida na wakati mwingine kupumua haraka haraka.

Hii ni mojawapo ya Dalili ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye koo ambapo koo linakuwa limearibiwa na bakteria na Maambukizi yanakuwa yameenea kwenye kifua ambapo kusababisha matatizo kwenye upumuaji na pengine mtoto upumua kwa haraka haraka.kwa hiyo tunapaswa kutofautisha kupumua kwa mafua ya kawaida na kupumua kwa sababu ya Maambukizi ya Dondakoo.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 4637

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 web hosting     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Ugonjwa wa saikolojia wa kujitenga na watu.

Ugonjwa wa kuharibika kwa mwili ni aina ya ugonjwa sugu wa Akili ambao huwezi kuacha kufikiria kuhusu kasoro katika mwonekano wako au ya kuwaziwa. Lakini kwako, mwonekano wako unaonekana kuwa wa aibu sana hivi kwamba hutaki kuonekana na mtu yeyote

Soma Zaidi...
Kuona damu kwenye mkojo

Kuona damu kwenye mkojo kunaweza kusababisha wasiwasi. Ingawa katika hali nyingi kuna sababu zisizofaa, Damu kwenye mkojo (hematuria) pia inaweza kuonyesha ugonjwa mbaya.

Soma Zaidi...
Yajue mashambulizi ya bacteria kwenye Ngozi (cellulitis)

Mashambulizi ya bacteria kwenye Ngozi hujitokeza sehemu yenye jeraha pia huonyesha wekundu wenye upele,Uvimbe na malengelenge.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa gonoria (gonorrhea)

UGONJWA WA GONORIA NA DALILI ZAKE (GONORRHEA)Gonoria (gonorrhea) ni katika maradhi yanayoambukizwa kwa njia ya ngono.

Soma Zaidi...
Dalili za U.T.I

'UTI (urinary tract infection) no ugonjwa wa maambukizi katika mfumo wa mkojo na maambukizi haya husababishwa na bacteria, fangasi,na virus. Pia unaweza athiri rethra, kibofu Cha mkojo na figo.lakini Mara nyingi UTI huathiri Hadi mfumo wa uzazi na w

Soma Zaidi...
Sababu za Uvimbe wa tishu za Matiti kwa wavulana au wanaume

posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe wa tishu za matiti kwa wavulana au wanaume, unaosababishwa na kutofautiana kwa homoni za estrojeni na testosterone. Pia unaweza kuathiri matiti moja au zote mbili, wakati mwingine bila usawa. Watoto wachanga,

Soma Zaidi...