Dalili zake mtoto mwenye Ugonjwa wa Maambukizi kwenye koo


image


Pisti hii inahusu zaidi dalili za mtoto mwenye Maambukizi ya ugonjwa wa Dondakoo, tunajua wazi kuwa ugonjwa huu uwashambulia hasa watoto wadogo ambao wako chini ya miaka mitano, kwa hiyo zifuatazo ni baadhi ya Dalili zinazoweza kujitokeza kwa watoto hawa.


Dalili za ugonjwa wa Dondakoo.

1. Kukoroma wakati wa kuingiza hewa.

Hii ni mojawapo ya Dalili ya kuwepo kwa ugonjwa wa Dondakoo kwa mtoto ambapo mtoto anapokuwa anaingiza hewa ndan huwa anakoroma  hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye koo, kwa hiyo walezi wa watoto wadogo wanapaswa kutambua Dalili hii mapema na kuchukua hatua, ingawa kukoroma kunaweza kufanana na mafua ya kawa ila kukoroma kwa maambukizi ya Dondakoo utokea pale hewa inapokuwa inaingia ndani .

 

2. Kiwango cha mapigo ya moyo kuongezeka.

Hii nayo ni mojawapo ya Dalili ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye koo yanayosababishwa na bakteria kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi hasa ya mda mrefu na sehemu mbalimbali za moyo ushambuliwa ambazo ufanya mapigo ya moyo kwenda mbio na wakati mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa homa pia usababisha mapigo ya moyo kuongezeka, kwa hiyo tunapaswa kutibu ugonjwa huu mapema ili kuepuka kuwepo kwa matatizo mengine.

 

3. Kuvimba kwa sehemu ya juu ya tezi.

Dalili hii ujitokeza kwa mtoto hasa hasa kama Ugonjwa umesbaa sana, matezi yanaanza kuvimba kwa sehemu ya juu, hali hii tunapaswa kuitafautisha na tonslis ambapo matezi ya chini ndo uvimba kwa hiyo tukiona tu matezi ya juu yamevimba na mtoto anashindwa kimeza vizuri moja kwa moja tunapaswa kutambua kuwa ni ugonjwa wa Dondakoo na kutafuta matibabu mara moja.

 

4. Vidonda kwenye koo na sauti kubwa nzito.

Kwa sababu ya Maambukizi kwenye koo, hali ya kooni ushambuliwa na kusababisha madonda ambayo uleta maumivu kwa mtoto kwa hiyo mtoto kushindwa kumeza na wakati mwingine kama ananyonya ushindwa kabisa kwa hiyo hali hii upelekea kuwepo kwa madonda ambayo usababisha sauti kubwa nzito, kama mtoto haongei utagundua pale anapolia ambapo sauti yake ibadilika kabisa, kwa hiyo walezi wanapaswa kugundua dalili hii mara moja na kupata matibabu.

 

5. Kupumua kwa shida na wakati mwingine kupumua haraka haraka.

Hii ni mojawapo ya Dalili ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye koo ambapo koo linakuwa limearibiwa na bakteria na Maambukizi yanakuwa yameenea kwenye kifua ambapo kusababisha matatizo kwenye upumuaji na pengine mtoto upumua kwa haraka haraka.kwa hiyo tunapaswa kutofautisha kupumua kwa mafua ya kawaida na kupumua kwa sababu ya Maambukizi ya Dondakoo.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Namna ya kuzuia Ugonjwa wa ini
Posti hii inaelezea namna na jinsi ya kujikinga au kuzuia Ugonjwa wa ini. Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa kisukari wakati wa ujauzito.
Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisukari wakati mama akiwa mjamzito.na yafuatayo ni Mambo hatari yanayotokea wakati Mama akiwa na ujauzito. Soma Zaidi...

image Dalili za UTI kwa wanaume
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UTI upande wa wanaume Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine. Soma Zaidi...

image Vyakula anavyopaswa kutumia mama mjamzito
Posti hii inahusu zaidi vyakula anavyopaswa kutumia mama mjamzito, mama mjamzito ni mama ambaye amebeba kiumbe ndani kwa hiyo anapaswa kutumia vyakula vyenye virutubisho mbalimbali vitakavyomsaidia mtoto kukua vizuri. Soma Zaidi...

image Namna ugonjwa wa herpes simplex unavyosambaa.
Posti hii inahusu zaidi namna ya ugonjwa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine. Soma Zaidi...

image Dalili za fangasi ukeni
Post hii inakwenda kukujulisha dalili za kuwa huwenda una fangasi sehemu zako za siri. Soma Zaidi...

image Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia Malaria kwa wajawazito na watoto wao wakiwa bado tumboni, tunajuwa wazi kuwa wajawazito wakipata Malaria inaweza kupelekea mimba kutoka kwa hiyo ili kuzuia tatizo hili zifuatazo ni njia zilizowekwa ili kuzuia Malaria kwa wajawazito. Soma Zaidi...

image Watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango
Post hii inahusu zaidi watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango, Ni watu ambao Wana matatizo mbalimbali endapo wakitumia wanaoweza kuleta madhara mbalimbali. Soma Zaidi...

image Fahamu Ugonjwa wa kipindupindu.
Kipindupindu ni ugonjwa wa bakteria ambao kawaida huenezwa kupitia maji machafu. Kipindupindu husababisha Kuhara na Upungufu wa maji mwilini. Soma Zaidi...