picha

Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

1. Dondakoo ni ugonjwa unaosababishwa na sumu ya bakteria ambaye kwa kitaalamu huitwa corynebacterium diphtheria, bakteria huyu ushambulia sehemu za pua, koo na wakati mwingine maumivu kwenye masikio hali hii upelekea mgonjwa kushindwa kupumua na wakati mwingine kushindwa kumeza, kwa sababu ugonjwa huu usababishwa na bakteria kuna dawa mbalimbali za antibiotics zinaweza kuponya ugonjwa huu, antibiotics hizo ni kama vile penicillin au erythromycin.

 

2. Ugonjwa huu ushambulia hasa watoto na unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwa njia zifuatazo kama vile  mtu akipiga chagua yale maji maji yakimgusa mtu mwingine hasa kinywani mtu huyo anaweza akapata, kwa hiyo wakati wa kupiga chafya tunapaswa kuwa makini au tunapopiga chafya tunapaswa kupigia kwenye vitambaa ili kuepuka kusambaza ugonjwa kutoka sehemu moja kwenda kwa mwingine, au kama mama au mlezi wa watoto wadogo wanapaswa kuwa makini sana wasije kuambukiza watoto.

 

3. Ugonjwa huu pia unaweza kusambaa kwa njia ya kutumia vitu vyenye bakteria kama vile kunywea maji kwenye kikombe au glass ya mtu mwenye Maambukizi, au kutumia kijiko bila kuosha kutoka kwa mtu mwenye Maambukizi kwa hiyo bakteria usambaa kutoka kwa mwenye Maambukizi kwenda kwa hasiye na Maambukizi, kwa hiyo kila mtu anapaswa kutumia vifaa vyake hasa hasa vile vinavyoongozwa moja kwa moja kinywani au ni vizuri kuosha vyombo kwa maji moto ili kuweza kuua wadudu wanaosambaza na Kuleta madhara.

 

4. Pia hawa wadudu wanaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwa kutumia vitu kwa pamoja kama vile taulo na nguo zenye jasho kutoka kwa mtu mwenye Maambukizi na vile vile watu wanaokula peni, penseli na vfutio ambavyo vimetumbukizwa kinywani na mtu mwenye maambukizi na ambaye hana Maambukizi naye akija kutumia na kuweka mdomoni anaweza kupata, kwa hiyo kila mtu anapaswa kutumia vifaa vyake hasa kwa watoto ambao wako chekechekea wanapaswa kuangaliwa kwa makini ili kuepuka kuongeza kwa Maambukizi.

 

5. Kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua kuwa ugonjwa huu upo kwenye jamii na usipotibiwa mapema unaweza kuleta madhara makubwa kwa hiyo tunapaswa kuwapeleka watoto  watoto wapewe chanjo mapema ili kuweza kuepuka madhara  mbalimbali ambayo yanaweza kutokea pia jamii inapaswa kujua Dalili zote za ugonjwa huu ili kuweza kuwahi mapema kwenda hospitalini na pia watu wajifunze kujua jinsi ugonjwa huu unavyoenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1637

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 ai web app     πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰5 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Ugonjwa wa UTI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa UTI

Soma Zaidi...
Minyoo Ni nini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana ya minyoo

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kupooza (Stroke): Dalili za mwanzo na kinga.

​Ugonjwa wa kupooza, unaojulikana kitabibu kama stroke au cerebrovascular accident (CVA), ni dharura kubwa ya kitabibu inayotokea wakati mtiririko wa damu kwenye sehemu ya ubongo unapoingiliwa au kukatika. Kila sekunde ni muhimu katika kuokoa tishu za ubongo na kupunguza ulemavu wa kudumu. Makala haya yanafafanua dalili za mwanzo, sababu za hatari, na mikakati madhubuti ya kuzuia ugonjwa huu kwa maisha yenye afya bora

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuepuka minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuiepuka minyoo

Soma Zaidi...
Dalili za kwanza za HIV na UKIMWI kuanzia wiki ya kwanza toka kuathirika

DALILI ZA HIV ZA MWANZO NA DALILI ZA UKIMWI ZA MWANZO Kama ilivyo magonjwa mengi hupitia hatua kadha kadha na kuonyesha dalili kadha katika hatua hizo.

Soma Zaidi...
Dawa za uzazi wa mpazi na athari zake kiafya.

awa za uzazi wa mpango ni nyenzo muhimu zinazosaidia wanandoa kupanga familia zao kulingana na mahitaji yao. Ingawa zina faida kubwa katika kuzuia ujauzito usiotarajiwa, dawa hizi hufanya kazi kwa kubadilisha uwiano wa homoni mwilini, jambo ambalo linaweza kuleta madhara au athari (side effects) kwa baadhi ya watumiaji. Makala hii inaangazia aina za dawa hizi na mambo ya kuzingatia kiafya.

Soma Zaidi...