picha

Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

1. Dondakoo ni ugonjwa unaosababishwa na sumu ya bakteria ambaye kwa kitaalamu huitwa corynebacterium diphtheria, bakteria huyu ushambulia sehemu za pua, koo na wakati mwingine maumivu kwenye masikio hali hii upelekea mgonjwa kushindwa kupumua na wakati mwingine kushindwa kumeza, kwa sababu ugonjwa huu usababishwa na bakteria kuna dawa mbalimbali za antibiotics zinaweza kuponya ugonjwa huu, antibiotics hizo ni kama vile penicillin au erythromycin.

 

2. Ugonjwa huu ushambulia hasa watoto na unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwa njia zifuatazo kama vile  mtu akipiga chagua yale maji maji yakimgusa mtu mwingine hasa kinywani mtu huyo anaweza akapata, kwa hiyo wakati wa kupiga chafya tunapaswa kuwa makini au tunapopiga chafya tunapaswa kupigia kwenye vitambaa ili kuepuka kusambaza ugonjwa kutoka sehemu moja kwenda kwa mwingine, au kama mama au mlezi wa watoto wadogo wanapaswa kuwa makini sana wasije kuambukiza watoto.

 

3. Ugonjwa huu pia unaweza kusambaa kwa njia ya kutumia vitu vyenye bakteria kama vile kunywea maji kwenye kikombe au glass ya mtu mwenye Maambukizi, au kutumia kijiko bila kuosha kutoka kwa mtu mwenye Maambukizi kwa hiyo bakteria usambaa kutoka kwa mwenye Maambukizi kwenda kwa hasiye na Maambukizi, kwa hiyo kila mtu anapaswa kutumia vifaa vyake hasa hasa vile vinavyoongozwa moja kwa moja kinywani au ni vizuri kuosha vyombo kwa maji moto ili kuweza kuua wadudu wanaosambaza na Kuleta madhara.

 

4. Pia hawa wadudu wanaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwa kutumia vitu kwa pamoja kama vile taulo na nguo zenye jasho kutoka kwa mtu mwenye Maambukizi na vile vile watu wanaokula peni, penseli na vfutio ambavyo vimetumbukizwa kinywani na mtu mwenye maambukizi na ambaye hana Maambukizi naye akija kutumia na kuweka mdomoni anaweza kupata, kwa hiyo kila mtu anapaswa kutumia vifaa vyake hasa kwa watoto ambao wako chekechekea wanapaswa kuangaliwa kwa makini ili kuepuka kuongeza kwa Maambukizi.

 

5. Kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua kuwa ugonjwa huu upo kwenye jamii na usipotibiwa mapema unaweza kuleta madhara makubwa kwa hiyo tunapaswa kuwapeleka watoto  watoto wapewe chanjo mapema ili kuweza kuepuka madhara  mbalimbali ambayo yanaweza kutokea pia jamii inapaswa kujua Dalili zote za ugonjwa huu ili kuweza kuwahi mapema kwenda hospitalini na pia watu wajifunze kujua jinsi ugonjwa huu unavyoenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1632

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya     ๐Ÿ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game     ๐Ÿ‘‰4 Dua za Mitume na Manabii     ๐Ÿ‘‰5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     ๐Ÿ‘‰6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Aina ya kisukari inayojulikana kama Diabety type 1

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisukari Aina ya kwanza ambapo kwa kitaalamu huitwa Diabetes type 1, ni hali ambayo utokea ambapo mwili ushindwa kutengeneza insulini ambayo uweka sukari kwenye hali ya usawa.

Soma Zaidi...
Kukosa usingizi (Insomnia): Sababu na njia za kutatua.

Kukosa usingizi, au insomnia, ni tatizo linalomfanya mtu ashindwe kupata usingizi wa kutosha au usingizi wenye ubora, licha ya kuwa na fursa ya kupumzika. Hali hii haileti uchovu tu, bali pia huathiri umakini kazini, hali ya hisia, na afya ya jumla ya mwili. Makala haya yanachunguza visababishi vikuu vya ukosefu wa usingizi na kutoa mbinu za kisayansi unazoweza kutumia ili kurejesha utaratibu wako wa kulala

Soma Zaidi...
Dalili za mimba kutunga nje ya kizazi (Ectopic Pregnancy).

Mimba kutunga nje ya kizazi (Ectopic Pregnancy) ni hali ya dharura ya kitabibu ambapo yai lililorutubishwa linajipandikiza nje ya mji wa mimba, mara nyingi katika mirija ya uzazi (Fallopian tubes). Hali hii ni hatari sana kwa maisha ya mama kwani kiumbe kinachokua hakiwezi kustahimili kukua nje ya mji wa mimba, na kinaweza kusababisha mrija kupasuka na kusababisha damu nyingi kuvuja ndani ya tumbo.

Soma Zaidi...
Jifunze zaidi mzunguko wa mfumo wa damu kwa binadamu

Posti hii inahusu zaidi mfumo wa mwili ambao huhusika na kusafirisha damu ,virutubisho na takamwili.mfumo huu unajumuisha damu,mishipa ya damu na moyo.moyo husukuma damu kupitia mishipa ya damu na kufika maeneo yote ya mwili.

Soma Zaidi...
Walio hatarini kupata gonorrhea (gonoria)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu watu walio hatarini kupata gonorrhea gonoria

Soma Zaidi...
Dalili za kwanza za ugonjwa wa kaswende na kisonono.

Kaswende (Syphilis) na Kisonono (Gonorrhea) ni magonjwa ya zinaa (STIs) yanayoambukizwa kupitia tendo la ndoa. Ingawa husababishwa na vimelea tofautiโ€”Kaswende (bakteria Treponema pallidum) na Kisonono (bakteria Neisseria gonorrhoeae)โ€”yote yanaweza kusababisha madhara makubwa mwilini ikiwa hayatatibiwa mapema. Makala hii inaangazia dalili zao za awali ambazo mtu yeyote anayeshiriki ngono anapaswa kuzifahamu.

Soma Zaidi...