Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.
Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.
1. Dondakoo ni ugonjwa unaosababishwa na sumu ya bakteria ambaye kwa kitaalamu huitwa corynebacterium diphtheria, bakteria huyu ushambulia sehemu za pua, koo na wakati mwingine maumivu kwenye masikio hali hii upelekea mgonjwa kushindwa kupumua na wakati mwingine kushindwa kumeza, kwa sababu ugonjwa huu usababishwa na bakteria kuna dawa mbalimbali za antibiotics zinaweza kuponya ugonjwa huu, antibiotics hizo ni kama vile penicillin au erythromycin.
2. Ugonjwa huu ushambulia hasa watoto na unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwa njia zifuatazo kama vile mtu akipiga chagua yale maji maji yakimgusa mtu mwingine hasa kinywani mtu huyo anaweza akapata, kwa hiyo wakati wa kupiga chafya tunapaswa kuwa makini au tunapopiga chafya tunapaswa kupigia kwenye vitambaa ili kuepuka kusambaza ugonjwa kutoka sehemu moja kwenda kwa mwingine, au kama mama au mlezi wa watoto wadogo wanapaswa kuwa makini sana wasije kuambukiza watoto.
3. Ugonjwa huu pia unaweza kusambaa kwa njia ya kutumia vitu vyenye bakteria kama vile kunywea maji kwenye kikombe au glass ya mtu mwenye Maambukizi, au kutumia kijiko bila kuosha kutoka kwa mtu mwenye Maambukizi kwa hiyo bakteria usambaa kutoka kwa mwenye Maambukizi kwenda kwa hasiye na Maambukizi, kwa hiyo kila mtu anapaswa kutumia vifaa vyake hasa hasa vile vinavyoongozwa moja kwa moja kinywani au ni vizuri kuosha vyombo kwa maji moto ili kuweza kuua wadudu wanaosambaza na Kuleta madhara.
4. Pia hawa wadudu wanaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwa kutumia vitu kwa pamoja kama vile taulo na nguo zenye jasho kutoka kwa mtu mwenye Maambukizi na vile vile watu wanaokula peni, penseli na vfutio ambavyo vimetumbukizwa kinywani na mtu mwenye maambukizi na ambaye hana Maambukizi naye akija kutumia na kuweka mdomoni anaweza kupata, kwa hiyo kila mtu anapaswa kutumia vifaa vyake hasa kwa watoto ambao wako chekechekea wanapaswa kuangaliwa kwa makini ili kuepuka kuongeza kwa Maambukizi.
5. Kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua kuwa ugonjwa huu upo kwenye jamii na usipotibiwa mapema unaweza kuleta madhara makubwa kwa hiyo tunapaswa kuwapeleka watoto watoto wapewe chanjo mapema ili kuweza kuepuka madhara mbalimbali ambayo yanaweza kutokea pia jamii inapaswa kujua Dalili zote za ugonjwa huu ili kuweza kuwahi mapema kwenda hospitalini na pia watu wajifunze kujua jinsi ugonjwa huu unavyoenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 web hosting 👉3 ai web app 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
je kukohoa kunaweza kuwa ni dalili ya minyoo?
Dalili za minyoo zipo nyingi kama kuumwa na tumbo, tumbo kujaa gesi, uchovu, kukosa hamu ya kula, kupata choo chenye uteute na kupunguwa uzito. je kukohoa kunaweza kuwa ni dalili ya minyoo?
Soma Zaidi...Namna ya kuzuia uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo,ni njia ambazo mtu anaweza kutumia Ili kuzuia uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.zifuatazo ni njia zinazoweza kutumika kama mtu amepata uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.
Soma Zaidi...Upungufu wa Vitamini D: Dalili na jinsi ya kuipata.
Vitamini D, inayojulikana kama "vitamini ya jua," ni kirutubisho muhimu ambacho mwili huhitaji ili kudumisha mifupa imara, kuimarisha mfumo wa kinga, na kusaidia kazi za kimsingi za seli. Pamoja na umuhimu wake, upungufu wa vitamini D ni janga la kimya kimya linaloikumba dunia nzima. Makala haya yanaangazia kwa kina dalili za upungufu huu, sababu zake, na njia bora za kuhakikisha unapata viwango sahihi vya kirutubisho hiki ili kudumisha afya bora.
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo chini ya kifua, upande wa kulia na chini ya kitomvu.
Afya ya tumbo ni ishara tosha ya umadhibuti wa afya ya mtu. Maradhi mengi wanayouguwa watu chanzo kile mti anachokula. Yapo maradhi sugu kama saratani ambayo husababishwa pia na vyakula. Post hii itakwenda kujibu swalo la muulizaji kuhusu maumivu ya tumbo
Soma Zaidi...Vimelea vya tumbo (Minyoo): Dalili za kuwepo mwilini na tiba.
Vimelea vya tumbo, maarufu kama minyoo, ni tatizo la kiafya linaloathiri watu wa rika zote, likichangia kwa kiasi kikubwa utapiamlo na upungufu wa damu. Makala haya yanatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu jinsi ya kutambua dalili za maambukizi, taratibu za utambuzi hospitalini, na mikakati madhubuti ya tiba na kinga ili kudumisha afya ya mfumo wa mmeng'enyo wa chakula.
Soma Zaidi...