Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.
Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.
1. Dondakoo ni ugonjwa unaosababishwa na sumu ya bakteria ambaye kwa kitaalamu huitwa corynebacterium diphtheria, bakteria huyu ushambulia sehemu za pua, koo na wakati mwingine maumivu kwenye masikio hali hii upelekea mgonjwa kushindwa kupumua na wakati mwingine kushindwa kumeza, kwa sababu ugonjwa huu usababishwa na bakteria kuna dawa mbalimbali za antibiotics zinaweza kuponya ugonjwa huu, antibiotics hizo ni kama vile penicillin au erythromycin.
2. Ugonjwa huu ushambulia hasa watoto na unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwa njia zifuatazo kama vile mtu akipiga chagua yale maji maji yakimgusa mtu mwingine hasa kinywani mtu huyo anaweza akapata, kwa hiyo wakati wa kupiga chafya tunapaswa kuwa makini au tunapopiga chafya tunapaswa kupigia kwenye vitambaa ili kuepuka kusambaza ugonjwa kutoka sehemu moja kwenda kwa mwingine, au kama mama au mlezi wa watoto wadogo wanapaswa kuwa makini sana wasije kuambukiza watoto.
3. Ugonjwa huu pia unaweza kusambaa kwa njia ya kutumia vitu vyenye bakteria kama vile kunywea maji kwenye kikombe au glass ya mtu mwenye Maambukizi, au kutumia kijiko bila kuosha kutoka kwa mtu mwenye Maambukizi kwa hiyo bakteria usambaa kutoka kwa mwenye Maambukizi kwenda kwa hasiye na Maambukizi, kwa hiyo kila mtu anapaswa kutumia vifaa vyake hasa hasa vile vinavyoongozwa moja kwa moja kinywani au ni vizuri kuosha vyombo kwa maji moto ili kuweza kuua wadudu wanaosambaza na Kuleta madhara.
4. Pia hawa wadudu wanaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwa kutumia vitu kwa pamoja kama vile taulo na nguo zenye jasho kutoka kwa mtu mwenye Maambukizi na vile vile watu wanaokula peni, penseli na vfutio ambavyo vimetumbukizwa kinywani na mtu mwenye maambukizi na ambaye hana Maambukizi naye akija kutumia na kuweka mdomoni anaweza kupata, kwa hiyo kila mtu anapaswa kutumia vifaa vyake hasa kwa watoto ambao wako chekechekea wanapaswa kuangaliwa kwa makini ili kuepuka kuongeza kwa Maambukizi.
5. Kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua kuwa ugonjwa huu upo kwenye jamii na usipotibiwa mapema unaweza kuleta madhara makubwa kwa hiyo tunapaswa kuwapeleka watoto watoto wapewe chanjo mapema ili kuweza kuepuka madhara mbalimbali ambayo yanaweza kutokea pia jamii inapaswa kujua Dalili zote za ugonjwa huu ili kuweza kuwahi mapema kwenda hospitalini na pia watu wajifunze kujua jinsi ugonjwa huu unavyoenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi juu ya ugonjwa wa kipindupindu.Ni dalili zinzojitokeza kwa magonjwa wa kipindupindu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Njia za kufanya Ili kupunguza maumivu ya tatizo la uti wa mgongo, ni njia unazopaswa kufanya pale unapokuwa na tatizo la uti wa Mgongo.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Saratani ya matiti ya Mwanaume ni Saratani nadra ambayo hutokea katika tishu za matiti za wanaume. Ingawa saratani ya matiti hufikiriwa zaidi kuwa ugonjwa wa wanawake, saratani ya matiti ya mwanaume hutokea. Saratani y
Soma Zaidi...posti hii inahusu dalili za Homa ya Manjano ni maambukizi ya virusi yanayoenezwa na aina fulani ya mbu. Maambukizi hayo ni ya kawaida zaidi na kuathiri wasafiri na wakazi wa maeneo hayo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za Maambukizi kwenye mifupa, ni dalili ambazo ukionyesha kwa mtu mwenye Maambukizi kwenye mifupa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ingawa sio watu wote wenye dalili kama hizi Wana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo Ila zikitokea mtu anapaswa
Soma Zaidi...Hawa ni fangasi ambao wanashambulia sana kwenye kucha za vidole vya mikonobna miguu.
Soma Zaidi...Hivi badovunasumbuliwa na fangasi kwenye mdomo ama ulimi. Ni dawa gani umeshatumia bila mafanikio?.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa Bawasiri. Bawasiri ni mishipa iliyovimba kwenye njia yako ya haja kubwa na sehemu ya chini ya puru. Bawasiri inaweza kutokana na kukaza mwendo wakati wa kwenda haja ndogo au kutokana na shinikizo la kuongeze
Soma Zaidi...