Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

1. Dondakoo ni ugonjwa unaosababishwa na sumu ya bakteria ambaye kwa kitaalamu huitwa corynebacterium diphtheria, bakteria huyu ushambulia sehemu za pua, koo na wakati mwingine maumivu kwenye masikio hali hii upelekea mgonjwa kushindwa kupumua na wakati mwingine kushindwa kumeza, kwa sababu ugonjwa huu usababishwa na bakteria kuna dawa mbalimbali za antibiotics zinaweza kuponya ugonjwa huu, antibiotics hizo ni kama vile penicillin au erythromycin.

 

2. Ugonjwa huu ushambulia hasa watoto na unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwa njia zifuatazo kama vile  mtu akipiga chagua yale maji maji yakimgusa mtu mwingine hasa kinywani mtu huyo anaweza akapata, kwa hiyo wakati wa kupiga chafya tunapaswa kuwa makini au tunapopiga chafya tunapaswa kupigia kwenye vitambaa ili kuepuka kusambaza ugonjwa kutoka sehemu moja kwenda kwa mwingine, au kama mama au mlezi wa watoto wadogo wanapaswa kuwa makini sana wasije kuambukiza watoto.

 

3. Ugonjwa huu pia unaweza kusambaa kwa njia ya kutumia vitu vyenye bakteria kama vile kunywea maji kwenye kikombe au glass ya mtu mwenye Maambukizi, au kutumia kijiko bila kuosha kutoka kwa mtu mwenye Maambukizi kwa hiyo bakteria usambaa kutoka kwa mwenye Maambukizi kwenda kwa hasiye na Maambukizi, kwa hiyo kila mtu anapaswa kutumia vifaa vyake hasa hasa vile vinavyoongozwa moja kwa moja kinywani au ni vizuri kuosha vyombo kwa maji moto ili kuweza kuua wadudu wanaosambaza na Kuleta madhara.

 

4. Pia hawa wadudu wanaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwa kutumia vitu kwa pamoja kama vile taulo na nguo zenye jasho kutoka kwa mtu mwenye Maambukizi na vile vile watu wanaokula peni, penseli na vfutio ambavyo vimetumbukizwa kinywani na mtu mwenye maambukizi na ambaye hana Maambukizi naye akija kutumia na kuweka mdomoni anaweza kupata, kwa hiyo kila mtu anapaswa kutumia vifaa vyake hasa kwa watoto ambao wako chekechekea wanapaswa kuangaliwa kwa makini ili kuepuka kuongeza kwa Maambukizi.

 

5. Kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua kuwa ugonjwa huu upo kwenye jamii na usipotibiwa mapema unaweza kuleta madhara makubwa kwa hiyo tunapaswa kuwapeleka watoto  watoto wapewe chanjo mapema ili kuweza kuepuka madhara  mbalimbali ambayo yanaweza kutokea pia jamii inapaswa kujua Dalili zote za ugonjwa huu ili kuweza kuwahi mapema kwenda hospitalini na pia watu wajifunze kujua jinsi ugonjwa huu unavyoenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1125

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Saratani (cancer)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maradhi ya cancer/saratani

Soma Zaidi...
Ni Nini husababisha kukosa choo? (Constipation)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na sababu zinazopelekea kukosa choo ,yaani kinyesi kuwa kigumu au kukosa kabisa choo.

Soma Zaidi...
Njia za kuangalia sehemu yenye maumivu

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia sehemu yenye maumivu, hili kugundua mahali mtu anaumia ushirikiano mkubwa unahitajika kati ya mgonjwa na mhudumu.

Soma Zaidi...
Dalili za mnungu'nguniko wa moyo

Manung'uniko ya moyo ni sauti wakati wa mzunguko wa mapigo ya moyo wako kama vile kutetemeka inayotolewa na damu yenye msukosuko ndani au karibu na moyo wako.

Soma Zaidi...
Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni.

Soma Zaidi...
ninaisi kma kunakitu kwenye koo alafu kuna ali ya weupe kwenye ulimi na Mashavu kwa ndan

Weupe kwenye ulimi unaweza kuwa ni hali ya kawaida. Weupe huu ukichanganyika na utandu huwenda ikaashiria uwepo wa hali fulani za kiafya.

Soma Zaidi...
Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Post hii inahusu zaidi Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, hali hii uwatokea sana wanawake zaidi ya wanaume, kwa kitaalamu hali hii ya kuwa na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo huitwa cystitis.

Soma Zaidi...
Fahamu matatizo ya ini kuwa na kovu

kovu (Fibrosis) ya ini inayosababishwa na aina nyingi za magonjwa na hali ya ini, kama vile Homa ya Ini na unywaji pombe kupita kiasi. Ini hufanya kazi kadhaa muhimu, ikiwa ni pamoja na kuondoa vitu vyenye madhara katika mwili wako, kusafisha damu yako

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa kaswende

Kaswende ni maambukizo ya bakteria ambayo kawaida huenezwa kwa kujamiiana. Ugonjwa huu huanza kama kidonda kisicho na maumivu kawaida kwenye sehemu zako za siri, puru au mdomo. Kaswende huenea kutoka kwa mtu hadi mtu kupitia ngozi. Kaswende ya Mapema

Soma Zaidi...
Dalili na madhara ya Kiungulia

post hii inaelezea kuhusiana na dalili au ishara na madhara ya Kiungulia ni maumivu ya moto kwenye kifua chako, nyuma ya mfupa wako wa kifua. Maumivu huwa mabaya zaidi wakati wa kulala au kuinama

Soma Zaidi...