Ni Nini husababisha kukosa choo? (Constipation)
Posti hii inazungumzia kuhusiana na sababu zinazopelekea kukosa choo ,yaani kinyesi kuwa kigumu au kukosa kabisa choo.
Zifuatazo Ni sababu zinazopelekea kukosa choo.
1.kutokunywa maji;maji yanasaidia kulainisha choo na mmeng'enyo wa chakula ili kinyesi kiweze kutoka sasa endapo hutokunjwa maji hupelekea kukosekana kupata choo.
2.kubana kinyesi; hii nayo Ni Hatari Sana kubana kinyesi endapo utasikia kuenda haja kubwa jitahidi kuenda chooni ili usisababishe kukosa choo.
3.kutokula mbogamboga na matunda ;matunda Kama papai, parachichi n.k na mboga za majani husaidia Sana usipate Ugumu wa choo.
4.kula vyakula vya wanga Sana Kama vile ugali wa sembe, unga wa ngano, husababisha mtu kupata choo kigumu Tena endapo utakula Kila siku na bila kunywa na maji.
5.nyama nyekundu; Kama vile mishikaki na supu kwa wale wanaotumia kwa Sana
6.vyakula vilivyosindikwa.
7.chips mayai na juisi hupelekea kukosa choo.
Dalili za kukosa choo Ni pamoja na;?
1.kukosa hamu ya kula
2.kupata maumivu ya kiuno
3.choo kuwa kigumu
4.mwili kuishiwa nguvu.
5.tumbo kuuma au kuvurugika.
Mwisho; kukosa choo kiafya Ni ugonjwa lakini Kuna watu wanaonaga Kama Kawaida hivyo basi ukiona dalili za kukosa choo Ni vyema kuwahi hospitali kupata matibabu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 ai web app 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
dalili za ukimwi kwa mwanaume
Katika post hii utakwenda kujifunza zaidi khusu dalili za ukimwi ama HIV kwa wanaume
Soma Zaidi...Vyakula Vinavyosaidia Afya ya Uzazi kwa Mwanamke
​Afya ya uzazi kwa mwanamke inategemea sana usawa wa homoni, ubora wa mayai, na mazingira salama ya mfuko wa uzazi. Lishe bora ni nguzo kuu katika kuboresha maeneo haya. Makala haya yanachambua vyakula muhimu vinavyoweza kuongeza uwezo wa kushika mimba, kusawazisha homoni, na kulinda mfumo wa uzazi kwa ujumla, yakisindikizwa na ukweli wa kisayansi
Soma Zaidi...Dalili na Sababu za homa ya manjano kwa watoto
Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili na Sababu za Homa ya manjano ya watoto wachanga ni kubadilika rangi kwa manjano katika ngozi na macho ya mtoto mchanga. Homa ya manjano ya mtoto hutokea kwa sababu damu ya mtoto ina ziada ya rangi ya
Soma Zaidi...Fahamu Magonjwa yanayowapata watoto chini ya miaka mitano
Posti hii inaelezea kuhusiana na Magonjwa mbalimbali ambayo watoto chini ya miaka wanaweza kuyapata kiurahi.
Soma Zaidi...