Madhara ya kutotibu uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo

Post hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu ugonjwa wa uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo,ni madhara yanayotokea kwenye mfumo mzima wa kupitisha mkojo na via vya uzazi kama ifuayavyo.

1. Maambukizi kwenye figo.

Kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo hali hii usababisha bakteria kusambaa kwenye sehemu mbalimbali za kibofu Cha mkojo na pengine maambukizi yanakuwa makubwa mno yanayopelekea kuaribika kwa figo na kumbuka figo ni kitu muhimu sana kwenye mwili kwa hiyo maambukizi yakiwa makubwa figo linakuwa kwenye hali ya hatari, kwa hiyo tunapaswa kutibu ugonjwa huu mapema Ili kuepuka kuepusha kuaribika kwa figo kwa sababu dawa hospitalin zipo na ugonjwa huu wa uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo unatibika kwa hiyo tutibu ugonjwa huu Ili kuepusha madhara mbalimbali.

 

2. Kuwepo na damu kwenye mkojo.

Kitendo Cha kuwepo kwa damu kwenye mkojo uonekana katika vipimo ,hii ni hali ya hatari kwa sababu maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo yanaonekana kuwa makubwa zaidi kwa sababu wadudu wameshakula sehemu mbalimbali na kusababisha mkojo kuwa na damu, kwa hiyo tunapaswa kuelimisha jamii kuhusu kuwepo kwa ugonjwa huu na kuwa unatibika mtu yeyote akiona dalili ya damu kwenye mkojo anapaswa kwenda hospitalini kupima Ili kuweza kupata matibabu kwa kuwa watu wengi wameugua ugonjwa huu na wamepona.

 

3. Uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo umfanya mgonjwa ajisikie vibaya kwenye jamii.

Hii utokea pale mgonjwa mwenye tatizo hili akiwa kwenye jamii anakojoa damu, mkojo una harufu mbaya, anahisi maumivu akiwa kwenye jamii ambayo haieleweki watu wanaweza kumcheka na mgonjwa anaweza kujisikia vibaya na kuendelea kuwa na wasiwasi na kuishi bila raha kwenye jamii.kwa hiyo tutibu ugonjwa huu na tuwaone wagonjwa wa hivi kama watu wengine na kuwasaidia kwenda hospitalini Ili wapate huduma kwa kuwa ni ugonjwa unaweza kumpata kila mtu yeyote hakuna mwenye nao.

 

4. Maambukizi kwenye via vya uzazi.

Ugonjwa huu ikiingia kwenye kibofu Cha mkojo na baadae maambukizi yanaweza kusambaa mpaka kwenye via vya uzazi na yakishambulia uko yanaweza kuleta madhara makubwa zaidi kwa hiyo Tiba ni lazima, maambukizi yakizidi yanaweza kuleta hata na Kansa iwapo mgonjwa hakutibiwa mapema.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Author Tarehe 2021/12/18/Saturday - 06:38:09 pm     Share On Facebook or WhatsApp Imesomwa mara 807

Post zifazofanana:-

Zijue sababu za kupoteza fahamu.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kupoteza fahamu, ni sababu ambazo umfanya mtu kupoteza fahamu kwa sababu mbalimbali kama ifuayavyo. Soma Zaidi...

Dawa ya Isoniazid na kazi zake
Posti hii inahusu zaidi dawa ya lsoniazid nA kazi zake, ni dawa ambayo inasaidia kutibu kifua kikuu kati ya madawa yaliyoteuliwa na kuwa na sifa ya kutibu kifua kikuu. Soma Zaidi...

Vitu vinavyochochea kuwepo kwa Ugonjwa wa ukimwi.
Posti hii inahusu zaidi vitu ambavyo vinasababisha kuongezeka kwa Ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na baada ya watu kujua Ugonjwa huu na matokeo ila bado ugonjwa unazidi kuongezeka. Soma Zaidi...

Madhara ya kutumia madawa ya kupunguza maumivu
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutumia madawa ya kupunguza maumivu,ni madhara ambayo utokea kwa mtu anayetumia madawa ya kupunguza maumivu. Soma Zaidi...

Dalili za macho makavu.
Posti hii inahusu zaidi njia za kutambua Dalili za macho makavu, kama tulivyotangulia kuona kubwa macho kuwa makavu Usababishwa na sehemu ya kuzalisha maji kwenye jicho kushindwa kufanya kazi na jicho hilo huwa kavu na Dalili zake ni kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Ugonjwa wa Uvimbe kwenye ubongo
Posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe au puto katika mshipa wa damu kwenye ubongo. Uvimbe kwenye'Ubongo'unaweza kuvuja au kupasuka, na kusababisha kuvuja damu kwenye ubongo. Mara nyingi, kupasuka kwa Uvimbe wa Ubongo'hutokea katika nafasi kati ya ubongo na tishu nyembamba zinazofunika ubongo. Aina hii ya Kiharusi cha kuvuja damu huitwa'Subarachnoid hemorrhage. Soma Zaidi...

Kondomu za kike
Posti hii inaonyesha Faida na hasara za Kondomu za kike Soma Zaidi...

Zifahmu Dalili za homa ya ini Kali ya pombe.
Posti hii inaonyesha dalili na Mambo Hatari yanayosababisha homa ya ini Kali ya pombe. Soma Zaidi...

Ains ya kisukari inayojulikana kama Diabety type 1
Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisukari Aina ya kwanza ambapo kwa kitaalamu huitwa Diabetes type 1, ni hali ambayo utokea ambapo mwili ushindwa kutengeneza insulini ambayo uweka sukari kwenye hali ya usawa. Soma Zaidi...

Ugonjwa wa surua kwa watoto.
Surua ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na homa na upele mwekundu, unaotokea utotoni. Wakati mtu aliye na virusi akikohoa au kupiga chafya, matone yaliyoambukizwa huenea angani na kutua kwenye sehemu zilizo karibu. Mtoto anaweza kupata virusi kwa kuvuta matone haya au kwa kugusa na kisha kugusa uso, mdomo, macho au masikio yao. Surua ni ugonjwa unaoambukiza sana unaosababishwa na virusi vya surua Soma Zaidi...

Dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo
Post hii inahusu zaidi dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ingawa sio watu wote wenye dalili kama hizi Wana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo Ila zikitokea mtu anapaswa kwenda hospitalini kupima Ili kupata uhakika wa afya, zifuatazo ni dalili za mtu Mwenye tatizo la uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo. Soma Zaidi...

Njia za kuzuia kiungulia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuzuia kiungulia Soma Zaidi...