Madhara ya kutotibu uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo
Post hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu ugonjwa wa uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo,ni madhara yanayotokea kwenye mfumo mzima wa kupitisha mkojo na via vya uzazi kama ifuayavyo.
1. Maambukizi kwenye figo.
Kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo hali hii usababisha bakteria kusambaa kwenye sehemu mbalimbali za kibofu Cha mkojo na pengine maambukizi yanakuwa makubwa mno yanayopelekea kuaribika kwa figo na kumbuka figo ni kitu muhimu sana kwenye mwili kwa hiyo maambukizi yakiwa makubwa figo linakuwa kwenye hali ya hatari, kwa hiyo tunapaswa kutibu ugonjwa huu mapema Ili kuepuka kuepusha kuaribika kwa figo kwa sababu dawa hospitalin zipo na ugonjwa huu wa uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo unatibika kwa hiyo tutibu ugonjwa huu Ili kuepusha madhara mbalimbali.
2. Kuwepo na damu kwenye mkojo.
Kitendo Cha kuwepo kwa damu kwenye mkojo uonekana katika vipimo ,hii ni hali ya hatari kwa sababu maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo yanaonekana kuwa makubwa zaidi kwa sababu wadudu wameshakula sehemu mbalimbali na kusababisha mkojo kuwa na damu, kwa hiyo tunapaswa kuelimisha jamii kuhusu kuwepo kwa ugonjwa huu na kuwa unatibika mtu yeyote akiona dalili ya damu kwenye mkojo anapaswa kwenda hospitalini kupima Ili kuweza kupata matibabu kwa kuwa watu wengi wameugua ugonjwa huu na wamepona.
3. Uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo umfanya mgonjwa ajisikie vibaya kwenye jamii.
Hii utokea pale mgonjwa mwenye tatizo hili akiwa kwenye jamii anakojoa damu, mkojo una harufu mbaya, anahisi maumivu akiwa kwenye jamii ambayo haieleweki watu wanaweza kumcheka na mgonjwa anaweza kujisikia vibaya na kuendelea kuwa na wasiwasi na kuishi bila raha kwenye jamii.kwa hiyo tutibu ugonjwa huu na tuwaone wagonjwa wa hivi kama watu wengine na kuwasaidia kwenda hospitalini Ili wapate huduma kwa kuwa ni ugonjwa unaweza kumpata kila mtu yeyote hakuna mwenye nao.
4. Maambukizi kwenye via vya uzazi.
Ugonjwa huu ikiingia kwenye kibofu Cha mkojo na baadae maambukizi yanaweza kusambaa mpaka kwenye via vya uzazi na yakishambulia uko yanaweza kuleta madhara makubwa zaidi kwa hiyo Tiba ni lazima, maambukizi yakizidi yanaweza kuleta hata na Kansa iwapo mgonjwa hakutibiwa mapema.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Yajuwe maradhi mbalmbali ya ini na chanzo chake
Ini ni moja ya ogani za mwili ambazo husumbuliwa na maradhi hatari sana. Katika post hii utakwend akuyajuwa maradh hatari ambayo hushambulia ini. Pia utajifunza jinsi a kujikinga na maradhi hayo.
Soma Zaidi...Ishara na dalilili za Mtoto mwenye kuhara
postii hii inazungumzia dalilili za Mtoto mwenye Kuhara. Kuhara maana yake ni kutokwa na kinyesi chenye maji matatu au zaidi, pamoja na au bila damu ndani ya masaa 24. Kuhara kunaweza kusababishwa na maambukizo ya bakteria na virusi, ugonjwa wa matumb
Soma Zaidi...Dalilili zinazotokea kwenye mrija wa mkojo
Mrija wa mkojo hutoa mkojo nje ya mwili lakini mrija huu unapoziba hufanya utoaji wa mkojo kutoka kwa shida au maumivu
Soma Zaidi...Fahamu mapacha wanavyounganishwa.
Mapacha walioungana ni watoto wawili wanaozaliwa wakiwa wameunganishwa kimwili. Mapacha walioungana hukua wakati kiinitete cha mapema kinapojitenga na kuunda watu wawili. Ingawa vijusi viwili vitakua kutoka kwa kiinitete hiki, wataendelea kushikamana mar
Soma Zaidi...Dondoo muhimu ya ki afya.
Posti hii inahusu zaidi maelekezo muhimu ya ki afya, ni maelekezo ambayo utolewa ili kuweza kuzifanya afya zetu ziwe bora zaidi na kuepuka madhara yoyote ya ki afya
Soma Zaidi...