Madhara ya kutotibu uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo
Post hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu ugonjwa wa uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo,ni madhara yanayotokea kwenye mfumo mzima wa kupitisha mkojo na via vya uzazi kama ifuayavyo.
1. Maambukizi kwenye figo.
Kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo hali hii usababisha bakteria kusambaa kwenye sehemu mbalimbali za kibofu Cha mkojo na pengine maambukizi yanakuwa makubwa mno yanayopelekea kuaribika kwa figo na kumbuka figo ni kitu muhimu sana kwenye mwili kwa hiyo maambukizi yakiwa makubwa figo linakuwa kwenye hali ya hatari, kwa hiyo tunapaswa kutibu ugonjwa huu mapema Ili kuepuka kuepusha kuaribika kwa figo kwa sababu dawa hospitalin zipo na ugonjwa huu wa uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo unatibika kwa hiyo tutibu ugonjwa huu Ili kuepusha madhara mbalimbali.
2. Kuwepo na damu kwenye mkojo.
Kitendo Cha kuwepo kwa damu kwenye mkojo uonekana katika vipimo ,hii ni hali ya hatari kwa sababu maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo yanaonekana kuwa makubwa zaidi kwa sababu wadudu wameshakula sehemu mbalimbali na kusababisha mkojo kuwa na damu, kwa hiyo tunapaswa kuelimisha jamii kuhusu kuwepo kwa ugonjwa huu na kuwa unatibika mtu yeyote akiona dalili ya damu kwenye mkojo anapaswa kwenda hospitalini kupima Ili kuweza kupata matibabu kwa kuwa watu wengi wameugua ugonjwa huu na wamepona.
3. Uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo umfanya mgonjwa ajisikie vibaya kwenye jamii.
Hii utokea pale mgonjwa mwenye tatizo hili akiwa kwenye jamii anakojoa damu, mkojo una harufu mbaya, anahisi maumivu akiwa kwenye jamii ambayo haieleweki watu wanaweza kumcheka na mgonjwa anaweza kujisikia vibaya na kuendelea kuwa na wasiwasi na kuishi bila raha kwenye jamii.kwa hiyo tutibu ugonjwa huu na tuwaone wagonjwa wa hivi kama watu wengine na kuwasaidia kwenda hospitalini Ili wapate huduma kwa kuwa ni ugonjwa unaweza kumpata kila mtu yeyote hakuna mwenye nao.
4. Maambukizi kwenye via vya uzazi.
Ugonjwa huu ikiingia kwenye kibofu Cha mkojo na baadae maambukizi yanaweza kusambaa mpaka kwenye via vya uzazi na yakishambulia uko yanaweza kuleta madhara makubwa zaidi kwa hiyo Tiba ni lazima, maambukizi yakizidi yanaweza kuleta hata na Kansa iwapo mgonjwa hakutibiwa mapema.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina ๐2 web hosting ๐3 Simulizi za Hadithi Audio ๐4 Kitau cha Fiqh ๐5 Madrasa kiganjani ๐6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Dalili za maambukizi kwenye milija(fallopian tube)
Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye milija (follapian tube) kwa kitaalamu huitwa salpingitis, ni maambukizi kwenye milija ambayo husababishwa na bakteria.
Soma Zaidi...Sababu ya maumivu ya magoti.
Posti hii inahusu zaidi sababu za maumivu ambayo yanasikika kwenye magoti, huu ni ugonjwa ambao umewapata walio wengi na bado ni kilio kwa walio wengi kwa vijana na kwa wazee, Kuna wataalamu mbalimbali ambao wameweza kugundua sababu za maumivu kwenye mago
Soma Zaidi...Je, Maumivu ya Tumbo ni Dalili ya Mimba?
โMaumivu ya tumbo ni jambo linaloweza kuleta wasiwasi kwa mwanamke yeyote anayehisi anaweza kuwa mjamzito. Makala hii inafafanua sababu za maumivu haya, kutofautisha kati ya maumivu ya kawaida na yale yanayohitaji tahadhari, na kutoa mwongozo wa hatua za kuchukua.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa kiseyeye na dalili zake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa kiseyeye na dalili zake
Soma Zaidi...KAMA UNASUMBULIWA NA FANGASI
Post hii fupi inakwenda kukujuza juu ya tatizo la fangasi na nini ufanye.
Soma Zaidi...Sababu za Ugonjwa wa Shinikizo la juu la Damu.
Shinikizo la juu la damu ni hali ya kawaida ambapo nguvu ya muda mrefu ya damu dhidi ya kuta za ateri yako ni kubwa vya kutosha hivi kwamba inaweza kusababisha matatizo ya kiafya, kama vileรย Ugonjwa wa Moyo.
Soma Zaidi...