picha

dalili za mimba changa ndani ya wiki moja

Je na wewe ni katika ambao wanahitaji kujuwa dalili za mimba ndani ya wiki moja? kama ndio makala hii ni kwa ajili yako. Utakwenda kuona dalili za mwanzo sana za ujauzito toka siku za mwanzoni.

Mimba huweza kutungwa baada ya mbegu ya kiume kukutana na yai na kulirutubisha. Mchakato huu kiasili hufanyika katika tumbo la uzazi katika mirija ya falopia ya mama. Siku hizi teknolojia imekuwa, mimba inaweza kutungishwa nje na baadaye yai kurudishwa kwa mama na tayari kukuwa kama mtoto. Watu wengi wamekuwa wakisumbuka na kutafuta ujauzito. Makala hii itakuwa na maada katika nyanja hii ya afya ya uzazi.

 

Dalili za mimba maana yake ni kuona mabadiliko katika mwili wa mwanamke baada ya kushiriki tendo la ndoa. Mabadiliko haya yawe yamesababishwa na kutungishwa kwa yai. Mabadiliko ya homoni katika mwili wa mwanamke huweza kuzungumza mabo mengi kuhusu afya ya mwanamke huyo. Miongoni mwa dalili za mwanzoni za ujauzito ni mabadiliko ya homoni. Mabadilko haya ndiyo baadaye yanasababisha kichefuchefu, kupata harufu, na mengineyo.

 

JE NI ZIPI DALILI ZA UJAUZITO NDANI YA WIKI MOJA?
Mwanamke anaweza kupatwa na mabadiliko ndani ya wiki moja ya ujauzito. Mabadiliko haya anaweza asiyahisi kwani yamekuwa yakifanana na hali za kawaida. Hii husababisha mwanamke ajegunduwa kuwa ana ujauzito hadi pale atakapokosa siku zake. Hapa nitakuletea baadhi ya mabadiliko ambayo huweza kuonekana mwanzoni sana mwa ujauzito ambayo huweza kuashiria dalili za mimba changa ndani ya wiki moja.


1.Kuona damu kidogo yneye rangi hafifu. Damu hii inaweza kuwa ni kitone ama mabadiliko ya rangi kwenye nguo ya ndani. Huwenda pia asigundue damu hii hadi wakati anapojisafisha. Damu hii kitaalamu hufahamika kama implantation bleeding. Kwa baadhi ya wanawake wanaweza kuiona damu hii mwanzoni kabisa katika wiki ya kwanza.

 

2.Maumivu ya tumbo. Maumivu haya yanafanana na tumbo la chango. Yanaweza kuuma kwamuda kama unachomwa kisha yanakata. Yanaweza kufanya hivikwa siku kadhaa kisha yanapotea. Kwa wanwake wengine yanaweza kuchukuwa muda mfupi sana hata kwa siku moja ama mbili hivi, ila wengine hata wiki.

 

3.Kichwa kuwa chepesi na kuwa na maumivu ya hapa na pale. Mwanamke anaweza kuhisi kizunguzungu yaani kichwa kinakuwa chepesi sana. Hali hii huweza kuambatana na maumivu ya kichwa ama joto la mwili kuongezeka.

 

4.Kuhisi uchovu. Uchovu ni hali za kawaida ambapo kila mtu anaweza kuihisi hali hii. Kuna sababu nyingi za kuwa na uchovu.lakni kwa mwanamke mwenye mimba hana sababu maalumu. Yaani ghafla anaweza kuhisi uchovu ambao hauna chanzo.

5.Tumbo kujaa gesi na kujaa nakuwa gumu. Hali hii inaweza kuambatana na kupungua kwa hamu ya kula na kukosa choo. Mwanamke atahisi tumbo kuwa limejaa, akila kidogo ameshiba hii ni kwa sababu ya gesi. Gesi hii hutokea kutokana na mabadiliko ya homoni aliyonayo.

 

Kwa ufupi hizo ni baadhi tu ya dalili za mwanzo sana za ujauzito. Mabadiliko haya pia yanaweza kuwa si ujauzito hivyo kuashiria shida nyingine za kiafya kwa mfano. Kuna baadhi ya maradhi yenyewe yanaweza kuwa na baadhi ya dalili za ujauzito kama:-
1.Mabadiliko ya homoni
2.UTI
3.PID
4.Fangasi
5.Shida kwenye kizazi

 

Je ni siku ipi ya kushiriki tendo la ndoa upate ujauzito?
Ujauzito huweza kupatikana katika siku chache sana zisizozidi 10 katika mzunguko wa siku za mwanamke. Siku hizi zipo ambazo nimujarabu sana kutafuta ujauzito na nyingine sio sana. Hivyo kama unataka kutafuta ujauzito zinagtia yafuatayo:
1.Shiriki tendo la ndoa katika siku hatari zote ama ruka kwa mojamoja
2.Shiriki tendo la ndoa siku ambayo una hamu sanna
3.Shiriki tendo la ndoa utakapoona majimaji ya ukeni yameongezeka
4.Shiriki tendo la ndoa utakapoona joto la mwili wako limeongezeka, si kwa sababu unahoama ama ulilala n.k.

Soma zaidi hapa

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 86404

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    ๐Ÿ‘‰4 Dua za Mitume na Manabii    ๐Ÿ‘‰5 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Matatizo ya unene kwa watoto (childhood obesity)

post Ina onyesha madhara na matatizo ya Unene Utoto ni hali mbaya ya kiafya inayoathiri watoto na vijana. Inatokea wakati mtoto yuko juu ya uzito wa kawaida kwa umri na urefu wake

Soma Zaidi...
nina maambukizi ya zinaha maumivu wakati wa kukojoa na usaha

Mimi nilifanya ngono isiyo salama Tar 14/07 mwaka huu, nilikutana tu na mwanamke ambae sikuwa hata na background yake yoyote hivyo baada ya siku tatu nilijikuta nina maambukizi ya zinaha (maumivu wakati wa kukojoa na usaha), hivyo nilienda hospital na kup

Soma Zaidi...
Mie ni mwanamke ninamaumivu chini ya kitovu upande wa kushoto, na nikishika tumbo nahisi kitu kigumu upande huo huo wa kushoto... hii itakua ni nini?

Je unasumbuliwa na maumivuvya tumbo chini ya kitovu upande wa kushito. Post hii itakuletea sababu za maukivubhayo na nini ufanye.

Soma Zaidi...
ujuwe ugonjwa wa gout na athari zake mwilini

Post hii itakwenda kuzungumzia ugonjwa wa gout unaosababishwa na ongezeko la asidi mwilini.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Kuvimba ubongo (Encephalitis)

Post hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa kuvimba kwa ubongo ambao kitaalamu huitwa Encephalitis, Ni Maambukizi ya virusi ni sababu ya kawaida ya hali hiyo. Ugonjwa wa Kuvimba ubongo unaweza kusababisha dalili zinazofanana na Homa, kama vileร‚ย Homaร‚ย au

Soma Zaidi...
maumivu makali sana juu ya tumbo yn kama kuna moto hivi na mgongon kama unadungwa sindano hivi je hizo ni dalili za vidonda vya tumbo?

Dr huwa nasikia maumivu makali sana juu ya tumbo yn kama kuna moto hivi na mgongon kama unadungwa sindano hivi je hizo ni dalili za vidonda vya tumbo?

Soma Zaidi...
Dalili kwa mtu anayeharisha

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kuharisha, kuharisha ni kitendo Cha kupitia kinyesi chenye maji inawezekana kina damu au kisichokuwa na damu.

Soma Zaidi...
Dalili za mkojo mchafu na rangi za mkojo na mkojo mchafu

Hapautajifunza rangi kuu za mkojo na dalili zako kiafya, mkojo mchafu na dalili zake

Soma Zaidi...
Maambukizi ya Kawaida ya zinaa (Chlamydia)

maambukizi ya kawaida ya zinaa (STI), Hujulikana Kama Chlamydia. Huenda usijue una Ugonjwa huu kwa sababu watu wengi hawapati dalili au ishara, kama vile maumivu ya sehemu za siri na kutokwa na uchafu kutoka kwa uke au uume. Maambukizi haya huathiri

Soma Zaidi...
DALILI ZA UTUMBO KUZIBA

Kuziba kwa utumbo ni kuziba kwa chakula au kimiminika kisipite kwenye utumbo mwembamba au utumbo mpana (colon). Kuziba kwa matumbo kunaweza kusababishwa na mikanda ya nyuzi kwenye fumbatio ambayo huunda baada ya upasuaji, mifuko iliyovimba au iliyoambuk

Soma Zaidi...