dalili za mimba changa ndani ya wiki moja

Je na wewe ni katika ambao wanahitaji kujuwa dalili za mimba ndani ya wiki moja? kama ndio makala hii ni kwa ajili yako. Utakwenda kuona dalili za mwanzo sana za ujauzito toka siku za mwanzoni.

Mimba huweza kutungwa baada ya mbegu ya kiume kukutana na yai na kulirutubisha. Mchakato huu kiasili hufanyika katika tumbo la uzazi katika mirija ya falopia ya mama. Siku hizi teknolojia imekuwa, mimba inaweza kutungishwa nje na baadaye yai kurudishwa kwa mama na tayari kukuwa kama mtoto. Watu wengi wamekuwa wakisumbuka na kutafuta ujauzito. Makala hii itakuwa na maada katika nyanja hii ya afya ya uzazi.

 

Dalili za mimba maana yake ni kuona mabadiliko katika mwili wa mwanamke baada ya kushiriki tendo la ndoa. Mabadiliko haya yawe yamesababishwa na kutungishwa kwa yai. Mabadiliko ya homoni katika mwili wa mwanamke huweza kuzungumza mabo mengi kuhusu afya ya mwanamke huyo. Miongoni mwa dalili za mwanzoni za ujauzito ni mabadiliko ya homoni. Mabadilko haya ndiyo baadaye yanasababisha kichefuchefu, kupata harufu, na mengineyo.

 

JE NI ZIPI DALILI ZA UJAUZITO NDANI YA WIKI MOJA?
Mwanamke anaweza kupatwa na mabadiliko ndani ya wiki moja ya ujauzito. Mabadiliko haya anaweza asiyahisi kwani yamekuwa yakifanana na hali za kawaida. Hii husababisha mwanamke ajegunduwa kuwa ana ujauzito hadi pale atakapokosa siku zake. Hapa nitakuletea baadhi ya mabadiliko ambayo huweza kuonekana mwanzoni sana mwa ujauzito ambayo huweza kuashiria dalili za mimba changa ndani ya wiki moja.


1.Kuona damu kidogo yneye rangi hafifu. Damu hii inaweza kuwa ni kitone ama mabadiliko ya rangi kwenye nguo ya ndani. Huwenda pia asigundue damu hii hadi wakati anapojisafisha. Damu hii kitaalamu hufahamika kama implantation bleeding. Kwa baadhi ya wanawake wanaweza kuiona damu hii mwanzoni kabisa katika wiki ya kwanza.

 

2.Maumivu ya tumbo. Maumivu haya yanafanana na tumbo la chango. Yanaweza kuuma kwamuda kama unachomwa kisha yanakata. Yanaweza kufanya hivikwa siku kadhaa kisha yanapotea. Kwa wanwake wengine yanaweza kuchukuwa muda mfupi sana hata kwa siku moja ama mbili hivi, ila wengine hata wiki.

 

3.Kichwa kuwa chepesi na kuwa na maumivu ya hapa na pale. Mwanamke anaweza kuhisi kizunguzungu yaani kichwa kinakuwa chepesi sana. Hali hii huweza kuambatana na maumivu ya kichwa ama joto la mwili kuongezeka.

 

4.Kuhisi uchovu. Uchovu ni hali za kawaida ambapo kila mtu anaweza kuihisi hali hii. Kuna sababu nyingi za kuwa na uchovu.lakni kwa mwanamke mwenye mimba hana sababu maalumu. Yaani ghafla anaweza kuhisi uchovu ambao hauna chanzo.

5.Tumbo kujaa gesi na kujaa nakuwa gumu. Hali hii inaweza kuambatana na kupungua kwa hamu ya kula na kukosa choo. Mwanamke atahisi tumbo kuwa limejaa, akila kidogo ameshiba hii ni kwa sababu ya gesi. Gesi hii hutokea kutokana na mabadiliko ya homoni aliyonayo.

 

Kwa ufupi hizo ni baadhi tu ya dalili za mwanzo sana za ujauzito. Mabadiliko haya pia yanaweza kuwa si ujauzito hivyo kuashiria shida nyingine za kiafya kwa mfano. Kuna baadhi ya maradhi yenyewe yanaweza kuwa na baadhi ya dalili za ujauzito kama:-
1.Mabadiliko ya homoni
2.UTI
3.PID
4.Fangasi
5.Shida kwenye kizazi

 

Je ni siku ipi ya kushiriki tendo la ndoa upate ujauzito?
Ujauzito huweza kupatikana katika siku chache sana zisizozidi 10 katika mzunguko wa siku za mwanamke. Siku hizi zipo ambazo nimujarabu sana kutafuta ujauzito na nyingine sio sana. Hivyo kama unataka kutafuta ujauzito zinagtia yafuatayo:
1.Shiriki tendo la ndoa katika siku hatari zote ama ruka kwa mojamoja
2.Shiriki tendo la ndoa siku ambayo una hamu sanna
3.Shiriki tendo la ndoa utakapoona majimaji ya ukeni yameongezeka
4.Shiriki tendo la ndoa utakapoona joto la mwili wako limeongezeka, si kwa sababu unahoama ama ulilala n.k.

Soma zaidi hapa

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 85775

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰3 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰4 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Habari nasumbuliwa na tumbo upande wakilia adi nikikojoa mkojo wa mwisho uwa wa kahawia tiba take nini?

Maumivu ya tumbo yanaweza kusababishwa na mambo mengi ikiwemo typhod, vidonda vya tumbo na shida nyingine kwenye mfumo wa chakula.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa coma

Coma ni hali ya kupoteza fahamu kwa muda mrefu ambayo inaweza kusababishwa na matatizo mbalimbali Jeraha la Kichwa, Kiharusi, Uvimbe kwenye ubongo, ulevi wa dawa za kulevya au pombe, au hata ugonjwa wa msingi,

Soma Zaidi...
Presha ya kushuka (hypotension) dalili zake na njia ya kukabiliana nayo

Presha ya kushuka ama kitaalamu huitwa hypotension, presha ya kushuka ni hatari kwa afya kama ilivyo presha ya kupanda, maana mwili unakosa nguvu kabisa.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kuchelewa kuganda kwa Damu unaojulikana Kama hemophilia.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na tatizo la Kurithi ambapo Damu inatoka kwa muda mrefu wakati au baada ya jeraha bila kuganda.

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni na dalili zake

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo kitovuni na dalili zake

Soma Zaidi...
Sababu za mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu.

Post hii inahusu zaidi mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu na kwa kitaalamu huitwa retention of urine.

Soma Zaidi...
Njia za kusambaa kwa ugonjwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine

Posti hii inahusu zaidi jinsi magonjwa yanavyosambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

Soma Zaidi...
Kiungulia na tiba zake kwa wajawazito.

Posti hii inahusu kiungulia kwa wanawake wajawazito na tiba yake, ni ugonjwa au hali inayowapata wajawazito walio wengi kwa sababu ya kuwepo kwa mabadiliko ya homoni wakati wa ujauzito.

Soma Zaidi...
Sababu na Chanzo cha vidonda vya tumbo

Zijuwe sababu za kutokea kwa vidonda vya tumbo. Sababu kuu za vidonda vya tumbo hizi hapa

Soma Zaidi...
Saratani ya tishu zinazounda Damu mwilini (leukemia)

Post hii inaelezea kuhusiana naร‚ย Sarataniร‚ย ya tishu zinazounda damu mwilini, ikijumuisha uboho na mfumo wa limfu.ugonjwa huu kitaalamu huitwa leukemia.

Soma Zaidi...