Menu



TAHADHARI KWENYE VYAKULA ILI KULINDA AFYA YAKO

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

TAHADHARI KWENYE VYAKULA ILI KULINDA AFYA YAKO

KUBORESHA AFYA
1.TAHADHARI KWENYE VYAKULA
Ukiweza kuchukuwa tahadhari kwenye vyakula na kujua chakula salama cha kukila kulingana na mahitaji ya mwili hapa unaweza kufanikiwa kuulinda mwili wako na maradhi mengi sana. Uwe na elimu sahihi ya vyakula na faida zake kwenye mwili. Kwani unaweza kukusanya vyakula vingi kumbe ni sawa na kual chakula kimoja

Vyakula vya protini ni m uhimu katika ukuaji wa watoto na ukuaji wa tishu. Vyakula hivi huhusika katika kuurekebisha mwili na ni muhimu hsana katika kuhakikisha afya ya mtu ipo kwenye msitari mzuri. Kwa ufupi tunasema kuwa vyakula vya protini ni vyakula vya kujenga mwili. Unaweza kupata protini kwenye maziwa, samaki, nyama, maini, maharage na mayai. Upungufu wowote wa vyakula hivi unaweza kuleta mdahara makubwa kama tulivyoona hapo juu.

Vyakula vya wanga ni mujarabu sana kwa ajili ya kuupa mwili nguvu. Tumia vyakula hivi hasa kama unafanya kazi za nguvu. Vyakula hivi pia ni muhimu kwa ajili ya kuhakikisha kuwa m ifumo ndani ya mwili inafanya kazi kwa usahihi. Kwa mfano mfumo wa upumuaji na uunguzwaji wa chakula (espiration) unahitajia vyakula hivi kwa ajili ya kuzalisha nguvu ya kutosha ndani ya mwili. Vyakula hivi vinaweza kupatikana kwenye nafaka kama mahindi, ngano na mchele.

Vyakula vya madini, Mwili unahitaji vyakula hivi ili uwezesj\he matumizi ya vyakula vingine yawe mazuri tunahitaji viyamini kwa kuulinda mwili dhidi ya magonkwa. Vitamin c hujulikana kwa kusaidia ugonjwa wa scuvy ugonjwa huu humfanya mtu atoke samu mwenue mafinzi. Vitamin A husaidia kurekebisha afya ya macho. Vitamin K husaidia kuganda kwa damu unapopata jeraha. Mwili unahitaji madini pia ili uweze kujikinga na hatari zingine. Madini ya chuma ni muhimu katika kujenga seli nyekundu za damu.madini ya calcium ni muhimu kwa afya ya mifupa na meno. Madini na vitamin hpatikana zaidi kwenye mboga za majani, na matunda. Matunda yenye uchachu kama limao, chungwa husaidia kwa vitamin C na mapapai pi hujulukana kwa kuwa na vitamin C. spinachi ni muhimu kwa vitamin A. samaki husaidia kwa madini mengine.

Vitamin ni muhimu katika kuhakikisha kuwa mwili unatumia virutubisho vingine kufanya kazi zake. Kuna vitamin A,B,C,D,E na K. vitamin B vimegawanyika katika makundi kama vitamin B1,B2,B6, na B12. Ukosefu wa vitamin vyovyote kati ya hivi unaweza ukapelekea matatizo makubwa kwa afya ya mtu. Vitamin A,D,E na K, vinaitwa fat soluble vitamin. Hivi nhuweza kuhifadhiwa ndani ya mwili. Hivyo hatuhitaji kula vyakula kuvipata kwa kila siku. Kwa upande mwengingine vitamin B na C huitwa water soluble vitamin, hivi havihifadhiwi ndani ya mwili, hivyo tunahitaji kula vyakula vyenye vitamin hivi kwa kila siku. Hivyo mtu awe na tahadhari zaidi juu ya kupangilia vyakula vyake. Tuatona zaidi aina hizi na madhara yake kwenye kurasa zijazo.

Unywaji wa maji ni jambo linalolazimishwa sana. Kwama mtu hana sababu yeyote anatakiwa anywe maji mengi zaidi. Wataalamu wa afya wanashauri angalau kwa siku mtu anywe maji bilauri (glass) nane kwa kiwango cha chini. Mwili wa kiumbe hai asilimia 50-90 ni maji. Hivyo maji yakipungua mwilini kunaweza kutokea madhara makubwa zaidi. Maji huhitajika karibia katika mifumo yote mwilini. Maji hutumika katika kurekebisha afya ya mtu.


                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 307

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

afya somo la 15

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
kitabu cha matunda

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuepuka magonjwa ya figo

Figo ni moja katika orgn zenye umuhimu sana mwilini na endapo itaatirika kwa namna yeyote ile, madhara makubwa kwenye mwili yanaweza kutokea na hata kifo. Katika post hii utajifunza jinsi ya kulinda mwili wako dhidi ya matatizo ya figo

Soma Zaidi...
utaratibu wa lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
YANAYOATHIRI AFYA KUTOKANA NA VIZAZI, FAMILIA NA KURITHI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Namna ya kufanya ngozi kuwa laini

Posti hii inahusu zaidi njia au namna ya kufanya ili ngozi iweze kuwa laini bila kuwa na make up yoyote.

Soma Zaidi...
KITABU CHA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...