Tembo ni katika wanyama wenye kushangaza sana.
Tembo wana maajabu makubwa kama utazingatia kwa umakini umbo lake zuri.
Tembo anaweza kufika urefu wa mita tatu (3) mpaka mita 4 yaani fkuanzia futi 10 mpaka 13. Tembo anaweza kufika uzito wa kilo elfu saba (kg 7000) yaani tani saba. Mimba ya tembo inaweza kuchukuwa miezi 20 mpaka 22 yaani miaka miwili kasoro miezi miwili.
Tembo mtoto ananyonya mpaka kufikia miaka mitatu mpaka minne. Tembo mtoto akiwa na umri wa miaka 10 uzito wake unaweza kufika kilo 900 mpaka 1,300. Tembo anaweza kuishi zaidi ya miaka 60.Inakadiriwa kuwa idadi ya tembo wote waliopo duniani leo ni kati ya laki nne mpaka tano (400,000 - 500,000).
Tembo anaweza kufundishwa na kutumika kwa shughuli kama kunyanyua mizigo ama usafiri. Tembo ana uwezo wa kusikia kwa umbali mrefu sana. Tembo hutumia mkonga wake wa ajili ya kuzungumza na wezie, kuwaonya na kuita mkutano. Pia hutumia mkonga wake kwa ajili ya kulia chakula, kuhifadhi maji ama kuoga. Tembo hutumia meno yake yaani mapembe kwa ajili ya kujilinda na kulinda familia yake dhidi ya wanyama walao nyama.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Dua za Mitume na Manabii π2 Bongolite - Game zone - Play free game π3 Kitabu cha Afya π4 ai web app π5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Bongoclass
Bongoclass ni darasa la kushiriika akili na maarifa kutoka kwa watu mbalimbali katika kutumia fursa zilizopo ili kuzalisha kipato na kuleta maendeleo katika jami
Soma Zaidi...Kitabu Cha Contact
Unaweza kuwasiliana nasi kwenye mitandao ya kijamii, kwa kutumia jina la Bongclass.
Soma Zaidi...