picha

Tembo

Posti hii inakwenda kukupa sifa za mnyama tembo

TEMBO

 

picTembo ni katika wanyama wa porini na ndiye mnyama mkubwa kuliko wote.Tembo anaweza kufika urefu wa mita tatu (3) mpaka mita 4 yaani fkuanzia futi 10 mpaka 13. Tembo anaweza kufika uzito wa kilo elfu saba (kg 7000) yaani tani saba. Mimba ya tembo inaweza kuchukuwa miezi 20 mpaka 22 yaani miaka miwili kasoro miezi miwili.

 

Tembo mtoto ananyonya mpaka kufikia miaka mitatu mpaka minne. Tembo mtoto akiwa na umri wa miaka 10 uzito wake unaweza kufika kilo 900 mpaka 1,300. Tembo anaweza kuishi zaidi ya miaka 60.Inakadiriwa kuwa idadi ya tembo wote waliopo duniani leo ni kati ya laki nne mpaka tano (400,000 - 500,000). Tembo majike huwa wanaishi kwenye makundi. Kundi hili la tembo lina watoto na wakee wanawake pamoja na mashangazi. Kiongozi wa kundi hili la tembo ni yule mkubwa kuliko wote. Watoto wa kiume wa tembo wanapofika umri wa miaka 6 hujitenga na kundi hili na kutembea pekee. Tembo majike hukutana na tembo matume unapofika muda wa kupata watoto.

 

picTembo ni katika wanyama wenye nguvu kwani anauwezo wa kuweza kung’oa mti pamoja na mizizi yake. Wataalamu wa sayansi wanashangazwa na uwezo wa nguvu za tembo. Kwani anauwezo wa kunyanyua vitu vikubwa na pia kwa mkinga wake anaweza kunyanyua vitu vyepesi kama tunda au majani. Wataalamu wa sayansi wametengeneza vifaa kama magreda kwa kuiga nguvu za tembo lakini bado vifaa vyao ijapokuwa vinanyanyua vitu vizito lakini havina uwezo wa kunyanyua vitu vyepesi.

 

Tembo anaweza kufundishwa na kutumika kwa shughuli kama kunyanyua mizigo ama usafiri. Tembo ana uwezo wa kusikia kwa umbali mrefu sana. Tembo hutumia mkonga wake wa ajili ya kuzungumza na wezie, kuwaonya na kuita mkutano. Pia hutumia mkonga wake kwa ajili ya kulia chakula, kuhifadhi maji ama kuoga. Tembo hutumia meno yake yaani mapembe kwa ajili ya kujilinda na kulinda familia yake dhidi ya wanyama walao nyama.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Mengineyo Main: Post File: Download PDF Views 3004

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Maumivu ya Chini ya Tumbo kwa Mwanamke: Sababu na Tiba

​Maumivu ya chini ya tumbo (nyonga) ni hali inayowapata wanawake wengi katika vipindi tofauti vya maisha yao. Maumivu haya yanaweza kuwa ya ghafla (kali) au ya muda mrefu (sugu), na yanaweza kusababishwa na mifumo mbalimbali mwilini ikiwemo mfumo wa uzazi, mkojo, au mmeng'enyo wa chakula. Makala hii inaangazia sababu kuu za maumivu haya na jinsi ya kukabiliana nayo.

Soma Zaidi...
Njia za Kutatua Migogoro Katika Ndoa

igogoro katika ndoa ni jambo lisiloepukika kutokana na ukweli kuwa wanandoa wawili ni watu tofauti wenye malezi, fikra, na matarajio tofauti. Hata hivyo, tofauti kati ya ndoa zinazostawi na zile zinazoshindwa si ukosefu wa migogoro, bali ni jinsi wanandoa wanavyoitatua. Makala hii inaangazia mbinu za kivitendo za kutatua migogoro ili kudumisha upendo na heshima.

Soma Zaidi...
Hasira za watoto na jinsi ya kuwasaidia kudhibiti mihemko.

Kumuona mtoto akipiga kelele, akijitupa chini, au akilia kwa hasira kali ni jambo linaloweza kuleta mkanganyiko na hata kuwakatisha tamaa wazazi. Hata hivyo, hasira hizi (tantrums) ni sehemu ya kawaida ya ukuaji wa mtoto. Makala haya yanakupa mbinu za kisaikolojia za kusaidia mtoto wako kuelewa na kudhibiti hisia zake wakati wa dhoruba za mihemko.

Soma Zaidi...
MAAJABU YA VIUMBE

MAAJABU YA VIUMBE Dunia ina maajabu sana lakini viumbe wana maajabu pia.

Soma Zaidi...