image

Tembo

Posti hii inakwenda kukupa sifa za mnyama tembo

TEMBO

 

picTembo ni katika wanyama wa porini na ndiye mnyama mkubwa kuliko wote.Tembo anaweza kufika urefu wa mita tatu (3) mpaka mita 4 yaani fkuanzia futi 10 mpaka 13. Tembo anaweza kufika uzito wa kilo elfu saba (kg 7000) yaani tani saba. Mimba ya tembo inaweza kuchukuwa miezi 20 mpaka 22 yaani miaka miwili kasoro miezi miwili.

 

Tembo mtoto ananyonya mpaka kufikia miaka mitatu mpaka minne. Tembo mtoto akiwa na umri wa miaka 10 uzito wake unaweza kufika kilo 900 mpaka 1,300. Tembo anaweza kuishi zaidi ya miaka 60.Inakadiriwa kuwa idadi ya tembo wote waliopo duniani leo ni kati ya laki nne mpaka tano (400,000 - 500,000). Tembo majike huwa wanaishi kwenye makundi. Kundi hili la tembo lina watoto na wakee wanawake pamoja na mashangazi. Kiongozi wa kundi hili la tembo ni yule mkubwa kuliko wote. Watoto wa kiume wa tembo wanapofika umri wa miaka 6 hujitenga na kundi hili na kutembea pekee. Tembo majike hukutana na tembo matume unapofika muda wa kupata watoto.

 

picTembo ni katika wanyama wenye nguvu kwani anauwezo wa kuweza kung’oa mti pamoja na mizizi yake. Wataalamu wa sayansi wanashangazwa na uwezo wa nguvu za tembo. Kwani anauwezo wa kunyanyua vitu vikubwa na pia kwa mkinga wake anaweza kunyanyua vitu vyepesi kama tunda au majani. Wataalamu wa sayansi wametengeneza vifaa kama magreda kwa kuiga nguvu za tembo lakini bado vifaa vyao ijapokuwa vinanyanyua vitu vizito lakini havina uwezo wa kunyanyua vitu vyepesi.

 

Tembo anaweza kufundishwa na kutumika kwa shughuli kama kunyanyua mizigo ama usafiri. Tembo ana uwezo wa kusikia kwa umbali mrefu sana. Tembo hutumia mkonga wake wa ajili ya kuzungumza na wezie, kuwaonya na kuita mkutano. Pia hutumia mkonga wake kwa ajili ya kulia chakula, kuhifadhi maji ama kuoga. Tembo hutumia meno yake yaani mapembe kwa ajili ya kujilinda na kulinda familia yake dhidi ya wanyama walao nyama.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Mengineyo Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1661


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zifazofanana:-

YAJUWE MAAJABU YA MBUZI PORI
1. Soma Zaidi...

Books
Vinjari ukiwa na vitabu vyetu ukiwa kwenye maktaba yetu Soma Zaidi...

Jifunze kupitia Bongoclass
Soma Zaidi...

Welcome to Online School
Soma Zaidi...

RAJABU ATHUMAN MAHEDE,(MAARUFU KAMA MWALIMU RAJABU ATHUMANI MAHEDE, AU OSTADHI RAJABU ATHUMANI MAHEDE)
Soma Zaidi...

BC
Soma Zaidi...

Bezoa goat (mbuzi pori)
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sifa za mnyama bezoa goat (mbuzi pori) Soma Zaidi...

Kitabu Cha Contact
Unaweza kuwasiliana nasi kwenye mitandao ya kijamii, kwa kutumia jina la Bongclass. Soma Zaidi...

The fastest (anakwenda mbio zaidi)
Posti hii inakwenda kukuletea sifa za mnyama anayekwenda mbio zaidi Soma Zaidi...

MAAJABU NA NGUZU ZA TEMBO
TEMBO Tembo ni katika wanyama wa porini na ndiye mnyama mkubwa kuliko wote. Soma Zaidi...

NAMNA YA KUFANYA KILA KITU KWA VITENDO KUTUMIA PICHA, VIDEO AMA SAUTI
Jifunze kufanya mambo mbalimbali kwa vitendo, kwa kutumia picha, sauti ama video Soma Zaidi...

Promo
Kama wewe ni Muandishi mzuri za hadithi au makala za kutoa elimu kwa watu na unataka kazi yako iwafikie watu wengi, au unataka kazi yako iweze kukuingizia kipato, Bongoclass ndio mtatuzi wako sasa. Soma Zaidi...