YAJUWE MAAJABU YA MBUZI PORI
1.
1. Bezoa goat (mbuzi pori)

Huyu ni mnyama aliyefanana sana na mbuzi isipokuwa huyu ana mapembe makubwa. Mnyama huyu ni katika wanyama wenye maajabu katika dunia hii. Wataalamu wa sayansi na viumbe hasa wale waliobobea kwenye maisha ya wanyama mwitu, wannashangazwa sana na fahamu alizonazo mnyama huyu.
Wataalamu wanaeleza kuwa mnyama huyu amepewa anaitwa Bezoar goat kwa lugha ya kiingereza na jina hili asili yake ni kutoka katika lugha za kifurs kwa maana ya medicine yaani dawa. Na hii ni kutokana na uwezo wake wa kujitibu pindi anapong’atwa na nyoka.
Mnyama huyu anaishi eneo ambalo mimea aina ya Euphorbia inapatikana. Mnyama huyu pindi anapong’atwa na nyoka haraka sana anawahi kula majani ya mimea hii na hatimaye sumu ya nyoka inakosa nguvu na mnyama huyu haendeleu kudhurika.
Kwa ufupi mnyama huyu ni katika wanyama wachache ambao wanaweza kujitibu dhidi ya sumu ya nyoka. Mwenyezi Mungu aliyetukuka ndie aliyempa elimu hii ya kujuwa tiba hii, kwani wapo wanyama wengi msituni waking’atwa na nyoka hawawezi kujitibu.
Mwenyezi Mungu mtukufu anatupa sisi masingatio kupitia maisha ya viumbe. Tukumbuke kuwa Mwenyezi Mungu ndiye ana uwezo wa kila kitu. Anampa elimu amtakaye katika viumbe vyake na anamnyima amtakaye. Atakayepewa amshukuru Allah na atakaye nyimwa pia amshukuru.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 ai web app 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
nataka niunganishe namba yangu kwa mtu mwingne ili kama kuna sms nimetumiwa ianzie kwa huyo mtu
Ikiwa nataka niunganishe namb yangu kwa mtu mwingne il kama kuna sms nime2miwa ianzie kwa huyo mtu nifanyeje?
Soma Zaidi...Buibui hupuruka ijapokuwa hana mbawa.
Nataka nikufundishe moja katika maajabu ya mdudu Buibui kwa lugha ya kimombo spider.
Soma Zaidi...WELCOME TO OUR LIBRARY
Karibu sana Kwenye Maktaba Yetu Sasa umefika kwenye maktaba ya vitabu.
Soma Zaidi...Nyoka wenye sumu kali zaidi duniani
Duniani kuna aina nyingi za nyoka, lakini wachache wao ndio wanaojulikana kwa sumu kali inayoweza kuua haraka. Miongoni mwao ni Inland Taipan, King Cobra, Black Mamba, na Tiger Snake. Sumu zao huathiri mfumo wa neva, damu, au misuli ya mwili wa binadamu.
Soma Zaidi...