image

Kujengwa upya al Kabah baada ya kuwa na mipasuko.

Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 18. Hapa utajifunza kuhusu tukio la kujengwa upya kwa al kaaba 🕋

 


 


KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAH
Itambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani. Kuna baadhi ya wanahistoria wanazungumza kuwa Al-ka’abah kwa mara ya kwanza ilijengwa na Malaika. Kisha ikawa inajengwa kwa kurekebishwa na kuboreshwa muda baada ya muda na binadamu wenyewe. Huenda pia aliyejenga al-ka’bah ni nabii Adamu. Kilicho sahihi zaidi katika maneno haya ni ile kauli ya Allah aliposema kwenye quran kuwa “kwa hakika nyumba ya kwanza kujengwa kwa na watu ni ile iliyopo Makka (al-ka’aba).



Kilipita kipindi kirefu toka kwa Nabii Adamu hadi kwa nabii Ibrahimu. Wakati huo wote al-ka’abah ilikuwa imebakia msingi tu lakini ulisha angukaga zamani sana. Nabii Ibrahimu na mtoto wake Nabii Ismaili (amani iwe juu yao) ndio waliokuja kuijenga upya baada ya kusahaulikwa kwa muda wa miaka mingi sana. Mitume hawa wawili waliweza kuzinyanyua kuta za al-ka’abah na kuunyanyua mjengo wake. Baada ya mitume hawa kujenga al-ka’abah watu wakatangaziwa hija na wakawa wanakwenda kutoka mataifa mbalimbali.



Al-ka’abah iliweza kudumu kwa muda wa miaka mingi bila hata ya kufanyiwa ukarabati upya. Miaka mingi ilisha pita hivyo kutokana na uzee jengo hili kuta zikawa zina nyufa, na zilipoteza ule upora wake. Hata hivyo jengo hili halikuwa madhubuti kwa wezi waliweza kuingia na kuiba baadhi ya hazina zilizohifadhiwa mule. Pia wakati huu al-ka’abah haikuwa na dari. Miaka mitano (5) kabla ya utume kulitokea mafuriko makubwa katika mji wa Makkah. Mafuriko haya yaliweza kuharibu mjengo huu na kuudhoofisha zaidi.



Baada ya tukio hili waarabu wakakaa shura ili wajadiliane namna ya kunusuru jengo hli. Katika shura yao wakakubaliana kujenga upya mjengo huu. Chifu wa maquraysh akaamuwa kuwa watatumia gharama (pesa) za kujengea mjengo huu peza za halali tu. Na hairuhusiwi kutumia pesa yeyote ya haramu kujenga mjengo huu. Baada ya makubaliano haya kazi ya kujenga al-ka’abah ilianza maramoja.



Mwanzo kabisa walikuwa wanaogopa kubomoa jengo hili tukufu. Woga wao uliendelea mpaka alipotokea Al-waleed bin al-Mugheerah al-makhzumi huyu ndie aliyeanza kubomowa ukuta, na baada ya waarabu kuona hakuna lolote baya lililomkuta ndipo wakaungana nae katika kubomoa kuta nyingine. Waliendelea kubomoa mpaka wakakuta msingi aloanzia nabii Ibrahim kujenga al-ka’abah. Waarabu wakagawana kazi kulingana na makabila yao, hivyo kila kabila likapewa jukumu lake.



Hivyo makabila yakaanza kuokota mawe na kazi ikaanza. Mtu ambaye alijenga msingi ni fundi mwenye asili ya kiroma aliyefahamika kwa jina la Baqum. Kazi ya kujenga al-ka’abah ilikwenda vizuri mpaka walipomaliza. Sasa kukawa na mzozo juu ya kulirudisha jiwe jeusi mahala pake. Hapa walitofautiana na mzozo ukawa mkubwa zaidi juu ya nani aweke ziwe tukufu jiwe jeusi mahala pake. Mzozo ulifikia hatua ya watu kuweza kupigana na hata kuwana.



Mzozo huu ukiendelea kati ya machifu wa makabila mpaka ukadumu kwa muda wa siku 4 ama 5 kila mmoja akitaka aipate yeye heshima ya kuliweka jiwe tukufu mahala pake. Mpaka pale mzee mmoja kwenye kuheshimika na mwenye budsara aliyetambulika kwa jina la Abu omaiyah bin Mughiirah al-Makhzum alipotowa rai ambayo ilikubwaliwa na watu wote rai ambayo ililenga kumaliza mzozo huu. Mzee huyu alitowa rai ya kuwa yeyote atakayekuwa wa kwanza kuingia msikitini awe ndiye hakimu wa kutoa maamuzi. Hivyo wote wakakubaliana kwa rai hii. Basi akawa mtu wa kwanza kuingia msikitini ni mtume muhammad (s.a.w).



Wazee wote walipomuona mtu wa kwanza kuingia Msikitini ni Muhammad basi walikubali kwa moyo mmoja kwani walimtambuwa ukweli na uaminifu wake. Na pia alikuwa ni kijana mwenye tabia njema kuliko vijana woote wa Makkah. Basi akachukiwa kilemba na akaliweka lile jiwe kisha akataka kila kiongozi wa kabila akamate ncha ya kilemba kie na kulinyanyua jiwe kwa pamoja. Walipofika sehemu yake akalichukuwa na kuliweka kwa mikono yake. Hapa wazee wote walimsifu na kumkubali kwa busara yake. Hatimaye walimaliza kulijenga jengo hili tukufu, wakati huu Mtume muhammad akiwa na umri wa miaka 35 yaani miaka mitano kabla ya kupea utume.

 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021/11/30/Tuesday - 08:56:31 am     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 758


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Vitimbi vya Makafiri Dhidi ya Nabii Salih(a.s) na Waumini na kuangamizwa kwao
Makafiri wa Kithamud hawakuishia tu kwenye kuukataa ujumbe wa Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na maandalizi ya mtume ki-wahay
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Je, Nabii Isa(a.s) ni Mtoto wa Mungu?
Mwenyezi Mungu si kiumbe. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Lut (a.s)
(i) Tujitahidi kwa kadiri ya uwezo wetu kuondoa maovu katika jamii kwa mikono yetu na ikiwa hatuwezi tuyakemee kama alivyofanya Nabii Lut(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KATIKA HARAKATI ZA KULINGANIA DINI
Soma Zaidi...

Maandalizi ya hijrah ya mtume na waislamu kuhamia madinah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Utekwaji wa Misri na Gavana Muawiya
Soma Zaidi...

Kulelewa kwa Mtume, maisha yake ya Utotoni na kunyonya kwake.
Historia na sura ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 06. Hapa utajifunza kuhusu historia ya Mtume akiwa mtoto. Soma Zaidi...

Mapambano Dhidi ya Maadui wa Dola ya Kiislamu
1. Soma Zaidi...

Mapambano ya Mtume Muhammad dhidi ya Wanafiki na hila zao Madina
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII MUSA(A.S) NA HARUN(A.S)
Nabii Musa(a. Soma Zaidi...

Kwanini mwanadamu hawezi kuunda dini sahihi
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...