SURATUL-KAFIRUN
Imeteremshwa maka na inaelezwa katika sababu za kushuka kwake ni kuwa Kundi la makafiri lilimfuata mtume (s.a.w) na kutoa rai ya kuwa Mtume (s.a.w) ajiunge nao na aabudu miungu yao kwa muda wa mwaka mmoja na wao wataabudu Mola wake kwa muda wa mwaka mmoja. Na kisha ikionekana dini ya mtume (s.a.w) ni bora zaidi wataifuata na kama yao itakuwa ni bora zaidi ataifuata. Allah akalipinga jambo hili na akateremsha sura hii.