Amri ya Kuchinja Ng'ombe

Amri ya Kuchinja Ng'ombe

Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Amri ya Kuchinja Ng'ombe

Amri ya Kuchinja Ng'ombe


Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr. Wakawa nao wanabuni miungu ya vitu vilivyo hai na visivyo hai. Moja ya miungu waliyoibuni ni ng'ombe mwenye sifa maalum. Asiye mzee sana wala mchanga, mwenye rangi ya dhahabu na asiyefanyishwa kazi. Kwa hiyo pamoja na kuwa baadhi ya Mayahudi walifuata sheria ya Musa(a.s), lakini bado athari ya ibada ya ng'ombe ikawa imesalia katika nafsi zao.



Katika mazingira hayo, Nabii Musa(a.s) alipewa amri na Mola wake awaamrishe wachinje ng'ombe. Huu ukiwa ni mtihani wa imani kwao kuthibitisha kwamba kweli wamemuamini Allah(s.w) au la. Mtihani huu ukawa mgumu sana kwao. Wakajaribu kuukwepa kwa kuleta maswali kadhaa ya udadisi. Lakini kila walivyozidi kudadisi juu ya ng'ombe waliyeambiwa wamchinje ndivyo walivyojiingiza mahali pagumu zaidi. Kwani majibu waliyokuwa wakiyapata yaliwataka wamchinje ng'ombe mwenye sifa sawa na yule wanayemuabudu. Basi hatima yake wakamchinja japo kwa shingo upande.



Fundisho lililokusudiwa lilipatikana kwani kile walichokidhania kitakatifu hata kukiabudu walikichinja kwa mikono yao wenyewe na wala hawakupata dhara lolote. Qur'an yabainisha tukio hili katika aya zifuatazo:




"Na Musa alipowaambia watu wake: "Hakika Mwenyezi Mungu anakuamrisheni mchinje ng'ombe". Wakasema: "Je! Unatufanyia mzaha?" Akasema "(La) Najikinga kwa Mwenyezi Mungu kuwa miongoni mwa wajinga. Wakasema: "Tuombee kwa Mola wako atupambanulie ni (wa umri) gani (ng'ombe huyo)?" Akasema: "Hakika Yeye anasema kwamba ng'ombe huyo si mzee wala si mchanga, bali ni wa katikati baina ya hao. Basi fanyeni mnavyoarishwa". Wakasema: "Tuombee kwa Mola wako atupambanulie ni vipi hali yake, hakika ng'ombe wanafanana; (basi yupi)? Na kwa hakika kama Mungu akipenda (tutafuata) tuwe wenye kuongoka". Akasema: "Yeye anasema: Kuwa huyo si ng'ombe aliyetiwa kazini kulima ardhi wala kutilia maji mimea, safi kabisa rangi yake, hana kipaku ndani yake". Wakasema: "Sasa umeleta (maneno ya) haki". Basi wakamchinja, na walikuwa mbali na kufanya hayo". (2:67-71).



Pamoja na fundisho kuu tulilolitaja awali la kujenga hoja dhidi ya shirk; lakini pia aya zinatutanabahisha kuwa tusijaribu kuzikwepa amri za Allah(s.w) kwa kuleta maswali ya udadisi na visingizio. Maadhali jambo limethibiti kuwa ni amri ya Allah basi hatuna hiari bali ni kulitekeleza kwa moyo mkunjufu.



                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 862

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Sababu za kushuka surat al Quraysh
Sababu za kushuka surat al Quraysh

Qurayh ni jina la kabila la Mtume Muhammad S.A.W. Sura hii itakwenda kukujulisha neema ambazo Maquraysh wamepewa na hawataoewa wao wowote baada ya wao.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MADD
HUKUMU ZA MADD

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Ni ipi aya ya mwisho kushuka katika Quran?
Ni ipi aya ya mwisho kushuka katika Quran?

Maulamaa katika elimu ya Quran wametofautiana juu ya aya ya mwisho kushuka. Hata hivyo hapa nitakutajia ambayo imependekezwa zaidi

Soma Zaidi...
quran na sayansi
quran na sayansi

YALIYOMONENO LA AWALI1.

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya sura za makkah na madinah
Tofauti kati ya sura za makkah na madinah

Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat Ikhlas
Sababu za kushuka surat Ikhlas

Surat Ikhlas ni katika sura za kitawhid ambazo zilishuka miaka siku za mwanzoni mwa utume. Sura hii imekuja kujibu maswali mengi kuhusu Allah ikiwemo, Allah ni nani?

Soma Zaidi...
IDGHAAM KATIKA LAAM
IDGHAAM KATIKA LAAM

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...