Navigation Menu



Amri ya Kuchinja Ng'ombe

Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr.

Amri ya Kuchinja Ng'ombe

Amri ya Kuchinja Ng'ombe


Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr. Wakawa nao wanabuni miungu ya vitu vilivyo hai na visivyo hai. Moja ya miungu waliyoibuni ni ng'ombe mwenye sifa maalum. Asiye mzee sana wala mchanga, mwenye rangi ya dhahabu na asiyefanyishwa kazi. Kwa hiyo pamoja na kuwa baadhi ya Mayahudi walifuata sheria ya Musa(a.s), lakini bado athari ya ibada ya ng'ombe ikawa imesalia katika nafsi zao.



Katika mazingira hayo, Nabii Musa(a.s) alipewa amri na Mola wake awaamrishe wachinje ng'ombe. Huu ukiwa ni mtihani wa imani kwao kuthibitisha kwamba kweli wamemuamini Allah(s.w) au la. Mtihani huu ukawa mgumu sana kwao. Wakajaribu kuukwepa kwa kuleta maswali kadhaa ya udadisi. Lakini kila walivyozidi kudadisi juu ya ng'ombe waliyeambiwa wamchinje ndivyo walivyojiingiza mahali pagumu zaidi. Kwani majibu waliyokuwa wakiyapata yaliwataka wamchinje ng'ombe mwenye sifa sawa na yule wanayemuabudu. Basi hatima yake wakamchinja japo kwa shingo upande.



Fundisho lililokusudiwa lilipatikana kwani kile walichokidhania kitakatifu hata kukiabudu walikichinja kwa mikono yao wenyewe na wala hawakupata dhara lolote. Qur'an yabainisha tukio hili katika aya zifuatazo:




"Na Musa alipowaambia watu wake: "Hakika Mwenyezi Mungu anakuamrisheni mchinje ng'ombe". Wakasema: "Je! Unatufanyia mzaha?" Akasema "(La) Najikinga kwa Mwenyezi Mungu kuwa miongoni mwa wajinga. Wakasema: "Tuombee kwa Mola wako atupambanulie ni (wa umri) gani (ng'ombe huyo)?" Akasema: "Hakika Yeye anasema kwamba ng'ombe huyo si mzee wala si mchanga, bali ni wa katikati baina ya hao. Basi fanyeni mnavyoarishwa". Wakasema: "Tuombee kwa Mola wako atupambanulie ni vipi hali yake, hakika ng'ombe wanafanana; (basi yupi)? Na kwa hakika kama Mungu akipenda (tutafuata) tuwe wenye kuongoka". Akasema: "Yeye anasema: Kuwa huyo si ng'ombe aliyetiwa kazini kulima ardhi wala kutilia maji mimea, safi kabisa rangi yake, hana kipaku ndani yake". Wakasema: "Sasa umeleta (maneno ya) haki". Basi wakamchinja, na walikuwa mbali na kufanya hayo". (2:67-71).



Pamoja na fundisho kuu tulilolitaja awali la kujenga hoja dhidi ya shirk; lakini pia aya zinatutanabahisha kuwa tusijaribu kuzikwepa amri za Allah(s.w) kwa kuleta maswali ya udadisi na visingizio. Maadhali jambo limethibiti kuwa ni amri ya Allah basi hatuna hiari bali ni kulitekeleza kwa moyo mkunjufu.



                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Quran Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 591


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

DARSA ZA QURAN
Soma Zaidi...

MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Ni nini maana ya Tajwid, na ni ipi nafasi yake kwenye uislamu
Hapa utajifunza maana ya Tajwid kilugha na kisheria. Pia nitakujuza jukumu ya kusoma tajwid. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat an-Nas na surat al Falaq
Sura mbili hizi pia hujulikana kwa jina la al muawidhatain ambazo ni surat an Nas na surat al falaq. Soma Zaidi...

Ni nini maana ya Idh-har katika usomaji wa Quran
Hapa utajifunza kuhusu hukumu ya Idh-har katika usomaji wa Quran. Soma Zaidi...

Aasbab Nuzul surat Ash sharh: sababu za kushuka alam nashrah (surat Ash sharh)
Makala hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa alam nasharah yaani Surat Ash sharh. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al Zilzalah
surat Zalzalah ni sura ya 99 katika mpangilio wa Quran, na ina aya 8. Sura hii imeteremshwa Madina ila pia kuna kauli zinathibitisha kuwa ni ya Makkah. Katika hadithi iliyopewa daraja la hassan na Imam Tirmidh Mtume S.A.W amesema kuwa kusoa surat Zilzalah Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat at Takaathur
Kuwa na tamaa huhitaji vitu vya watu si jambo jema. Ila kama tamaa hii itakuhamasisha na wewe kutafuta kitu hicho, kwa uwezo ambao Allah amekupa bila ha kuvuka mipaka yake, hili sio tatizo. Sura hii itakufundisha mengi Soma Zaidi...

Adabu za kusikiliza quran
ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI 1. Soma Zaidi...

Kulaaniwa Bani Israil
Pamoja na kuteuliwa na Allah(s. Soma Zaidi...