Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr.
Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr. Wakawa nao wanabuni miungu ya vitu vilivyo hai na visivyo hai. Moja ya miungu waliyoibuni ni ng'ombe mwenye sifa maalum. Asiye mzee sana wala mchanga, mwenye rangi ya dhahabu na asiyefanyishwa kazi. Kwa hiyo pamoja na kuwa baadhi ya Mayahudi walifuata sheria ya Musa(a.s), lakini bado athari ya ibada ya ng'ombe ikawa imesalia katika nafsi zao.
Katika mazingira hayo, Nabii Musa(a.s) alipewa amri na Mola wake awaamrishe wachinje ng'ombe. Huu ukiwa ni mtihani wa imani kwao kuthibitisha kwamba kweli wamemuamini Allah(s.w) au la. Mtihani huu ukawa mgumu sana kwao. Wakajaribu kuukwepa kwa kuleta maswali kadhaa ya udadisi. Lakini kila walivyozidi kudadisi juu ya ng'ombe waliyeambiwa wamchinje ndivyo walivyojiingiza mahali pagumu zaidi. Kwani majibu waliyokuwa wakiyapata yaliwataka wamchinje ng'ombe mwenye sifa sawa na yule wanayemuabudu. Basi hatima yake wakamchinja japo kwa shingo upande.
Fundisho lililokusudiwa lilipatikana kwani kile walichokidhania kitakatifu hata kukiabudu walikichinja kwa mikono yao wenyewe na wala hawakupata dhara lolote. Qur'an yabainisha tukio hili katika aya zifuatazo:
"Na Musa alipowaambia watu wake: "Hakika Mwenyezi Mungu anakuamrisheni mchinje ng'ombe". Wakasema: "Je! Unatufanyia mzaha?" Akasema "(La) Najikinga kwa Mwenyezi Mungu kuwa miongoni mwa wajinga. Wakasema: "Tuombee kwa Mola wako atupambanulie ni (wa umri) gani (ng'ombe huyo)?" Akasema: "Hakika Yeye anasema kwamba ng'ombe huyo si mzee wala si mchanga, bali ni wa katikati baina ya hao. Basi fanyeni mnavyoarishwa". Wakasema: "Tuombee kwa Mola wako atupambanulie ni vipi hali yake, hakika ng'ombe wanafanana; (basi yupi)? Na kwa hakika kama Mungu akipenda (tutafuata) tuwe wenye kuongoka". Akasema: "Yeye anasema: Kuwa huyo si ng'ombe aliyetiwa kazini kulima ardhi wala kutilia maji mimea, safi kabisa rangi yake, hana kipaku ndani yake". Wakasema: "Sasa umeleta (maneno ya) haki". Basi wakamchinja, na walikuwa mbali na kufanya hayo". (2:67-71).
Pamoja na fundisho kuu tulilolitaja awali la kujenga hoja dhidi ya shirk; lakini pia aya zinatutanabahisha kuwa tusijaribu kuzikwepa amri za Allah(s.w) kwa kuleta maswali ya udadisi na visingizio. Maadhali jambo limethibiti kuwa ni amri ya Allah basi hatuna hiari bali ni kulitekeleza kwa moyo mkunjufu.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Kujifunza tajwid ni katika mambo muhimu wakati wa kusoma Quran
Soma Zaidi...Je Qur-an ilikusanywa na kuandikwa katika msahafu wakati wa uongozi wa Abu-Bakr(r.
Soma Zaidi...SURATUN-NASR Sura hii imeteremka wakati Mtume (s.
Soma Zaidi...Mada zipo katika makundi mawili ambayo ni madda far-iy na mdada twab-iy.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu srat al fatiha, faida zake na maudhui zake
Soma Zaidi...