Menu



Khalifa na Uendeshaji wa Dola kwa ujumla, kulinda wasio waislamu na haki zao na mali zao.

Khalifa na Uendeshaji wa Dola kwa ujumla, kulinda wasio waislamu na haki zao na mali zao.

Khalifa na Uendeshaji wa Dola kwa ujumla



Khalifa ndiye mtendaji mkuu wa Serikali. Kwa hiyo jukumu lake la kwanza lilikuwa kuhakikisha kuwa maelekezo na amri za mamlaka kuu ya uendeshaji zinatekelezwa. Katika kuendesha shughuli za kila siku za Serikali alisaidiwa na shura – ambayo mfano wake katika Serikali za leo ni Baraza la Mawaziri au


Cabinet. Majlisi shura au Tume ya ushauri ilitumiwa na kila Khalifa katika makhalifa wanne wa Mtume(s.a.w). Hakukua na idadi maalumu ya wajumbe wa shura. Wajumbe hawa waliteuliwa na khalifa kwa misingi ya ucha Mungu na mchango wao katika Uislamu na kujitoa muhanga kwao. Miongoni mwao walikuwemo maswahaba maarufu wakiwemo Abubakar, Umar, Uthman, Ali Abdurahman bin Auf, Talha, Zubair, Saad Ibn Waqqas, Abu Ubaidah Ibn Jarrah na Said Ibn Zaid. Viongozi maarufu kutokana Muhajirin na Answar walijumuishwa kwenye shura.


Haki za wasiokuwa Waislamu chini ya uongozi wa Khalifa.


Uislamu una vumilia dini nyingine ingawa ni za kishirikina. Kwa hiyo wasio Waislamu, walitekeleza sheria zao kwa mujibu wa dini zao hasa katika masuala ya urithi, ndoa, talaka, namna ya kupata viongozi wao, uendeshaji wa ibada zao n.k. Kwa kweli walikuwa na uhuru kamili. Vile vile kama wangependa walikuwa na uhuru wa kupeleka kesi zao kwaKadhi(hakimu).Kesi inapopelekwa kwa hakimu haikuruhusiwa kuiondoa mahakamani.


Sheria ya makosa ya jinai, sheria ya ushahidi na mikataba iliwahusu Waislamu na wasio Waislamu. Katika kuwaadhibu wahalifu dhidi ya ubinaadamu kama uzinzi, mauaji, wizi, kupora, n.k. sheria ya Kiislamu ilitumika kwa Waislamu na wasio Waislamu.


Kama mzozo ulizuka baina ya Muislamu na asiye Muislamu kesi ya namna hii ilipelekwa mahakamani na utaratibu ulikuwa kama ifuatavyo: Katika masuala ya ubinaadamu asiye Muislamu alihukumiwa sawa na Muislamu. Kwa mfano kama asiye Muislamu amemuua Muislamu adhabu atayopewa ni sawa na ile, kama kosa lile lingefanywa na Muislamu.


Tukio la kihistoria lifuatalo linaonesha haki ilivyo katika Uislamu hata kama asiye Muislamu alimkosea Khalifa.


Wakati Khalifa Ali alipokuwa anaondoka kwenda katika vita vya Siffin - alipoteza zirah yake. Aliporudi toka vitani alimuona Myahudi mmoja na zirah yake. Khalifa alimuuliza yule Myahudi aliipataje ile zirah wakati ni yake na hajampa mtu wala hajaiuza. Yule Myahudi alijibu kijeuri: “Kwa kuwa ninayo mimi basi kiasili ni mali yangu”. Khalifa pamoja na kuwa ndiye mkuu wa Serikali hakuwa na jinsi isipokuwa kulikepeleka suala hili mahakamani. Kadhi Shurayb alimuuliza Khalifa aliyekuwa pamoja naye sababu ya kuwepo kwake pale mahakamani. Ndipo Khalifa akaeleza: “zirah aliyonayo huyu Myahudi ni yangu kwa vile sijampa mtu yeyote na sijaiuza”.


Yule Myahudi alipotakiwa kujieleza alieleza kuwa kwa kuwa zirah iko mkononi mwake basi ni mali yake. Hapo ndipo hakimu alipomtaka Khalifa atoe ushahidi, lakini alipotaka kuwaleta mwanae Hassan na mfanyakazi wake Qanbar kama mashahidi hakimu hakukubali ushahidi wao kutokana na uhusiano wao na Khalifa. Kwa hali hii Myahudi alishinda kesi na akaachiwa aende na ile zirah. Myahudi huyu alishangazwa na hali hii ya Khalifa kusimama mahakamani na raia wake tena wa dini nyingine na hata hivyo akashindwa kesi na akaridhika. Hali hii ilimfanya akiri kuwa ile zirah ni ya Khalifa akamrudishia na yeye akasilimu”.34




                   


Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 541


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Mbinu za Da’wah Alizotumia Nuhu(a.s)
Katika kufikisha ujumbe huu kwa watu wake Nuhu(a. Soma Zaidi...

Mafunzo ya sura zilizochaguliwa
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Tukio la kupasuliwa kifua Mtume Muhammad S.A.W
Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 7 Soma Zaidi...

CHANZO CHA VITA VYA VITA VYA AL-FIJAR NA ATHARI ZAKE
MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU). Soma Zaidi...

Uendeshaji wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA BANI ISRAIL
Nabii Musa na Harun walikuwa na kazi kubwa mbili; kwanza, kuwakomboa Bani Israil kutokana na dhuluma waliyokuwa wakifanyiwa na Firaun na Serikali yake, na pili, kuwarudisha kwenye nchi yao takatifu ya Palestina. Soma Zaidi...

Nabii Yunus(a.s) Amuomba Allah(s.w) Msamaha
Ndani ya tumbo la samaki, Nabii Yunus(a. Soma Zaidi...

Kuandaliwa Mtume(s.a.w) maandalizi ya kimafunzo na maandalizi ya ki ilham
Mitume huzaliwa Mitume. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SULEIMAN
Soma Zaidi...

Mapambano ya Dola ya kiislamu dhidi ya maadui wa kikristo (warumi) wakati wa Mtume
Soma Zaidi...