Hadithi Ya 29: Muabudu Allaah Na Usimshirikishe Na Chochote

Hadithi Ya 29: Muabudu Allaah Na Usimshirikishe Na Chochote

Hadithi Ya 29: Muabudu Allaah Na Usimshirikishe Na Chochote

الحديث التاسع والعشرون

"تعبد الله لا تشرك به شيئا"

عن معاذِ بن جبلٍ رضي الله عنه قال: قلت: يا رسول الله، أخْبِرني بِعَمَلٍ يُدْخِلُني الجنَةَ ويُبَاعِدُني عَنِ النارِ. قال: ((لَقَدْ سألْتَ عَنْ عَظيمٍ، وإنَهُ لَيَسيرٌ عَلى من يَسَّرَهُ اللهُ تعالى عَلَيْهِ : تَعْبُدُ اللهَ لا تُشْرِكُ بِهِ شَيئاً، وتُقيمُ الصَّلاةَ  ،وتُؤتي الزكاةَ، وتصومُ رمضانَ، وتَحُجُّ البيتَ)) .ثم قال:  (( ألا أَدُلُّكَ على أبْوَابِ الخيرِ؟: الصَّومُ جُنَّةٌ، والصَّدقةُ تُطْفِىءُ الخَطِيئةَ كما يُطْفىءُ الماءُ النارَ، وصَلاةَ الرَّجُلِ في جَوْفِ الَّليْلِ، ثم تلا: {تَتَجَافَى جُنُوبُهُمْ عَنْ الْمَضَاجِعِ} - حتى بلغ - {يَعْمَلُونَ}   السجدة: 16-17 .

ثم قال:  ((ألا أُخْبِرُكَ بِرَأسِ الأمْرِ وَعَمودِهِ وَذِرْوَةِ سَنَامِهِ؟)) قلتُ: بَلىَ يا رسول الله. قال:  (( رَأْسُ الأمْرِ الإسلامُ، وعَمُودُهُ الصَّلاةُ، وَذِرْوَةُ سَنَامِهِ الجِهادُ )).

ثم قال: (( ألا أخْبِرُكَ بِمِلاكَ ذَلِكَ  كلِّهِ ؟)) فَقُلْتُ بَلَى يا رَسول الله، فأخَذَ بِلِسانِهِ وقال:   ((كُفَّ عَلَيْكَ هذا)) . قلت : يا نبيَّ الله، وإنَّا لمؤاخَذُونَ بِما نَتَكَلَّمُ بِه ؟)) فقال: (( ثَكِلَتْكَ أمُّكَ يَا مُعَاذُ,  وَهَلْ يَكُبُّ الناسَ في النارِ على وُجُوهِهِمْ ))   أو قال: ((على مناخِرِهِم - إلاَّ حَصَائدُ  ألسِنَتهم))

 

رَوَاهُ التِّرْمِذِيُّ   وَقَالَ: حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ. 

 


HADITHI YA  29 MUABUDU ALLAAH  NA USIMSHIRIKISHE NA CHOCHOTE

 

Kutoka kwa  Mu'aadh Ibn Jabal رضي الله عنه  amesema:

Nilisema: Ewe Mtume صلى الله عليه وسلم  , niambie kitendo ambacho kitanipeleka peponi na kitaniokoa na moto.  Akasema : Umeniuliza jambo kubwa lakini ni rahisi kwa yule ambae Mola anaemsahilishia.   Muabudu Allaah wala usimshirikishe na chochote, Swali, toa Zaka, funga             Ramadhani, nenda kuhiji (Makka).  Kisha akasema:  Je? Nikuonyeshe  milango ya kheri?  Saumu ni ngao, sadaka inazima dhambi kama vile maji yanavyozima moto, na kuswali katikati ya usiku: Kisha akasoma  {Mbavu zao zinaachana na vitanda kwa kumwomba Mola wao Mlezi kwa khofu na kutumaini, na hutoa kutokana na tulivyo waruzuku. Nafsi yoyote haijui waliyo fichiwa katika hayo yanayo furahisha macho - ni malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda}

 Sura As-Sajda  32: 16 na 17

Tena akasema:  Je, nikwambie kilele cha hilo jambo; nguzo yake na sehemu yake ya juu kabisa?  Nikasema : Ndio ewe Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu.  Akasema:  kilele chake ni Uislamu, nguzo yake ni Swala na sehemu yake ya juu kabisa ni Jihaad.   Kisha akasema : Je, nikwambie muhimili wa yote haya?  Nikasema:  Ndio ewe Mjumbe  wa Mwenyeezi Mungu.   Akaukamata ulimi wake na akasema;  Uzuie huu.  Nilisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu; yale tunayoyasema tutahukumiwa  kwayo? Akasema:  mama yako akuhurumie ewe Mu'aadh!  Kuna kitu zaidi kinachowaangusha watu kifudifudi motoni kama si mavuno ya ndimi zao?

Imesimuliwa na At-Tirmidhi na ni hadithi Hasan.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 859

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Sura za kujikinga na Uchawi na mashetani

Post hii itakwenda kukufundisha sura katika Quran ambazo ni kinga dhidi ya Wachawi, uchawi na Masheitwani.

Soma Zaidi...
Uandishi wa hadithi wakati wa Matabii tabiina (tabiitabiina)

Hii ni historia ya uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina. Yaani wafuasi wa wale wafuasi wa Masahaba

Soma Zaidi...
Dua za kuomba wakati unapokuwa na maumivu kwenye mwili

Posti hii inakwenda kukufundisha dua za kuomba wakati wa kuwa na maumivu kwenye mwili wako.

Soma Zaidi...
MAANA YA HADITHI SUNNAH

Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila.

Soma Zaidi...
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA

NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA.

Soma Zaidi...
SWALA YA MTUME (s.a.w)

SWALA YA MTUME Kumswalia Mtume (s.

Soma Zaidi...
DUA 85 - 93

SWALA YA MTUME 85.

Soma Zaidi...
Adabu ya kukaa na kula katika nyumba za watu

"Si vibaya kwa kipofu, wala si vibaya kwa kiguru, wala si vibaya kwa mgonjwa, wala kwenu, kama mkila katika nyumba zenu, au nyumba za baba zenu, au nyumba za mama zenu, au nyumba za ndugu zenu, au nyumba za dada zenu, au nyumba za ami zenu, au nyumba za s

Soma Zaidi...
Haki za Muislamu kwa Muislamu mwenzie

Katika makala hii utakwenda kujifunza kuhusu haki za Muislamu kwa Muislamu mwenzie

Soma Zaidi...