الحديث التاسع والعشرون
"تعبد الله لا تشرك به شيئا"
عن معاذِ بن جبلٍ رضي الله عنه قال: قلت: يا رسول الله، أخْبِرني بِعَمَلٍ يُدْخِلُني الجنَةَ ويُبَاعِدُني عَنِ النارِ. قال: ((لَقَدْ سألْتَ عَنْ عَظيمٍ، وإنَهُ لَيَسيرٌ عَلى من يَسَّرَهُ اللهُ تعالى عَلَيْهِ : تَعْبُدُ اللهَ لا تُشْرِكُ بِهِ شَيئاً، وتُقيمُ الصَّلاةَ ،وتُؤتي الزكاةَ، وتصومُ رمضانَ، وتَحُجُّ البيتَ)) .ثم قال: (( ألا أَدُلُّكَ على أبْوَابِ الخيرِ؟: الصَّومُ جُنَّةٌ، والصَّدقةُ تُطْفِىءُ الخَطِيئةَ كما يُطْفىءُ الماءُ النارَ، وصَلاةَ الرَّجُلِ في جَوْفِ الَّليْلِ، ثم تلا: {تَتَجَافَى جُنُوبُهُمْ عَنْ الْمَضَاجِعِ} - حتى بلغ - {يَعْمَلُونَ} السجدة: 16-17 .
ثم قال: ((ألا أُخْبِرُكَ بِرَأسِ الأمْرِ وَعَمودِهِ وَذِرْوَةِ سَنَامِهِ؟)) قلتُ: بَلىَ يا رسول الله. قال: (( رَأْسُ الأمْرِ الإسلامُ، وعَمُودُهُ الصَّلاةُ، وَذِرْوَةُ سَنَامِهِ الجِهادُ )).
ثم قال: (( ألا أخْبِرُكَ بِمِلاكَ ذَلِكَ كلِّهِ ؟)) فَقُلْتُ بَلَى يا رَسول الله، فأخَذَ بِلِسانِهِ وقال: ((كُفَّ عَلَيْكَ هذا)) . قلت : يا نبيَّ الله، وإنَّا لمؤاخَذُونَ بِما نَتَكَلَّمُ بِه ؟)) فقال: (( ثَكِلَتْكَ أمُّكَ يَا مُعَاذُ, وَهَلْ يَكُبُّ الناسَ في النارِ على وُجُوهِهِمْ )) أو قال: ((على مناخِرِهِم - إلاَّ حَصَائدُ ألسِنَتهم))
رَوَاهُ التِّرْمِذِيُّ وَقَالَ: حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ.
Kutoka kwa Mu'aadh Ibn Jabal رضي الله عنه amesema:
Nilisema: Ewe Mtume صلى الله عليه وسلم , niambie kitendo ambacho kitanipeleka peponi na kitaniokoa na moto. Akasema : Umeniuliza jambo kubwa lakini ni rahisi kwa yule ambae Mola anaemsahilishia. Muabudu Allaah wala usimshirikishe na chochote, Swali, toa Zaka, funga Ramadhani, nenda kuhiji (Makka). Kisha akasema: Je? Nikuonyeshe milango ya kheri? Saumu ni ngao, sadaka inazima dhambi kama vile maji yanavyozima moto, na kuswali katikati ya usiku: Kisha akasoma {Mbavu zao zinaachana na vitanda kwa kumwomba Mola wao Mlezi kwa khofu na kutumaini, na hutoa kutokana na tulivyo waruzuku. Nafsi yoyote haijui waliyo fichiwa katika hayo yanayo furahisha macho - ni malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda}
Sura As-Sajda 32: 16 na 17
Tena akasema: Je, nikwambie kilele cha hilo jambo; nguzo yake na sehemu yake ya juu kabisa? Nikasema : Ndio ewe Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu. Akasema: kilele chake ni Uislamu, nguzo yake ni Swala na sehemu yake ya juu kabisa ni Jihaad. Kisha akasema : Je, nikwambie muhimili wa yote haya? Nikasema: Ndio ewe Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu. Akaukamata ulimi wake na akasema; Uzuie huu. Nilisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu; yale tunayoyasema tutahukumiwa kwayo? Akasema: mama yako akuhurumie ewe Mu'aadh! Kuna kitu zaidi kinachowaangusha watu kifudifudi motoni kama si mavuno ya ndimi zao?
Imesimuliwa na At-Tirmidhi na ni hadithi Hasan.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inakwenda kukifundisha nibhali zipi ukiwa nazo, basi dua yako kuhubaliwa kwa urahisi.
Soma Zaidi...Posti hii inakwenda kukufundisha ni kwa nini dua ya kafiri inawwza kujibiwa wakati ya muumini haijibiwi.
Soma Zaidi...DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani.
Soma Zaidi...Katika hadithi hii utakwenda kujifunza nguzo za uislamu
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukugundisha ni nyakati zipi ambazo Allah hukubali dua kwa urahisi.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukupa tahadhari juu ya mambo ya halali na mambo ya haramu.
Soma Zaidi...