image

Hadithi Ya 29: Muabudu Allaah Na Usimshirikishe Na Chochote

Hadithi Ya 29: Muabudu Allaah Na Usimshirikishe Na Chochote

Hadithi Ya 29: Muabudu Allaah Na Usimshirikishe Na Chochote

الحديث التاسع والعشرون

"تعبد الله لا تشرك به شيئا"

عن معاذِ بن جبلٍ رضي الله عنه قال: قلت: يا رسول الله، أخْبِرني بِعَمَلٍ يُدْخِلُني الجنَةَ ويُبَاعِدُني عَنِ النارِ. قال: ((لَقَدْ سألْتَ عَنْ عَظيمٍ، وإنَهُ لَيَسيرٌ عَلى من يَسَّرَهُ اللهُ تعالى عَلَيْهِ : تَعْبُدُ اللهَ لا تُشْرِكُ بِهِ شَيئاً، وتُقيمُ الصَّلاةَ  ،وتُؤتي الزكاةَ، وتصومُ رمضانَ، وتَحُجُّ البيتَ)) .ثم قال:  (( ألا أَدُلُّكَ على أبْوَابِ الخيرِ؟: الصَّومُ جُنَّةٌ، والصَّدقةُ تُطْفِىءُ الخَطِيئةَ كما يُطْفىءُ الماءُ النارَ، وصَلاةَ الرَّجُلِ في جَوْفِ الَّليْلِ، ثم تلا: {تَتَجَافَى جُنُوبُهُمْ عَنْ الْمَضَاجِعِ} - حتى بلغ - {يَعْمَلُونَ}   السجدة: 16-17 .

ثم قال:  ((ألا أُخْبِرُكَ بِرَأسِ الأمْرِ وَعَمودِهِ وَذِرْوَةِ سَنَامِهِ؟)) قلتُ: بَلىَ يا رسول الله. قال:  (( رَأْسُ الأمْرِ الإسلامُ، وعَمُودُهُ الصَّلاةُ، وَذِرْوَةُ سَنَامِهِ الجِهادُ )).

ثم قال: (( ألا أخْبِرُكَ بِمِلاكَ ذَلِكَ  كلِّهِ ؟)) فَقُلْتُ بَلَى يا رَسول الله، فأخَذَ بِلِسانِهِ وقال:   ((كُفَّ عَلَيْكَ هذا)) . قلت : يا نبيَّ الله، وإنَّا لمؤاخَذُونَ بِما نَتَكَلَّمُ بِه ؟)) فقال: (( ثَكِلَتْكَ أمُّكَ يَا مُعَاذُ,  وَهَلْ يَكُبُّ الناسَ في النارِ على وُجُوهِهِمْ ))   أو قال: ((على مناخِرِهِم - إلاَّ حَصَائدُ  ألسِنَتهم))

 

رَوَاهُ التِّرْمِذِيُّ   وَقَالَ: حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ. 

 


HADITHI YA  29 MUABUDU ALLAAH  NA USIMSHIRIKISHE NA CHOCHOTE

 

Kutoka kwa  Mu'aadh Ibn Jabal رضي الله عنه  amesema:

Nilisema: Ewe Mtume صلى الله عليه وسلم  , niambie kitendo ambacho kitanipeleka peponi na kitaniokoa na moto.  Akasema : Umeniuliza jambo kubwa lakini ni rahisi kwa yule ambae Mola anaemsahilishia.   Muabudu Allaah wala usimshirikishe na chochote, Swali, toa Zaka, funga             Ramadhani, nenda kuhiji (Makka).  Kisha akasema:  Je? Nikuonyeshe  milango ya kheri?  Saumu ni ngao, sadaka inazima dhambi kama vile maji yanavyozima moto, na kuswali katikati ya usiku: Kisha akasoma  {Mbavu zao zinaachana na vitanda kwa kumwomba Mola wao Mlezi kwa khofu na kutumaini, na hutoa kutokana na tulivyo waruzuku. Nafsi yoyote haijui waliyo fichiwa katika hayo yanayo furahisha macho - ni malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda}

 Sura As-Sajda  32: 16 na 17

Tena akasema:  Je, nikwambie kilele cha hilo jambo; nguzo yake na sehemu yake ya juu kabisa?  Nikasema : Ndio ewe Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu.  Akasema:  kilele chake ni Uislamu, nguzo yake ni Swala na sehemu yake ya juu kabisa ni Jihaad.   Kisha akasema : Je, nikwambie muhimili wa yote haya?  Nikasema:  Ndio ewe Mjumbe  wa Mwenyeezi Mungu.   Akaukamata ulimi wake na akasema;  Uzuie huu.  Nilisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu; yale tunayoyasema tutahukumiwa  kwayo? Akasema:  mama yako akuhurumie ewe Mu'aadh!  Kuna kitu zaidi kinachowaangusha watu kifudifudi motoni kama si mavuno ya ndimi zao?

Imesimuliwa na At-Tirmidhi na ni hadithi Hasan.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 431


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Dua za kuwaombea wazazi
Kwenye Quran kuna duaambazo Allah ametufundisha tuziombe kwa ajili ya wazazi, familia na kwa ajili yetu wenyewe. Soma Zaidi...

Hadithi Ya 25: Wenye Mali Wameondoka Na Fungu (jaza) Kubwa
Soma Zaidi...

DUA 32 - 40
32. Soma Zaidi...

Mipaka katika kumtii mzazi, na mambo yasiyopasa kumtii mzazi
Soma Zaidi...

Namna ya kumuosha maiti hatua kwa hatua, nguzo na sunnah za josho la maiti
1. Soma Zaidi...

Dua za wakati wa shida na taabu
Hizi ni Dua ambazo unatakiwa uziombe wakati wa shida na taabu Soma Zaidi...

SWALA YA MTUME (s.a.w)
SWALA YA MTUME Kumswalia Mtume (s. Soma Zaidi...

Hadithi Ya 40: Kuwa Duniani Kama Vile Mgeni Au Mpita Njia
Soma Zaidi...

Hadithi Ya 32: Kusiwe Na Kudhuriana Wala Kulipiza Dhara
الحديث الثاني والثلاثون "لا ضرر ولا ضرار" عَنْ أَبىِ سَعيدٍ سَعْدِ بْن مَالكِ بْن سِنَانٍ الْخُدريِّ رضي الله عنه  أَنَّ رَسُولَ اللّ?... Soma Zaidi...

DUA ZA WAKATI WA HASIRA
DUA ZA WAKATI UNAPOKUWA NA HASIRA. Soma Zaidi...

Dua sehemu ya 04
Soma dua mbalimbali za kila siku ambazo unatakiwa uzijuwe. Dua 120 ambazo muislamu anatakiwa kuzijua Soma Zaidi...

Matendo ('amal) hulipwa kutokana na nia (makusudio)
Soma Zaidi...