viapo

20.

20.Kujiepusha na Viapo



Waislamu tumekatazwa kuapa apa ovyo ovyo. Kiapo kinakubalika tu pale inapobidi kutolewa mbele ya Kadhi kama ushahidi. Mara nyingi mtu anayeapa apa ovyo ovyo ni muongo. Anaapa ili ahalalishe uwongo. Anahisi kuwa akisema bila kuapa watu hawatamuamini. Kuapa apa ovyo ni tabia ya kinafiki. Tunafahamishwa katika Qur-an kuwa wanafiki wakati wa Mtume (s.a.w) walikuwa wakificha ubaya wao dhidi ya Uislamu na Waislamu kwa kutoa viapo mbele ya Mtume (s.a.w). Lakini Allah (s.w) alimfahamisha Mtume wake kuwa asiamini viapo vyao kwani wao ni waongo.



21.Kujiheshimu na kuwaheshimu wengine


Katika Uislamu kila mtu anayo haki ya kuheshimiwa. Heshima ni haki ya mwanaadamu aliyozaliwa nayo. Miongoni mwa mambo ya msingi aliyousia Mtume (s.a.w) katika khutuba yake ya kuaga aliyoitoa katika uwanja wa Arafa 9 Dhul-Hijjah 10A.H, ni kulinda heshima ya kila mtu. Aliusia:
โ€œEnyi watu hakika damu yenu (yaani uhai wenu), mali zetu na heshima yenu ni vitu vitakatifu kamwe visiharibiwe hadi mtakaposimamishw a mbele ya Mola w enu, kw a utukufu w a vitu hivyo ni kama ulivyo Utukufu wa siku hii, na mwezi huu na mji huu. Kwa hakika mtakutana na Mola wenu na atakuulizeni juu ya vitendo vyema. Je, nimefikisha ujumbe? Ee! Allah shuhudia โ€.



Kutokanana usia huu kila Muumini analazimika kuwaheshimu wanaadamu wenzake wakubwa na wadogo. Aseme nao kwa uzuri, asiwadharau, asiwadhalilishe, asiwafedheheshe na asiwavunjie heshima kwa namna yoyote ile. Awatii wazazi, wenye mamlaka juu yake na walio wakubwa kwake katika mambo yote yanayowafikiana na Qur-an na Sunnah, awahurumie na kuwasikiliza walio chini yake au wadogo zake. Kwani Mtume (s.a.w) amesema:
โ€œSi katika sisi yule ambaye hamheshimu mkubwa wetu na kumhurumia mdogo wetu โ€.
Kuwaheshimu watu kama ilivyosisitizwa katika Qur-an ni pamoja


Kuzungumza na watu kwa kauli nzuri, kwa upole na huruma. Qur-an inatuamrisha:
โ€œ... Na semeni na watu kwa wema...โ€ (2:83).


(ii) Kuwatii wazazi, kuwahurumia na kusema nao kwa vizuri:


~ ~ ~
โ€œ... Na sema nao (wazazi) kwa msemo wa heshima (kabisa)โ€. (17:23).


โ€œNa wanapofika wale wanaoamini aya zetu wambie โ€œAssalaam alaykumโ€ (yaani amani iwe juu yenu)...โ€ (6:54)
(iv)Kurudishia saalam kwa ucheshi baada ya kusalimiwa:


โ€œNa mnapoamkiwa kwa maamkio yoyote yale; basi itikieni kwa yaliyo bora kuliko hayo, au rejesheni hayo hayo. (4:86)
(v)Kuwaheshimu watu wa dini nyingine kwa kutowabughudhi, kutowadharau au kutowadhalilisha kwa namna yoyote ile:


โ€œWala msiwatukane ambao wanaabudu kinyume cha Allah, was ije wakamtukana Allah kwa jeuri zao bila kujua....โ€ (6:108).


โ€œWaite (watu) katika njia ya Mola wako kw a hekima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora. Hakika Mola wako ndiye anayemjua aliyepotea katika njia yake.. (16:125).
(vi)Kuwakaribisha wageni na kuwapisha kwenye viti au nafasi ya kukaa:



โ€œEnyi mlioamini mnapoambiw a (katika mikutano): โ€œWafanyieni w asaa wenzenu katika (nafasi za) kukaaโ€, wafanyieni nafasi. Na Mwenyezi Mungu atakufanyieni nafasi (Duniani na Akhera). Na (hata) ikisemwa, โ€œSimameniโ€, (ondokeni muw apishe w enzenu), basi ondekeni. Mwenyezi Mungu atawainua wale walioamini miongoni mwenu, waliopewa elimu watapata daraja zaidi. Na Mwenyezi Mungu anazo habari za mnayoyatenda โ€. (58:11)



Ili mtu aheshimiwe hana budi kujiheshimu yeye mwenyewe na kuwaheshimu wengine.Mtu asiyejiheshimu hujidharaulisha yeye mwenyewe kwa wanaadamu wenzake. Muheshimiwa zaidi mbele ya Allah ni yule anayemheshimu na kumtii Allah (s.w) na Mtume wake.


โ€œ... Hakika aheshimiw aye sana miongoni mwenu mbele ya Allah ni yule amchaye Allah zaidi katika nyinyi. Kwa yakini Allah ni Mjuzi Mwenye habari(za mambo yote).โ€ (49:13)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 754

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰2 web hosting    ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    ๐Ÿ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Umbwaji wa mwanadamu kutoka Nutfa (tone la mbegu za uzazi), alaqah (tone la damu, mudgha (pande la nyama) na kuwa mtu kamili

ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ุนูŽุจู’ุฏู ุงู„ุฑูŽู‘ุญู’ู…ูŽู†ู ุนูŽุจู’ุฏู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุจู’ู†ู ู…ูŽุณู’ุนููˆุฏู ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ู‚ูŽุงู„ูŽ: ุญูŽุฏูŽู‘ุซูŽู†ูŽุง ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ...

Soma Zaidi...
jamii somo la 26

(vii)Hufanya bias hara na Allah (s.

Soma Zaidi...
Kitabu Cha Darsa za dua

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
Kitabu Cha Dua 120

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kitabu Cha Darsa za Funga

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
Je wajuwa kuwa jua hujizungurusha kwenye mhimili wake?

Tulipokuwa shule tulisoma kuwa jua halizunguruki, ila dunia ndio huzunguka jua.

Soma Zaidi...