image

viapo

20.

20.Kujiepusha na Viapo



Waislamu tumekatazwa kuapa apa ovyo ovyo. Kiapo kinakubalika tu pale inapobidi kutolewa mbele ya Kadhi kama ushahidi. Mara nyingi mtu anayeapa apa ovyo ovyo ni muongo. Anaapa ili ahalalishe uwongo. Anahisi kuwa akisema bila kuapa watu hawatamuamini. Kuapa apa ovyo ni tabia ya kinafiki. Tunafahamishwa katika Qur-an kuwa wanafiki wakati wa Mtume (s.a.w) walikuwa wakificha ubaya wao dhidi ya Uislamu na Waislamu kwa kutoa viapo mbele ya Mtume (s.a.w). Lakini Allah (s.w) alimfahamisha Mtume wake kuwa asiamini viapo vyao kwani wao ni waongo.



21.Kujiheshimu na kuwaheshimu wengine


Katika Uislamu kila mtu anayo haki ya kuheshimiwa. Heshima ni haki ya mwanaadamu aliyozaliwa nayo. Miongoni mwa mambo ya msingi aliyousia Mtume (s.a.w) katika khutuba yake ya kuaga aliyoitoa katika uwanja wa Arafa 9 Dhul-Hijjah 10A.H, ni kulinda heshima ya kila mtu. Aliusia:
“Enyi watu hakika damu yenu (yaani uhai wenu), mali zetu na heshima yenu ni vitu vitakatifu kamwe visiharibiwe hadi mtakaposimamishw a mbele ya Mola w enu, kw a utukufu w a vitu hivyo ni kama ulivyo Utukufu wa siku hii, na mwezi huu na mji huu. Kwa hakika mtakutana na Mola wenu na atakuulizeni juu ya vitendo vyema. Je, nimefikisha ujumbe? Ee! Allah shuhudia ”.



Kutokanana usia huu kila Muumini analazimika kuwaheshimu wanaadamu wenzake wakubwa na wadogo. Aseme nao kwa uzuri, asiwadharau, asiwadhalilishe, asiwafedheheshe na asiwavunjie heshima kwa namna yoyote ile. Awatii wazazi, wenye mamlaka juu yake na walio wakubwa kwake katika mambo yote yanayowafikiana na Qur-an na Sunnah, awahurumie na kuwasikiliza walio chini yake au wadogo zake. Kwani Mtume (s.a.w) amesema:
“Si katika sisi yule ambaye hamheshimu mkubwa wetu na kumhurumia mdogo wetu ”.
Kuwaheshimu watu kama ilivyosisitizwa katika Qur-an ni pamoja


Kuzungumza na watu kwa kauli nzuri, kwa upole na huruma. Qur-an inatuamrisha:
“... Na semeni na watu kwa wema...” (2:83).


(ii) Kuwatii wazazi, kuwahurumia na kusema nao kwa vizuri:


~ ~ ~
“... Na sema nao (wazazi) kwa msemo wa heshima (kabisa)”. (17:23).


“Na wanapofika wale wanaoamini aya zetu wambie “Assalaam alaykum” (yaani amani iwe juu yenu)...” (6:54)
(iv)Kurudishia saalam kwa ucheshi baada ya kusalimiwa:


“Na mnapoamkiwa kwa maamkio yoyote yale; basi itikieni kwa yaliyo bora kuliko hayo, au rejesheni hayo hayo. (4:86)
(v)Kuwaheshimu watu wa dini nyingine kwa kutowabughudhi, kutowadharau au kutowadhalilisha kwa namna yoyote ile:


“Wala msiwatukane ambao wanaabudu kinyume cha Allah, was ije wakamtukana Allah kwa jeuri zao bila kujua....” (6:108).


“Waite (watu) katika njia ya Mola wako kw a hekima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora. Hakika Mola wako ndiye anayemjua aliyepotea katika njia yake.. (16:125).
(vi)Kuwakaribisha wageni na kuwapisha kwenye viti au nafasi ya kukaa:



“Enyi mlioamini mnapoambiw a (katika mikutano): “Wafanyieni w asaa wenzenu katika (nafasi za) kukaa”, wafanyieni nafasi. Na Mwenyezi Mungu atakufanyieni nafasi (Duniani na Akhera). Na (hata) ikisemwa, “Simameni”, (ondokeni muw apishe w enzenu), basi ondekeni. Mwenyezi Mungu atawainua wale walioamini miongoni mwenu, waliopewa elimu watapata daraja zaidi. Na Mwenyezi Mungu anazo habari za mnayoyatenda ”. (58:11)



Ili mtu aheshimiwe hana budi kujiheshimu yeye mwenyewe na kuwaheshimu wengine.Mtu asiyejiheshimu hujidharaulisha yeye mwenyewe kwa wanaadamu wenzake. Muheshimiwa zaidi mbele ya Allah ni yule anayemheshimu na kumtii Allah (s.w) na Mtume wake.


“... Hakika aheshimiw aye sana miongoni mwenu mbele ya Allah ni yule amchaye Allah zaidi katika nyinyi. Kwa yakini Allah ni Mjuzi Mwenye habari(za mambo yote).” (49:13)




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 255


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

KULA HALALI NA ZILICHO KIZURI NI AMRI KATIKA UISLAMU
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم "إنَّ اللَّهَ طَيِّبٌ لَا يَقْبَلُ إلَّا طَي... Soma Zaidi...

Zingatio:
Swala husimama kwa kuhifadhiwa na kuswaliwa kwa khushui na kudumu na swala katika maisha yote. Soma Zaidi...

Kujiepusha na Chuki na Uadui
26. Soma Zaidi...

Zoezi - 4
Soma Zaidi...

Zijuwe Faida za Kuwa na Istiqama (Msimamo Thabiti)
38. Soma Zaidi...

Zoezi la 3
Kipengele hichi kina maswali mbalimbali kuhusiana na dini na mitazamo mbalimbali. Soma Zaidi...

tawhid
Soma Zaidi...

Kuepuka mabishano na madhara ya kugombana
16. Soma Zaidi...

Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba wa mtume (s.a.w)
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Husaidia wenye matatizo katika jam ii
Huwa wepesi wa kutoa msaada kwa hali na mali kwa wanaadamu wenziwe wanaohitajia msaada. Soma Zaidi...

swali langu nikwamba Mimi nimeolewa make wa pili nimeishi ndaniya ndoa miaka 22 mume akafikwa na mauti je ninahaki ya kupata mirathi?
Ni ipi haki ya mwanamke kwenye mirathi endapo atafiwa na mume wake, ilihali yeye ni mke wa pili? Soma Zaidi...

Zoezi
Maswali mbalimbali yanayohusu elimu ya dini ya kiislamu na mwongozo wa elimu na elimu mazingira. Soma Zaidi...