Nini maana ya Uchoyo, na madhara yake kwenye jamii

Nini maana ya Uchoyo, na madhara yake kwenye jamii

31.

Download Post hii hapa

Nini maana ya Uchoyo, na madhara yake kwenye jamii

31. Kuepuka Uchoyo na Ubahili



Uchoyo na ubahili ni kinyume cha ukarimu. Mtu mchoyo ana kasoro katika imani yake. Anaona kuwa chochote alichonacho amekipata kwa jitihada na akili yake tu. Pia anahofu kuwa akitoa kumpa mwingine atapungukiwa au atafilisika. Mtume (s.a.w) anatutanabahisha katika Hadithi zifuatazo:



Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Mtu anasema: “Hiki changu! Hiki changu! Lakini ukweli ulivyo ni kwamba, vilivyo vyake katika mali yake ni vitu vitatu: “Kile alichokula au nguo aliyoivaa ikachakaa au kile alichokitoa sadaqa (hakika) amekiweka akiba, na kingine chochote zaidi ya hivi, hakika si vyake (si vyenye kumfaa) na ataondoka awaachie watu ”. (Muslim)



Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Chakula cha watu wawili kina watosha watu watatu, na chakula cha watu watatu kinawatosha watu wanne”.(Bukhari na Muslim)



Jabir bin Abdullah (r.a) ameeleza: Mtume w a Allah amesema: “Chakula cha mtu mmoja kinawatosha watu wawili na chakula cha watu wawili


kinawatosha watu wanne na chakula cha watu wanne kinawashibisha watu wanane”. (Muslim).
Hivyo ukizingatia Hadithi hizi, utaona kuwa hapana sababu ya Muislamu kuwa mchoyo au bahili. Uchoyo na ubahili ni tabia mbaya na malipo yake ni kwenda Motoni kama inavyobainishwa katika Qur-an:


Yule anayetoa (zaka na sadaka) na kumcha Mwenyezi Mungu. Na kusadiki jam bo jem a (akalifuata). Tutamsahilishia njia ya kw enda Peponi. Na afanyae ubakhili, asiwe na haja ya viumbe wenzake, na akakadhibisha mambo mema (asiyafanye). Tutamsahilishia njia ya kwendea Motoni. Na mali yake haitamfaa atakapokuwa anadidimia (Motoni humo). (92:5-11).




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 2161

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina
Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
HISTORIA YA UANDISHI WA HADITHI
HISTORIA YA UANDISHI WA HADITHI

Historia fupi ya uandishi wa Hadith za Mtume (s.

Soma Zaidi...
quran na sayansi
quran na sayansi

2:UUMBWAJI KWA MAJI YA UZAZIUumbwaji wa mwanadamu umepitia hatua mbalimbali na haya yote yamefanywa kwa sababumaalumu ili tipate mazingatio.

Soma Zaidi...
NENO LA AWALI
NENO LA AWALI

Darasa la elimu inayohusu ujauzito na namna ya kulea mimba

Soma Zaidi...
 Umbwaji wa mwanadamu kutoka Nutfa (tone la mbegu za uzazi), alaqah (tone la damu, mudgha (pande la nyama) na kuwa mtu kamili
Umbwaji wa mwanadamu kutoka Nutfa (tone la mbegu za uzazi), alaqah (tone la damu, mudgha (pande la nyama) na kuwa mtu kamili

عَنْ أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: حَدَّثَنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم ...

Soma Zaidi...
nini maana ya Unafiki na sifa za unafiki katika quran na sunnah
nini maana ya Unafiki na sifa za unafiki katika quran na sunnah

Mnafiki ni yule anayeukubali Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha.

Soma Zaidi...