image

Nini maana ya Uchoyo, na madhara yake kwenye jamii

31.

Nini maana ya Uchoyo, na madhara yake kwenye jamii

31. Kuepuka Uchoyo na Ubahili



Uchoyo na ubahili ni kinyume cha ukarimu. Mtu mchoyo ana kasoro katika imani yake. Anaona kuwa chochote alichonacho amekipata kwa jitihada na akili yake tu. Pia anahofu kuwa akitoa kumpa mwingine atapungukiwa au atafilisika. Mtume (s.a.w) anatutanabahisha katika Hadithi zifuatazo:



Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Mtu anasema: “Hiki changu! Hiki changu! Lakini ukweli ulivyo ni kwamba, vilivyo vyake katika mali yake ni vitu vitatu: “Kile alichokula au nguo aliyoivaa ikachakaa au kile alichokitoa sadaqa (hakika) amekiweka akiba, na kingine chochote zaidi ya hivi, hakika si vyake (si vyenye kumfaa) na ataondoka awaachie watu ”. (Muslim)



Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Chakula cha watu wawili kina watosha watu watatu, na chakula cha watu watatu kinawatosha watu wanne”.(Bukhari na Muslim)



Jabir bin Abdullah (r.a) ameeleza: Mtume w a Allah amesema: “Chakula cha mtu mmoja kinawatosha watu wawili na chakula cha watu wawili


kinawatosha watu wanne na chakula cha watu wanne kinawashibisha watu wanane”. (Muslim).
Hivyo ukizingatia Hadithi hizi, utaona kuwa hapana sababu ya Muislamu kuwa mchoyo au bahili. Uchoyo na ubahili ni tabia mbaya na malipo yake ni kwenda Motoni kama inavyobainishwa katika Qur-an:


Yule anayetoa (zaka na sadaka) na kumcha Mwenyezi Mungu. Na kusadiki jam bo jem a (akalifuata). Tutamsahilishia njia ya kw enda Peponi. Na afanyae ubakhili, asiwe na haja ya viumbe wenzake, na akakadhibisha mambo mema (asiyafanye). Tutamsahilishia njia ya kwendea Motoni. Na mali yake haitamfaa atakapokuwa anadidimia (Motoni humo). (92:5-11).




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1041


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

jamii somo la 34
Soma Zaidi...

Aina za hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Zoezi la 5
Maswali mbalimbali kuhusu fiqih Soma Zaidi...

HADITHI YA MZEE WA KWANZA NA MBUZI
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA MZEE WA KWANZA NA MBUZI WAKE. Soma Zaidi...

Zoezi - 3:
1. Soma Zaidi...

jamii zoezi
Zoezi 2:1 1. Soma Zaidi...

Umbwaji wa mwanadamu kutoka Nutfa (tone la mbegu za uzazi), alaqah (tone la damu, mudgha (pande la nyama) na kuwa mtu kamili
عَنْ أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: حَدَّثَنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم ... Soma Zaidi...

tawhid
Soma Zaidi...

Uandishi wa hadithi wakati wa tabiina (wafuasi wa maswahaba)
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maswali juu ya hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya) Soma Zaidi...

jamii somo la 26
(vii)Hufanya bias hara na Allah (s. Soma Zaidi...

quran na sayansi
2:UUMBWAJI KWA MAJI YA UZAZIUumbwaji wa mwanadamu umepitia hatua mbalimbali na haya yote yamefanywa kwa sababumaalumu ili tipate mazingatio. Soma Zaidi...