image

tamaa

33.

33. Kuepuka Tamaa na Kuombaomba



Kinyume cha kutosheka ni kuwa na tamaa au kutotosheka. Kutotosheka ni ufakiri wa moyo. Moyo wa kutotosheka huzaa tabia nyingi mbaya ikiwa ni pamoja na upupiaji mali, husuda, uchoyo, na kuomba omba. Muislamu anatakiwa ajitahidi kutosheka na alichonacho na hata kama anahisi yuko katika dhiki ajitahidi kujizuilia kunyoosha mkono wa kuomba chochote kwa yeyote kwa kadiri iwezekanavyo.
Tumekatazwa katika Qur-an kutamani vitu vya watu:


“Wala msitam ani vile am bavyo Mw enyezi Mungu am ew afadhilisha baadhi yenu kuliko wengine. Wanaume wanayo sehemu (kamili) ya vile walivyovichuma; na wanawake nao wanayo sehemu (kamili) ya vile


w alivyovichuma;. Na mw ombeni Mwenyezi Mungu fadhila zake.Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.” (4:32).
Kuhusu suala la omba omba Mtume (s.a.w) ametuusia katika Hadithi zifuatazo:
Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Yule aombaye ili aongezee mali yake, haombi lingine ila moto wa maisha. (Muslim).
Ibn Umar (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: “Kama mmoja wenu ataomba bila ya sababu ya msingi atakutana na Allah na uso usiokuwa na nyama ”. (Bukhari na Muslim)



Ibn Umar (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah alipokuwa Mimbarini akitoa khutba juu ya kutoa sadaqa na kujizuia na kuomba omba alisema: “Mkono wa juu ni bora kuliko mkono wa chini. Mkono wa juu ni ule unaotoa na wa chini ni ule unaoomba”. (Bukhari na Muslim).
Kuomba kunaruhusiwa kwa dharura zifuatazo:



(i)Mtu aliyesimama kumdhamini mtu mwingine ili kuleta suluhu kati ya wagomvi wawili huyu anaruhusiwa kuomba hata akiwa tajiri. Kwa mnasaba huu, wadhamini wa Misikiti, madrasa, na shughuli mbali mbali za Kiislamu wanaruhusiwa kuomba michango ya Waislamu ili kufanikisha shughuli hizo.
(ii)Mtu aliyepata ajali na kuharibikiwa kabisa vitu vyote kama vile ajali ya moto, mafuriko, n.k.



(iii)Mtu ambaye amepigwa na ufukara na amekosa kabisa mahitaji muhimu ya maisha kama chakula, malazi na makazi. Lakini mtu akiwa kama na angalau chakula cha siku moja na malazi na akawa na dirham 50 mkononi mwake haruhusiwi kuomba kama tunavyofahamishwa katika Hadithi zifuatazo:



Abdullah bin Mas ’ud (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: Anayeomba omba watu na ilhali ana mahitaji muhimu ya maisha atakuja siku ya Kiyama na kuomba omba kwake kama mikwaruzo, vidonda au majeraha usoni mwake. Iliulizwa: Ee Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni kiasi gani kinachomtosha mtu? Akajibu: Dirham 50 au thamani yake ya dhahabu (Abu Daud, Tirmidh, Nasai na Ibn Majah)



Sahl (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Yeyote yule anayeomba na ilihali anajitosheleza kw a mahitaji muhimu, anaomba


moto (Jahannam). Nufali (r.a) ambaye ni miongoni mwa wasimulizi wa hadithi hii katika sehemu nyingine aliuliza: Ni yupi mwenye uwezo ambaye kuomba ni haram? Akajibu Mtume (s.a.w): Yule mwenye uwezo wa kupata chakula cha asubuhi na usiku. Mahali pengine amesema: Yule mwenye chakula cha siku moja (Usiku na mchana). (Abu Daud).





                   




           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 59


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Kazi ya madini mwilini
Posti hii inakwenda kukueleza kuhusu kazi za madini mwilini Soma Zaidi...

Kwanini mbu hawezi kuambukiza ukimwi
Somo Hili linakwenda kukueleza sababu za kwanini mbu hawezi kuambukiza ukimwi Soma Zaidi...

Je, utamsaidia vipi mtu aliyeumwa na nyuki?
Posti hii inazungumzia kuhusiana na kumsaidia mwenye aliyeumwa na nyuki.nyuki na wadudu ambao wakikushambulia Sana na ukikosa msaada unaweza kufa au kuwa katika Hali mbaya. Soma Zaidi...

Aina za mishipa inayosafilisha damu mwilni
Post hii inahusu zaidi mishipa inayosafilisha damu mwilni, ni Aina tatu za mishipa ambazo usafilisha damu kutoka sehemu Moja kwenda nyingine Soma Zaidi...

Mambo yanayopunguza nguvu za kiume
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Mambo yanayopunguza nguvu za kiume Soma Zaidi...

Mbinu za kuondoa sumu mwilini.
Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuondoa sumu mwilini, ni njia mbalimbali ambazo uweza kutumika ili kuondoa sumu mwilini. Soma Zaidi...

Utaratibu wa lishe kwa wajawazito na wanaonyonyeaha
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wajawazito na wanaonyonyesha Soma Zaidi...

Upungufu wa vitamin
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vitamin Soma Zaidi...

Jifunze kuhusu msukumo wa damu kwa kitaalamu huitwa pressure
Kupanda kwa msukumo wa damu ni ktendo ambapo moyo husukuma damu kwa nguvu kuliko kawaida ambapo hupelekea matatizo mengi kwenye mwili Soma Zaidi...

Mambo yanayosababisha kupona kwa vidonda.
Posti hii inahusu mambo yanayochangia katika kupona kwa kidonda, ni mambo ambayo yapo kwa mgonjwa mwenyewe kama ifuayavyo. Soma Zaidi...

Matokeo ya maumivu makali.
Posti hii inahusu zaidi matokeo ya maumivu makali , kuna wakati mwingine mgonjwa anapata maumivu makali ya viungo na dawa mbalimbali uweza kutolewa kwa mgonjwa huyo lakini matokeo yake huwa ni kuendelea kwa maumivu kwa hiyo yafuatayo ni matokeo ya maumivu Soma Zaidi...

Upungufu wa vyakula vya madini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula vya madini Soma Zaidi...