Navigation Menu



image

tamaa

33.

33. Kuepuka Tamaa na Kuombaomba



Kinyume cha kutosheka ni kuwa na tamaa au kutotosheka. Kutotosheka ni ufakiri wa moyo. Moyo wa kutotosheka huzaa tabia nyingi mbaya ikiwa ni pamoja na upupiaji mali, husuda, uchoyo, na kuomba omba. Muislamu anatakiwa ajitahidi kutosheka na alichonacho na hata kama anahisi yuko katika dhiki ajitahidi kujizuilia kunyoosha mkono wa kuomba chochote kwa yeyote kwa kadiri iwezekanavyo.
Tumekatazwa katika Qur-an kutamani vitu vya watu:


“Wala msitam ani vile am bavyo Mw enyezi Mungu am ew afadhilisha baadhi yenu kuliko wengine. Wanaume wanayo sehemu (kamili) ya vile walivyovichuma; na wanawake nao wanayo sehemu (kamili) ya vile


w alivyovichuma;. Na mw ombeni Mwenyezi Mungu fadhila zake.Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.” (4:32).
Kuhusu suala la omba omba Mtume (s.a.w) ametuusia katika Hadithi zifuatazo:
Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Yule aombaye ili aongezee mali yake, haombi lingine ila moto wa maisha. (Muslim).
Ibn Umar (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: “Kama mmoja wenu ataomba bila ya sababu ya msingi atakutana na Allah na uso usiokuwa na nyama ”. (Bukhari na Muslim)



Ibn Umar (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah alipokuwa Mimbarini akitoa khutba juu ya kutoa sadaqa na kujizuia na kuomba omba alisema: “Mkono wa juu ni bora kuliko mkono wa chini. Mkono wa juu ni ule unaotoa na wa chini ni ule unaoomba”. (Bukhari na Muslim).
Kuomba kunaruhusiwa kwa dharura zifuatazo:



(i)Mtu aliyesimama kumdhamini mtu mwingine ili kuleta suluhu kati ya wagomvi wawili huyu anaruhusiwa kuomba hata akiwa tajiri. Kwa mnasaba huu, wadhamini wa Misikiti, madrasa, na shughuli mbali mbali za Kiislamu wanaruhusiwa kuomba michango ya Waislamu ili kufanikisha shughuli hizo.
(ii)Mtu aliyepata ajali na kuharibikiwa kabisa vitu vyote kama vile ajali ya moto, mafuriko, n.k.



(iii)Mtu ambaye amepigwa na ufukara na amekosa kabisa mahitaji muhimu ya maisha kama chakula, malazi na makazi. Lakini mtu akiwa kama na angalau chakula cha siku moja na malazi na akawa na dirham 50 mkononi mwake haruhusiwi kuomba kama tunavyofahamishwa katika Hadithi zifuatazo:



Abdullah bin Mas ’ud (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: Anayeomba omba watu na ilhali ana mahitaji muhimu ya maisha atakuja siku ya Kiyama na kuomba omba kwake kama mikwaruzo, vidonda au majeraha usoni mwake. Iliulizwa: Ee Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni kiasi gani kinachomtosha mtu? Akajibu: Dirham 50 au thamani yake ya dhahabu (Abu Daud, Tirmidh, Nasai na Ibn Majah)



Sahl (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Yeyote yule anayeomba na ilihali anajitosheleza kw a mahitaji muhimu, anaomba


moto (Jahannam). Nufali (r.a) ambaye ni miongoni mwa wasimulizi wa hadithi hii katika sehemu nyingine aliuliza: Ni yupi mwenye uwezo ambaye kuomba ni haram? Akajibu Mtume (s.a.w): Yule mwenye uwezo wa kupata chakula cha asubuhi na usiku. Mahali pengine amesema: Yule mwenye chakula cha siku moja (Usiku na mchana). (Abu Daud).





                   







           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 317


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zifazofanana:-

Nna swali mimi nimefanya Romance na mtu ambaye sijampima kbsa sasa naogopa anaeza kuwa mgonjwa na mm nkaupata
Muulizaji anauliza he kula denda, ama kumbusu ama kufanya romance na muathirika was HIV na wewe uta ambukizwa? Soma Zaidi...

Ratiba ya chanjo ya kifua kikuu
Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia kifua kikuu, hiii ni ratiba ambayo chanjo hii utolewa na ushauri mbalimbali utolewa ili kuweza kufanikisha kazi ya chanjo hii Soma Zaidi...

Namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa
Posti hii inahusu namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa,ni njia unazopaswa kufuata wakati unamsafisha mgonjwa kinywa hasa wale walio mahututi. Soma Zaidi...

Kazi ya chanjo ya Surua
Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya Surua kwa watoto, ni Aina ya chanjo ambayo utolewa kwa watoto na kufanya kazi mbalimbali mwilini ambazo ni kumkinga mtoto asipatwe na magonjwa. Soma Zaidi...

Sababu za kumwosha Mgonjwa mwili mzima.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kumwosha Mgonjwa mwili mzima,ni sababu ambazo umsaidie mgonjwa ili aweze kupata nafuu mapema na kumsaidia kama tutakavyoona hapo chini Soma Zaidi...

Kazi za vitamin B na makundi yake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu kazi za vitamin B na makundi take Soma Zaidi...

Njia za kujikinga na vidonda vya tumbo
Kama unahitaji kujuwa namna ya kuweza kujikinga na vidonda vya tumbo, basi makala hii ni kwa ajili yako. Hapa utaweza kuzijuwa hatuwa zote za kujikinga na kupata vidonda vya tumbo. Soma Zaidi...

Njia za kujikinga na UTI
Somo hili linakwenda kukuletea njia za kujikinga na UTI Soma Zaidi...

Je unaweza ukapona macho kama huoni vizuri kwa sababu ya vitamini A,
Jiamini A ni katika vitamini inayojulikana sana kuboresha na kuimarisha afya vya macho na uoni. Tafiti zinaonyesha kuwa kuna kundi kubwa la watoto wanaopata tayizobla kutokuona kutokana na ukosefu wa vitamini A vya kutosha. Soma Zaidi...

Mambo ya kuzingatia unapokuwa unatoa huduma ya kwanza
Huduma ya kwanza ni huduma inayotolewa kwa mtu yeyote aliyepata ajali au mgonjwa yeyote kabla hajapelekwa hospitalini Soma Zaidi...

Kazi za mifupa mwilinj
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa mifupa mwilini, mifupa ni mojawapo ya tushy zilizounganika na ufanya kazi kubwa kwenye mwili. Soma Zaidi...

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPATWA NA KWIKWI
Kwikwi sio hatari sana kwa afya, lakini inaweza kuwa hatari zaidi kwa mu aliyefanyiwa upasuaji kwenye tumbo. Soma Zaidi...