image

HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

SURA YA SABA
HUKUMU ZA TAFKHIM NA TARQIQ AT-TAFKHIYM NA AT-TARQIYQ
1.At-Tarqiyq - Kufanya Nyembamba au Nyepesi
Ni kuitamka herufi kwa kuifanya nyembaba au nyepesi. Hali hii hutokea wakati ulimi uanapokuwa mbali na sakafu la kinywa yaani ulimu unakuwa chini. Tarqiyq hutokea katika herufi za chini yaani إسْتِفال (isfal-herufi za kuinamisha) isipokuwa isipokuwa herufi mbili ر na ل.
2.At-Tafkhiym - Kufanya Nene Au Nzito
Hutokea pale inapotamkwa herufi kwa kuifanya kuwa nene au nzito. Hukumu hii hutokea kwa zile hurufi za اٌلإسْتِعْلاء al-isti’ala yaani herufi za kupanda. Herufi hizi hutamkwa wakati ulimu unapokuwa juu ya sakafu la kinywa.
TAFKHEEM

3.Baina ya Tafkhiym na Tarqiyq
Kuna baadhi ya herufi zinaweza kubeba hukumu zote mbili zilizotajwa hapo juu. Yaani wakati mwingine huwa taeqitq na wakati mwingine huwa tafkheem. Herufi hizo ni kama;-
i) Alif ( ا ) ya madd
ii) Laam ( ل ) ya Lafdhw Al-Jalaalah ( (لله
iii) Raa ( ر)
Laam ( ل ) ya Lafdhw Al-Jalaalah
Kawaida herufi ya ل ni nyepesi ila inapotokea katika jina la Allaah ( ,(سبحانه وتعالى hapo huwa ima ni tafkhiym au tarqiyq kutegemea na i’raab inayotangulia. Ikiwa jina la Allaah ( سبحانه وتعالى ) Limetanguliwa na herufi ya kasrah au ي (yaa) saakinah, hutamkwa kwa tarqiyq. Ama jina la Allaah ( (سبحانه وتعالى Linapotanguliwa na fat-hah, dhwammah au و (waaw) saakinah linatamkwa kwa tafkhiym.
TAFKHEEM

At-Tafkhiym na At-Tarqiyq katika ( ر ) Raa
Halikadhalika herufi hii raa inaweza kuwa nzito au nyepesi, nene au nyembamba kulingana na kanuni za tajweed. Hivyo basi itakuwa tafkhiym katika hali zifuatazo;-
1.itakapokuwa ina fataha au dhummah
2.Inakapokuwa na sakinah na nyuma yake kuna herufi yenye fataha au dhumah
3.Itakapokuwa na sakinah na nyuma yake kukawa na kasra na mbele yake kukawa na herufi za isti’laa
4.Itakapokuwa ina sakina na nyuma yake kukawa na hamzatul-waswl yaani hamza ya kuungia.
5.Itakaposimamiwa kwa sakina halafu nyuma yake kukawa na sakina na nyuma ya hiyo sakina kukawa na fataha au dhumah.

Pia itakuwa nyepezi au nyembaba itakapokutana na hali zifuatazo;-
1.itakapokuwa na kasra
2.Itakapokuwa na sakina na nyuma yake kuna fataha
3.Itakaposimamiwa na sakina na kukawa nyuma yake kuna sakina iliyotanguliwa na kasra.
4.- 5 Inayoitwa الراء الممالة (ar-raa al-mumaalah) ambayo inasomwa kwa vokali ya ‘e’ badala ya kasrah. Hii ni kutokana na riwaayah ya Hafsw ‘an Aaswim. Nayo ni katika neno la pekee katika Qur-aan, na huwa ni ya tarqiyq inapatikana katika surat hud aya ya 41 (11:41)


                   



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 432


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Maisha ya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 19. Hapa utajifunza maisha ya Mtume kabla ya utume. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat al_ikhlas (qul huwallahu) na fadhila zake
3. Soma Zaidi...

HUKUMU ZA QALQALA
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Maswali yanayohusu quran
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Sababu za kushuka Surat al Kafirun
Sura hii imekuja kukata rai ya Makafiri wa Makka kuhusu ibada ya ushirika. Hivi leo tungesema kuhusu dini mseto. Soma Zaidi...

Ni zipi hukumu za nuni yenye sakina au tanwin?
Hapa utajifunza usomaji wa Quran pindi utakapokuta nuni yenyebsakina au tanwin Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al-Fiyl
Al fiyl ni neno la Kiarabu lenye maana ya tembo. Sura hii inazungumziakisa cha jeshi lenye tembo. Jeshi hili lilikuwa na nia ya kuvunja al qaaba Soma Zaidi...

Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid
Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo. Soma Zaidi...

Saratul-asr 103
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Asbab nuzul surat at Tin, Sababu za kushuka surat at Tin (watin wazaitun)
Post hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa surat at Tin (watin wazaitun). Soma Zaidi...

HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...