fadhila za kusoma quran

fadhila za kusoma quran

Fadhila na umuhimu wa kusoma quran 1.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

fadhila za kusoma quran

Fadhila na umuhimu wa kusoma quran
1.quran ni kamba,ponyo,kinga,nuru na ni kitu chenye kuokoa.
Kwa ufupi unaweza kusema qurani ina kila kitu ambacho tunakihitajia katika maisha yetu. Qurani inaweza kutumika kama tiba ya kuondoa maradhi ana kinga dhidi ya maradhi, uadui na husda. Pia ni nuru inayoweza kumuongoza mtu wapi apite. Qurani humkinga mtu na maadui, maradhi, husda na kila kitu kubada. Maneno haya unaweza kuyakuta katika hadithi ndeefu aliyoipokea al-haakim katika mapokeza ya ‘Ablahhah Ibn Mas’ud kuwa Mtume amesema “……hakika hii qurani ni kamba ya Allah, na ni nuru iliyo wazi, na ni pozo lenye kunufaisha, na ni ngome (ya kujikinga) kwa mwenye kushikamana nayo na ni kitu chenye kuokoa kwa mwenye kuifuata.…..”

2.Qurani ni yenye kuombea shifaa siku ya qiyama.
Watu watakuwa katika hali na wakati mgumu siku ya qiyama. Katika tabu za namna hiyo qurani itakuwa ni yenye kuwaombea watu wake wapate shifaa mbele ya Allah. Amasimulia Abuu Umamah kuwa “nimemsikia Mtume akisema ‘isomeni qurani, kwani hakika itakuja siku ya kiyama hali yakuwa ni yenye kuwaombea watu wake’” (amepokea Muslin)

3.Ukisoma herufi moja unaandikiwa mema (thawabu) 10.
Amesimulia Ibn msud kuwa mtume amesema “mwenye kusoma herufi moja katika kitabu cha Allah atapata jema moja, na jema moja hulipwa kwa mara kumi kwa mfano wake.…”(amepokea Tirmidh). Katika muendelezo wa hadithi Mtume anasema ukisema ALM hizi ni herufi tatu, hivyo kila moja hulipwa kwa kumi.

4.Wenye kusoma qurani ndio watu bora.
Mtume amewapa nafasi kubwa sana watu ambao wanaisoma qurani. Katika masimulizi ya ‘Uthman Ibn ;Afan mtume amesema “mbora wenu ni yule mwenye kujifundisha qurani kisha akaifundisha.” (amepokea Bukhari, Abuu Dauw na Tirmidh).

5.Mtu atapandishwa darsa kwa kiasi alichohifadhi qurani peponi.
Watu watakapoingia peponi watapandishwa madaraja ya peponi kulingana na kiasi cha mtu anachoweza kusoma katika qurani. Amesimulia Abdallah Ibn Umar kuwa Mtume amesema ataambiwa mtu aliyeisoma qurani (akiwa peponi) soma na upande darja na uisome kama ulivyokuwa ukiisoma ulivyokuwa dunianai. Kwa hakika makazi yako yataishia pale itakapoishia aya ya mwisho utakayoisoma”. (amepokea Abuu Dawd na tirmidh).

6.Mwenye kusoma vizuri qurani atakuwa na malaika.
Amesimulia Aisha kuwa mtume amasema mwenye kusoma qurani na akawa mahiri nayo (anaisoma vizuri) atakuwa pamoja na malaika wema wenye kutii. Na yule mwenye kuisoma na akawa anakwamakwama (hajaiweza vizuri na anajitahidi aiweze) na huku anashaka atapata malipo mara mbili” (amepokea bukhari, Muslim na wengine).


                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1877

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Khalid Ibn al walid katika vita vya Muta
Khalid Ibn al walid katika vita vya Muta

Yiomyokea khalid Ibn al walid katika vita vya Muta

Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na mkataba wa aqabah katika kuandaa ummah
Mafunzo yatokanayo na mkataba wa aqabah katika kuandaa ummah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
HISTORIA YA KUJENGWA UPYA KWA AL-KA'BAH (NYUMBA TUKUFU YA ALLAH)
HISTORIA YA KUJENGWA UPYA KWA AL-KA'BAH (NYUMBA TUKUFU YA ALLAH)

KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAHItambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani.

Soma Zaidi...
Kuandaliwa kwa Muhammad wakati na baada ya kupewa utume
Kuandaliwa kwa Muhammad wakati na baada ya kupewa utume

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
tarekh 09
tarekh 09

KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana.

Soma Zaidi...
Mfumo wa ulinzi na usalama katika fola ya uislamu madinah
Mfumo wa ulinzi na usalama katika fola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...