Biashara haramu na njia zake katika uislamu

Biashara haramu na njia zake katika uislamu

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Biashara haramu na njia zake katika uislamu

Njia za Biashara Haramu Katika Uislamu

Miongoni mwa biashara zilizoharamu hata kama zimetokana na bidhaa halali ni;

i. Muzabanah

- Ni kunufaika kibiashara kutokana na matatizo ya watu (muuzaji na mnunuzi).


ii. Mu’awamah

- Ni uuzaji au ununuzi wa matunda au mazao shambani kabla ya kukomaa kwake na kufaa kuliwa.


iii. Hablul-Habalah

- Ni kuuza au kununua kilichoko tumboni mwa mnyama kabla hakijazaliwa.



iv. Kuuza au kununua bidhaa kabla haijafika sokoni.

Ibn Abbas (r.a) ameeleza:

“Katika mauzo aliyoyaharamisha Mtume (s.a.w) ni mauzo ya chakula mpaka

yawe mikononi mwa mnunuzi…” (Bukhari na Muslim)



v. Kuuza au kununua bidhaa iliyouzwa au kununuliwa tayari na mtu mwingine kwa kuongeza bei au namna nyingineyo.


vi. Kuuza maji au majani asili yasiyogharamiwa kwa chochote.

Jaabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amekataza kuuza maji ya asili.

(Muslim)


vii. Kuuza au kununua samaki walioko baharini, ndege asiyefugwa (anayeruka angani), maziwa yangali hayajakamuliwa, kiumbe kilicho tumboni mwa mnyama, n.k.

viii. Kuuza au kununua damu, uhuru wa mtu, nywele au maziwa ya binaadamu, n.k.

ix. Kuuza au kununua mbwa, nguruwe, pombe, mizoga, masanamu, picha za watu au wanyama, n.k.

x. Ulanguzi (kuhodhi bidhaa) au kuifanya bidhaa iwe adimu sokoni ili baadae uuze kwa bei yak juu unayotaka.

xi. Kuuza au kununua kwa kupunja au kuharibu vipimo.

“Maangamizo yatawathubutikia wapunjao (wenzao vipimo)……….” (83:1-3)

xii. Kuuza kwa kuficha dosari ya bidhaa, n.k.

xiii. Kuuza au kununua bidhaa kwa wizi, hongo, rushwa, riba, n.k.

Rejea Qur’an (2:276-279)

xiv. Aina zote za kamari kama ramli, kupiga bao, utabiri, n.k.

Rejea Qur’an (5:90-91)

xv. Aina zote za miziki, ngoma, n.k.



Bidhaa Haramu Katika Uislamu

Miongoni mwa bidhaa haramu hata kama biashara yake itafanywa kihalali ni;

i. Pombe za aina zote ii. Mizoga, damu, n.k
iii. Mbwa, nguruwe, paka, n.k

iv. Masanamu, picha za watu au wanyama, n.k v. Bidhaa ya wizi, n.k.





                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1765

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Mambo muhimu ya kuzingatia katika kujenga uchumi wa kiislamu
Mambo muhimu ya kuzingatia katika kujenga uchumi wa kiislamu

Nazingatio muhimu katika uchumi unaofuata sheria za kiislamu.

Soma Zaidi...
Mgogoro wa kuandama kwa mwezi, Je mwezi wa Kimataifa ama kila Mji na mwezi wake?
Mgogoro wa kuandama kwa mwezi, Je mwezi wa Kimataifa ama kila Mji na mwezi wake?

Mwezi ukionekana sehemu moja, Waislamu wote ulimwenguni watalazimika kufunga?

Soma Zaidi...
Uislamu unavyokemea tabia ya ombaomba
Uislamu unavyokemea tabia ya ombaomba

Uislamu umekataza tabia ya kuombaomba kama ndio njia ya kuendesha maisha. Pia ukaweka suluhisho la kukomesha tabia hiyo

Soma Zaidi...
Jinsi ya kushona sanda ya maiti na kumvisha yaani kumkafini
Jinsi ya kushona sanda ya maiti na kumvisha yaani kumkafini

Hapa utajifunza taratibu za kumkafini maiti wa kiislamu. Yaani kushona sanda yake na kumvisha.

Soma Zaidi...
Mambo anayofanyiwa mtu anayekaribia kufa
Mambo anayofanyiwa mtu anayekaribia kufa

Haya ni maandalizi anayofanyiwa mtu aliye katika kilevi cha kifo yaani sakaratul maut

Soma Zaidi...
Ni ipi hukumu ya muislamu anayekula mwezi wa Ramadhani bila ya sababu ya kisheria
Ni ipi hukumu ya muislamu anayekula mwezi wa Ramadhani bila ya sababu ya kisheria

Endapo muislamu hatafunga mwezi wa Ramadhani bila ya ruhusa je atatakiwa afanye nini. Je ataweza kuilipa funga hiyo?

Soma Zaidi...
Dhamana ya Kuchunga Ahadi Katika Uislamu
Dhamana ya Kuchunga Ahadi Katika Uislamu

Kuchunga au kutekeleza ahadi ni miongoni mwa vipengele muhimu vya tabia ya muumini wa kweli.

Soma Zaidi...