Wanaoongozwa na wasioongozwa na quran

Wanaoongozwa na wasioongozwa na quran

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Wanaoongozwa na wasioongozwa na quran

Wanaoongozwa na Qur-an:



Lengo la kushushwa Qur-an kama ilivyobainishwa katika Qur-an yenyewe ni kuwaongoza binaadamu wote katika njia iliyonyooka. Njia iliyonyooka ni njia sahihi ya maisha itakayomuwezesha binaadamu kufikia lengo la kuumbwa kwake. Pamoja na Qur-an kuwa muongozo kwa watu wote, haiwaburuzi kwa nguvu kwenye uongofu bila ya wao wenyewe kudhamiria kuongoka.Qur-an huongoza wacha-Mungu tu kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:


"Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake, ni uwongozi kwa wamchao Mwenyezi Mungu.Ambao huyaamini yasiyoonekana (maadam yamesemwa na Mwenyezi Mungu na Mtume wake) na husimamisha Swala na hutoa katika yale Tuliyowapa.Na ambao wanaamini yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako na wanaamini (kuwa iko) Akhera. Hao wako juu ya uongozi utokao kwa Mola wao, na hao ndio wenye kufaulu." (2:2-5)



Kwa mujibu wa aya hizi wanaongozwa na Qur-an ni wacha-Mungu wenye sifa zifuatazo:
- Waumini wa kweli wa vipengele vyote vya nguzo za Imani. - Wasimamishaji Swala. (Rejea juzuu ya pili).
- Wanaotoa yale aliyowaruzuku Allah (s.w) kwa ajili ya kuwahurumia wanaadamu wenye kuhitajia msaada na katika kusimamisha Dini ya Allah(s.w). Aliyoturuzuku Allah (s.w)ni kila tulichonacho ikiwa ni pamoja na mali, elimu, afya, nguvu,vipaji na kadhalika.


Wasioongozwa na Qur-an:
Tunajifunza katika Qur-an kuwa makundi mawili ya watu Makafiri (na washirikina) na Wanafiki hawataongozwa na Qur-an. Kuhusu makafiri na washirikina tunafahamishwa:


Hakika wale waliokufuru ni sawa kwao ukiwaonya (kwa hii Qur-an) au usiwaonye; hawataamini. (Kama kwamba) Mwenyezi Mungu amepiga muhuri juu ya nyoyo zao na juu ya masikio yao; na juu ya macho yao pana vifuniko; basi watakuwa na adhabu kubwa. (2:6-7)



Pamoja na Qur-an kuwa na sifa ya ukweli na uwazi kama majina yake yanavyodhihirisha, haiwezi kuwaongoza wapinzani (makafiri) wa wazi wa Mwenyezi Mungu(sw) na ujumbe wake. Haiwezi kwa sababu binaadamu amepewa uhuru na Mola wake wa kuamua na kufanya atakavyo. Akiamua kutii anaweza na akiamua kuasi anaweza. Hivyo mtu aliyeamua kuukataa mwongozo huu kwa makusudi huna namna ya kumuongoza.



Kuhusu wanafiki tunafahamishwa:


"Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao "Tumemuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho" na hali ya kuwa si wenye kuamini. Wanataka kumdanganya Mwenyezi Mungu na wale walioamini, lakini hawadanganyi ila nafsi zao, nao hawatambui. Nyoyoni mwao mna maradhi, na Mwenyezi Mungu amewazidishia maradhi. Basi watakuwa na adhabu iumizayo kwa sababu ya kule kusema kwao uongo.(2:8-10)


Na wanapoambiwa msifanye uharibifu ulimwenguni Husema "Sisi ni watengenezaji." Hakika wao ndio waharibuji, lakini hawatambui. Na wanapoambiwa: "Aminini kama walivyoamini watu, "husema "Oh! Tuamini kama walivyoamini wapumbavu?" Hakika wao ndio wapumbavu lakini hawajui. (2:11-13)


Na wanapokutana na walioamini husema, "Tumeamini," na wanapokuwa peke yao kwa mashetani wao husema: "Hakika sisi tu pamoja nanyi, tunawacheza shere tu." Na Mwenyezi Mungu atalipa shere yao na kuwawacha katika upotofu wao wakitangatanga ovyo. Hao ndio waliokhiari upotofu kuliko uongofu, lakini biashara yao haikupata faida wala hawakuwa wenye kuongoka." (2:14-16)



Wanafiki pamoja na kujiita Waislamu na pengine wakawa ni wanachuoni wa Qur-an walio mahiri katika kuifasiri Qur-an kwa kutumia balagha, mantiq, sarfu, n.k; hawataongozwa na Qur-an maadamu wamekhiari maslahi ya dunia kinyume na mwongozo wa Mwenyezi Mungu(sw). Si tu hawa wasomi wa Qur-an wenye sifa hizo zilizoainishwa katika aya hizi hawataongozwa na Qur-an bali pia Allah (s.w) amewafananisha na mbwa katika aya zifuatazo:


"Na wasomee (Ewe Muhammad) habari za wale tuliowapa Aya zetu (kuzijua), kisha wakajivua nazo (wasizifuate). Na shetani akawaandama na, wakawa miongoni mwa waliopotea.Na kama tungelitaka tungeliwanyanyua kwazo, lakini wao waligandamana na ardhi (kutaka maslahi ya kidunia wakayapuuza ya Akhera) na wakayafuata matamanio yao. Basi hali yao ni kama hali ya mbwa; ukimpigia kelele (hukimbia na huku) anahema, na ukimwacha pia huhema.Hiyo ndio hali ya watu waliokadhibisha Aya zetu. Basi simulia hadithi, huenda wakatafakari. "(7:1 75-176)



Hivyo, kwa mujibu wa Aya hizi, mnafiki hata akiwa ni A’alim (Sheikh) wa Qur-an na Hadith, kamwe hawezi kuongozwa na Qur-an.




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1214

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Hoja juu ya kukubalika hadithi
Hoja juu ya kukubalika hadithi

Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kukusanywa na kuhifadhiwa kwa quran
Kukusanywa na kuhifadhiwa kwa quran

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
ADABU ZA KUSOMA QURAN
ADABU ZA KUSOMA QURAN

Adabu wakati wa kusoma quran 1.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al adiyat
Sababu za kushuka surat al adiyat

Sura hii iliposhuka ilikuwa kama imekuja kuwasuta Wanafiki waliokuwa wakizungumzahabari za uongo kuhusu jeshi alilolituma Mtume wa Allah.

Soma Zaidi...
Kitabu Cha  Darsa za Quran
Kitabu Cha Darsa za Quran

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
Ni zipi hukumu za nuni yenye sakina au tanwin?
Ni zipi hukumu za nuni yenye sakina au tanwin?

Hapa utajifunza usomaji wa Quran pindi utakapokuta nuni yenyebsakina au tanwin

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al Fatiha
Sababu za kushuka surat al Fatiha

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu srat al fatiha, faida zake na maudhui zake

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka suratul al-quraysh na fadhila zake
Sababu za kushuka suratul al-quraysh na fadhila zake

SURAT AL-QURAYSH Sura hii ina majina mawili.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa Surat al-Kawthar na fadhila zake
Sababu za kushuka kwa Surat al-Kawthar na fadhila zake

SURATUL-KAUTHAR Imeteremshwa maka, na sura hii imeshuka kwa sababu al-aAs ibn Waail.

Soma Zaidi...