Matunda yenye vitamin C kwa wingi
Somo hili linakwenda kukuletea matunda yenye vitamin C kwa wingi
MATUNDA YENYE VITAMINI C KWA WINGI
Vitamini C ni katika vitamini ambavyo wili unavihitajia kwa wingi kwa lengo la kuboresha mfumo wa kinga mwilini. Tunaweza kupata vitamini hivi sana kutoka kwenye matunda. Katika makala hii nitakwenda kukutajia matunda aina 7 ambayo yana vitamini c kwa wingi sana.
Aina ya matunda yenye vitamini C
1.Embe, embe linafahamika kwa utamu wake na uchachu wake. Vitamini C vinapatikana kwa wingi zaidi kwenye matunda yenye uchachu.
2.Mapera; tunda hili limeenea maeneo mengi, kula pera likiwa limewiva ama likiwa limekomaa na tayari kulila.
3.Papai, mapapai ni katika matunda mabyo yana rangi ya njano. Matunda haya yana sifa ya kuwa na vitamini hivi kwa wingi
4.Karoti, kitaalamu karoti si tunda. Lakini nimependa kuliweka kwenye orodha hii kwa sababu watu hutafuna karoti na kuifanya kama tunda.
5.Limao na ndimu, hapa ndipo penyewe kwa vitamini C. limao na ndimu ndio matunda yenye uchachu kwa wingi na hivyo kukusanya vitamini C.
6.Nanasi, tunda hili pia ni katika matunda yenye rangi ya njano. Sifa hii hufanya tunda hili liwe miongoni mwa vyanzo vikuu vya vitamini C.
7.Chungwa, machungwa yana faida nyingi mwilini ikiwemo kutupatia vitamini C kwa wingi.
8.Nyanya, pensheni, palachichi, tufaha na pilipili haya ni katika matunda mengine yenye vitamini C kwa wingi kabisa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
FAIDA ZA KULA ZABIBU
Somo hili litakwenda kukueleza kuhusu faida za kula zabibu na umuhimu wake kiafya
Soma Zaidi...Faida za kiafya za kula magimbi/ taro roots
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula magimbi
Soma Zaidi...Aina kuu tatu za vyakula na kazi zake
Posti hii inahusu zaidi Aina kuu tatu za vyakula na kazi zake, hii ni Aina tatu za vyakula na kazi zake jinsi zinavyofanya kazi, hufanya kazi kama ifuatavyo,
Soma Zaidi...Faida za kiafya za kula kungumanga/nutmeg
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kungumanga/nutmeg
Soma Zaidi...Faida za biringanya/ eggplant
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za biringanya/ eggplant
Soma Zaidi...