image

Historia ya Dhulqarnain

Dhulqarnain sio jina la mtu bali cheo, maana yake ikiwa: “Mwenye Pembe Mbili”.

Historia ya Dhulqarnain

Historia ya Dhulqarnain


Dhulqarnain sio jina la mtu bali cheo, maana yake ikiwa: “Mwenye Pembe Mbili”. Qur’an haibainishi Dhulqarnain aliishi wapi na wakati gani wa historia. Lakini kwa vile habari zake zinasimuliwa ndani ya Qur’an kama jibu la Mtume(s.a.w) kwa Maquraish kutokana na swali walilopewa na Mayahudi wamwulize Mtume; ni dhahiri kuwa:

(a) Dhulqarnain aliishi miaka mingi kabla ya Mtume (s.a.w).
(b) Historia yake haikuwa inafahimika Arabuni.
(c) Mayahudi walikuwa wakifahamu historia yake.



Wafasiri wengi wa Qur’an na watu wa historia wanamtaja Dhulqarnain kuwa ni mmoja wa wafalme wa Kifursi ambaye aliuangusha ufalme wa Babylon na kuwafanya Waisrail wawe huru. Hii ilitokea kiasi cha maika 1000 kabla ya Mtume(s.a.w). Akiitwa Dhulqarnain (Mwenye Pembe Mbili) kwa vile nchi aliyokuwa anatawala ilikuwa ni nchi mbili zilizoungana na kufanya umbo la Pembe Mbili. Dhulqarnain alikuwa mtawala mwenye nguvu lakini muadilifu pia. Aidha Mwenyezi Mungu alimneemesha kwa kumpa njia za kupatia kila kitu.

“Sisi Tulimmakinisha katika ardhi na Tukampa njia za kupatia kila kitu” (18:84).



Kwa uwezo aliopewa Dhulqarnain alipanua ufalme wake toka Magharibi kuelekea Mashariki na Kaskazini na Kusini. Haya yametajwa katika Qur’an kwa lugha ya Ishara kuwa alisafiri nchi za Maghabribi, Mashariki n.k. Rejea Qur’an (18:83-93).




Basi akafuata njia. Mpaka alipofika machweo ya jua. (Nchi za Magharibi) aliliona linatua katika chemchem (ziwa) yenye matope mengi. Na pale akawakuta watu. Tukasema: “Ewe Dhulqarnain waadhibu au wafanyie wema”. Akasema: “Ama anayedhulumu basi tutamuadhibu, kisha atarudishwa kwa Mola wake, naye atamuadhibu adhabu mbaya kabisa”. Na yule mwenye kuamini na kufanya vitendo vizuri, atapata ujira mwema, nasi tutamwambia (tutamfanyia) lililo jepesi katika amri yetu” (18:85-88).



Uadilifu na wema wa Dhulqarnain unaonekana pia pale alipowakuta watu wanaovamiwa na kuonewa na watu wa makabila mengine. Katika Asia ya Kati yalikuwepo makabila yaliyojulikana kama Tartus, Mongolis, Huns na Scythians. Katika hawa baadhi yao ndio waliotajwa kama Yaajuju na Maajuju. Hawa walikuwa wakizivamia baadhi ya tawala na kuleta uharibifu.



Raia wa tawala hizo walimuomba Dhulqarnain awajengee ukuta kuzunguka nchi hizo ili iwe kinga kuwazuia Yaajuju na Maajuju wasiwavamie. Japo walipendekeza wampe ujira Dhulqarnain kwa kazi hiyo, lakini Dhulqarnain hakutaka malipo. Aliwasaidia bure kwa kutaraji malipo bora zaidi kutoka kwa Allah(s.w). Rejea kisa hiki katika aya zifuatazo:



Wakasema: “Ewe Dhulqarnain! Hakika Yaajuju na Maajuju wanafanya uharibifu katika ardhi. Basi je; tukupe ujira ili utie baina yetu na baina yao kizuizi?” Akasema” Yale ambayo Mola wangu amenimakinishia (amenipa) ni bora (kuliko ujira wenu). Lakini nisaidieni kwa nguvu (kazi). Nitaweka baina yenu na baina yao kizuizi imara”. “Nileteeni vipande vya chuma”. Hata alipoijaza (kwa hicho chuma) nafasi iliyo katikati ya milima miwili alisema: “Pulizeni (moto)” mpaka alipokifanya (kile



chuma) kuwa (kama) moto alisema: “Nileteeni shaba iliyoyayuka niimwage juu yake”. Basi (Yaajuju na Maajuju) hawakuweza kuukwea wala hawakuweza kuutoboa”.
Akasema: “Hii ni rehema itokayo kwa Mola wangu”. Na itakapofika ahadi ya Mola wangu, atauvunjavunja. Na ahadi ya Mola wangu ni kweli tu” (18:94-98).



Katika juhudi za Maquraish kumpinga Mtume(s.a.w) walikuwa wakichukua maswali kutoka kwa Mayahudi na kumuuliza Mtume. Lengo likiwa kupata kisingizio cha kumkana endapo atashindwa kujibu kwa usahihi. Moja ya maswali waliyomuliza ni kutaka kujua juu ya Dhulqarnain.



“Na wanakuuliza habari za Dhulqarnain. Waambie
“Nitakusomeeni baadhi ya hadithi yake” (18:83).



Jawabu la Mtume halikuishia kuelezea tu kuwa Dhulqarnain alikuwa mfalme katika zama fulani. Lakini zilimbainisha kama mtu aliyekuwa Mcha-Mungu na Muadilifu. Mfalme aliyenemeshwa kwa mali na nguvu kubwa na juu ya hayo hakutakabari. Bali akawa anamkumbuka Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo maelezo ya Mtume(s.a.w) yakawa yanawaongezea Maquraish ujumbe wa Tawhiid.



Katika zama zetu za leo watawala walio wengi nguvu za kisiasa na kiuchumi walizo nazo, imekuwa ndio sababu ya wao kutakabari na kufanya ufisadi katika ardhi.



Nchi kama Marekani leo hii inaonekana ndio taifa lenye nguvu
– “Super Power”, lakini kwa vile limejengwa katika misingi ya kikafiri na ushirikina, viongozi wake wameshindwa kuwa waadilifu kwa amana waliyopewa. Pale wanapotetea maslahi yao ya kidunia hutumia maguvu yao kumwaga damu za watu na kuharibu mali za wengine kwa dhulma. Lakini hawapo tayari kutetea haki ya



mnyonge kama kufanya hivyo hakuna maslahi kwao. Ni tofauti na Dhulqarnain alivyotumia maguvu yake kuwakinga watu walioishi katikati ya milima miwili wasishambuliwe na Yaajuju na Maajuju, bila ya malipo. Hii inatufikisha kwenye fundisho la msingi kuwa, amani, utulivu na utengamano katika jamii, hauwezi kupatikana kwa watu wote bila ya watu kumtambua Muumba wao na kuishi kufuatana na Mwongozo wake.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 659


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Vita vya uhudi
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Historia ya maimam Wanne wa fiqh
Soma Zaidi...

TAREKH, HISTORIA NA SIRA YA UISLAMU NA MTUME MUHAMMAD KUTOKA KUZALIWA MPAKA KUFARIKI NA HARAKATI ZAKE
1. Soma Zaidi...

Mapambano ya Mtume Muhammad dhidi ya Wanafiki na hila zao Madina
Soma Zaidi...

Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake
Miezi miwili baada ya Hijjat-al-Wada, Mtume(s. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME ILYASA(A.S)
Mtume Ilyasa ni mmoja wa Mitume waliotumwa kupitia kizazi cha Bani Israil. Soma Zaidi...

tarekh 07
KUPASULIWA KWA KIFUA MTUMEWAKATI AKIWA MTOTO. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Bani Israil
Soma Zaidi...

KUCHIMBWA UPYA KWA KISIMA CHA ZAMZAMA NA KUNYWA MAJI YA ZAMZAMA KISIMA KILICHO BARIKIWA
KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba. Soma Zaidi...

Kwanini mwanadamu hawezi kuunda dini sahihi
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kiapo ya Mtume Ayub na utekelezwaji wake
Mkewe Ayyuub(a. Soma Zaidi...

Umuhimu wa jihad katika kusimamisha uislamu katika jamii
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...