Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Musa(a.s) na Harun(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Musa(a.s) na Harun(a.s)

Kutokana na Historia ya Nabii Musa na Harun(a.

Download Post hii hapa

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Musa(a.s) na Harun(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Musa(a.s) na Harun(a.s)

Kutokana na Historia ya Nabii Musa na Harun(a.s) tunajifunza yafuatayo:

(i) Tunajifunza kuwa ni muhimu kuweka mipango katika kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii. Allah(s.w) anauwezo wa kukiamrisha kitu “kiwe” na kikawa pale pale, lakini bado tunaona ameweka mpango wa muda mrefu wa



(ii) Vile vile mpango huu wa Allah(s.w) wa kuwakomboa Bani Israil,unatufunza kuwa kuibadilisha jamii ya kijahili kuwa ya Kiislamu ni jambo linalohitaji muda na subira.



(iii) Elimu na siha ni nyenzo muhimu za kumuwezesha mtu kuwa khalifa katika ardhi. Nabii Musa alipewa siha nzuri na kuruzukiwa akili na elimu.



(iv) Hakuna hila wala nguvu zinazoweza kuzuia jambo analotaka Allah(s.w) liwepo au lisiwepo katika jamii, yeye anazo namna nyinyi za kumlinda mja wake na vile vile anaweza kumuangamiza mbabe yeyote awaye.



(v) Tabia njema na kuwatendea watu wema ni nyenzo muhimu katika harakati za kusimamisha Uislamu katika jamii. Nabii Musa(a.s)kwa wema wake aliletewa taarifa ya mipango ya Firaun dhidi yake; pia kwa huruma yake alipata hifadhi kwa mzee wa Madian.



(vi) Hakuna binaadamu asiyeteleza na kumkosea Allah(s.w), lakini muumini anakuwa mwepesi wa kurejea kwa Allah (s.w).Musa(a.s) aliteleza kwa kuingilia ugomvi asioujua na kumuua mtu,alirejea kwa Mola wake haraka haraka–Qur-an (28:16).



(vii)Muumini wa kweli hanabudi kuchukia vitendo vya dhuluma na kuwa tayari kuwatetea wanaodhulumiwa haki zao kwa kadiri ya uwezo wake.



(viii)Ni muhimu kuwekeana mikataba ya kazi tunapoajiri au kuajiriwa. Nabii Musa(a.s) aliwekeana mkataba wa kazi na mzee wa Madian.



(ix) Nyenzo muhimu ya kutuwezesha kusimamisha Uislamu katika jamii baada ya Elimu ni kusimamisha Swala za Faradh na sunah,Qiyamullayl na kuleta dhikiri kwa wingi – Qur-an(20:14), (73:1-10), (74:1-7).



(x) Miujiza ni katika dalili za kuwepo Allah(s.w).



(xi) Katika harakati za kusimamisha Uislamu katika jamii tunatakiwa tusimvamie tu kila mtu na kumuingiza kwenye harakati, bali tuanze na ndugu, jamaa na rafiki wa karibu ambao tunajua fika tabia na mwenendo wao. Nabii Musa (a.s) aliomba ndugu yake Harun awe msaidizi wake si kwa kuwa alikuwa ndugu yake tu, bali alimfahamu fika kwa ucha Mungu wake.



(xii)Muumini mwanaharakati hahongeki kwa fadhila atakazofanyiwa na madhalimu ili arudi nyuma katika kusimamisha uadilifu. Musa(a.s) alilelewa katika nyumba ya mfalme,lakini hakuacha kudhihirisha kwa matendo udhalimu wa Firaun na serikali yake ikawa ndio sababu ya kuhukumiwa kifo.



(xiii)Ni kawaida ya matwaghuti kufanya propaganda dhidi ya wanaharakati na kuwapachika majina mabaya. Firaun na serikali yake alimpakazia Nabii Musa(a.s) uwendawazimu na uchawi.



(xiv)Hapana yeyote wa kumchelea katika kutekeleza amri ya Allah(s.w) ya kusimamisha Uislamu katika jamii. Musa na Harun(a.s) walimkabili Firaun na wakuu wake wa Dola waliozungukwa na majeshi na kuwafikishia ujumbe wa Allah(s.w).



(xv)Hapana yeyote mwenye uwezo wa kutweza au kutengua maamuzi ya nafsi ya mwanaadamu.Wachawi walipobainikiwa na Haki na wakasilimu, Firaun hakuweza kuwaritadisha pamoja na adhabu kali aliyoitoa dhidi yao – Qir-an (26:49-51).



(xvi)Toba inayokubalika ni ile inayoletwa haraka kabla ya kufikwa na mauti – Qur-an (4:18).



(xvii)Kuishi nje ya shahada na kutarajia kufa ndani ya shahada ni muhali. Allah(s.w) ametuamrisha tuishi na shahada na tujitahidi kubakia nayo mpaka kufa kwetu– Qur-an (3:102).



                   

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1685

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Kazi alizokuwa akizifanya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume.
Kazi alizokuwa akizifanya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume.

Historia na sifa ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 14. Hapa utajifunza kuhusu kazi alizozifanya Mtume s.a.w Enzo za ujana wake kabla ya utume.

Soma Zaidi...
tarekh 02
tarekh 02

FAMILIA YA MTUME (S.

Soma Zaidi...
Ukasha bin Mihsan ni Sahaba aliyechangamkia Fursa
Ukasha bin Mihsan ni Sahaba aliyechangamkia Fursa

Katika somo hili utakwnda kujifunz anamna nambavyo Sahaba Ukasha alivyochangamkia fursa katika mambo ya heri

Soma Zaidi...
Nani alikuwa ni Sahaba wa kwanza kufariki akiwa Shahidi
Nani alikuwa ni Sahaba wa kwanza kufariki akiwa Shahidi

Sahaba wa kwanz akufariki akiwa shahidi, alifariki kwa sababu ya mateso aliyoyapata kutoka kwa Makafiri wa ki Quraysh

Soma Zaidi...
Kuandaliwa kwa Muhammad kabla ya kupewa utume
Kuandaliwa kwa Muhammad kabla ya kupewa utume

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ni jitihada gan alizo zifanya sayyidna othman katika kuihifadh qur an ?
Ni jitihada gan alizo zifanya sayyidna othman katika kuihifadh qur an ?

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Jitihada alizozifanya Khalifa wa Tatu katika kuilinda Quran

Soma Zaidi...
tarekh 08
tarekh 08

KULELEWA NA MAMA YAKE ALIPOFIKA MIAKA MINNEMtume (s.

Soma Zaidi...