Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Musa(a.s) na Harun(a.s)

Kutokana na Historia ya Nabii Musa na Harun(a.

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Musa(a.s) na Harun(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Musa(a.s) na Harun(a.s)

Kutokana na Historia ya Nabii Musa na Harun(a.s) tunajifunza yafuatayo:

(i) Tunajifunza kuwa ni muhimu kuweka mipango katika kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii. Allah(s.w) anauwezo wa kukiamrisha kitu โ€œkiweโ€ na kikawa pale pale, lakini bado tunaona ameweka mpango wa muda mrefu wa



(ii) Vile vile mpango huu wa Allah(s.w) wa kuwakomboa Bani Israil,unatufunza kuwa kuibadilisha jamii ya kijahili kuwa ya Kiislamu ni jambo linalohitaji muda na subira.



(iii) Elimu na siha ni nyenzo muhimu za kumuwezesha mtu kuwa khalifa katika ardhi. Nabii Musa alipewa siha nzuri na kuruzukiwa akili na elimu.



(iv) Hakuna hila wala nguvu zinazoweza kuzuia jambo analotaka Allah(s.w) liwepo au lisiwepo katika jamii, yeye anazo namna nyinyi za kumlinda mja wake na vile vile anaweza kumuangamiza mbabe yeyote awaye.



(v) Tabia njema na kuwatendea watu wema ni nyenzo muhimu katika harakati za kusimamisha Uislamu katika jamii. Nabii Musa(a.s)kwa wema wake aliletewa taarifa ya mipango ya Firaun dhidi yake; pia kwa huruma yake alipata hifadhi kwa mzee wa Madian.



(vi) Hakuna binaadamu asiyeteleza na kumkosea Allah(s.w), lakini muumini anakuwa mwepesi wa kurejea kwa Allah (s.w).Musa(a.s) aliteleza kwa kuingilia ugomvi asioujua na kumuua mtu,alirejea kwa Mola wake haraka harakaโ€“Qur-an (28:16).



(vii)Muumini wa kweli hanabudi kuchukia vitendo vya dhuluma na kuwa tayari kuwatetea wanaodhulumiwa haki zao kwa kadiri ya uwezo wake.



(viii)Ni muhimu kuwekeana mikataba ya kazi tunapoajiri au kuajiriwa. Nabii Musa(a.s) aliwekeana mkataba wa kazi na mzee wa Madian.



(ix) Nyenzo muhimu ya kutuwezesha kusimamisha Uislamu katika jamii baada ya Elimu ni kusimamisha Swala za Faradh na sunah,Qiyamullayl na kuleta dhikiri kwa wingi โ€“ Qur-an(20:14), (73:1-10), (74:1-7).



(x) Miujiza ni katika dalili za kuwepo Allah(s.w).



(xi) Katika harakati za kusimamisha Uislamu katika jamii tunatakiwa tusimvamie tu kila mtu na kumuingiza kwenye harakati, bali tuanze na ndugu, jamaa na rafiki wa karibu ambao tunajua fika tabia na mwenendo wao. Nabii Musa (a.s) aliomba ndugu yake Harun awe msaidizi wake si kwa kuwa alikuwa ndugu yake tu, bali alimfahamu fika kwa ucha Mungu wake.



(xii)Muumini mwanaharakati hahongeki kwa fadhila atakazofanyiwa na madhalimu ili arudi nyuma katika kusimamisha uadilifu. Musa(a.s) alilelewa katika nyumba ya mfalme,lakini hakuacha kudhihirisha kwa matendo udhalimu wa Firaun na serikali yake ikawa ndio sababu ya kuhukumiwa kifo.



(xiii)Ni kawaida ya matwaghuti kufanya propaganda dhidi ya wanaharakati na kuwapachika majina mabaya. Firaun na serikali yake alimpakazia Nabii Musa(a.s) uwendawazimu na uchawi.



(xiv)Hapana yeyote wa kumchelea katika kutekeleza amri ya Allah(s.w) ya kusimamisha Uislamu katika jamii. Musa na Harun(a.s) walimkabili Firaun na wakuu wake wa Dola waliozungukwa na majeshi na kuwafikishia ujumbe wa Allah(s.w).



(xv)Hapana yeyote mwenye uwezo wa kutweza au kutengua maamuzi ya nafsi ya mwanaadamu.Wachawi walipobainikiwa na Haki na wakasilimu, Firaun hakuweza kuwaritadisha pamoja na adhabu kali aliyoitoa dhidi yao โ€“ Qir-an (26:49-51).



(xvi)Toba inayokubalika ni ile inayoletwa haraka kabla ya kufikwa na mauti โ€“ Qur-an (4:18).



(xvii)Kuishi nje ya shahada na kutarajia kufa ndani ya shahada ni muhali. Allah(s.w) ametuamrisha tuishi na shahada na tujitahidi kubakia nayo mpaka kufa kwetuโ€“ Qur-an (3:102).



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1805

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰2 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰4 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰5 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Mtume amezaliwa mwaka gani?

Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake.

Soma Zaidi...
HISTORIA YA MTUME DHUL-KIFL(A.S)

Mtume Dhul-kifl ananasibishwa na Ezekiel anayetajwa ndani ya Biblia.

Soma Zaidi...
Nabii Isa(a.s) Azungumza Akiwa Mtoto Mchanga

Maryam akamtwaa mwanawe, akaenda naye kwa jamaa zake amembeba.

Soma Zaidi...
Kusingiziwa Nabii Sulaiman Uchawi

Pamoja na Ucha-Mungu aliokuwa nao Nabii Sulaiman watu hawakuacha kumsingizia mambo machafu.

Soma Zaidi...
tarekh 09

KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee โ€˜Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana.

Soma Zaidi...