image

Ujumbe wa Nabii Ibrahiim(a.s) kwa Mfalme Namrudh

Ujumbe wa Nabii Ibrahiim(a.s) kwa Mfalme Namrudh

Ujumbe wa Nabii Ibrahiim(a.s) kwa Mfalme Namrudh


Nabii Ibrahim anavunja masanamu

NabiiIbrahiim(a.s) hakuishia kulingania Uislamu kwa baba yake na watu wa kawaida tu bali alisonga mbele na kumkabili Mfalme Namrudh kwa mjadala juu ya upweke wa Allah(s.w). Mfalme Namrudh alikuwa akiwanyonya na kuwadhulumu watu kama ilivyo kawaida ya watawala wa kitwaghuti kupitia kanuni na sharia za dini za kishirikina. Namrudh alijipa uungu kama inavyodhihiri katika majadiliano yake na Ibrahiim(a.s):



Hukumsikia yule aliyehojiana na Ibrahimu juu ya Mola wake kwa sababu Mwenyezi Mungu alimpa Ufalme? Ibrahimu aliposema: “Mola wangu ni yule ambaye huhuisha na hufisha,” yeye akasema: “Mimi pia nahuisha na kufisha.” Ibrahimu akasema: “Mwenyezi Mungu hulichomozesha jua mashariki, basi wewe lichomozeshe magharibi.” Akafedheheka yule aliyekufuru; na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu. (2:258)



Nabii Ibrahimu avunja masanamu

Ibrahim(a.s) Avunja Masanamu Kuwatanabahisha Washirikina. NabiiIbrahiim(a.s) alijitahidi kwa kadiri ya uwezo wake, kuwaonesha watu wake kwa hoja madhubuti udhaifu wa masanamu wanayoyaabudu badala ya Allah(s.w),



Na hakika tulimpa Ibrahimu uwongofu wake zamani na tulikuwa tukimjua (vizuri). (Wakumbushe alipowaambia watu wake): “Ni nini masanamu haya mnayakalia wakati wote (kuyaabudu)?” (21:51-52)



Wakasema, “Tuliwakuta babu zetu wakiyaabudu, (basi na sisi tunayaabudu).Akasema: “Bila shaka nyinyi na baba zenu mulikuwa katika upotofu (upotevu) ulio dhahiri.” Wakasema: “Je! Umetujia kwa (maneno ya) haki au umo miongoni mwa wachezaji?” (21:53-55)



Akasema:“(Siyo! Mimi si mchezaji) Bali Mola wenu ni yule Mola wa mbingu na ardhi ambaye ndiye aliyeziumba. Nami ni miongoni mwa wenye kuyashuhudia haya.” (21:56)



Na wasomee habari za (Nabii) Ibrahimu. Alipomwambia baba yake na kaumu yake: “Mnaabudu nini?” Wakasema: “Tunaabudu masanamu, daima tunawaabudu.” Akasema: “Je, yanakusikieni mnapoyaita?” (26:69-72)



Au yanakufaeni (mkiyaabudu) au yanakudhuruni (mkiacha kuyaabudu)?” Wakasema: “(Hayafanyi haya) lakini tumewakuta baba zetu wakifanya hivi.” Akasema: “Je, mumewaona hawa mnaowaabudu” “Nyinyi na wazee wenu waliotangulia?(26:73-76)




Bila shaka hao ni adui zangu (basi nitawadhuru. Mimi simuabudu) ila Mola wa walimwengu wote. Ambaye ameniumba na Yeye ananiongoza. Na ambaye ndiye anayenilisha na kuninywesha, (anayenipa chakula na kinywaji). Na ninapougua; Yeye ndiye anayeniponesha. Na ambaye atanifisha kisha atanihuisha. Na ndiye ninayemtumaini kwamba atanisamehe makosa yangu siku ya malipo.(26:77-82)



Alipoona watu wake hawamuelewi, Nabii Ibrahim (a.s) aliazimia kuvunja masanamu yao atakapopata mwanya ili kuwaonesha kwa vitendo udhaifu wa miungu wanayoiabudu. Alipopata fursa ya kuingia Hekaluni, bila ya kuonekana, aliyavunja masanamu yote yaliyokuwemo na kuacha lile kubwa lao.




“Oh! Kwa uzushi tu, miungu badala ya Mwenyezi Mungu – ndiyo mnayoitaka?” “Basi nini fikira yenu juu ya Mola wa walimwengu wote? (Mnamuona hatoshelezi ndio mnatafuta waungu wengine?)” Kisha akatazama mtazamo (mkubwa) katika nyota (akasema “Nitachukua fursa ya kuwajulisha uwongo wa Dini yao kwa kuwaonyesha kuchomoza kwake hizo nyota wanazoziabudu na kuchwa kwake).” Akasema: “Hakika mimi ni mgonjwa.” Nao wakamuacha, wakampa kisogo (wakenda zao viungani katika mandari zao). Basi alikwenda kwa siri kwa miungu yao akaiambia (kwa stihzai): “Muna nini? Mbona hamli? (Vyakula hivi vya mihanga mlivyowekewa?)” “Mumekuwaje! Hamsemi?” Kisha akawageukia kuwapiga kwa mkono wa kulia, (kwa mwisho wa nguvu zake). (37:86-93)



“Basi akayavunja vipande vipande isipokuwa lile kubwa lao (aliliacha) ili wao walirudie.” (21:58)




Watu wa Nabii Ibrahiim(a.s) walipokuta miungu yao imefanywa vile walihamaki.
Wakasema: “Nani aliyeifanya hivi miungu yetu? Hakika huyo yu miongoni mwa madhalimu (wakubwa)”. Wakasema: “Tulimsikia kijana mmoja akiwataja anayeitwa Ibrahimu.” Wakasema:“Basi mleteni mbele ya macho ya watu, wamshuhudie (kwa ubaya wake huo).”(21:59-61)



Makemeo yaIbrahiim(a.s) dhidi ya masanamu hayo, hayakuwa siri. Hivyo walimtuhumu kuwa ndiye aliyefanya kitendo hicho, wakamkamata na kumshitaki hadharani:



“Wakasema: Je! Wewe umeifanya hivi miungu yetu, ee Ibrahim? (21:62) Kwa kuulizwa swali hili Nabii Ibrahim (a.s) alipata fursa adhimu aliyokuwa akiitafuta:



Akasema: “Siyo, bali amefanya (hayo) huyu mkubwa wao, basi (muulizeni na) waulizeni (pia hao waliovunjwa) kama wanaweza kunena!” Basi wakajirudi nafsi zao, (wakafikiri udhalilifu wa waungu hao walio nao, wasioweza kujipigania) na wakasema: “Hakika nyinyi mlikuwa madhalimu (wa nafsi zenu kwenda kuwaabudu wasiokuwa na maana). Kisha wakainamisha vichwa nyao, (wakasema) “Hakika umekwishajua ya kwamba hawasemi (kwanini unatucheza shere?(21:63-65)



Akasema:“Je! Mnaabudu badala ya Mwenyezi Mungu (miungu) isiokufaeni chochote(mnapowaabudu)wala kukudhuruni (chochote mnapoacha kuwaabudu)?” Kefule (udhalilifu) yenu na ya hivyo mnavyoviabudu kinyume cha Mwenyezi Mungu. Je! Hamfikiri? (21:66-67)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 422


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Mafunzo yatokanayo na kuanzishwa kwa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kuandaliwa kwa Muhammad kabla ya kupewa utume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SHU’AYB(A.S)
Nabii Shu’ayb(a. Soma Zaidi...

fadhila za kusoma quran
Fadhila na umuhimu wa kusoma quran 1. Soma Zaidi...

Kuibuka kwa kundi la khawarij baada ya vita vya Siffin
Soma Zaidi...

Kuandaliwa Mtume(s.a.w) maandalizi ya kimafunzo na maandalizi ya ki ilham
Mitume huzaliwa Mitume. Soma Zaidi...

Nabii Yunus(a.s) Amuomba Allah(s.w) Msamaha
Ndani ya tumbo la samaki, Nabii Yunus(a. Soma Zaidi...

Sifa au vigezo vya dini sahihi
Dini sahihi anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na maandalizi haya ya ki ilhamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Matukio mbalimbali katika historia ya uislamu kabla na baada ya Mtume (s.a.w) na makhalifa wake wanne
1. Soma Zaidi...

Kusilimu kwa Wachawi wa Firaun
Mawaziri waliokuwa washauri wakuu wa Firauni wakataka wakusanywe magwiji waliobobea katika uchawi nchi nzima, kisha wapambanishwe na Nabii Musa(as). Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII HUD(A.S) NA WATU WA 'AD
Baada ya Nuhu(a. Soma Zaidi...