image

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ayyuub(a.s)

Kutokana na kisha hiki cha Nabii Ayyuub(a.

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ayyuub(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ayyuub(a.s)


Kutokana na kisha hiki cha Nabii Ayyuub(a.s) tunajifunza
yafuatayo:

(i) Binaadamu hapa ulimwenguni yuko mtihanini kama Qur-an inavyobainisha:



Ametukuka yule ambaye Mkononi mwake umo ufalme (wote); Naye ni mwenye uweza juu ya kila kitu. Ambaye ameumba mauti na uhai ili kukujaribuni (kukufanyieni mtihani); ni nani miongoni mwenu mwenye vitendo vizuri zaidi. Naye ni Mwenye nguvu na Mwenye Msamaha. (67:1-2)



Kwa hakika tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyochanganyika; (ya mwanamume na mwanamke), ili tumfanyie mtihani (kwa amri zetu na makatazo yetu); kwa hiyo tukamfanya ni Mwenye kusikia (na) Mwenye kuona. (76:2)



Mwanaadamu anachoweza kufanya si kuepa mitihani bali kutekeleza wajibu wake kwa kadiri ya uwezo wake na kufanya subira juu ya mazito mbali mbali yatakayomfika huku akimtegemea Allah(s.w) ipasavyo



(ii) Muumini baada ya kumcha-Allah(s.w) ipasavyo alipokee kwa moyo mkunjufu lolote litakalomfika likiwa la kheri au lenye sura ya shari, kwani Allah yuko pamoja na waja wake.



(iii) Kwa elimu ndogo ya mwanaadamu kuna matukio mengine yanamtokea mwanaadamu kwa sura ya shari, kumbe ni ya kheri kwake na kinyume chake kama Allah(s.w) anavyotutanabahisha katika aya ifuatayo:



Mmelazimishwa kupigana vita (kwa ajili ya dini). Nalo ni jambo zito kwenu. Lakini huenda mkachukia kitu, nacho ni kheri kwenu. Na huenda mkapenda kitu nacho ni shari kwenu. Na Mwenyezi Mungu ndiye anayejua, (lakini) nyinyi hamjui. (2:216)


(iv) Muumini wa kweli anatakiwa awe anamkumbuka Allah(s.w) nyakati zote katika hali zote, akiwa na dhiki au wasaa. Na mtu anapokuwa katika dhiki ndio anazijua na kuzithamini vizuri neema mbali mbali alizoneemeshwa na Mola wake na ndio anakuwa na nafasi nzuri ya kushukuru. Kwa mfano ni kweli kuwa mtu hawezi kujua thamani ya shibe kama hajafikiwa na dhiki ya njaa.



(v) Waumini wanalazimika kutekeleza ahadi au viapo wanavyotoa katika kufanya mambo ya kheri.



(vi) Hapana kizuizi chochote kiwezacho kuwazuia waumini kumcha-Mola wao na kusimamisha Uislamu katika jamii.



(vii) Matatizo yanayowafika waumini pasina yale ya kujitakia (ya uzembe), ni nyenzo muhimu za kunoa imaniyao juu ya Allah na kuwapa hamasa na msukumo wa kusimamisha Uislamu katika jamii.





                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 442


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

HISTORIA YA MTUME ILYASA(A.S)
Mtume Ilyasa ni mmoja wa Mitume waliotumwa kupitia kizazi cha Bani Israil. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Daud(a.s)
Kutokana historia ya Nabii Daud (a. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Hud(a.s)
(i) Tuanze kulingania kwa kuonesha upweke wa Allah(s. Soma Zaidi...

Kukomeshwa kwa Riddah na Chokochoko Nyingine katika dola ya kiislamu
Soma Zaidi...

Historia ya Vijana wa Pangoni
Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s. Soma Zaidi...

tarekh 06
MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S. Soma Zaidi...

Mkataba wa 'Aqabah na vipiengele vyake na mafunzo tunayoyapata katika mkataba wa aqaba
Mtume (s. Soma Zaidi...

Uendeshaji na Kupanuka kwa Dola ya Kiislamu Kipindi cha Makhalifa Waongofu
Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na maandalizi haya ya ki ilhamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Khalid Ibn al walid katika vita vya Muta
Yiomyokea khalid Ibn al walid katika vita vya Muta Soma Zaidi...

Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.
Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah. Soma Zaidi...

Sifa au vigezo vya dini sahihi
Dini sahihi anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...