Adam(a.
Adam(a.s) ni mtu na Mtume wa Allah(s.w) wa kwanza. Adam(a.s) ameumbwa kwa udongo uliofinyangwa ukafanywa kuwa sanamu la mtu kisha likapuliziwa roho na kuwa mtu kamili kama tunavyofahamishwa katika Qur-an:
Na (kumbuka) Mola wako alipowaambia Malaika, “Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo mkavu unaotoa sauti, wenye kutokana na matope meusi yaliyovunda.”“Basi nitakapomkamilisha na kumpulizia roho inayotokana na Mimi, basi mumuangukie kwa kumtii.” (15:28-29)
(Kumbuka) Mola wako alipowaambia Malaika: Hakika mimi nitaumbwa mtu kwa udongo. Na nitakapomkamilisha na kumpulizia roho inayotokana na mimi basi msujudieni (kama ishara ya kumheshimu). (38:71-72).
Hadhi ya Adam(a.s) na Kizazi Chake
Kabla ya Adam(a.s) kuumbwa, Allah(s.w) aliwafahamisha Malaika kuwa atamleta Khalifa (kiongozi) katika ardhi atakayesimamisha Ufalme wa Allah(s.w) (Dola ya kiislamu) kwa kufuata mwongozo wake Allah(s.w). Mazungumzo baina ya Allah(s.w) na Malaika wake juu ya ukhalifa wa Adam(a.s) na kizazi chake tunayapata katika aya zifuatazo:
(Wakumbushe watu khabari hii): Wakati Mola wako alipowambia Malaika: “Mimi nitaleta Khalifa katika ardhi.”
Wakasema (Malaika): “Utaweka humo watakaofanya uharibifu humo na kumwaga damu, hali sisi tunakutukuza kwa sifa zako na kukutaja kwa utakatifu wako?” Akasema (Mwenyezi Mungu): “Hakika Mimi nayajua msiyoyajua.”(2:30)
Na (Mwenyezi Mungu) akamfundisha Adam majina ya vitu vyote, kisha akaviweka mbele ya Malaika, na akasema (kuwaambia Malaika): “Niambieni majina ya vitu hivi ikiwa mnasema kweli (kuwa nyinyi ndio wajuzi wa mambo).”(2:31)
Wakasema (Malaika): “Utakatifu ni wako! Hatuna ilimu isipokuwa ile uliyotufundisha; bila shaka wewe ndiye Mjuzi na ndiye Mwenye hikima.” (2:32).
Akasema (Mwenyezi Mungu): “Ewe Adam! Waambie majina yake.” Alipowaambia majina yake alisema (Mwenyezi Mungu) “Sikukwambieni kwamba mimi najua siri za mbinguni na za ardhi; tena najua mnayoyadhihirisha na mliyokuwa mnayaficha?”.(2:33)
Na (wakumbushe watu khabari hii): Tulipowaambia Malaika “Msujudieni Adam”. Wakamsujudia wote isipokuwa Iblis; akakataa na akajivuna; na (tokea hapo) alikuwa katika makafiri(2:34)
Kutokana na aya hizi tunajifunza yafuatayo:
Kwanza ,Adam(a.s) na kizazi chake(wanaadamu) wamekusudiwa kuwa Makhalifa wa Allah (s.w) katika ardhi, yaani kuwa wasimamishaji wa Ufalme wa Allah(s.w) katika ardhi (Dola ya Kiislamu) kwa niaba yake pamoja na kuwa yeye mwenyewe ni Muweza wa kuusimamisha kwa kusema: “kuwa” na “ukawa”.
Pili, ili kuweza kusimamisha ukhalifa katika ardhi watu hawanabudi kuwa na ujuzi wa kutosha juu ya mazingira ya ardhi na namna ya kukabiliana nayo. Nabii Adam(a.s) kufundishwa “majina ya vitu vyote” ni kielelezo kuwa alifunzwa fani zote za elimu zinazohitajika katika kuendea kila kipengele cha maisha ya binafsi na ya jamii ya mwanaadamu hapa ardhini. Pamoja na elimu ya vitu mbali mbali (elimu ya mazingira), Adam(a.s) na kizazi chake waliahidiwa kuletewa mwongozo kutoka kwa Allah(s.w) utakaowawezesha kusimamisha ukhalifa na kuvuna matunda yake ambayo ni kuishi kwa furaha na amani na kupata radhi za Allah(s.w) hapa duniani na huko akhera kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:
“Tukasema: Shukeni humo nyote (kutoka peponi) na kama ukikufikieni uwongozi utokao kwangu, wale watakaoufuata uwongozi wangu huo, haitakuwa khofu juu yao wala hawatahuzunika.(2:38)
Lakini wenye kukufuru na kuyakadhibisha maneno yetu, hao ndio watakaokuwa watu wa motoni, humo watakaa milele”. (2:39)
Tatu, kusimamisha ukhalifa katika ardhi au kusimamisha Uislamu katika jamii ni jambo linalompandisha mwanaadamu hadhi na daraja mbele ya Allah(s.w) kuliko ile hadhi na daraja ya Malaika mbele ya Allah(s.w). Hili linadhihirika pale Malaika walipoamrishwa kumsujudia Adam(a.s). Sijda ni kitendo cha heshima ya hali ya juu kinachomstahiki Allah(s.w) peke yake, lakini kama ishara ya kuonesha hadhi ya Khalifa (Naibu) wa Allah(s.w), hapa ardhini, Allah(s.w) aliwaamrisha Malaika wamsujudie Adam na wakatii. Ubora wa kusimamisha Ukhalifa (Uislamu) katika jamii pia unadhihirishwa katika aya zifuatazo:
“Enyi mlioamini! Je! Nikujulisheni biashara itakayokuokoeni na adhabu iumizayo?(61:10)
(Biashara yenyewe ni hii);- Muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na piganieni Dini ya Mwenyezi Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu, haya ni bora kwenu ikiwa mnajua”. (61:-11)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 3640
Sponsored links
👉1
Madrasa kiganjani
👉2
Kitabu cha Afya
👉3
kitabu cha Simulizi
👉4
Kitau cha Fiqh
👉5
Simulizi za Hadithi Audio
👉6
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
HISTORIA YA KUJENGWA UPYA KWA AL-KA'BAH (NYUMBA TUKUFU YA ALLAH)
KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAHItambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani. Soma Zaidi...
Uchaguzi wa Ali bin Abu Twalib kuwa Khalifa wa nne na chanzo cha Makundi katika Uislamu
Soma Zaidi...
historia na maisha ya Mtume IS-HAQ(A.S.) NA YA‘AQUUB(A.S.)
Is-haq(a. Soma Zaidi...
HISTORIA YA FAMILIA YA MTUME MUHAMMAD S.A.W
Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 02. Soma Zaidi...
Nabii Ibrahiim(a.s) Kuulingania Uislamu kwa Jamii Yake
Nabii Ibrahim(a. Soma Zaidi...
Maswali kuhusu hali ya bara arabu zama za jahiliyyah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Historia ya uislamu wakati wa Makhalifa wanne: Abubakar, Umar, Uthman na Ally
Soma Zaidi...
Kiapo ya Mtume Ayub na utekelezwaji wake
Mkewe Ayyuub(a. Soma Zaidi...
Mbinu za Mtume Salih(a.s) Katika Kulingania Uislamu
Kama Mitume waliotangulia, Nabii Salih(a. Soma Zaidi...
Mapambano ya waislamu dhidi ya maadui wa kiyahudi madina
Mayahud Mwanzoni Mayahud walipoona kuwa Waislamu wanafunga siku ya Ashura pamoja nao na wanaelekea Qibla cha Baitul- Muqaddas pamoja nao hawakuonyesha chuki ya dhahiri dhidi ya Mtume(s. Soma Zaidi...