image

Utunzaji wa betri la kifaa chako

Posti hii inakwenda kukupa elimu kuhusu utunzaji wa betri la kifaa chako

UTUNZAJI WA BETRY YA KIFAA CHAKO:

 

Kabla ya kuona njia za kutunza betry ya kifaa chako kwanza tuone adui mkubwa ambaye anachangia kuharibu betry yako kwa kiwango kikubwa. Jambo hatari sana linalosababisha kuharibika kwa bety hako ni kupata joto. Eric Limer alizungumza hivi "What's far more dangerous to a battery's well-being is heat. Lithium-ion batteries despise heat. A li-ion battery that's been exposed to temperatures of around 100 degrees Fahrenheit for a year will lose about 40 percent of its overall charge capacity. At 75 degrees, it'll lose only about 20 percent."?hivyo joto ni katika adui mkubwa wa betry yako ya simu au kompyuta. Betry ikiwa inapata joto jin gi wakati wa kutumika inaweza kupoteza uwezo wake wa kufanya kazi kwa haraka zaidi na kwa kiwango kikubwa kama alivyosema katika nukuu za hapo juu kuwa betry iliyowekwa katika joto la 100 Fahrennheit kwa mwaka inapoteza asilimia 40% za uwezo wake wa kijumla wa kuchaji, na likiwa joto hilo ni 75% inapoteza 20% ya uwezo wake wa kuchaji. hivyo kama utaizuia betry yako kupata joto jingi kwa muda mrefu unapofanya kazi utaweza kudhibiti uwezo wa betry yako wa kufanya kazi. Sasa kwakuwa tumeshaona adui mkubwa wa betry zetu hebu tuone sasa namna ya kutunza betry zetu.Njia za kutunza betry

1. Towa betry yako katika kifaa chako ili ipowe kama imepata moto kwa muda mrefu bila ya kupozwa. simu au laptop zingine huwa zikipata joto huchelewa kupowa hivyo kitendo hiki kitafanya betry yako iendelee kuathirika. hivyo kamma utakuwa umemaliza shughuli zako unaweza kuitowa nje betry yako ili iweze kupowa.

2.weka kifaa chako katika mazingira yasiyo na joto la hali ya juu. kwa mfano usiweke simu yako juu ya PS ambapo pana joto au juu ya laptop au kompyuta iliyo na joto. pia jiepushe kuiweka simu yako juu ya deki iliyo na joto. Halikadhalika kwa betry ya laptop yako epusha kuiweka katika mazingira nambayo yataifanya ipate joto la juu kwa mfano kuiweka juu ya godoro au kitu ambacho itasababisha joto la kompyuta yako lisipungue kwani godoro linaweza kuziba matundu ambayo yamewekwa kwa ajili ya kupunguza joto la ziada.

3.Hifadhi betry yako ikiwa ina chaji kiasi walau kidogo.Inatokea unazaidi ya betri oja na unataka kuipunzisha betry ya zamani hivyo inashauriwa kuihifadhi ikiwa ina kiasi cha chaji. pia nivizuri kuiwacha betry katika kifaa chako ikiwa ina kiasi cha chaji walau kidogo.Mengineyo katika kutunza bety: Tokeo la picha la wifi

1.funga wi-fi kama hautumii. wireless ni katika vyanzo ambavyo pindi ikiwa ON na ipo connected inaweza kutumia chaji nyingi sana kwa wakati mfupi ambapo kitendo hiki pia kianaweza kuhatarisha uhai wa betry yako.

2. funga bluetooth na funguza mwanga wa screen yako na punguza muda wa kudisplay screen yako

3.funga shughuli zote zinazofanyika kwa kufificha yaan background activities.

4. mwisho kama betry yako inaendelea kusumbuwa ni vizuri kwendakuibadilisha ni vizuri kununuwa mpya tofauti na kunu uwa kwa mtu. nenda dukani ukapate betry yako mpya uendelee kuvinvjari ukiwa na kifaa chako.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1475


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Simu au Kompyuta inastak? (inasumbua)
Jifunze matumizi ya simu yako na namna ya kutatua matatizo mbalimbali kwenye simu na kompyuta.. Soma Zaidi...

Chanzo
Jifunze matumizi ya simu yako na namna ya kutatua matatizo mbalimbali kwenye simu na kompyuta.. Soma Zaidi...

Kama simu a computer yako inastack
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kufanya endapo simu yako au computer itastack Soma Zaidi...

TEKNOLOJIA NA MAWASILIANO
Soma Zaidi...

KULINDA AKAUNT YAKO YA FACEBOOK DHIDI YA WAHALIFU WA KIMTANDAO
Watu wengi wanalalamika kuwa akaunti zao za facebook zimehakiwa, yaani zimeshambuliwa na wahalifu wa kimtandano. Soma Zaidi...

Matatizo katika hard disk
Posti hii inakwenda kukupa baadhi ya matatizo katika hard disk Soma Zaidi...

TEKNOLOJIA, HABARI NA MAWASILIANO
Soma Zaidi...

Kulinda account yako ya Facebook dhidi ya waharifu wa kimtandao
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kulinda account yako ya Facebook dhidi ya waharifu wa kimtandao Soma Zaidi...

JIFUNZE KUFUNGUA EMAIL KWA USAHIHI
Soma Zaidi...

KIPI KINGINE UTAFANYA UKIWA FACEBOOK: matumizi mengine ya facebook
Facebook ni mtandao wa kwanza wa kijamii (social media) unaotembelewa na watu wengi. Soma Zaidi...

Njia rahisi ya kudownload video YouTube
Posti hii inakwenda kukuelekeza kuhusu njia rahisi ya kudownload video YouTube Soma Zaidi...

Chanzo
Jifunze matumizi ya simu yako na namna ya kutatua matatizo mbalimbali kwenye simu na kompyuta.. Soma Zaidi...