picha

Mambo yanayohitajika kabla ya kuanza upasuaji

Posti hii inahusu zaidi mambo yanayohitajika kabla ya kuanza upasuaji ni mambo muhimu ambayo yanapaswa kufanyika kwanza na baadaye upasuaji unaweza kuendelea.

Mambo yanayopaswa kufanyika kabla ya kuanza upasuaji.

1.Kwanza kabisa mazingira yanapaswa kuandaliwa.

Kuhakikisha kuwa chumba kimeandaliwa vizuri na kumfanya mgonjwa ajisikie huru, kuhakikisha kubwa hakuna alama yoyote ya kuwepo kwa maambukizi na kuwepo usalama katika chumba hicho na kuhakikisha kwamba kila mgonjwa anakuwa na utofauti na mwingine katika maandalizi hii inategemea na hali ya mgonjwa na Ugonjwa alio nao.

 

2.Kuandaa vifaa vyote vinavyohitajika wakati wa upasuaji.

Hivi vifaa vinaandaliwa na mhudumu maalumu ambaye amechaguliwa kuandaa vifaa hivyo na kuhakikisha kubwa vifaa vinaandaliwa kadri ya  ugonjwa alionao au kadri ya hali ya mgonjwa kwa hiyo kila hospitali inapaswa kuwa na vifaa vya kutosha ambapo akitoka mgonjwa huyu anaingia mwingine na seti za vifaa vinavyotumika ni tofauti tofauti ili kuweza kuepuka Maambukizi.

 

3. Kumwandaa mgonjwa.

Hii ni hatua ya msingi sana ambapo wahudumu wanapaswa kumwandaa mgonjwa na kumhakikishia kuwa upasuaji utaenda vizuri na kumwambia kwa nini wanafanya upasuaji na kuhakikisha kuwa mgonjwa anasaini fomu maalumu kwa ajili ya kukubali kuwa upasuaji ufanyike na kupima vipimo vyote kama vile mapigo ya moyo, upumuaji, msukumo wa damu na joto la mwili kabla ya kufanyika upasuaji wowote ule.

 

4.Maandalizi ya wahudumu.

Na wahudumu wenyewe wanapaswa kujiandaa kwa kila mtu na kazi yake kuhakikisha kuwa dawa zinazohitajika zimepatiwa kwa mgonjwa , kuhakikisha kuwa fomu imesainiwa na kuandaa mavazi na kujua historia ya mgonjwa kama upasuaji ni wa kwanza au vipi na kuandaa dawa kwa ajili ya kumpatia dawa kadri ya uchaguzi wa mgonjwa au ushauri wa wahudumu.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/02/07/Monday - 09:01:30 pm Topic: Jifunze Main: Afya File: Download PDF Views 1319

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

kitabu cha afya

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
JIFUNZE NAMNA YA KUKABILIANA NA UGONJWA WA MAFUA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
afya somo la 15

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Kujiepusha na Vishawishi vya Zinaa

Kujiepusha na Vishawishi vya ZinaaKatika macho ya sheria kitendo cha zinaa kinahesabiwa pale wanapokutana kimwili mwanamume na mwanamke nje ya ndoa.

Soma Zaidi...
Dondoo za afya 1-20

Somo Hili linakwenda kukuletea dondoo mbalimbali za afya

Soma Zaidi...
TAHADHARI KWENYE VYAKULA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
MAWAKALA WA MARADHI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...