picha

Mambo yanayohitajika kabla ya kuanza upasuaji

Posti hii inahusu zaidi mambo yanayohitajika kabla ya kuanza upasuaji ni mambo muhimu ambayo yanapaswa kufanyika kwanza na baadaye upasuaji unaweza kuendelea.

Mambo yanayopaswa kufanyika kabla ya kuanza upasuaji.

1.Kwanza kabisa mazingira yanapaswa kuandaliwa.

Kuhakikisha kuwa chumba kimeandaliwa vizuri na kumfanya mgonjwa ajisikie huru, kuhakikisha kubwa hakuna alama yoyote ya kuwepo kwa maambukizi na kuwepo usalama katika chumba hicho na kuhakikisha kwamba kila mgonjwa anakuwa na utofauti na mwingine katika maandalizi hii inategemea na hali ya mgonjwa na Ugonjwa alio nao.

 

2.Kuandaa vifaa vyote vinavyohitajika wakati wa upasuaji.

Hivi vifaa vinaandaliwa na mhudumu maalumu ambaye amechaguliwa kuandaa vifaa hivyo na kuhakikisha kubwa vifaa vinaandaliwa kadri ya  ugonjwa alionao au kadri ya hali ya mgonjwa kwa hiyo kila hospitali inapaswa kuwa na vifaa vya kutosha ambapo akitoka mgonjwa huyu anaingia mwingine na seti za vifaa vinavyotumika ni tofauti tofauti ili kuweza kuepuka Maambukizi.

 

3. Kumwandaa mgonjwa.

Hii ni hatua ya msingi sana ambapo wahudumu wanapaswa kumwandaa mgonjwa na kumhakikishia kuwa upasuaji utaenda vizuri na kumwambia kwa nini wanafanya upasuaji na kuhakikisha kuwa mgonjwa anasaini fomu maalumu kwa ajili ya kukubali kuwa upasuaji ufanyike na kupima vipimo vyote kama vile mapigo ya moyo, upumuaji, msukumo wa damu na joto la mwili kabla ya kufanyika upasuaji wowote ule.

 

4.Maandalizi ya wahudumu.

Na wahudumu wenyewe wanapaswa kujiandaa kwa kila mtu na kazi yake kuhakikisha kuwa dawa zinazohitajika zimepatiwa kwa mgonjwa , kuhakikisha kuwa fomu imesainiwa na kuandaa mavazi na kujua historia ya mgonjwa kama upasuaji ni wa kwanza au vipi na kuandaa dawa kwa ajili ya kumpatia dawa kadri ya uchaguzi wa mgonjwa au ushauri wa wahudumu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 1510

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 web hosting     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

KIJUWE KISUKARI CHANZO CHAKE, DALILI ZAKE NA KUKABILIANA NACHO

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Dondoo za afya 1-20

Somo Hili linakwenda kukuletea dondoo mbalimbali za afya

Soma Zaidi...
darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
Nini hutokea unapokuwa kwenye ndoto ukiwa usingizini umelala

Ndoto ni moja ya mamba ambayo yanatokea mwanadamu na sayansi haina uelewa hasa nini hutokea. Hata hivyo yapo machache tafiti za kisayansi zinatueleza.

Soma Zaidi...
MAZINGIRA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kupiga push up kiafya

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kupiga push up kiafya, ni mambo au faida zipatikanazo ki afya kwa wapigaji wa push up kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...