image

Mambo yanayohitajika kabla ya kuanza upasuaji

Posti hii inahusu zaidi mambo yanayohitajika kabla ya kuanza upasuaji ni mambo muhimu ambayo yanapaswa kufanyika kwanza na baadaye upasuaji unaweza kuendelea.

Mambo yanayopaswa kufanyika kabla ya kuanza upasuaji.

1.Kwanza kabisa mazingira yanapaswa kuandaliwa.

Kuhakikisha kuwa chumba kimeandaliwa vizuri na kumfanya mgonjwa ajisikie huru, kuhakikisha kubwa hakuna alama yoyote ya kuwepo kwa maambukizi na kuwepo usalama katika chumba hicho na kuhakikisha kwamba kila mgonjwa anakuwa na utofauti na mwingine katika maandalizi hii inategemea na hali ya mgonjwa na Ugonjwa alio nao.

 

2.Kuandaa vifaa vyote vinavyohitajika wakati wa upasuaji.

Hivi vifaa vinaandaliwa na mhudumu maalumu ambaye amechaguliwa kuandaa vifaa hivyo na kuhakikisha kubwa vifaa vinaandaliwa kadri ya  ugonjwa alionao au kadri ya hali ya mgonjwa kwa hiyo kila hospitali inapaswa kuwa na vifaa vya kutosha ambapo akitoka mgonjwa huyu anaingia mwingine na seti za vifaa vinavyotumika ni tofauti tofauti ili kuweza kuepuka Maambukizi.

 

3. Kumwandaa mgonjwa.

Hii ni hatua ya msingi sana ambapo wahudumu wanapaswa kumwandaa mgonjwa na kumhakikishia kuwa upasuaji utaenda vizuri na kumwambia kwa nini wanafanya upasuaji na kuhakikisha kuwa mgonjwa anasaini fomu maalumu kwa ajili ya kukubali kuwa upasuaji ufanyike na kupima vipimo vyote kama vile mapigo ya moyo, upumuaji, msukumo wa damu na joto la mwili kabla ya kufanyika upasuaji wowote ule.

 

4.Maandalizi ya wahudumu.

Na wahudumu wenyewe wanapaswa kujiandaa kwa kila mtu na kazi yake kuhakikisha kuwa dawa zinazohitajika zimepatiwa kwa mgonjwa , kuhakikisha kuwa fomu imesainiwa na kuandaa mavazi na kujua historia ya mgonjwa kama upasuaji ni wa kwanza au vipi na kuandaa dawa kwa ajili ya kumpatia dawa kadri ya uchaguzi wa mgonjwa au ushauri wa wahudumu.



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/02/07/Monday - 09:01:30 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 687


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

darasa la lishe
Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe Soma Zaidi...

Dondoo 100 za Afya
Soma Zaidi...

SHUGHULI ZA KILA SIKU
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

darasa la lishe
Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe Soma Zaidi...

matunda na mboga
Soma Zaidi...

ZIJUWE NYANJA KUU 6 ZA AFYA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

Kitabu Cha Magonjwa Sugu
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

MAZINGIRA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

NIJUZE KUHUSU AFYA
Soma Zaidi...

Dondoo za afya 81-100
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dondoo za afya Soma Zaidi...

KAULI ZA WATU MASHUHURI KUHUSU AFYA
Soma Zaidi...

MAWAKALA WA KUSABABISHA NA KUSAMBAZA MARADHI
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...