HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

SURA YA SABA
HUKUMU ZA TAFKHIM NA TARQIQ AT-TAFKHIYM NA AT-TARQIYQ
1.At-Tarqiyq - Kufanya Nyembamba au Nyepesi
Ni kuitamka herufi kwa kuifanya nyembaba au nyepesi. Hali hii hutokea wakati ulimi uanapokuwa mbali na sakafu la kinywa yaani ulimu unakuwa chini. Tarqiyq hutokea katika herufi za chini yaani إسْتِفال (isfal-herufi za kuinamisha) isipokuwa isipokuwa herufi mbili ر na ل.
2.At-Tafkhiym - Kufanya Nene Au Nzito
Hutokea pale inapotamkwa herufi kwa kuifanya kuwa nene au nzito. Hukumu hii hutokea kwa zile hurufi za اٌلإسْتِعْلاء al-isti’ala yaani herufi za kupanda. Herufi hizi hutamkwa wakati ulimu unapokuwa juu ya sakafu la kinywa.
TAFKHEEM

3.Baina ya Tafkhiym na Tarqiyq
Kuna baadhi ya herufi zinaweza kubeba hukumu zote mbili zilizotajwa hapo juu. Yaani wakati mwingine huwa taeqitq na wakati mwingine huwa tafkheem. Herufi hizo ni kama;-
i) Alif ( ا ) ya madd
ii) Laam ( ل ) ya Lafdhw Al-Jalaalah ( (لله
iii) Raa ( ر)
Laam ( ل ) ya Lafdhw Al-Jalaalah
Kawaida herufi ya ل ni nyepesi ila inapotokea katika jina la Allaah ( ,(سبحانه وتعالى hapo huwa ima ni tafkhiym au tarqiyq kutegemea na i’raab inayotangulia. Ikiwa jina la Allaah ( سبحانه وتعالى ) Limetanguliwa na herufi ya kasrah au ي (yaa) saakinah, hutamkwa kwa tarqiyq. Ama jina la Allaah ( (سبحانه وتعالى Linapotanguliwa na fat-hah, dhwammah au و (waaw) saakinah linatamkwa kwa tafkhiym.
TAFKHEEM

At-Tafkhiym na At-Tarqiyq katika ( ر ) Raa
Halikadhalika herufi hii raa inaweza kuwa nzito au nyepesi, nene au nyembamba kulingana na kanuni za tajweed. Hivyo basi itakuwa tafkhiym katika hali zifuatazo;-
1.itakapokuwa ina fataha au dhummah
2.Inakapokuwa na sakinah na nyuma yake kuna herufi yenye fataha au dhumah
3.Itakapokuwa na sakinah na nyuma yake kukawa na kasra na mbele yake kukawa na herufi za isti’laa
4.Itakapokuwa ina sakina na nyuma yake kukawa na hamzatul-waswl yaani hamza ya kuungia.
5.Itakaposimamiwa kwa sakina halafu nyuma yake kukawa na sakina na nyuma ya hiyo sakina kukawa na fataha au dhumah.

Pia itakuwa nyepezi au nyembaba itakapokutana na hali zifuatazo;-
1.itakapokuwa na kasra
2.Itakapokuwa na sakina na nyuma yake kuna fataha
3.Itakaposimamiwa na sakina na kukawa nyuma yake kuna sakina iliyotanguliwa na kasra.
4.- 5 Inayoitwa الراء الممالة (ar-raa al-mumaalah) ambayo inasomwa kwa vokali ya ‘e’ badala ya kasrah. Hii ni kutokana na riwaayah ya Hafsw ‘an Aaswim. Nayo ni katika neno la pekee katika Qur-aan, na huwa ni ya tarqiyq inapatikana katika surat hud aya ya 41 (11:41)


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1824

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Hukumu za waqfu na Ibtida

waqfu ni misimamo ambapo msomaji wa Quran anaruhusiwa kusimama, kuhema au kumeza mate. Na ibtidai ni kuanza baada ya kutoka kwenye waqf

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al Mauun

Sura hii ni katika sura ambazo zinahitaji kusomwa kwa mazingatio sana. Wanaoswali bila ya kuzingatia swala zao, wameonywa vikali sana. Wanaowatesa na kuwanyanyasa mayatima wameonywa vikali. Wanaowanyima wenye haja na masikini huku wakiwakaripia nakuwasem

Soma Zaidi...
Quran na sayansi

3; Mchujo wa maji dhaliliKatika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha yakuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalilina pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran??

Soma Zaidi...
IDGHAAM KATIKA LAAM

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA

SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( مْ).

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa Surat At-Takaathur

Wanazuoni wengi zaidi wanakubaliana ya kuwa sura hii surat At-Takaathur ilishuka Makka, na hizi ndio sababu za kushuka kwa sura hii

Soma Zaidi...
sura ya 11

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Aina za Madda twabiy kwenye usomaji wa Quran

Madda zimegawanyika katika maeneo makuu mawili ambayo ni madda twabiy na madda fariy

Soma Zaidi...
Ni zipi hukumu za nuni yenye sakina au tanwin?

Hapa utajifunza usomaji wa Quran pindi utakapokuta nuni yenyebsakina au tanwin

Soma Zaidi...