TAHARUKI Siku hiyo kamaralzamani Feki alikuwa ufukweni kukaguwa mendeleo, alikuwa yeye na mke mwenzie.
TAHARUKI
Siku hiyo kamaralzamani Feki alikuwa ufukweni kukaguwa mendeleo, alikuwa yeye na mke mwenzie. Wakiwa wanakaguwa mara wakaona chombo kipya kinaingia. Wakasogea karibu. Ilikuwa ni kawaida ya kisiwa cha Serendib kuwa hakuuzwi bidhaa yeyote mpaka ikaguliwe. Katika ukaguzi ikafahamika kuwa mmilikiwa maboga hayupo kwenye dau. Baada ya kufuatilia kumbe alikimbiwa. Sasa bibi aliyejifanya Kamaralzaman akanunua maboga yale na kuwarudishia pesa ili wakampe mwenye maboga. Mzigo ukapelekwa kwa Binti mfalme wa Serendib kwa masharti kuwa asiyapasue mtu maboga kwani anataka kujifunsisha upishi wa maboga kutoka kwa mtoto wa Mfalme wa Nchi za China.
Basi baada ya kufanya kazi zao hapo wakarudi kwao na kuanza kuchambuwa maboga yao waanza upishi. Walikuwa wanatabia hii ya kupika wenyewe siku mojamoja. Watu walikuwa wakifurahi wakijuwa kuwa Kamaralzaman na me wake ndio wanapika. Ilikuwa haruhusiwa mtu kuingia jikoni wakati wawili hawa wanapika. Hii ilikuwa ni njia yao ya kufcha siri yao. Sasa wakiwa wameanza kuyachambuwa vyema maboga yao wakagundua kuna kitu. Walipopasua loo ni vipande vya dhahabu tupu walipolipasua lile kubwa bint mfalme wa nzi cha china alichikwa na butwaa kuona kamkufuu kake. Alifurahi sana akiamini kuwa sasa anakwenda kumuona mume wake. Akamueleza kila kitu kuhusu ule mkufu mke mwenzie.
Kwa haraka wakaagiza nahodha wa marekebu ile aitwe haraka. Alipokuja wakamwambia aende saa hivi akamchukuwe mwenye maboga bila hiyo mizigo yao na watu wote hawatatoka pale. Basi hakuwakuwa na budi ila ni kuanza safari ya kwenda kumchukuwa Kamarakzaman. Walipofuka kule walimbeba na kummalizia stori zote kwenye dau. Baada ya mwendo wa wiki mbili wakafika serendib. Kwa siri waliagizwa wamvalishe kitambaa sikijulikane. Moja kwa moja akachukuliwa na walinzi na kupelekwa kwa binti sultani. Hakujuwa kinachoendelea baada ya kuoga kuvaa nguo safi na kupata chakula kila mtu alikuwa akimuhedhimu akidhani ndio mume wa binti Sultani.
Alipomaliza kila kitu akachukuliwa kwa mabinti hawa wawili na kupewa habari nzima. Siku ilofata wakamuita mfalme na kumueleza kila kitu. Kwakweli walifurahi watu wote wa furaha kubwa sana. Pia walimsifu binti wa nchi za uchina kwa uvymilivu na ujasiri.basi ndoa ikafungwa tena hapa. Na Kamaralzaman akawa na wake wawili. Aliweza kupata watoto kutoka kwa wake zake wote. Watoto wake waliweza kurithi madaraka ya mababu zao. Baada ya miaka alirudi kwao Peshia na wake zake. Wajukuu zake alibakia kwa mababu zao waweze kuwaliwaza. Maisha ya Kamaralzaman na wawekake yalikuwa ni ya furaha sana.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Siku ya tano Nurdini alipata taarifa kutoka kwa watu wake yaani wafanyakazi wa chumba chake kuwa kuna binti mgeni ameletwa ila ametengewa sehemu yake maalumu.
Soma Zaidi...NDOA YA UTATA KISIWANI Mfalmee wa serendib alipouona msafara ule alivutiwa sana.
Soma Zaidi...Kama wasemavyo waliokula chumvi nyingi kuwa muomba mungu hachoki, basi waziri Faridi aliendelea kuomba Mungu hata siku moja akapata taarifa kuwa kuna watumwa wametokea nchi za Uajemi.
Soma Zaidi...Alikuwepo mfalme aliyetambulika kwa jina la Muhammad Suleiman Azeyn.
Soma Zaidi...Hadithi za Alif lela u lela kitabu cha tatu sehemu ya nane
Soma Zaidi...HADITHI YA CAMARALZAMANI PRINCE PEKEE Inapata mwendo wa safari ya siku 4 kwa farasi kutokea nchi ya Peshia alikuwepo mfalme maarufu sana aliyefahamika kwa jina la Shahzaman.
Soma Zaidi...NDOA YA HAMU Basi hali ikawa kama hivyo wawili hawa binamu na Kamaralzamani wakaanza kupanga njama ya kuweza kuondoka eneo lile kuelekea nchi za mbali kwa ajili ya kukutana na binti mfalme.
Soma Zaidi...