image

kamaralzamani

HADITHI YA CAMARALZAMANI PRINCE PEKEE Inapata mwendo wa safari ya siku 4 kwa farasi kutokea nchi ya Peshia alikuwepo mfalme maarufu sana aliyefahamika kwa jina la Shahzaman.

HADITHI YA CAMARALZAMANI PRINCE PEKEE
Inapata mwendo wa safari ya siku 4 kwa farasi kutokea nchi ya Peshia alikuwepo mfalme maarufu sana aliyefahamika kwa jina la Shahzaman. Mfalme huyu alikuwa ni mkarimu sana kwa mawaziriwake na kwa wananchi pia. Huwenda ukarimu ulizidi kwa sababu hakuwa na mtoto hata mmoja. Mfalme alikuwa na kila kitu lakini katika wake zake wanne wato hakuna hata aliyesubutu kupata walau mtoto mmoja. Mfalme aliendelea kutekeleza majukumu yake, laki I kuna muda huwa anakaa na kuwaza kuhusu mtoto ambaye angekuja kurithi madaraka yake. Fikra zake zote huwa hazina majibu sahihi. Wakati mwingine hudhani lamda wake zake ni matasa. Wakati mwingine hugombana na wake zake juu ya kupata mtoto.



Siku moja mfalme alimuita waziriwake mkuu na kumtaka shauri kuhusu swala la kupata mtoto. Waziri hakuwa namaneno mengin sana maana alitambuwa kuwa mfalme wake hakuwa mtu wa kuzunguka anapotaka jambo. Mfalme alipendelea sana mtu kuzungumza naye kwa uwazi na moja kwa moja bila ya kufichaficha maneno. Basi waziri akamshauri mfalme kwa kubwambia “mfalme, swala la kupata mtoto lipo nje ya uwezo wa binadamu ni Mungu pekee ndiye anaweza hivyo, nakushauri uwaite viongozi wa dini, uandae zawadi na sadaka, ili wakufanyie duwa, huwenda Mungu akakuhurumia”. mfalme aliupenda sana ushauri huo na akafanya kama alivyoelezwa. Zawadi mbalimbali aliandaa na sadaka pia.




Ijumaa iliyofuwata kundi kubwa la viongozi wa dini likawasiri. Duwa kubwa ikafanywa na zawadi zikatolewa. Sadaka mbalimbali zilitolewa ikiwemo chakula, dhahabu, vifaa vya nymbani na pesa. Hakika watu walifurahi sana. Huwenda hata Mwenyezi Mungu alifurahi pia, hivyo haukupita mwezi mke mkubwa wa mfalme akapata ujauzito. Furaha ilitawala kwa wananchi, viongozi walioomba duwa na viongozi wa nchi. Furaha zaidi ni kwa mfalme. Hatimaye miezi 9 ikatimia. Ndani ya kasri la Mfalme Shahzaman mtoto wa kiume akazaliwa.



Kwa kuwa malezi ya ujauzito yalikuwa vyema, basi mtoto alikuwa na afya nzuri na mwenye sura nzuri ya utotoni. Jina alilopewa lilikuwa ni Kamaralzamani yaani mwezi wa nchi. Viongozi walioomba duwa wakampa jina la uani kama badrudin. Mtoto huyu alilelewa katika maisha ya furaha sanna kwa kuwa alikuwa ni wa pekee na ni wa kiume pia. Kila alipokuwa maisha yake yote yalikuwa yakifuatiliwa kila hatuwa. Walimu wake walikuwa ni bora zaidi kuliko walimu wa watoto wa mawaziri.usiku asingeweza kung’atwa hata na upepe kama ungeliuwa unag’ata. Alikuwa akilindwa muda wote.


Kamaral zamani au Badrudin kama walivyomuita wengine, licha ya kuwa anapendwa na watu kwa upekee wake na kuwa ni mtoto wa mfalme, lakini pia alikuwa na sura nzuri sana. Mabinti watoto wa mawaziri walikuwa wakimfananisha uzuri wake kama mwezi yaani aling’aa sana. Haikuwa kawaida kwa mtoto wa kiume kuwa mzuri kiasi kile lakini ilitokea hivyo kwa kamaralzamani. Maisha yalikwenda vyema hata kamaralzamani alipoingia umri wa kubalehe. Mabinti hawakuweza kupata kile walichotarajia kutoka kwa kamaralzamani, ijapokuwa walijiweka karibu sana naye.


Siku moja mfalme akamuita waziri wake na kumwambia kuna “ninataka kujivuwa madaraka ya ufalme na kumpatia kamaralzamani, je unaonaje jambo hili”. waziri alikaa kimya kwa muda huku akifikiri jibu sahihi. Kisha akasema “ni wazo zuri ewe mfalme, ila mimi sikubaliani nalo kwa saababu kuu tatu, kwanza wewe bado una nguvu na uwezo wa kuliongoza taifa bado unao na ni mkubwa. Pili Kamaralzamani bado ni mdogo,hajajuwa siasa wala hajawahi kuongoza. Tatu unaonaje kwanza Kamaralzamani angeoa hii ingemletea heshima kubwa hata kabla ya kuwa mfalme.”. hoja hizi alizikubali mfalme, hivyo akatamani aanze na kumuozesha mwanaye kwanza. Pia Kamaralzamani aanze kuhudhuria vikao vya kiuongozi pamoja na mawaziri, ashiriki kwenye majukumu na kutowa maamuzi.



Basi siku ilifata mfalme akamuita mtoto wake Kamaralzaman na kumwambia “mwanangu tambuwa kuwa wewe ndio mtoto wangu wa pekee, nakupendasana kijana changu. Ninataka kuwanzia kesho uhudhurie vikao vya mabaraza yote ya mawaziri, na ushiriki katika kutoa maamuzi.” kijana alionekana kupenda sana wazo hili, kanakwamba alikuwa anaisubiria siku kama hii toka zamani. Ukweli ni kuwa kijana alikuwa ana akili sana na mwenye busara. “nimekubali baba, na nitatii kwa umakini na katu sintokuangusha katika hili” yalikuwa ni maneno ya Kamaral zamani.swa hilo ni moja ila pia kuna jingine. Ni lipi hilo babi. Mfalme alikaa kimya kwa muda.


Baada ya kupiga kutwi ya maji mfalme akatamka “mwanangu, natambuwa sasa umeshaingia utu uzima, ninataka nikupatie mke, je unalionaje jambo hili”? kamaral zamani alinyamaza kwa muda kana kwamba ana mzingo mzito wa mawazo. “baba wazo lako nimelisikia ila kwa sasa sijatamani kutekeleza hilo jambo. Huwenda baada ya muda nitakuwa na wazo hili, ila kwa sasa naomba unipe muda nifikirie.” yalikuwa ni majibu ambayo mfalme hakupendezewa nayo.


Basi mfalme akakutana tena na waziri wake na kumueleza yaliyotokea. Waziri akaendelea kumsisitiza mfalme awe na subira. Kwani alishakuwa na subira sana toka hana mtoto mpaka akapata. Waziri alimsisitiza ampe mwaka mzima ili aendelee kuwa na subira. Lengo la waziri ni kuwa mpaka mwaka kufika binti yake atakuwa tayari kuolewa na ataweza kutengeneza mazingira ya kuwakutanisha wawili hawa. Mfalme hakuelewa mawazo ya waziri. Mfalme alikubaliana na ushauri ule.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 89


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

HATMA YA NURDINI NA NCHI YAKE
Hadithi za alif lela u lela kitabu cha tatu sehemu ya 9 Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 03: Nurdini na Mtumwa
Siku ya tano Nurdini alipata taarifa kutoka kwa watu wake yaani wafanyakazi wa chumba chake kuwa kuna binti mgeni ameletwa ila ametengewa sehemu yake maalumu. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 03: Mtumwa wa Gharama
Kama wasemavyo waliokula chumvi nyingi kuwa muomba mungu hachoki, basi waziri Faridi aliendelea kuomba Mungu hata siku moja akapata taarifa kuwa kuna watumwa wametokea nchi za Uajemi. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 04: Mtihani wa Nurdini
Mama aliendelea kugomba sana kisha akamfungia binti ndani na kuweka walinznwa kiume, kisha akawaambia “haruhusiwi kuingia wala kutoka yeyote humu ndnai, hata mbwa Nurdini” neno mbwa lilimtoka tu mama Nurdini kisha akajilaumu kwa kumfana nisha ... Soma Zaidi...

Kamaralzaman arudi kwao
SAFARI YA KURUDI NYUMBANI Kamaralzamani siku hiyo akamfuata baba mkwe wake na kmueleza ukweli wa mambo na kuwa yeye si mganga. Soma Zaidi...

Ndoa ya utata ya Kamaralzaman
NDOA YA UTATA KISIWANI Mfalmee wa serendib alipouona msafara ule alivutiwa sana. Soma Zaidi...

TAHARUKI YA MFALME WA BAGHADANI
Soma Zaidi...

kamaralzamani
HADITHI YA CAMARALZAMANI PRINCE PEKEE Inapata mwendo wa safari ya siku 4 kwa farasi kutokea nchi ya Peshia alikuwepo mfalme maarufu sana aliyefahamika kwa jina la Shahzaman. Soma Zaidi...

Taharuki na mwisho wa Kmaralzaman Feki
TAHARUKI Siku hiyo kamaralzamani Feki alikuwa ufukweni kukaguwa mendeleo, alikuwa yeye na mke mwenzie. Soma Zaidi...

Kamaralzaman akiwa katika ndoto ya kweli
NDOTO AMA KWELI? Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 05: Rafiki wa Kweli
Mungu ashukuriwe sana, hatimaye miezi kadhaa ikapita bila ya waziri Masoud kugundua siri nzito. Soma Zaidi...

HADITHI ZA ALIF LELA U LELA KITABU CHA TATU: HADITHI YA NURDINI
Soma Zaidi...