Kamaralzaman akiwa katika ndoto ya kweli

NDOTO AMA KWELI?

Kamaralzaman akiwa katika ndoto ya kweli

NDOTO AMA KWELI?
Siku zikaenda hatimaye mwaka ukafika. Kamaralzamani akiwa bado anafikiria na kuwazuwa. Hatimaye mfalme akamuita tena na kumwambia “mwanangu, numekupa muda mrefu wa kusubiria jibu lako. Natamani sasa ni muda wa wewe kutoa maamuzi”. kamaralzamani akamueleza kuwa “baba bado sijafikiri kuoa, kwani bado sijaona anayenifaa na aliyenipendeza”. majibu haya yalikuwa kama mwiba kwenye masikio ya Mfalme.


Mwanangu mwaka mzima umeshindwa kumpata wa kukufaa. Ni maneno ya masikitiko ya mfalme. Mfalme akaondoka kwa jazba huku akimueleza kuwa kesho atatakiwa atoe maamuzi yake ya mwisho kabla ya kulazimishwa. Mfalme akamuendea mkewake na kumueleza hali nzima kisha akamtaka ashiriki katika kumshauri mtoto waokipenzi. Malkia alimuita Kamaralzamani na kumtaka azungumze bila ya kificho kuhusu kinachomsubuwa.


“mama sitoweza kuoa mwanamke nisiyempenda, tambuwa kuwa maamuzi ya ndoa ni maamuzi ya kimaisha eidha nijefurahia maisha ama niwe katika dhiki. Nitakapomuona atakayenipendeza nitakuwa tayari kuoa” ni maneno ya Kamaral zamani akimueleza mama yake. Kesho mfalme akamuita tena Kamaralzamani ili kujuwa maamuzi yake ya mwisho. Kamaralzamani akamueleza baba yake yale yale aliyomueleza mama yake. Mfalme alikasirika sana. Mfalme alitamani sana kumuona mjukuu wake haraka iwezekanavtyo.


Mfalme akaagiza kuwa Kamaralzamani afungiwe kwenye nyumba yake iliyo mbali na ikilu na ulinzi mkali uwe hapo. Asiruhusiwe kutoka nje mpaka pale atakapobadili maamuzi yake. Kwa upande mwingine Kamaralzamani alifurahia maamuzi haya kwa ni sasa angeweza kupata muda mwingi kusoma vitabu na kupumzika. Ijapokuwa kwa waliozoea kuchakarika kuambiwa uwe sehemu moja ni adhabu tosha. Basi mambo yakawa hivyo kama alivyotaka mfalme. Na Kamaralzamani aliwekwa ulinzini hata ikatimia wiki.


Katika lijumba ambalo kamaralzamani amefungiwa kulikuwa na kisima cha zamani sana. Kisima hicho inasemekana ina miaka kati ya 30 mpaka 50. hakuna aliyeweza kudhibiti vyema hesabu ya kisima hicho. Katka kisima hicho kuliishi familia moja kubwa ya majini. Jini Maimuna akiwa ni mmoja wapo wa majini hao. Sikumoja usiku jini naimuna alitoka kwenye kisima. Aliingia ndani ya jumba hilo na kukuta sura ngeni. Loo alikuwa ni kijana mwenye sura nzuri kamwe hajapatapo kutokea katika nchi ile.


Jini maimuna alistaajabu sana kwa uzuri wa kijana hata akatamani angelikuwa yeye binadamu aolewe. Baada ya kustaajabu kwa muda mrefu Maimuna aliondoka na kupotelea angani akielekea nchi za mashariki ya mbali, hata akafika mipakani mwa china na India, pembezoni mwa milima mirefu sana. Huko akakutana na jini Makata. Jini makata alikuwa na nguvu sana na mbawa zake zilikuwa na sauti za kunguruma hewani. Jini maimuna aliogopa sana kwani hakuwa na amani mbele ya jini makata.


Makata: “unatoka wapi maimuna” Natokea nchi za mashariki ya kati” Je una mpya yeyote unisimulie”, ndio nimekuytana na akijana Mzuri sana huko nitokako, kwa uzuri huo hata mwanamke wa kumzidi hajapatikana.na kijana huyo ni wa kiume” “ wee basi kijana wako hawezi kushinda uzuri wa binti niliyemuona huko kwa mfalme wa china, uzuri ambao duniani hajapatapo kutokea zaidi yake” yalikuwa ni majibizano kati ya makata na Mainuna.


Siku zoyte makata alikuwa anashinda kwenye ugomvi wa majibishano kutokana na ukubwa wake, ujeuri, hasira na uwezo wake wa kubishana. Lakini leo maimuna nae aliendelea kukomaa na ubishi. Mwisho wa mapishano waliamuwa kutafuta suluhu.wakaamuwa kumtafuta mwenzao awasuluhishe mgogoro wao. Katika kupitapita ndipo wakakutana na Subiani jini wa Misituni. Baada ya kuelezwa ugomvi subiani akaamuwa kuwakutanisha vijana wote wawili kisha aamshwe mmojammoja, atakayestaajabu zaidi kwa mwenzie atakuwamshindi wa pili.


Basi wakamchukuwa Binti wa china na kumpeleka mashariki ya kati kwa kamaralzamani. Katika kitanda kimoja wakawalaza. Wakaanza kumuamsha binti, aliyejulikana kwam jiana la Nurati. Alipoamshwa alistaajabu sana kuona kuna kijana mzuri sana pembeni yake. Nurat alitokea kumpenda palepale kijana yule, akachukuwa pete mbili alizokuwa nazo kisha akamvisha pete moja kama ishara ya upendo. Hapo majini wale wakampulizia usingizi na akalala fofofo.


Kisha wakamuamsha kamaralzamani naye alistaajabu kama alivyostaajabu mwenzie. Akajiuta ana pete kama ya yile binti pale alipolala. Pete zilifanana. Kamaralzamani akajuwakuwa ni huyu binti amemvalisha. Kisha wale majini wakampulizia usingizi naye akalala fofofo. Majini hawa wakamrudisha Nurat huko walikomtoa na Kamaralzamani wakamrudisha kwenye kitanda chake. Majini walipata suluhisho kuwa wote wawili ni wazuri sana hakuna aliyemzidi mwenzie maana wanafanana sura zao. Majini wale waliondoka huku wamesahau kuaachanisha zile pete zao.


Asubuhi kamaralzamani anaamka akawaza alichokiona jana, akaangalia godoro tupu. Mwanzo akajiwa ni ndoto tu lakini alipoangalia kidoleni mwake kuna pete akajuwa ni kweli si ndoto. Hali kama hii nayo ilikuwa kwa binti wa mfalme wa nzchi za mashariki ya mbali Nurat ambaye naye alijuwa ni ndoto ila alipoona pete hana amebakiwa na moja akajuwa ni kweli.



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 233


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

kamaralzamani
HADITHI YA CAMARALZAMANI PRINCE PEKEE Inapata mwendo wa safari ya siku 4 kwa farasi kutokea nchi ya Peshia alikuwepo mfalme maarufu sana aliyefahamika kwa jina la Shahzaman. Soma Zaidi...

TAHARUKI YA MFALME WA BAGHADANI
Soma Zaidi...

NURDINI ANARUDI KWAO NA BARUA YA MFALME WA BAGHADAD
Hadithi za Alif lela u lela kitabu cha tatu sehemu ya nane Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 03: Nurdini na Mtumwa
Siku ya tano Nurdini alipata taarifa kutoka kwa watu wake yaani wafanyakazi wa chumba chake kuwa kuna binti mgeni ameletwa ila ametengewa sehemu yake maalumu. Soma Zaidi...

ASUBUHI YA VARANGATI NA KAMARALZAMAN
VARANGATI ASUBUHI; Baada ya kugunduwa kuwa haikuwa ndoto kamaralzamani aliamini kuwa yule ndio mke ambaye baba yake alimchagulia. Soma Zaidi...

Ndoa ya utata ya Kamaralzaman
NDOA YA UTATA KISIWANI Mfalmee wa serendib alipouona msafara ule alivutiwa sana. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 04: Mtihani wa Nurdini
Mama aliendelea kugomba sana kisha akamfungia binti ndani na kuweka walinznwa kiume, kisha akawaambia 'haruhusiwi kuingia wala kutoka yeyote humu ndnai, hata mbwa Nurdini' neno mbwa lilimtoka tu mama Nurdini kisha akajilaumu kwa kumfana nisha ... Soma Zaidi...

Kamaralzaman arudi kwao
SAFARI YA KURUDI NYUMBANI Kamaralzamani siku hiyo akamfuata baba mkwe wake na kmueleza ukweli wa mambo na kuwa yeye si mganga. Soma Zaidi...

Ndoa ya kwanza ya kamaralzamani
NDOA YA HAMU Basi hali ikawa kama hivyo wawili hawa binamu na Kamaralzamani wakaanza kupanga njama ya kuweza kuondoka eneo lile kuelekea nchi za mbali kwa ajili ya kukutana na binti mfalme. Soma Zaidi...

Taharuki na mwisho wa Kmaralzaman Feki
TAHARUKI Siku hiyo kamaralzamani Feki alikuwa ufukweni kukaguwa mendeleo, alikuwa yeye na mke mwenzie. Soma Zaidi...

HADITHI ZA ALIF LELA U LELA KITABU CHA TATU: HADITHI YA NURDINI
Soma Zaidi...

HATMA YA NURDINI NA NCHI YAKE
Hadithi za alif lela u lela kitabu cha tatu sehemu ya 9 Soma Zaidi...