image

Kamaralzaman arudi kwao

SAFARI YA KURUDI NYUMBANI Kamaralzamani siku hiyo akamfuata baba mkwe wake na kmueleza ukweli wa mambo na kuwa yeye si mganga.

Kamaralzaman arudi kwao

SAFARI YA KURUDI NYUMBANI
Kamaralzamani siku hiyo akamfuata baba mkwe wake na kmueleza ukweli wa mambo na kuwa yeye si mganga. Historia hii ilibidi iandikwe kwa wino wa dhahabu na ihifadhiwe kwenye kumbukumbu za kifalme. Mfalme alifurahi sana baada y akusikia kuwa Kamaralzamani alikuwa ni mtoto wa mfalme wa nchi ya Peshia. Basi baada ya mazungumzo Kamaralzamani akaomba apewe ruhusa ya kwenda nyumbani kwenda kuwaona wazazi. Hakukuwa na kipingamizi kwa upande wa sultani hivyo akawakubalia waende ila alipenda zaidi warudi wote kwa pamoja.


Safari ikaanza kutoka nchi za mbali kuelekea Peshia. Wakiwa kwenye gaei la kuendeshwa na farasi wawili, kijumba kidogo kilichobeba watu wawili kilikuwa kikikokotwa taratibu. Kwenye kidole kimoja kati ya kila mmoja kuna pete yenye kupendeza sana. Shingoni mwa binti sultani kulikuwa na mkufu wenye cheni ya dhahabu lakini ua kifurushi kinning;inia. Unaweza kusema ni kijiwe chenye thamani sana lakini ukweli wa mambo kuna siri nzito ndani yake. Wawili hawa walikwenda hata siku inaisha wakalala na siku inayofaa ikaisha wakalala tena. Kutoka kwao mpaja Peshia wataweza kuchukuwa mwendowa mwezi mmoja kutokana na mwendo wao.


Siku ya 6 ya safari walipumzika chini ya mti wakati wa jioni. Kamaralzamani akiwa anamsifia mewe aliyelala uzuri wake. Ghafla akataka kujuwa kuna nini kwenye kile kifurushi kilicho kwenye shingo ya binti sultani. Alipomvua kwa upole sasa wakati anakiangalia akaja panya na kukibeba akizani ni nyama ama chakula. Panya yule alitoka nje ya hema na kuelekea msituni. Kamaralzamani akiwa anamfarilia panya yule ghafla panya akabebwa na bund. Kamaralzamani akawa sasa anamkimbiza bundi ambaye alimeza kale kafurushi alipokuwa anajaribu kumla panya. Kamaralzamani akiwa anamkimbiza pundi ghafla budi yule aling’atwa na nyoka aliwa juu ya mti. Alipoangauka alibebwa na kunguru mmoja mkubwa sana. Ukubwa wa knguru huyu si wa kawaida.


Bundi alianza kuliwa. Kamaralzamani hakuweza kufanya kitu maana alipomchukuwa akakwea ne juu sana ya mtu. Sasa Kamaralzamani akasubiri chini ya mti eidha mkufu uanguke ama atakaposhiba ataweza kumpata. Kwa kuwa kunguru anapeda kula utumbo kuliko nyama, aliweza kuumeza mkufu na kuanguasha chini mzoga mtupu. Sasa Kamaralzamani akawa anamkimbiza kunguru. Usiku ukaingia wote wakalala kunguru juu ya mti na kamaralzamani chini. Aubuhi kamaralzamani akaanza kumtafuta tena na kuendelea kumkimbiza. Hadi alipokata tamaa akakumbuka kumbe alikuwa akisafiri na binti sultani. Loo hakuwa na la kufanya na hata njia aliisahau.


Loo kamaralzamani yupo matatizoni sasa. Akaanza japo kutafuta pa kutokea baada ya mwendo wa siku moja na nusu mcha na akakuta kuna kijiji karibu. Akaona kuna nyumba ipo pale. Akapiga hodi na kuanza kujieleza alipotoka na anapokwenda. Yule mzee aliyemlkuta kwenye kibanda kle akamueleza kuwa kutoka hapa mpaka huko unakokusema ni mwendo wa mwezi, na hakuna njia zaidi ya kupitia baharini. Na hapa tulipo dau la kwenda huko kuja kila baada ya mwaka mmoja. Hivyo kwenda huko usubiri mpaka mwaka uingi emaana dau limeondoka yapata siku tatu nyuma.


Kwa hali hii kamaralzamani alianza kuishi kwa huyu mzee maisha mapya. Kwa upande wa binti sultani aliweza kumsubiri kamaralzamani pela kwa siku mbili. Aliogunduwa kuwa mumewe hayupo hakutaka watu waelewe siri ile. Basi kwa kuwa walikuwa wakifanana aliachukuwa nguo za mumewe na kuzivaa. Alikuwa kama vile yeye ndie Kamaralzammani. Safari ikaanza. Kale kafurushi kalikuwa ni hirizi aliyopewa na mmoja kati ya waganga na akamwambia ukikapoteza kahirizi haka ujuwe hutoweza kuishi maisha ya furaha kamwe. Na hii ndio sababu ya kuwa alikuwa akikavaa kahirizi kale huku watu wakajuwa ni mkufu. Sasa kahirizi hakapo tena na mumewe hauypo tena wapi atapata furaha?


Walipofika kisiwa cha Serendib wakaomba kuvushwa. Ilikuwa ni lazima uruhusiwe na mfalme ama waziri ama kwa ushahidi maalumu ndio utoke nje ya kisiwa hiki. Hakuna njia ya mkato ila mpaka ukatishe kisiwa hii. Siku hiyo mfalme wa kisiwa hiki alikuwa akitembea maeneo ya baharini. Mfalme huyu alikuwa naye hana mtoto wa kiume na ana wa kike mmoja tu. Siku zote alikuwa akimtaka mwanae aolewe lakini mtoto hakutaka kuolewa. Mtoto stori yake ni kama wenzie alitaka mchumba ambaye atakuwa anampenda yeye na si kwa sababu ya madaraka ya baba. Hivyo alikuwa kila akiletewa mchumba hakubali. Naye ikafikia hatuwa ya kufungiwa ndani.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 293


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

HADITHI YA NURDINI 05: Rafiki wa Kweli
Mungu ashukuriwe sana, hatimaye miezi kadhaa ikapita bila ya waziri Masoud kugundua siri nzito. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 03: Mtumwa wa Gharama
Kama wasemavyo waliokula chumvi nyingi kuwa muomba mungu hachoki, basi waziri Faridi aliendelea kuomba Mungu hata siku moja akapata taarifa kuwa kuna watumwa wametokea nchi za Uajemi. Soma Zaidi...

ASUBUHI YA VARANGATI NA KAMARALZAMAN
VARANGATI ASUBUHI; Baada ya kugunduwa kuwa haikuwa ndoto kamaralzamani aliamini kuwa yule ndio mke ambaye baba yake alimchagulia. Soma Zaidi...

Ndoa ya kwanza ya kamaralzamani
NDOA YA HAMU Basi hali ikawa kama hivyo wawili hawa binamu na Kamaralzamani wakaanza kupanga njama ya kuweza kuondoka eneo lile kuelekea nchi za mbali kwa ajili ya kukutana na binti mfalme. Soma Zaidi...

HATMA YA NURDINI NA NCHI YAKE
Hadithi za alif lela u lela kitabu cha tatu sehemu ya 9 Soma Zaidi...

Taharuki na mwisho wa Kmaralzaman Feki
TAHARUKI Siku hiyo kamaralzamani Feki alikuwa ufukweni kukaguwa mendeleo, alikuwa yeye na mke mwenzie. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 03: Nurdini na Mtumwa
Siku ya tano Nurdini alipata taarifa kutoka kwa watu wake yaani wafanyakazi wa chumba chake kuwa kuna binti mgeni ameletwa ila ametengewa sehemu yake maalumu. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 02: mawaziri wa Mfalme
Alikuwepo mfalme aliyetambulika kwa jina la Muhammad Suleiman Azeyn. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 04: Mtihani wa Nurdini
Mama aliendelea kugomba sana kisha akamfungia binti ndani na kuweka walinznwa kiume, kisha akawaambia “haruhusiwi kuingia wala kutoka yeyote humu ndnai, hata mbwa Nurdini” neno mbwa lilimtoka tu mama Nurdini kisha akajilaumu kwa kumfana nisha ... Soma Zaidi...

Kamaralzaman akiwa katika ndoto ya kweli
NDOTO AMA KWELI? Soma Zaidi...

TAHARUKI YA MFALME WA BAGHADANI
Soma Zaidi...

Ndoa ya utata ya Kamaralzaman
NDOA YA UTATA KISIWANI Mfalmee wa serendib alipouona msafara ule alivutiwa sana. Soma Zaidi...