HADITHI YA NURDINI 03: Nurdini na Mtumwa

HADITHI YA NURDINI 03: Nurdini na Mtumwa

Siku ya tano Nurdini alipata taarifa kutoka kwa watu wake yaani wafanyakazi wa chumba chake kuwa kuna binti mgeni ameletwa ila ametengewa sehemu yake maalumu.

HADITHI YA NURDINI 03: Nurdini na Mtumwa

NURDINI AMLAGHAI MTUMWA.






Siku ya tano Nurdini alipata taarifa kutoka kwa watu wake yaani wafanyakazi wa chumba chake kuwa kuna binti mgeni ameletwa ila ametengewa sehemu yake maalumu. Na kuna walinzi wa kike hivyo haruhusiwi mwanaume yeyote kwenda hasahasa nurdini. Nurdini alitabasamu kusikia hivyo. Tabasamu lililowaacha wafanyakazi wa chumba chake mioyo yao kuwaenda mbio. hakikaNurdini alikuwa ni kijana mzuri. Sharubu zake fupi zilizokuwa zikichomoza kama mbegu za mpunga zinazoota sasa, pua iliuotokeza kwa mbele kidogo, mashavu yaliyojaza na kutengeneza uso usio duara kama wanawake wa nchi za Balkan.





Siku hiyo Nurdini hakuamua ubaya ila alitamani kwenda kumuona huyo mtumwa japo kwasiri. Alipenda kujiridhisha macho yake kama huyo mtumwa ni kiwango cha kuweza kuchukuliwa na mfalme kama ilivyokusudiwa na baba yake. Siku hiyo mtumwa alikwenda kuoga, Nurdin alitumia fursa hiyo kuingia chumbani kwa binti kisha akajificha nyuma ya pazia. Alipomaliza kuoga binti akaingia ndani, hapo Nurdini akajifanya anamtafuta mama yake. Wakati anaulizia yule binti akapatapo kusikia sautti ya kijana Nurdini, na hapo nafsi yake ikaingia udadisi kutaka kujuwa hasa kama sauti ya kijana huo imemridhisha kiasi kile vipi sura yake.





Binti akatoka kwenda varandani kumuona kijana aliyekuwa akimuuliza mama yake, Loo akakutana na sura nzuri. Hapo alitamani hata kumkumbatia, loo pepo la uchafu na hisia za uharibifu zikaanza kuzunguka kaiyao kama kibirinzi. Nurdini akajifanya kusema maneno ya uwongo “dah ivi wewe ndiye mtumwa ambaye baba yangu amekununua kwa ajili yangu, binti bila hata kufikiri akajibu “ndio bwana wangu”. Nurdini akasogea karibu, akamuangalia vyema, kisha akaongeza ukaribu hata pasibakie na nafasi kati yao. Nurdini akamuangalia vyema kisha akasema “kwa hakika baba amenichagulia mke na si mtumwa”





Maneno haya yalipenya ndani sana kwenye moyo wa binti na kuchokoa hisia zilizolala toka zamani sana. Kisha nurdini akaongeza “je utakubali kuwa mke wangu, ama kuwa mtumwa sehemu nyingine” nyundo ya mapenzi ikapenya ndani zaidi na kwenda kugonga msumari wa mapenzi uliokuwa umelegea kwenye moyo wa binti. Hapo akajikuta kuruhusu hisia zake kupokea Nurdini. Binti hakujibu kitu, ila kwa ishara ya macho Nurdini alishatambua jibu. Nurdini akamkumbatia na kumpusu, hapo binti akaanza kutetemeka. Hakuna hakika kama sababu I baridi, uwoga ama ndio mambo ymefana.





Wakiwa katika hali hiyo ghafla mlango ukafunguliwa na loo! Mama Nurdini akashuhudia wawili hawa wakiwa wamekumbatiana. Mama nurdini akaangalia vyema akagundua kuwa binti alikuwa bado amevaa zile nguo alizotoka nazo kuoga. Mama nurdini alikasirika sana, ila kwa upande wa pili aliona pia bora iwe hivi maana mwanzo alikuwa akimuonea wivu mtumwa kwa mumewe. Lakini sasa mwanaye ndiye amemchukuwa mtumwa kabla ya kufikishwa kwa mfalme. Kilichokuwa kikimpataaba mama ni kuwa mumwe wake mzee faridi atachukuwa maamuzi gani?





Nurdini kuona vile alikimbia kwa kumuogopa mama yake. Yule binti moyo ulimruka na kutamani ardhi ipasuke ili apotelee ardhini. Mama Nurdini alimpiga kibao kimoja kizito sana. “huna hata haya wewe, hivi ukaribu wote mume wangu aliokupa ndio unamuharibia hivyo, ataiweka wapi sura yake mume wangu pindi mfalme akigundua jambo hili, ivi unajuwa kuwa ulichokifanya unaweza kuhatarisha maisha ya familia nzima, ikiwemo huyo kibwana chako Nurdini, shetani mkubwa wewe” yalikuwa ni maneno ya mama Nurdini. Hakika yule mtumwa alijiona ni mkosaji sana. Kisha akasema “nisamehe mama, ila Nurdini ndio chaguo langu, la kwanza na ni la mwisho”.







Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 209


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

HADITHI YA NURDINI 03: Nurdini na Mtumwa
Siku ya tano Nurdini alipata taarifa kutoka kwa watu wake yaani wafanyakazi wa chumba chake kuwa kuna binti mgeni ameletwa ila ametengewa sehemu yake maalumu. Soma Zaidi...

Ndoa ya utata ya Kamaralzaman
NDOA YA UTATA KISIWANI Mfalmee wa serendib alipouona msafara ule alivutiwa sana. Soma Zaidi...

KWENYE BOSTANI LA MFALME WA
KATIKA BOSTANI LA KIFALME BAGHADADBasi Nurdini na mke wake bila hata ya kujuwa wapi watafikia waliingia kwenye mashua na kuwasili Baghada wakati wa jioni. Soma Zaidi...

NURDINI ANARUDI KWAO NA BARUA YA MFALME WA BAGHADAD
Hadithi za Alif lela u lela kitabu cha tatu sehemu ya nane Soma Zaidi...

Kamaralzaman akiwa katika ndoto ya kweli
NDOTO AMA KWELI? Soma Zaidi...

Kamaralzaman arudi kwao
SAFARI YA KURUDI NYUMBANI Kamaralzamani siku hiyo akamfuata baba mkwe wake na kmueleza ukweli wa mambo na kuwa yeye si mganga. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 03: Mtumwa wa Gharama
Kama wasemavyo waliokula chumvi nyingi kuwa muomba mungu hachoki, basi waziri Faridi aliendelea kuomba Mungu hata siku moja akapata taarifa kuwa kuna watumwa wametokea nchi za Uajemi. Soma Zaidi...

Ndoa ya kwanza ya kamaralzamani
NDOA YA HAMU Basi hali ikawa kama hivyo wawili hawa binamu na Kamaralzamani wakaanza kupanga njama ya kuweza kuondoka eneo lile kuelekea nchi za mbali kwa ajili ya kukutana na binti mfalme. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 04: Mtihani wa Nurdini
Mama aliendelea kugomba sana kisha akamfungia binti ndani na kuweka walinznwa kiume, kisha akawaambia 'haruhusiwi kuingia wala kutoka yeyote humu ndnai, hata mbwa Nurdini' neno mbwa lilimtoka tu mama Nurdini kisha akajilaumu kwa kumfana nisha ... Soma Zaidi...

TAHARUKI YA MFALME WA BAGHADANI
Soma Zaidi...

kamaralzamani
HADITHI YA CAMARALZAMANI PRINCE PEKEE Inapata mwendo wa safari ya siku 4 kwa farasi kutokea nchi ya Peshia alikuwepo mfalme maarufu sana aliyefahamika kwa jina la Shahzaman. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 05: Rafiki wa Kweli
Mungu ashukuriwe sana, hatimaye miezi kadhaa ikapita bila ya waziri Masoud kugundua siri nzito. Soma Zaidi...