HADITHI YA NURDINI 03: Nurdini na Mtumwa

HADITHI YA NURDINI 03: Nurdini na Mtumwa

Siku ya tano Nurdini alipata taarifa kutoka kwa watu wake yaani wafanyakazi wa chumba chake kuwa kuna binti mgeni ameletwa ila ametengewa sehemu yake maalumu.

HADITHI YA NURDINI 03: Nurdini na Mtumwa

NURDINI AMLAGHAI MTUMWA.






Siku ya tano Nurdini alipata taarifa kutoka kwa watu wake yaani wafanyakazi wa chumba chake kuwa kuna binti mgeni ameletwa ila ametengewa sehemu yake maalumu. Na kuna walinzi wa kike hivyo haruhusiwi mwanaume yeyote kwenda hasahasa nurdini. Nurdini alitabasamu kusikia hivyo. Tabasamu lililowaacha wafanyakazi wa chumba chake mioyo yao kuwaenda mbio. hakikaNurdini alikuwa ni kijana mzuri. Sharubu zake fupi zilizokuwa zikichomoza kama mbegu za mpunga zinazoota sasa, pua iliuotokeza kwa mbele kidogo, mashavu yaliyojaza na kutengeneza uso usio duara kama wanawake wa nchi za Balkan.





Siku hiyo Nurdini hakuamua ubaya ila alitamani kwenda kumuona huyo mtumwa japo kwasiri. Alipenda kujiridhisha macho yake kama huyo mtumwa ni kiwango cha kuweza kuchukuliwa na mfalme kama ilivyokusudiwa na baba yake. Siku hiyo mtumwa alikwenda kuoga, Nurdin alitumia fursa hiyo kuingia chumbani kwa binti kisha akajificha nyuma ya pazia. Alipomaliza kuoga binti akaingia ndani, hapo Nurdini akajifanya anamtafuta mama yake. Wakati anaulizia yule binti akapatapo kusikia sautti ya kijana Nurdini, na hapo nafsi yake ikaingia udadisi kutaka kujuwa hasa kama sauti ya kijana huo imemridhisha kiasi kile vipi sura yake.





Binti akatoka kwenda varandani kumuona kijana aliyekuwa akimuuliza mama yake, Loo akakutana na sura nzuri. Hapo alitamani hata kumkumbatia, loo pepo la uchafu na hisia za uharibifu zikaanza kuzunguka kaiyao kama kibirinzi. Nurdini akajifanya kusema maneno ya uwongo “dah ivi wewe ndiye mtumwa ambaye baba yangu amekununua kwa ajili yangu, binti bila hata kufikiri akajibu “ndio bwana wangu”. Nurdini akasogea karibu, akamuangalia vyema, kisha akaongeza ukaribu hata pasibakie na nafasi kati yao. Nurdini akamuangalia vyema kisha akasema “kwa hakika baba amenichagulia mke na si mtumwa”





Maneno haya yalipenya ndani sana kwenye moyo wa binti na kuchokoa hisia zilizolala toka zamani sana. Kisha nurdini akaongeza “je utakubali kuwa mke wangu, ama kuwa mtumwa sehemu nyingine” nyundo ya mapenzi ikapenya ndani zaidi na kwenda kugonga msumari wa mapenzi uliokuwa umelegea kwenye moyo wa binti. Hapo akajikuta kuruhusu hisia zake kupokea Nurdini. Binti hakujibu kitu, ila kwa ishara ya macho Nurdini alishatambua jibu. Nurdini akamkumbatia na kumpusu, hapo binti akaanza kutetemeka. Hakuna hakika kama sababu I baridi, uwoga ama ndio mambo ymefana.





Wakiwa katika hali hiyo ghafla mlango ukafunguliwa na loo! Mama Nurdini akashuhudia wawili hawa wakiwa wamekumbatiana. Mama nurdini akaangalia vyema akagundua kuwa binti alikuwa bado amevaa zile nguo alizotoka nazo kuoga. Mama nurdini alikasirika sana, ila kwa upande wa pili aliona pia bora iwe hivi maana mwanzo alikuwa akimuonea wivu mtumwa kwa mumewe. Lakini sasa mwanaye ndiye amemchukuwa mtumwa kabla ya kufikishwa kwa mfalme. Kilichokuwa kikimpataaba mama ni kuwa mumwe wake mzee faridi atachukuwa maamuzi gani?





Nurdini kuona vile alikimbia kwa kumuogopa mama yake. Yule binti moyo ulimruka na kutamani ardhi ipasuke ili apotelee ardhini. Mama Nurdini alimpiga kibao kimoja kizito sana. “huna hata haya wewe, hivi ukaribu wote mume wangu aliokupa ndio unamuharibia hivyo, ataiweka wapi sura yake mume wangu pindi mfalme akigundua jambo hili, ivi unajuwa kuwa ulichokifanya unaweza kuhatarisha maisha ya familia nzima, ikiwemo huyo kibwana chako Nurdini, shetani mkubwa wewe” yalikuwa ni maneno ya mama Nurdini. Hakika yule mtumwa alijiona ni mkosaji sana. Kisha akasema “nisamehe mama, ila Nurdini ndio chaguo langu, la kwanza na ni la mwisho”.





đź“„ Download Post hii
Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Aliflela3 Main: Burudani File: Download PDF Views 1036

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

kamaralzamani
kamaralzamani

HADITHI YA CAMARALZAMANI PRINCE PEKEE Inapata mwendo wa safari ya siku 4 kwa farasi kutokea nchi ya Peshia alikuwepo mfalme maarufu sana aliyefahamika kwa jina la Shahzaman.

Soma Zaidi...
ASUBUHI YA VARANGATI NA KAMARALZAMAN
ASUBUHI YA VARANGATI NA KAMARALZAMAN

VARANGATI ASUBUHI; Baada ya kugunduwa kuwa haikuwa ndoto kamaralzamani aliamini kuwa yule ndio mke ambaye baba yake alimchagulia.

Soma Zaidi...
HATMA YA NURDINI NA NCHI YAKE
HATMA YA NURDINI NA NCHI YAKE

Hadithi za alif lela u lela kitabu cha tatu sehemu ya 9

Soma Zaidi...
Ndoa ya kwanza ya kamaralzamani
Ndoa ya kwanza ya kamaralzamani

NDOA YA HAMU Basi hali ikawa kama hivyo wawili hawa binamu na Kamaralzamani wakaanza kupanga njama ya kuweza kuondoka eneo lile kuelekea nchi za mbali kwa ajili ya kukutana na binti mfalme.

Soma Zaidi...
Taharuki na mwisho wa Kmaralzaman Feki
Taharuki na mwisho wa Kmaralzaman Feki

TAHARUKI Siku hiyo kamaralzamani Feki alikuwa ufukweni kukaguwa mendeleo, alikuwa yeye na mke mwenzie.

Soma Zaidi...
HADITHI YA NURDINI 04: Mtihani wa Nurdini
HADITHI YA NURDINI 04: Mtihani wa Nurdini

Mama aliendelea kugomba sana kisha akamfungia binti ndani na kuweka walinznwa kiume, kisha akawaambia “haruhusiwi kuingia wala kutoka yeyote humu ndnai, hata mbwa Nurdini” neno mbwa lilimtoka tu mama Nurdini kisha akajilaumu kwa kumfana nisha ...

Soma Zaidi...
HADITHI YA NURDINI 02: mawaziri wa Mfalme
HADITHI YA NURDINI 02: mawaziri wa Mfalme

Alikuwepo mfalme aliyetambulika kwa jina la Muhammad Suleiman Azeyn.

Soma Zaidi...
NURDINI ANARUDI KWAO NA BARUA YA MFALME WA BAGHADAD
NURDINI ANARUDI KWAO NA BARUA YA MFALME WA BAGHADAD

Hadithi za Alif lela u lela kitabu cha tatu sehemu ya nane

Soma Zaidi...