HADITHI YA NURDINI 04: Mtihani wa Nurdini

HADITHI YA NURDINI 04: Mtihani wa Nurdini

Mama aliendelea kugomba sana kisha akamfungia binti ndani na kuweka walinznwa kiume, kisha akawaambia “haruhusiwi kuingia wala kutoka yeyote humu ndnai, hata mbwa Nurdini” neno mbwa lilimtoka tu mama Nurdini kisha akajilaumu kwa kumfana nisha ...

HADITHI YA NURDINI 04: Mtihani wa Nurdini

NURDINI HATIANI




Mama aliendelea kugomba sana kisha akamfungia binti ndani na kuweka walinznwa kiume, kisha akawaambia “haruhusiwi kuingia wala kutoka yeyote humu ndnai, hata mbwa Nurdini” neno mbwa lilimtoka tu mama Nurdini kisha akajilaumu kwa kumfana nisha mwanaye na Mbwa. Kwani si katika vitendo vya waungwana kuwafananisha watu na wanyama kwa ubaya. Nurdini aliamua kukibia na kuelekea shambani. Mama nurdini aliendelea kumsubiri mumewe ampe habari nzima. Lakini katika nafsi ya mama Nurdini alikusudia kuja kumhauri mumewe amuozeshe Nurdini kumuozesha yule Mtumwa.



Mpaka inafika jioni Nurdini hajarudi nyumbani. Wakati huo ndio mzee Farid anaingia nyumbani. Siku zote waziri Farid alizoea kupokelewa mizigo yake na mkewe ama mtoto wake. Lakini leo hakuna yeyote aliyekuja kumpokea. Jambo hili lilimtia wasiswasi sana. Akaelekea ndani Loo akamkuta mke wake macho mekundu kwa huzuni. Baada ya salamu na kula chakula mke akamueleza mumewe kila kilichotokea. Alikasirika sana na kuhamaki, kuona jambo hili lilitokeaje. Mzee aliona sasa nimeshaharibikiwa. Alitangaza kuwa nitamchinja Nurdini muda wowote nitakapomona.



Kupitia mashushushu wake Nurdini aliupata ujumbe huu. Siku hiyo alirudi saa nane za usiku. Akanyata na kwenda kula chakula. Mzee faridi alihofia sana mali zake na maisha ya familia yake. Mkewake wakati wa usiku alitumia fuesa hiyo kumshauri mumewe amuozeshe Nurdini yule mtumwa. Hapo mzee akamwambia “mke wangu sihofii kumpatia mtumwa huyu mwanangu, ninahofia vipi waziri Masoud atafanya baada ya kuzipata habari hizi. Kwani jambo hili litaweza kupelekea uhasama kati yake na mfalme, na kuweza kupoteza maisha yake, ya familia yake na upotevu wa mali. Mambo haya aliyawaza sana mzee faridi, jash lilimtiririka kila anapowaza hali hii.



Siku tatu zilipita bila ya baba wala mama kumuona mtoto wao kipenzi. Mama alipatwa na hofu. Akaanza kufuatilia wapi mtoto wake anakula na kulala. Aligundua kuwa saa nane za usiku anakuja kula, na ifikapo saa kumi na moja anaondoka. Mama alihuzunika sana. Alimueleza mume wake hali ya mtoto wao. Alitaka kujuwa namna ya kumsaidia. Kwa upande wa binti yeye alikuwa akiendelea kulia kila siku. Akiamini nea katu hatoweza kumuona Nurdini tena. Aliamini kuwa sasa nitakwenda kuuzwa kwingine, na nisimuone tena Nurdini.



Mama naye alitumia fursa ya usiku kwa mara nyingine kuendelea kumshauri mume wake awaozeshe Nurdini na yule mtumwa. Mama alipoona baba nurdini hataki kuelewa somo, akajifanya kumjia juu “ama ndio ulikuwa unamtaka wewe yule mtumwa, maana nilikuwa sikuelewi, mtumwa gani anayewekewa wafanyakazi, pia kama mtumwa alikuwa ni kwa ajili ya mfalme, kwa nini usingempeleka siku ilelile ama siku ya pili yake, kama hutamuozesha Nurdini huyo mtumwa basi muondoe hapa kwangu, maana sitaweza kuwa na mke mwenzangu aliyekutana na mwanangu.” baada ya kuyasema maneno haya mama nurdini akaanza kulia tena kulia sana.



Kwa hakika wanawake wanajuwa madhaifu ya wanaume yapo wapi. Kwa kweli mzee Faridi aliguswa kweli. Alianza sasa kumbembeleza mkewe huku akijitetea wee kuwa yule mtumwa hakuwa na habai nae hizo. Mama nurdini alipoona kuwa sasa somo limempata akakandamiza tena “basi muezeshe mwanangu” saswa nimekubali, ila tuwe tayari na mashambulizi kutoka kwa Masoud. Siku hhiyo baba na mama wakaenda kumvamia Nurdini. Walimkuta jikoniakipakuwa chakula. Baba alijifanya anataka kumchinja, hapo mama akajifanya anakwenda kuamulia. Mwishowe mama akajifanya anapatanisha. Na Nurdini akapigwa ndoa siku ilofata. Mambo haya yote yalifanyika kwa siri sana, bila ya wengine kutambuwa.



Basi Nurdini aliishi na mke wake kwa amani sana katika masiku yale. Wote walitegemea kula kwa baba na mama. Nurdini katu hakujifunzaga kufanya kazi za kuzalisha kipato. Siku zote alitegemea kwa baba kwa kila kitu. Nurdini alikuwa na marafiki wengi lakini ukweli ni kuwa wote walikuwa wakimnyonya Nurdini na kwa pamoja walikuwa wakiwanyonya wazazi wa Nurdini.





Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 246


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

ASUBUHI YA VARANGATI NA KAMARALZAMAN
VARANGATI ASUBUHI; Baada ya kugunduwa kuwa haikuwa ndoto kamaralzamani aliamini kuwa yule ndio mke ambaye baba yake alimchagulia. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 03: Mtumwa wa Gharama
Kama wasemavyo waliokula chumvi nyingi kuwa muomba mungu hachoki, basi waziri Faridi aliendelea kuomba Mungu hata siku moja akapata taarifa kuwa kuna watumwa wametokea nchi za Uajemi. Soma Zaidi...

NURDINI ANARUDI KWAO NA BARUA YA MFALME WA BAGHADAD
Hadithi za Alif lela u lela kitabu cha tatu sehemu ya nane Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 04: Mtihani wa Nurdini
Mama aliendelea kugomba sana kisha akamfungia binti ndani na kuweka walinznwa kiume, kisha akawaambia 'haruhusiwi kuingia wala kutoka yeyote humu ndnai, hata mbwa Nurdini' neno mbwa lilimtoka tu mama Nurdini kisha akajilaumu kwa kumfana nisha ... Soma Zaidi...

KWENYE BOSTANI LA MFALME WA
KATIKA BOSTANI LA KIFALME BAGHADADBasi Nurdini na mke wake bila hata ya kujuwa wapi watafikia waliingia kwenye mashua na kuwasili Baghada wakati wa jioni. Soma Zaidi...

HATMA YA NURDINI NA NCHI YAKE
Hadithi za alif lela u lela kitabu cha tatu sehemu ya 9 Soma Zaidi...

Taharuki na mwisho wa Kmaralzaman Feki
TAHARUKI Siku hiyo kamaralzamani Feki alikuwa ufukweni kukaguwa mendeleo, alikuwa yeye na mke mwenzie. Soma Zaidi...

kamaralzamani
HADITHI YA CAMARALZAMANI PRINCE PEKEE Inapata mwendo wa safari ya siku 4 kwa farasi kutokea nchi ya Peshia alikuwepo mfalme maarufu sana aliyefahamika kwa jina la Shahzaman. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 03: Nurdini na Mtumwa
Siku ya tano Nurdini alipata taarifa kutoka kwa watu wake yaani wafanyakazi wa chumba chake kuwa kuna binti mgeni ameletwa ila ametengewa sehemu yake maalumu. Soma Zaidi...

HADITHI ZA ALIF LELA U LELA KITABU CHA TATU: HADITHI YA NURDINI
Soma Zaidi...

Ndoa ya kwanza ya kamaralzamani
NDOA YA HAMU Basi hali ikawa kama hivyo wawili hawa binamu na Kamaralzamani wakaanza kupanga njama ya kuweza kuondoka eneo lile kuelekea nchi za mbali kwa ajili ya kukutana na binti mfalme. Soma Zaidi...

Ndoa ya utata ya Kamaralzaman
NDOA YA UTATA KISIWANI Mfalmee wa serendib alipouona msafara ule alivutiwa sana. Soma Zaidi...