Namna ya kutawadha yaani kuchukuwa udhu


image


Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu.


Ili uweze kutawadha kwanza unatakiwa uandae maji yaliyo safi.  Maji safi ni yale ambayo hayajachanganyika na najisi na yakawa yamenajisika. 

 

Baada ya kuandaa maji yako sasa ni wakati wa kutekeleza ibada ya udhu.  Vyemakuanza kupigamswaki.  Kwani kupiga mswaki ni sunnah ambazo zimesisiyizwa sana katika Uislamu. 

 

Hatuwa za kuchukuwa udhu:

1. Kutia nia:

Nia ni kukusudia kitendo. Hii ni hatuwa ya kwanza na muhimu kwani Mtume s.a.w amesema "kila jambo hulipwa kwa kuzinhatia nia" hadithi ni sahihi. 

 

2. Anza na kupiga bismillah kisha osha kiganja vya mikono.  Osha kwanza kabla hujatumbukiza mikono kwenye chombo. 

 

3. Kisha osha uso: 

Uso unatakiwa uoshwe kwa marefu hake na mapana.  Hakikisha unaziosha sehemu zote za uso kama kwenye kidevu na kufika hadi kwenye maoteo ha masikio.  Uoshaji wa uso unaambatana na kusukutuwa na kuingiza maji puani. 

 

Hivyo basi kwa mpanhilio utaanzakusukutuwa kisha utaingiza maji puani.  Utafanya hivi mara tatu kisha ndipo utaosha uso pia utaosha mafa tatu.  Pia utaosha na kwenye ndevu kuhakikisha kuwa ngozi ya kidefu imepata maji. 

 

4. Kuosha mikono. 

Baada ya kumalizakuosha uso utaosha mikonokwa utaratibu utaanza mkono wa kulia mara tatu kisha mkono wa kushoto mara tatu. Hakikisha kuwa mkono unauosha mpakakwenye kiwiko.  Vyema ukafika juu zaidi. 

 

Endapo mkonoutakuwa huna amaumekatwa utaosha kipande kilichopo.  Baa ya kumaliza mkono wa kulia utaosha wa kushoto. 

 

5. Kupaka maji kichwani: 

Hapa utafanya hivi mara moja kama alivyokuwa akifanya Mtume S.A.W. Hata hivyo hakuna ubaya ukizidisha.  Lengo hapa ni kuoaka maji kichwani na si kuosha nywele. 

 

Upakaji wa maji utaendana na kupaka maji kwenye masikio. Nje ya masikio nandani yake. Kidole cha cha shahada kiingie ndani yavsikio na gumba kipake juu ya sikio. 

 

Ni katika sunnah kutumia maji yaleyale yaliotumika kupakakichwa.  Yaani baada ya kupaka maji kichwani utaingiza kidole cha shahada ndani ya sikio,  kisha gumba wwka juu ya pindo za sikio kwa juu na kupaka maji. 

 

Unapopaka kichwa utaanzia mbele kuja nyuma kisha utatoa nyumana kuleta mbele,  kisha ndipp utamalizia masikioni .

 

6. Kuosha miguu

Kisha utaosha miguu miwili mara tatutatu.  Utaanza wa kulia na kumalizia wa kushoto.  Hakikisha maji yanaingia mpaka kwenye mipasuko ya miguu yaani magaga.  Hakikisha unaosha mpaka kwenye fundo zamiguu yaani kungu za miguu. Vyema ukizidisha mpaka kwenye ugoko. 

 

Baada ya hapo utakuwa umeshatia udhu. Usikose post inayofuata itazungumzia dua ya kumaliza kutia udhu. 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Jifunze Fiqh    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja
Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja. Soma Zaidi...

image Usawa na uhuru wa kuchuma mali katika uislamu
Uchumi wa uislamu umeweka taratibu mbalimbali katika kuchuma mali. Soma Zaidi...

image Je ni zipi nguzo za uislamu, na ni ngapi nguzo za uislamu?
Post hii itakujuza maana ya uislamu na nguzo zake. Soma Zaidi...

image Fadhila za usiku waalylat al qadir
Zijuwe fadhila za usiku wenye cheo kuliko nyusiku ya miezi 1000. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kuelekea qibla katika swala.
Je unadhani ni kwa nini waislamu wanaelekea kibla, na jinsi gani utaweza kukipata kibla. Soma Zaidi...

image Sera ya uchumi katika uislamu
Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu. Soma Zaidi...

image Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja
Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu. Soma Zaidi...

image Nafasi ya serikali katika ugawaji
Serikali ina nafasi katika kufanya mgawanyiko katika uchumi. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa
Post hii itakufundisha taratibu za kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa. Soma Zaidi...

image Sunnah za swaumu, sunnah ambazo zinaambatans ns kufungabmwezi wa Ramadhani
Yajuwe mambo ambayo yanapendeza kuyafanya wakati ukiwa umefunga Ramadhani. Soma Zaidi...