Sababu kuu za maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, Tumbo la ngiri na chango
Makala hii inakwenda kukuletea somo linalozungumzia maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, na tumbo la ngiri kwa wanaume, na tumbo la chango kwa wanawake
NINI HUSABABISHA MAUMIVU YA TUMBO CHINI YA KITOMVU KWA WANWAKE NA WANAUME?
Watu wengi wamekuwa wakilalamikajuu ya maumivu makali ya tumbo chini ya kitomvu. Tatizo hili linaweza kuwapata wanawake na wanaume pia. Kwa upande wa wanawake tatizo hili limekuwa ni kawaida hasa wakati wa kukaribia kuingia siku zao. Kawaida maumivu haya hayana shida sana kiafya lakini ikzidi uangalizi wa dakatari unahitajika. Je na wewe ni muhusika wa maumivu haya? Makala hii itakuwa ni jibu lako.
Makala hii inakwenda kukuletea somo linalozungumzia maumivu ya tumbo chini ya kitomvu. Ni katika maumivu amaboyo kwa wanaume mara nyingi huhusishwa an ngiri na kwa upande wa wanawake huhusishwa na chango hasa pale wanapokaribia kuingia katika siku zao. Makala hii itakuletea sababu za maumivu ya tumbo chini ya kitomvu kwa wanwake na wanaume.
Maumivu ya tumbo kitomvuni
Eneo hili la kitomvuni kitaalamu hufahamika kama umblical region. Eneo hili la tumbo linahusisha viungo kama tumbo la chakula, utumbo mdogo, utumbo mkubwa na kongosho. Hivi ni katika viungo muhimu sana katika mmengenyo wa chakula, na afya ya mtu kwa ujumla.
SABABU ZA MAUMIVU YA TUMBO KITOMVUNI
1.Kuwepo na uvimbe kwenye njia ya chakula (digestive track) kitaalamu hufahamika kama gastroenteritis. Hali hii inaweza kusababishwa na virusi, bakteria ama parasite. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu na yanaweza kuwa ni makali sana. Mara nyingi maumivu haya yanapoa yenyyewe bila hata kuhitaji matibabau ha huondoka ndani ya siku chache. Ila ni vyema kumuona daktari kwa uchunguzi zaidi.
2. Kuvimba kwa appendix. Maumivu ya tumbo kwenye kitomfu yanaweza kuashiria ugonjwa wa appendix, kitaalamu hufahamika kama appendicitis. Kama utahisi maumivu makali ya tumo kitomvuni kisha ghafla yanahamia upande wa kulia wa tumbo kwa chini, huashiria tatizo hili.
3.Vidonda vya tumbo
Yes maumivu ya tumbo kitomvuni yanaweza kuwa yamesababishwa na vidonda vya tumbo, huwenda vipo kwenye tumbo la chakula ama sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayotambulika kama duodenum.
3. Matatizo kwenye kongosho
Huu ni ugonjwa unaosababisha kuvimba kwa kongosho kitaalamu huitwa Pancreatitis. Maradhi haya yanaweza kuja ghafla sana bila ya kuonyesha ishara za awali.
5.Kuwa na ngriri ya henia
Ugonjwa huu huwapata wanaume, na hutokea pale ambapo baadhi ya tishu za tumboni zinapoingia kwenye misuli ya tumboni karibu na kitomvu. Kwa watu wazima upasuaji hufanyika ili kutibu tatizo.
6.Kama kuna kizuizi katika utumbo kinachozuia chakula kutembea. Tatizo hili likichelewa kutibiwalinaweza kuwa hatari zaidi. Tatizo hili huweza kusababishwa na:-
1.Mashambulizi ya bakteria
2.Henia
3.Uvimbe
4.Kama kulitokea shida wakati wa kufanyiwa upasuaji.
7.Matatizo katika mishipa mikuu ya damu kwenye tumbo (aortic aneurysm). hili ni tatizo la kiafya linalosababishwa na kudhoofu na kutanuka kwa kuta za mishipa mikuu ya damu. Hali hii inaweza kuhatarisha maisha ya mtu kama mishipa ya damu itapasuka na kupelekea damu kuingia tumboni, hii inaweza kupelekea maumivu makli. Maumivu haya yanaweza kuathiri na viungo vingine.
8.Kama kutakuwa na shida wakati wa mzunguko wa damu katika tumbo (mesenteric ischemia). hii hutokea endapodamu inayotembea kwenye utumbo mdogo itapata usumbufu, kwa mfano ikiganda. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu makali ya tumbo. Maumivu haya huandamana na dalili kama:-
1.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo
2.Kuona damu kwenye choo
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 web hosting 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Jinsi ya kutambua mimba kwa vipimo vya kawaida vya mkojo.
Kujitambua mimba mapema ni hatua muhimu katika kuanza safari ya uzazi salama. Makala haya yanaelezea misingi ya kisayansi ya vipimo vya mkojo vya nyumbani (Pregnancy Test Strips/Sticks), njia sahihi ya kuvitumia, muda mwafaka wa kupima, na jinsi ya kusoma matokeo ili kupata usahihi wa hali ya juu.
Soma Zaidi...je Kama utaonekana kupatwa na homa,kichwa,tumbo, kiharisha kwa siku moja( ya kwanza) na vyote kupona siku nyingine (ya pili kupona) pasipo kutumia dawa inaweza kuwa Ni dalili ya ugonjwa wa zinaa ?
Homa ni moka ya dalili inayohusiana na maradhi mengi sana. Unaweza kuwa na homa ikawa pia si maradhi kumbe ni stress tu. Je unasumbuliwa na homa za mara kwamara, Makala hii ni kwa ajili yako
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa ,kwa kawaida Ugonjwa huu utokea kuanzia kwenye wiki ya pili mpaka mwaka mmoja na hapo Ugonjwa unakuwa bado haujaonesha Dalili na Dalili zikishaonekana ni vigumu kutibika.
Soma Zaidi...ninasumbuliwa Sana na mapunye ya kichwani nimetumia dawa takribani miaka 3
Habari, samahani ninasumbuliwa Sana na mapunye ya kichwani nimetumia dawa takribani miaka 3 ila yanapona Tena baada ya Muda flani yanatokea.
Soma Zaidi...Dawa za kuua wadudu (Antibiotics): Matumizi sahihi na hatari zake.
​Dawa za kuua vimelea, maarufu kama antibiotics, ni moja ya uvumbuzi muhimu zaidi katika historia ya tiba ya kisasa. Zimeokoa mamilioni ya maisha kwa kutibu maambukizi ya bakteria. Hata hivyo, matumizi yasiyo sahihi, yasiyo ya lazima, na yasiyokamilika yamesababisha ongezeko la hatari ya "usugu wa dawa" (Antimicrobial Resistance - AMR). Makala haya yanachunguza kwa kina jinsi ya kutumia dawa hizi kwa usahihi, madhara yake, na hatua za kuchukua ili kulinda ufanisi wa dawa hizi kwa vizazi vijavyo.
Soma Zaidi...