Vyakula na vinywaji hatari na vilivyo salama kwa mgonjwa wa kisukari

Hapa utajifunza vyakula hatari kwa mgonjwa wa kisukari, pia utajifunza vyakula salama anavyotakiwa ale mgonjwa wa kisukari, Pia ujajifunza njia za kujikinga na kisukari

Vyakula na vinywaji hatari na vilivyo salama kwa mgonjwa wa kisukari

VYAKULA SALAMA NA HATARI KWA MWENYE KISUKARI
Kisuari ni hali ya mwili kushindwa kudhibiti kiwango cha sukari hivyo kuachia sukari yote kuishia kwenye damu bila ya kuingia kwenye seli ili kutumika maeneo mbalimbali ya mwili. Na hutokea endapo uzalishwaji wa homoni ya insulini utakuwa katika shida. Eidha hutokea kwa sababu homoni ya insulini inayozalishwa si yenye kutosheleza ama mwili wenyewe unashindwa kuitumiahomoni ya insulini. Homoni ya insulin ndio ambayo hudhibiti kiwango cha sukari.



Vipi kisukari hutokea?
Mwili unahitaji sukari kwa ajili ya kuzalisha nishati yaani nguvu. Mwili pia unahifadhi sukari kwa matumizi ya baadaye. Endapo sukari mwilini itakuwa ni nyingi basi homoni ya insulini huzaliwa kwa wingi ili kupunguza sukari iliyozidi n akuihifadhi kwa matumizi yaa baadaye. Na endapo sukari itakuwa ni kidogo mwilili homoni ya insulini huzuiliwa hivyo mwili hutumua sukari iliyohifadhiwa. Kwa kufanya hivi kiwango cha sukari hudhibitiwa.



Sasa endapo kutatokea shida yeyote katika matumizi ya homoni ya insulini mwili utashindwa kuhifadhi sukari pia kuitumia sukari. Hivyo sukari itabakia kwenye damu bila ya kwenda kokote kwa matumizi. Hali hii ikitokea ndipo mtu huambiwa ana kisukari. Kisukari kinaweza kuwa ni kwa muda mfupi kama kwa baadhi ya wajawazito. Pia kinaweza kuwa ni cha kudumu, na hapa tunazungumzia type1 na type 2.



Mtu mwenye kisukari anatakiwa kuwa makini sana katika matumizi ya vyakula na vinywaji. Vinginevyo anaweza kuingia kwenye matatizo makubw aya kiafya. Je unavijuwa vyakula salama kwa nmwemye kisukari? Na je unavijuwa vyakula hatari kwa mwenye kisukari? Endelea na makala hii hadi mwisho:-



VYAKULA SALAMA KWA MWENYE KISUKARI
1. Samaki hasa wale wenye fati kwa wingi kama samlon na sardines
2. Mbogamboga za majani
3. Palachichi
4. Mayai
5. Mbegu za chia
6. Maharagwe
7. Kitunguu thaumu
8. Nyama yandege wafugwao kama kuku
9. Kahawa
10. Vinywaji visivyowekwa sukari
11. Jusi za mbogamboga
12. Usikoboe mahindi, mchele, na mtama
13. Matunda kwa uchache



VYAKULA HATARI KWA MWENYE KISUKARI
1. Nafaka zilizokobolewa
2. Nafaka zilizoongezwa sukari
3. Mikate yenye sukari
4. Nafaka zisizo na kini
5. Mboga zenye chumvi nyingi
6. Mboga zilizoongezwa maziwa
7. Vinywaji vyote vya sukari usitumie mpaka kiwango chako cha sukari kiwe kipo katika udhibiti hata asali epukana nayo kwanza
8. Juisi zilizowekwa sukari ama zenye utamu kama za matunda
9. Vinywaji vya energy (energy drink)
10. Nyama ya kuoka
11. Nyama zenye mafuta mengi
12. Nyama ya ngurue
13. Maziwa fresh
14. Samaki wa kuoka
15. Soda



Njia za kujikinga na kisukari
1. Dhibiti uzito wako. Hakikisha huna uzito w akupitiliza
2. Fanya mazoezi mara kwa mara
3. Kula mlo kamili
4. Punguza misongo ya mawazo
5. Kunywa maji kwa wingi
6. Wacha kuvuta sigara
7. Punguza ama wacha unywaji wa pombe
8. Punguza ulaji wa sukari kwa wingi
9. Pendelea kunywa kahawa
10. Tumia dawa za asili kiasi uwezavyo





                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 2111

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Parachichi (avocado)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za parachichi

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za nyanya

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula nyanya

Soma Zaidi...
Vyakula vya madini kwa wingi, na kazi za madini mwilini

Utajifunza vyakula vyenye madini kwa wingi, kazi za madini mwilini na athari za upungufu wake

Soma Zaidi...
Faida za limao au ndimu

Post hii itakwenda kukueleza umuhimu wa limao kiafya

Soma Zaidi...
KITABU HA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
Rangi za matunda

Fida za matunda huanzia kwenye rangi zake, je unajuwa kama rangi ya matunda inaeleza jambo?

Soma Zaidi...
Boga (pumpkin)

Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula maboga

Soma Zaidi...
Faida za kula Tangawizi

tangawizi ni katika viungio vya mboga vyenye faida, pia ni kinywaji, zijuwe leo faida za tangawizi

Soma Zaidi...
Vyakula vya vitamin K

Some Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya vitamin K

Soma Zaidi...