Ni nini husababisha mate kujaa mdomoni, na ni yapi matibabu yake

Ni nini husababisha mate kujaa mdomoni, na ni yapi matibabu yake

Hapa tutaangalia baadhi ya sababu zinazopelekea mdomo kujaa mate na namna ya kutibu tatizo la kujaa kwa mate mdomoni

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Ni nini husababisha mate kujaa mdomoni, na ni yapi matibabu yake

NI NINI HUSABABISHA MATE KUJAA MDOMONIKutokwa na mate mengi mdomoni si ugojwa ni hali inayoweza kutokea kwa mtu yeyote. Mara nyingi hali hii haihitaji matibabu wa dawa, na huondoka yenyewe. Lakini hutokea baadhi ya nyakati ikawa mate yanatoka zaidi mdomoni. Je na wewe ni miongoni mwao? Makala hii ni kwa ajili yako. Hapa tutaangalia baadhi ya sababu zinazopelekea mdomo kujaa mate. Sababu hizi zipo nyingine ni kwa wanawake tu, pia zipo ambazo ni kwa watu wa jinsia zote. Tunatarajia baada ya kusoma makala hii utaweza kuzijuwa sababu zinazopelekea mdomo kujaa mate, pia utaweza kupata kujuwa nini unatakiwa ufanye kulingana na tatizo lako.


KUJAA KWA MATE MDOMONI NI NINI HASA?
Kitaalamu kitendo hiki cha kujaa kwa mate mdomoni hufahamika kama hypersalivation. Hiki ni kitendo cha mdomo kujaa mate na wakati mwengine hutokea mate yakatoka yenyewe kwenye midomo baada ya kujaa. Kitaalamu kitendo hiki sio ugonjwa ila ni dalili ya kuwepo kwa tatizo lakiafya ama kuwepo kwa jambo lililopelekea mabadiliko ya mwili na kiafya.


JE MATE NI NINI?
Mate ni kimiminika cheupe kinachopatikana mdomoni ambacho hutengenezwa kwenye tezi za mate zinazojulikana kama salivary glands. Mate yana vichochezi (enzymes) ambavyo hutumika katika mmeng'enyo wa chakula hasa chakula cha wanga mdomoni. Mate pia husaidia katika kulainisha chakula na kuweka mgomo katika hali ya usafi, usalama na ubichibichi.
Tafiti zinaeleza kuwa mtu wa kawaida anaweza kuzalisha mate yanayofikia lita moja na nusu kwa siku. mate huzalishwa kwa wingi mtu anapokula na uzalishaji huu hupunguwa pale anapolala.


MADHARA YA KUWA NA MATE KIDOGO
Kwa kuwa mate yana faida kubwa mwilini hivyo endapo uzalishaji wa mate hautakuwa wa kutosheleza madhara huweza kumpata mtu ni kama:-
1. mdomo kuwa mkavu
2. Mmeng'enyo wa chakula kutofanyika vyema mdomoni kwa vyakula vya wanga
3. Mtu anaweza kupata taabu wakati wa kumeza
4. Anaweza kupata vidonda vya mdomo
5. Mdomo utaweza kuathiriwa kwa urahisi na fangasi, bakteria na sumu na kemikali za kwenye vyakula
6. Hata kuzungumza kunaweza kuathiriwa endapo mtu atakosa mate ya kutosha


MADHARA GANI ATAYAPATA MTU KAMA ATAKUWA NA MATE MENGI ZAIDI?
Kama ilivyokuwa kuna hasara kwa mate kukosekana mwilini, halikadhalika endapo mate yatakuwa mengi zaidi pia hali hii itakuwa na madhara yake. Madhara hayo ni kama:-
1. Matatizo wakati wa kusema, yaani hatoweza kuema vyema kama mate yatakuwa yamejaa mdomoni
2. Itakuwa vigumu kuufunga mdomo
3. Pia mdomo utaweza kupata mashambulizi ya bakteria kwa urahisi.
4. Mtu atashindwa kujiamini na kukaa na watu kwa sababu ya mate yake.


NINI HUSABABISHA MDOMO KUJAA MATE?
Hizi ni katika sababu ambazo hupelekea mate kujaa mdomoni:-
1. Kuongezeka kwa uzalishwaji wa mate mdomoni
2. Kama mtu atakuwa na shida na kushindwa kumeza mate ama mdomo kuondoa mate yote wakati wa kutema
3. Kama mtu atakuwa na matatizo ya kutoweza kuufunga mdomo


NINI HUSABABISHA ONGEZEKO LA UZALISHAJI WA MATE MDOMONI
Kama ulivyoona hapo juu sababu za kuwa na mate mengi mdomoni ni ongezeko la uzalishwaji wa mate mdomoni. Sasa swali la msingi kuwa "ni nini husababisha hili ongezeko la uzalishwaji wa mate mdomoni" . Sababu gizo ni kama:-
1. Kichefuchefu
2. Homa ya asubuhi na ujauzito
3. Kama kuna maabukizi na mashambulizi ya bakteria na virusi kwenye koo, tonsil na meneo mengine ya mdomoni
4. Kama umeng'atwa na buibui mwenye sumu, ama umekula uyoga ama umeng'atwa na wadudu
5. Kama unatumia meno ya bandia
6. Kama hufanyi usafi wa kinywa kwa umakini
7. Kama una maambukizi ya T.B ama ugonjwa wa rabies
8. Kama una kiungulia cha mara kwa mara
9. Mipasuko kwenye taya ma amifupa ya taya kutojipanga vyema
10. Vidonda vywnyw mfumo wa mmeng'enye wa chakula kama mdomoni, kooni na tumboni


NINI HUSABABISHA KUSHINDWA KUMEZA MATE AMA KUTEMA MATE YOTE?
Kama tulivyoona kuwa katika sababu zinazopelekea mate kujaa mdomoni ni kushindwa kuyameza yote, ama kuyatema yote. Sasa ni kitu gani husababisha hali hii?
1. Kuwa na shida ya kiafya kwenye mfumo wa fahamu
2. Kuwa na shida ya kiafyakwenye figo


SABABU NYINGINE ZINAZOPELEKEA MDOMO KUJAA MATE
1. Mpangilio mbaya wa meno
2. Majeraha kwenye mdomo
3. Hewa mbaya
4. Upungufu wa maji mwilini
5. Matatizo kwenye mfumo wa fahamu hasa katika kuhisi ladha ya chakula
6. Kama una maradhi ya pneumonia


NINI UFANYE KAMA UNA HILI TATIZO:
1. Kwa kupitia dalili zilizotajwa hapo juu, angalia ambayo huwenda ndio sababu kwako.
2. Kawaida tatizo hili halihitaji dawa, ila kama imezidi fika hospitali kwa uchunguzi zaidi.
3. Fika kituo cha afya kwa vipimo zaidi kama hali yako itaendelea kwa muda bila kurudi nyuma.



                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 17433

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Je na kwa upande wa mwanaume kuumwa upande wa kushoto wa tumbo kuna shida gani?
Je na kwa upande wa mwanaume kuumwa upande wa kushoto wa tumbo kuna shida gani?

Maumivu ya tumbo upande wa kushoti, kwa mwanamke huwenda ikawa ni ujauzito ama shida nyingine za kiafya kama tumbo kujaa gesi, kukosa choo na kadhalika. Sasa vipi kwa wanaume ni ipi hasa sababu❔

Soma Zaidi...
 Ugonjwa wa Saratani ya ini.
Ugonjwa wa Saratani ya ini.

Saratani ya ini ni Saratani inayoanzia kwenye seli za ini lako.

Soma Zaidi...
Dalilili za Ngozi kuwa kavu
Dalilili za Ngozi kuwa kavu

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ngozi kuwa kavu si mbaya, lakini inaweza kusumbua na isipendeze, ikitengeneza mistari laini na Mikunjo.

Soma Zaidi...
Aina za minyoo
Aina za minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya aina za minyoo

Soma Zaidi...
Dalili za fangasi uken
Dalili za fangasi uken

Posti hii inahusu zaidi dalili za fangasi uken, hizi ni baadhi ya dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la fangasi uken.

Soma Zaidi...
Nini husababisha maumivu ya tumbo chini ya kitomvu kwa wanawake na wanaumr?
Nini husababisha maumivu ya tumbo chini ya kitomvu kwa wanawake na wanaumr?

Makala hii inakwenda kukuletea somo linalozungumzia maumivu ya tumbo chini ya kitomvu. Ni katika maumivu amaboyo kwa wanaume mara nyingi huhusishwa an ngiri na kwa upande wa wanawake huhusishwa na chango hasa pale wanapokaribia kuingia katika siku zao. Ma

Soma Zaidi...
Kupambana na kisukari
Kupambana na kisukari

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na kisukari

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa degedege na dalili zake
Ugonjwa wa degedege na dalili zake

Ugonjwa wa degedege ni ugonjwa unaowapata sana watoto chini ya miaka mitano ingawa na watu wazima wanapatwa na ugonjwa huo

Soma Zaidi...
Dalili za saratani ya kwenye Njia ya haja kubwa.
Dalili za saratani ya kwenye Njia ya haja kubwa.

Saratani ya kwenye Njia ya haja kubwa ni aina isiyo ya kawaida ambayo kitaalamu hujulikana Kama saratani ya mkundu.Mfereji wa mkundu ni mirija fupi iliyo mwisho wa puru yako ambayo kinyesi hutoka mwilini mwako. Saratani ya kwenye Njia ya  ha

Soma Zaidi...