Simulizi za Hadithi EP 5 Part 12: Sehemu ya tano ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza...
SAFARI YA TANO YA SINBAD
Baada ya watu kukusanyika siku ilofata sinbad akaanza kusimulia stori ya safari yake ya tano. Akaanza kusema kuwa “niliamua kutokuenda tena safari yoyote ya majini. Hali ilikuwa hivyo lakini baada ya miezi mingi nikapata wazo la kutengeneza jahazi langu ambalo litakuwa ni madhubutizaidi. Kwa mali nilizo nazo wakati huu nikaanza kuandaa jahazi kubwa na la kisasa lililo madhubuti sana. Muda ulitimia na jahazi kubwa na la kisasa zaidi lilikamilika.
Nikaanza kualika wafanyabiashara wakubwawakubwa na walio wazoefu zaidi. Tuliandaa bidhaa zetu na tukamtafuta nahodha aliye mahiri na safari hizi. Maandalizi yalipokamilika tukaanza safari usiku kwa kulingana na uwepo wa upepo.
Kwa hakika safari ilikuwa njema, tuliweza kupita kwenye mikondo mikubwa na tukaingia visiwa kadhaa. Kwa hakika nahodha huyu alikuwa ni hodari na ni mzoefu, kwani hatukupita kisiwa ila alikuwa akitueleza habari zake. Hata visiwa visivyoishiwa na watu alikuwa akitueleza habari zake. Tulipita kenye kisiwa cha mawe yanayolia. Tukamueleza nahodha atuambie habari za mawe yale kaanza kutusimulia hadithi hii;
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 web hosting 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 ai web app 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Mtumwa wa mfalme na mawaziri
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha tatu.....
Soma Zaidi...Simulizi za Hadithi EP 4 Part 13: Simulizi ya nyani kibadilika kuwa chongo
Mwendelezo wa hadithi zetu nzuri na za kusisimua kutoka katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.....
Soma Zaidi...Simulizi za Hadithi EP 3 Part 3: Kisa cha mke na kasuku
Simulizi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza simulizii hii inasimulia kisa cha mke na Kahuku wake....
Soma Zaidi...Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Hadithi ya Nurdini Mtoto wa Waziri
Hii ni hadithi ya kitabu cha tatu cha hadithi za HALIF LELA U LELA...
Soma Zaidi...