Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza...
SAFARI YA TANO YA SINBAD
Baada ya watu kukusanyika siku ilofata sinbad akaanza kusimulia stori ya safari yake ya tano. Akaanza kusema kuwa “niliamua kutokuenda tena safari yoyote ya majini. Hali ilikuwa hivyo lakini baada ya miezi mingi nikapata wazo la kutengeneza jahazi langu ambalo litakuwa ni madhubutizaidi. Kwa mali nilizo nazo wakati huu nikaanza kuandaa jahazi kubwa na la kisasa lililo madhubuti sana. Muda ulitimia na jahazi kubwa na la kisasa zaidi lilikamilika.
Nikaanza kualika wafanyabiashara wakubwawakubwa na walio wazoefu zaidi. Tuliandaa bidhaa zetu na tukamtafuta nahodha aliye mahiri na safari hizi. Maandalizi yalipokamilika tukaanza safari usiku kwa kulingana na uwepo wa upepo.
Kwa hakika safari ilikuwa njema, tuliweza kupita kwenye mikondo mikubwa na tukaingia visiwa kadhaa. Kwa hakika nahodha huyu alikuwa ni hodari na ni mzoefu, kwani hatukupita kisiwa ila alikuwa akitueleza habari zake. Hata visiwa visivyoishiwa na watu alikuwa akitueleza habari zake. Tulipita kenye kisiwa cha mawe yanayolia. Tukamueleza nahodha atuambie habari za mawe yale kaanza kutusimulia hadithi hii;
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Simulizi hii inatoka kwenye kitabu cha kwanza cha hadidhi za HALIF LELA U LELA.
Soma Zaidi...Hii ni simulizi iliyopo ndani ya kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA......
Soma Zaidi...Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili....
Soma Zaidi...Simulizi za HALIF LELA U LELA ni nziri sana tuwe pamoja kusikiliza kisa cha mzee wa pili na mbwa wawili weusi...
Soma Zaidi...Hadithi hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA....
Soma Zaidi...