Simulizi za Hadithi EP 4 Part 2: Kisa cha kinyozi msiri..

Karibuni tuendelee kusimuliana stori za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza, stori nzuri sana na za kuvutia zimeandaliwa kwaajili ya kujifunza na kujiburudisha pia.....

KINYOZI MSIRI WA MFALME.

 

Hapo zamani za kale katika nchi moja kulikuwepo na mfalme aliyependa kufuga nywele. Mfalme huyu alikuwa akinyowa nywele zake mara nne kwa mwaka. Mfalme huyu alipenda kuvaa kilemba kichwani kama ilivyo kawaida katika tamaduni za kiislamu. Watu wengi walipenda uvaaji wa mfalme wao na yeye alilijuwa hili kwa muda mrefu. Kumbe mfalme alikuwa anasiri kubwa katika uvaaji ule. Mfalme alikuwa akinyolewa na kinyozi maalumu. Ilipita masiku na miaka mingi hata yule kinyozi wa mfalme akafariki. Ilibidi mfalme atangaze kumtafuta kinyozi mwingine. Uchunguzi ulifanyika kumtafuta kinyozi muadilifu na mwenye maadili. Zaidi ya sifa hizi mfalme alitaka kinyozi mwenye sifa ya kutunza siri. Sifa hii aliitaka mfalme kwa kuwa kuna siri kubwa kwenye kichwa chake. Basi alipatikana kinyozi mmoja kijana mwenye familia ya watoto wanne. Alikuwa ana maadili mazuri na ni muadilifu pia.

 

Ilitokea siku moja mfalme akataka kunyolewa. Akamuita kinyozi wake na kumwambia “kwa mara ya kwanza ndo unakiona kichwa changu, utakachokiona kwenye kichwa changu iwe siri yako mpaka utakapoingia kaburini”. Kinyozi akaapa mbele ya mfalme kuwa katu hataizungumza siri ile kwa yeyote. Kinyozi kufunguwa kilemba cha mfalme alishikwa na mshangao kkubwa baada kuona siri kubwa katika kichwa cha mfalme. Kinyozi akajuwa kumbe hii ndio sababu ya mfalme kuvaa kilemba na kufuga nywele.

 

Basi kinyozi yule alikaa na siri ile kwa siku nyingi sana. Alithubutu hata kukimbia nchi kwa kuogopa kutoa siri ya mfalme. Hali iliendelea kama hivyo anamnyoa kinyozi na anaenelea kutunza siri ya mfalme. Kama ujuavyo siri ikikaa sana kwenye moyo utadhani moyo unataka kutumbuka. Kinyozi akawaza hii siri ya mfalme siwezi kuotoa nitafanya nini sana. “ningejua kama mfalme ana pembe katu nisingekubali kukifunua kichwa cha mfalme”. Ni maneno ya kinyozi.

 

Basi siku moja akatoka na chepe lake na jembe kwenda porini. Kufika kule akachimba shimo kubwa mpaka kiunoni. Baada ya hapo akainama na kuanza kuimba “mfalme anapembe, mfalme anapembe”. Aliimba hivi kwa muda mpaka alipoona moyo wake umetulia na umepoa kwa kuiweka siri ya mfalme kwa muda. Basi baada ya hapo akafukia shimo lake na akaondoka kurudi nyumbani. Haukupita muda mrefu shimo like likaota majani na pakaota mti mkubwa sana.

 

Ni miaka 15 sasa imepita toka mti ule uote sasa mti ule ukabakia na siri ile aloiacha kinyozi miaka 15 iliyopita. Mti ule ulipofikia kutoa maua ukawa upepo ukaja unarudia ule mwimbo wa alouacha kinyozi miaka 15 ilopita. Hivyo ukaja upepo mti unaimba “mfalme ana peembe mfalme anapembe, waaa waaa waaa”. Ikatokea siku moja wawindaji wakapita karibu na mti ule wakastaajabu kusikia wimbo wa ajabu unaozungumza kuwa mfalme ana pembe.

 

Basi habari zikaanza kusambaa kwa kasi sana mpaka ikamfikia kinyozi. Watu wakawa wanafunga safari kwenda kuuangalia mti uanoimba kuwa mfalme ana pembe. Habari zilisambaa mpaka zikamfikia mfalme. Mafalme akatoka na msafara wake nae akashuhudie mti unaotoa siri yake ya pembe kichwani. Alishangaa sana, ilibidi siku ilofata aitishe mkutano mkubwa kwa kila atakaetaka kuhudhuria kwenye eneo lile lenye mti ule.

 

Basi watu walikusanyika sana eneo lile, watoto, wazee na vijana walimwaika eneo lile la tukio. Baada ya muda watu walipokusanyika akasimama na kuanza kuhutubia, kisha akavua kilembe chake watu wote wakashuhudia pembe kichwani mwake. Kisha akasema “nimeamini hakuna siri”. Na huu ndio mwisho wa hadithi ya kinyozi msiri wa mfalme. Basi Amina na Sadie walifurahi sana na wakamruhusu kijana aenelee kubakia pale.

 

Basi pale ndani chakula kikapikwa na watu wakawa wanakula na kunya na kufurahi. Mashairi yaliimbwa na furaha zaidi. Wakatowa pombe wakanywa na wakaendelea kufurahi pale ndani. Nyakati za swala pia ziliwapita palelpale walipokaa. Mapaka wanakuja kutambua ni jioni na kigiza kinakaribia kuingia. Zubeida akamwambia kijana “amka uende zako, muda wa kutengana na wewe umekaribia”. Kijana akaanza kujitetea tena kuwa amelewa sana hivyo hataweza kufika kwake. Kama watamruhusu alale pale mpaka kesho ataondoka na kurudi kwake.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Mankaa image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Burudani File: Download PDF Views 265

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 15: Mji uliogeuzwa mawe

Hadithi hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 4: Kilema mtanashati asiye na mkono

Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 19: Kinyozi

Hii ni simulizi iliyopo ndani ya kitabi cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 1: Muuaji ni nani?

Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 6: Sehemu ya tatu ya safari ya Sinbad

Muendelezo wa sehemu ya tatu ya safari ya Sinbad iliyopo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 16: Usaliti

Hadithi za HALIF LELA U LELA zipo nyingi sana na zinavutia na zinasomwa na kusikilizwa kwa wakubwa na wadogo na hii simulizi inatoka kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA......

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 1 Part 2: Simulizi ya kisa cha mfugaji na mkewe

Simulizii hii ni inatoka katika kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 20: Waliodhulumiwa kufanyiwa suluhisho

Ni mojawapo ya simulizi iliyopo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA....

Soma Zaidi...