image

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 2: Kisa cha kinyozi msiri..

Karibuni tuendelee kusimuliana stori za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza, stori nzuri sana na za kuvutia zimeandaliwa kwaajili ya kujifunza na kujiburudisha pia.....

KINYOZI MSIRI WA MFALME.

 

Hapo zamani za kale katika nchi moja kulikuwepo na mfalme aliyependa kufuga nywele. Mfalme huyu alikuwa akinyowa nywele zake mara nne kwa mwaka. Mfalme huyu alipenda kuvaa kilemba kichwani kama ilivyo kawaida katika tamaduni za kiislamu. Watu wengi walipenda uvaaji wa mfalme wao na yeye alilijuwa hili kwa muda mrefu. Kumbe mfalme alikuwa anasiri kubwa katika uvaaji ule. Mfalme alikuwa akinyolewa na kinyozi maalumu. Ilipita masiku na miaka mingi hata yule kinyozi wa mfalme akafariki. Ilibidi mfalme atangaze kumtafuta kinyozi mwingine. Uchunguzi ulifanyika kumtafuta kinyozi muadilifu na mwenye maadili. Zaidi ya sifa hizi mfalme alitaka kinyozi mwenye sifa ya kutunza siri. Sifa hii aliitaka mfalme kwa kuwa kuna siri kubwa kwenye kichwa chake. Basi alipatikana kinyozi mmoja kijana mwenye familia ya watoto wanne. Alikuwa ana maadili mazuri na ni muadilifu pia.

 

Ilitokea siku moja mfalme akataka kunyolewa. Akamuita kinyozi wake na kumwambia “kwa mara ya kwanza ndo unakiona kichwa changu, utakachokiona kwenye kichwa changu iwe siri yako mpaka utakapoingia kaburini”. Kinyozi akaapa mbele ya mfalme kuwa katu hataizungumza siri ile kwa yeyote. Kinyozi kufunguwa kilemba cha mfalme alishikwa na mshangao kkubwa baada kuona siri kubwa katika kichwa cha mfalme. Kinyozi akajuwa kumbe hii ndio sababu ya mfalme kuvaa kilemba na kufuga nywele.

 

Basi kinyozi yule alikaa na siri ile kwa siku nyingi sana. Alithubutu hata kukimbia nchi kwa kuogopa kutoa siri ya mfalme. Hali iliendelea kama hivyo anamnyoa kinyozi na anaenelea kutunza siri ya mfalme. Kama ujuavyo siri ikikaa sana kwenye moyo utadhani moyo unataka kutumbuka. Kinyozi akawaza hii siri ya mfalme siwezi kuotoa nitafanya nini sana. “ningejua kama mfalme ana pembe katu nisingekubali kukifunua kichwa cha mfalme”. Ni maneno ya kinyozi.

 

Basi siku moja akatoka na chepe lake na jembe kwenda porini. Kufika kule akachimba shimo kubwa mpaka kiunoni. Baada ya hapo akainama na kuanza kuimba “mfalme anapembe, mfalme anapembe”. Aliimba hivi kwa muda mpaka alipoona moyo wake umetulia na umepoa kwa kuiweka siri ya mfalme kwa muda. Basi baada ya hapo akafukia shimo lake na akaondoka kurudi nyumbani. Haukupita muda mrefu shimo like likaota majani na pakaota mti mkubwa sana.

 

Ni miaka 15 sasa imepita toka mti ule uote sasa mti ule ukabakia na siri ile aloiacha kinyozi miaka 15 iliyopita. Mti ule ulipofikia kutoa maua ukawa upepo ukaja unarudia ule mwimbo wa alouacha kinyozi miaka 15 ilopita. Hivyo ukaja upepo mti unaimba “mfalme ana peembe mfalme anapembe, waaa waaa waaa”. Ikatokea siku moja wawindaji wakapita karibu na mti ule wakastaajabu kusikia wimbo wa ajabu unaozungumza kuwa mfalme ana pembe.

 

Basi habari zikaanza kusambaa kwa kasi sana mpaka ikamfikia kinyozi. Watu wakawa wanafunga safari kwenda kuuangalia mti uanoimba kuwa mfalme ana pembe. Habari zilisambaa mpaka zikamfikia mfalme. Mafalme akatoka na msafara wake nae akashuhudie mti unaotoa siri yake ya pembe kichwani. Alishangaa sana, ilibidi siku ilofata aitishe mkutano mkubwa kwa kila atakaetaka kuhudhuria kwenye eneo lile lenye mti ule.

 

Basi watu walikusanyika sana eneo lile, watoto, wazee na vijana walimwaika eneo lile la tukio. Baada ya muda watu walipokusanyika akasimama na kuanza kuhutubia, kisha akavua kilembe chake watu wote wakashuhudia pembe kichwani mwake. Kisha akasema “nimeamini hakuna siri”. Na huu ndio mwisho wa hadithi ya kinyozi msiri wa mfalme. Basi Amina na Sadie walifurahi sana na wakamruhusu kijana aenelee kubakia pale.

 

Basi pale ndani chakula kikapikwa na watu wakawa wanakula na kunya na kufurahi. Mashairi yaliimbwa na furaha zaidi. Wakatowa pombe wakanywa na wakaendelea kufurahi pale ndani. Nyakati za swala pia ziliwapita palelpale walipokaa. Mapaka wanakuja kutambua ni jioni na kigiza kinakaribia kuingia. Zubeida akamwambia kijana “amka uende zako, muda wa kutengana na wewe umekaribia”. Kijana akaanza kujitetea tena kuwa amelewa sana hivyo hataweza kufika kwake. Kama watamruhusu alale pale mpaka kesho ataondoka na kurudi kwake.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa Tarehe 2024-09-09 13:41:15 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 41


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 3: Mlevi asimuliwa hadithi
Muendelezo wa simulizi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 2: Ni ndoto ama kweli???
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 4: Mshenga wa Aladini
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Nurdini na Barua ya mfalme wa baghadad
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 10: Hadithi ya Ndoto ya binti mgonjwa wa mfalme
Skmulizi hii ipo ndani ya kitabu cha kwanza kwenye hadithi za HALIF LELA U LELA...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 12: Sehemu ya tano ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 8 Part 3: Kijana mchonganishi
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 3 Part 1: Kisa cha mvuvi na jini
Simulizii hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA .... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 1: Carmaralzamani prince pekee
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 14: Simulizi ya binti wa kwanza na mbwa
Tuendeleee kuburudika na simulizii zetu nzuri kutoka katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 8: Aliyekatwa kidole gumba
Kojawapo ya simulizi iliyopo kwenye kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Taharuki kwa mfalme
Muendelezo..... Soma Zaidi...